apologize
JF-Expert Member
- Jul 22, 2015
- 710
- 568
Habari wakuu?
Kuna binti nipo nae kwenye mahusiano kwa miezi sita sasa. Nilikutana nae kwenye mgahawa mmoja nilipokuwa naenda kupata chakula. Mimi bado sijaoa na sina familia maisha yangu mengi nakula kwenye migahawa.
Nilimpenda kiukweli hatimaye nikawa nae. Binti huyu akuniambia mama ameolewa ( tena ndoa ya kanisani) na alinificha mwanzo kama amezaa lakini nilipofanyana nae mapenzi kwa mara ya kwanza nilitambua Hilo nikamuuliza akakubari kuwa amezaa, Swala la ndoa hakusema.
Inshu ya ndoa nilikuja kujua kwa boss wake anapofanyia kazi wakati napiga nae story akanieleza huyu binti ameolewa tena ndoa halali ya kanisani wametengana na Mme wake kama miaka miwili nyuma.
Nilibidi nimuulize kuhusu Hilo swala alikiri kweli lakini wameachana kabisa. Nikamuuliza utaratibu gani mlitumia anasema waliandikishana ofisi za kijiji Tu hakuna alioenda mahakamani kudai talaka. ( Unafahamu mambo ya kijijini wanachukulia vitu rahisi).
Changamoto ninayo kutana nayo ni kuwa binti kamueleza mama yake kuwa Yuko na mimi na huwa namsikia anaongea nae kwenye simu na mama akisema msalimie mwenzako maana huyu binti mara nyingi anakuja kwangu anapika na kulala kwa siku ambazo haiingii kazini. Na kulala analala Kariba Kila siku kwangu.
Shida ninayo kutananayo nikimwambia mjulishe mama yako kuwa wewe ni mjamzito tuone anasemaje. Hawezi kumwambia mpaka mimba iwe kubwa ya almost miezi Saba au mimi niwaambie wazazi wangu kuwa yeye ni mjamzito.
Mimi nitawezaje kuwaeleza wazazi wangu kuwa Nimempa binti mjamzito kumbuka ni mke wa mtu ambaye hana talaka na pia binti anataka kuishi wote rasmi akiwa mjamzito japo maisha yangu ya kujitafuta lakini naishi kwa bajeti ya laki 2 na 50 kwa mwezi.
Naombeni Ushauri juu ya hilo kwa wazoefu na mnisamehe siyo mzuri kwenye kuandika masimulizi.
Kuna binti nipo nae kwenye mahusiano kwa miezi sita sasa. Nilikutana nae kwenye mgahawa mmoja nilipokuwa naenda kupata chakula. Mimi bado sijaoa na sina familia maisha yangu mengi nakula kwenye migahawa.
Nilimpenda kiukweli hatimaye nikawa nae. Binti huyu akuniambia mama ameolewa ( tena ndoa ya kanisani) na alinificha mwanzo kama amezaa lakini nilipofanyana nae mapenzi kwa mara ya kwanza nilitambua Hilo nikamuuliza akakubari kuwa amezaa, Swala la ndoa hakusema.
Inshu ya ndoa nilikuja kujua kwa boss wake anapofanyia kazi wakati napiga nae story akanieleza huyu binti ameolewa tena ndoa halali ya kanisani wametengana na Mme wake kama miaka miwili nyuma.
Nilibidi nimuulize kuhusu Hilo swala alikiri kweli lakini wameachana kabisa. Nikamuuliza utaratibu gani mlitumia anasema waliandikishana ofisi za kijiji Tu hakuna alioenda mahakamani kudai talaka. ( Unafahamu mambo ya kijijini wanachukulia vitu rahisi).
Changamoto ninayo kutana nayo ni kuwa binti kamueleza mama yake kuwa Yuko na mimi na huwa namsikia anaongea nae kwenye simu na mama akisema msalimie mwenzako maana huyu binti mara nyingi anakuja kwangu anapika na kulala kwa siku ambazo haiingii kazini. Na kulala analala Kariba Kila siku kwangu.
Shida ninayo kutananayo nikimwambia mjulishe mama yako kuwa wewe ni mjamzito tuone anasemaje. Hawezi kumwambia mpaka mimba iwe kubwa ya almost miezi Saba au mimi niwaambie wazazi wangu kuwa yeye ni mjamzito.
Mimi nitawezaje kuwaeleza wazazi wangu kuwa Nimempa binti mjamzito kumbuka ni mke wa mtu ambaye hana talaka na pia binti anataka kuishi wote rasmi akiwa mjamzito japo maisha yangu ya kujitafuta lakini naishi kwa bajeti ya laki 2 na 50 kwa mwezi.
Naombeni Ushauri juu ya hilo kwa wazoefu na mnisamehe siyo mzuri kwenye kuandika masimulizi.