Naomba Ushauri

JOPA

Member
Feb 26, 2014
8
1
Naombeni ushauri jaman!mimi na mchumba wangu(hatujafunga ndoa) tumefanikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume!lakini tangu hapo kumekuwa na malumbano makubwa sana kiasi kwamba hadi sasa hivi mawasiliano ni hafifu.na mara nyingi nikiwa nahitaji pesa ya matumizi,inachukua mda kunipatia na nikisema nimkumbushe ananijibu anakumbuka lakini hajali shida yangu ya haraka.nikiwa namuhitaji anadai anafanya biashara yuko busy na hata akija hawezi akakaa zaidi ya mwezi,nikimtumia sms nzuri za mapenzi mwenzangu anapotezea,mara hajibu!kiukweli napata shida sana kiasi kwamba mimi mwenyewe nashawishika kutafuta mtu wa kuniliwaza ili nisiwe na mawazo zaidi!inshort yani mme wangu yupo busy zaidi na kazi kuliko familia!kwani hatuishi pamoja!mimi nipo kikazi Dodoma yeye yupo Mwanza na nikirudi nalazimika kwenda nyumbani kwetu,mana yeye hataki nikaishi kwake hadi tufunge ndoa!NAOMBENI USHAURI WAPENDWA NIFANYAJE?
 
Ooooh, Mianaume mingine ni Big ZERO (0) yaani majanga na hawajitambui ! having a baby ..hawajui kushukuru .
Shosti komaa na ujiwekee uamuzi wa kuishi pekee hadi Mungu atakufungulia heri mbele. usijali, usimjali.
 
Mi naona huyo bwana ana mtu pembeni kwanini anakuzuia kufikia kwake mpaka mfunge ndoa wakati nshapata mtoto?
 
mimi nipo kikazi dodoma yeye yupo mwanza na nikirudi nalazimika kwenda nyumbani kwetu,mana yeye hataki nikaishi kwake hadi tufunge ndoa!naombeni ushauri wapendwa nifanyaje?

funga ndoa...
 
Naombeni ushauri jaman!mimi na mchumba wangu(hatujafunga ndoa) tumefanikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume!lakini tangu hapo kumekuwa na malumbano makubwa sana kiasi kwamba hadi sasa hivi mawasiliano ni hafifu.na mara nyingi nikiwa nahitaji pesa ya matumizi,inachukua mda kunipatia na nikisema nimkumbushe ananijibu anakumbuka lakini hajali shida yangu ya haraka.nikiwa namuhitaji anadai anafanya biashara yuko busy na hata akija hawezi akakaa zaidi ya mwezi,nikimtumia sms nzuri za mapenzi mwenzangu anapotezea,mara hajibu!kiukweli napata shida sana kiasi kwamba mimi mwenyewe nashawishika kutafuta mtu wa kuniliwaza ili nisiwe na mawazo zaidi!inshort yani mme wangu yupo busy zaidi na kazi kuliko familia!kwani hatuishi pamoja!mimi nipo kikazi Dodoma yeye yupo Mwanza na nikirudi nalazimika kwenda nyumbani kwetu,mana yeye hataki nikaishi kwake hadi tufunge ndoa!NAOMBENI USHAURI WAPENDWA NIFANYAJE?

Naona kama umenichanganya sana
Enewei.............
 
1. Ulishaanza kujishauri kupata mtu wa kukuliwaza (too bad location yako hainiruhusu kuchangamkia fursa)

2. Kwa huyo mwanaume mtoto ni 'bahati mbaya' so it seems. Ni zaidi kama hakuwa na mpango wa kukaa kwako sema ndo hivyo tena 'mtoto hapenned'

3. Au kichwani anajiona bado mdogo kuanza majukumu ya kulea na familia na vitu kama hivyo. anajiona bado ana mengi ya kufanya. So he is kind of 'stressed'

4. Mna mipango gani kwenye maisha yenu? Ndoa au kulea mtoto tu?

4. Siku zote shilingi huwa na pande mbili. Nachelea kuwaza upande wa pili wa shilingi una hadithi gani ya kusema? Nikifika hapo naona ni bora nisitoe ushauri...mnajuana wenyewe vyema!!! Ninyi ndio watu perfect kuweza kutatua suala lenu.
 
endelea na maisha yako achana nae anaonekna bado utoto unamsumbua kila penye Giza nuru ipo mbeleni so best tafuta kazi Lea mwanao ukishfankiwa atajisogeza tu ww tupa kuleee
 
Unataka ushauri gani,

"unashawishika kujiliwaza na w/me wengine kupunguza mawazi" how doesn't that work??
-no wonder we ndo tatizo....
 
Mmmh mambo mengine hadi nashindwa kushangaa, eti hataki ukae kwake hadi mtakapooana.. Huku tayari mshajuana wee hadi na mtoto juu, sasa sijui mnasubiri nini kuishi pamoja as if kuzaa kabla ya ndoa ni acceptable. Aisee huyo ana mambo yaake
 
huyo anamwanamke mwingine tayar amini nachokuambia...... achana nae fanya yako japo ni ngum kwa mwanaume anaekupenda kutoka moyoni tena unamtoto wake hawez kukufanyia hayo ...
 
Aiseee! Bora umejua ndugu! Lea mwanao na nakuambia kuna aliye kwa ajili yako anakuja! Nilishakutana na situation hii ila nilijiambia good to goooooo! Na niligoo kweli hadi sasa niko kwenye ndoa ya aman na Upendo halafu alivo kichaa et akaanza kunitafta adai turudiane nilimtoaje baruuuu! Hadi sasa miaka 5 imepita ypo tuu anatoa macho mtaan! Wanaume bwana sijui wana nini et! Fanya maamuz magumu ya kumsahau japo c rahisi ila inawezekana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom