Naomba yatokee haya Tanzania...

Aaaah, Police marufuku kuishiwa. maana wakiishiwa hawa jamaa raia ndo tutakayekoma. Watakuwa wanaangalia tu nyumba wanayoona ina unafuu wanavamia wanasema unahisiwa jambazi. Unakaa ndani kama siku tatu hivi hadi ukung'ute hela yote uliyonayo. watakuwa wanamkamata yeyote aliyevaa vizuri humo njiani ili awape chochote. Watatuomba lunch kwa sana, halafu tukikataa tutatishiwa kusingiziwa makosa. Watawatuma vibaka wakusanye simu zetu ili hela wagawane. Haya yanafanywa na polisi hivi sasa ambapo wana unafuu wa maisha, je wakiishiwa?

Wanafunzi pia wasipate ziro, manake wakipata ziro hatutafaidika chochote zaidi ya kuwa na kizazi cha wajinga. Walimu waishiwe, ilii wagome lakini watoto wetu tunataka wafaulu. Na ukumbuke kwamba ukiombea watoto wafeli, basi watakaofeli ni watoto wa walala hoi na si watoto wa walala hai. Maana ni watoto wa walala hoi ndio wanaosoma kwenye shule ambazo mwalimu wake analipwa na serikali.

Lakini zaidi ya yote, ninyi ni kuku tu, tangu lini dua lenu likampata mwewe. Endeleeni tu kuomba hizo dua na katu hazitakaa zitokee na wala hayo mapinduzi hayatatokea kwa kutegemea hizo bahati nasibu. Cha msingi kila mmoja mahali pake kama anaona anapunjwa au anaonewa kwa namna yoyote ile basi achukue hatua. Ili mapambano yaanze na si kusubiri eti yatokee mabaya zaidi. Maana nayo yana kero zake.
mkuu hapa watu hawako sirias

ni kupunguza presha za maisha tu
 
you have just missed the mickey out of our government

hahahaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa... JF ni kiboko, kuwanza tu hivi lazima kuna ujinias fulani au fyuzi moja mbili zimeblow



duh

Ni hakika mkuu.
 
mtoboa siri ametumia tu lugha ya picha, anachomaanisha ni Je nini kifanyike ili kuamsha mbongo za watanzania wengi ili wajue kuwa wao ndio watakaoleta mabadiliko na kujenga Tanzania mpya tunayo itamani...nchi zingine wakiguswa kidogo tu haraka wanaamka na kuchukua hatua na mambo yanada uzuri, e.g kenya, tunisia..(just few to mention) Sisi watanzania tumekabwa kila kona tuna hema juu juu lakini wapi ..bado hatuchukui hatua, Tatizo ni nini??????
 
Asante mkuu.

mtoboa siri ametumia tu lugha ya picha, anachomaanisha ni Je nini kifanyike ili kuamsha mbongo za watanzania wengi ili wajue kuwa wao ndio watakaoleta mabadiliko na kujenga Tanzania mpya tunayo itamani...nchi zingine wakiguswa kidogo tu haraka wanaamka na kuchukua hatua na mambo yanada uzuri, e.g kenya, tunisia..(just few to mention) Sisi watanzania tumekabwa kila kona tuna hema juu juu lakini wapi ..bado hatuchukui hatua, Tatizo ni nini??????
<br />
<br />
 
mtoboa siri ametumia tu lugha ya picha, anachomaanisha ni Je nini kifanyike ili kuamsha mbongo za watanzania wengi ili wajue kuwa wao ndio watakaoleta mabadiliko na kujenga Tanzania mpya tunayo itamani...nchi zingine wakiguswa kidogo tu haraka wanaamka na kuchukua hatua na mambo yanada uzuri, e.g kenya, tunisia..(just few to mention) Sisi watanzania tumekabwa kila kona tuna hema juu juu lakini wapi ..bado hatuchukui hatua, Tatizo ni nini??????
kwaajili tuna maisha bora kuliko hizo nchi hapo juu.
 
Back
Top Bottom