Naomba msaada wa ushauri mtoto mtukutu

moghaka

JF-Expert Member
May 16, 2011
252
143
Wakuu tafadhalini sana naomba msaada wenu, kijana mkorofi, mtukutu amemaliza f4-2010 matokeo ana D moja tu ya biology,veta hataki anataka kuunga certificate ya business, akaomba ali-sit mwaka huu 2011, shuleni fujo, walimu wanadai anakunywa pombe, sigara, kutoroka n.k wamemfukuza na malalamishi km hayo alikuwanayo akiwa f4, nimechoka sana, naomba msaada wenu wa kila hali niko tayari na ndio first born, je pana shule ya WATUKUTU kama hawa ?
 
nionavyo mimi

1. Maombi

2. hiyo ni adolescence inamsumbua kaa nae chini muulize mipango yake ya maisha na usiwe mkali sana, relax muulekeze bila kumgombeza kama anataka kuwa mtu huku dunia anapaswa kuenenda vipi? kwa sababu yeye anaona anavyofanya hayo ndo maisha

3. msome mtoto kama sio adolescence pengine ana frustration fulani na anaona hiyo ndio njia.

4. chunguza kwa umakini makundi ya huyo mtoto na akiwa nyumbani dont let him be so loose keep him busy by different activities whether he likes them or not.

5. usiwe na wasiwasi hilo ni jaribu tu katika familia yako litapita

6. kama unaweza pata shule ya masista au mapadri watakusaidia pia kumnyoosha

7. mkazanie sana kujifunza mambo ya dini ili aone hayo matendo yake si sawa hata kwa Mungu

8. punguza kiasi cha pesa unachompa coz anapata wapi hela ya pombe.

9. muambie hautakuwa nae milele he has to get his own life on track.

10. usichoke kumpenda
 
Wakuu tafadhalini sana naomba msaada wenu, kijana mkorofi, mtukutu amemaliza f4-2010 matokeo ana D moja tu ya biology,veta hataki anataka kuunga certificate ya business, akaomba ali-sit mwaka huu 2011, shuleni fujo, walimu wanadai anakunywa pombe, sigara, kutoroka n.k wamemfukuza na malalamishi km hayo alikuwanayo akiwa f4, nimechoka sana, naomba msaada wenu wa kila hali niko tayari na ndio first born, je pana shule ya WATUKUTU kama hawa ?

Kwanini usijaribu kumpeleka jeshini?
 
umesahau hz methali? Samaki mkunje angali mbichi..!
ama
Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.
Ushauri wangu ni kwamb jaribu kuongea naye na umcctize nini muhtasar wa maisha yake ya baadaye after ur decease (pole) na kama haelewi mwombe mungu ambadilishe.
my take: analinga na hzo mali zako ama cheo chako.
 
nionavyo mimi

1. Maombi

2. hiyo ni adolescence inamsumbua kaa nae chini muulize mipango yake ya maisha na usiwe mkali sana, relax muulekeze bila kumgombeza kama anataka kuwa mtu huku dunia anapaswa kuenenda vipi? kwa sababu yeye anaona anavyofanya hayo ndo maisha

3. msome mtoto kama sio adolescence pengine ana frustration fulani na anaona hiyo ndio njia.

4. chunguza kwa umakini makundi ya huyo mtoto na akiwa nyumbani dont let him be so loose keep him busy by different activities whether he likes them or not.

5. usiwe na wasiwasi hilo ni jaribu tu katika familia yako litapita

6. kama unaweza pata shule ya masista au mapadri watakusaidia pia kumnyoosha

7. mkazanie sana kujifunza mambo ya dini ili aone hayo matendo yake si sawa hata kwa Mungu

8. punguza kiasi cha pesa unachompa coz anapata wapi hela ya pombe.

9. muambie hautakuwa nae milele he has to get his own life on track.

10. usichoke kumpenda


Aina hiyo ya mtoto na hao hapo kwenye red si kitawaka?
 
yah huyo mpeleke jeshini tu labda kama atagoma...lakini kule ndo kwa wakuu atafunzwa nidhamu ya ukubwani
 
Kuna wakati wenye matatizo ni wazazi katika njia za malezi, katika umri alionao NEEMA ya Mungu yahitajika katika kumrejesha katika njia iliyo sahihi au la hasha DUNIA NDIYO ITAKAYOMFUNZA. Watoto wanaelekezwa katika umri wa 0 - 12 (ndipo hapo husemwa SAMAKI MKUNJE ANGALI MBICHI) , akivuka miaka 12 hekima ya ziada yahitajika katika kumwelekeza mto njia impasayo. Hivyo basi kwa sasa jitahidi kumuomba Mungu kwa ajili yake, mshirikishe katika mambo yahusuyo familia mara kwa mara ili atambue kwamba yeye ni sehemu ya familia na anahitajika sana huku mkimkumbusha wajibu wake wa baadae katika kuchukua majukumu ya familia. Usimchukie kwa yale anayoyatenda; kama unasikia anakunywa Pombe au Kuvuta sigara mpe uhuru wa kutumia mbele yako, huku mkimkumbusha madhara ya kufanya hivyo bila ya kumhukumu. Hii itakusaidia wewe kumfahamu badala ya kusikia tu kutoka kwa walimu na watu wengineo, wakati mwingine wanaweza kuwa wanamhukumu katika mambo asiyoyatenda. Wakati nikiwa sekondari Baba yangu alikuwa anaelezwa kwamba mimi navuta bangi na yeye alikuwa anaamini hivyo, hii ilitokana na mimi kuambatana na marafiki ambao wanavuta bangi. Lakini ukweli ni kwamba kwa wakati huo nilikuwa sijawahi hata kujaribu.
 
Wakuu tafadhalini sana naomba msaada wenu, kijana mkorofi, mtukutu amemaliza f4-2010 matokeo ana D moja tu ya biology,veta hataki anataka kuunga certificate ya business, akaomba ali-sit mwaka huu 2011, shuleni fujo, walimu wanadai anakunywa pombe, sigara, kutoroka n.k wamemfukuza na malalamishi km hayo alikuwanayo akiwa f4, nimechoka sana, naomba msaada wenu wa kila hali niko tayari na ndio first born, je pana shule ya WATUKUTU kama hawa ?

POLE KWA MKASA.INGEKUWA VEMA KAMA UNGETUJUZA NANI ALIMLEA ALIPOKUWA MDOGO?JE ALIKUWA ANAADHIBIWA ALIPOKUWA ANAFANYA MAKOSA PINDI ALIPOKUWA MDOGO?ALIKWENDA SHULE AKIWA NA KIASI GANI CHA MATUMIZI?KULIKUWA KUNA UTARATIBU WA KUMSEMA ANAPOFANYA MAKOSA?NYUMBANI KUNA MALI INAYOMPA KIBURI?ANAVUTA BANGI?NIJIBU HAYO ILI NIKUPE MENGINE.TAFUTA MZEE WA HESHIMA AMBAYE ATAMPA DARASA LA KUTOSHA JUU YA MAISHA NA TARATIBU ZAKE.kuna uwezekano ujana unamsumbua!pia wakati mwingine jaribuni kutomjali ili ajue umuhimu wenu!Pia akileta utata mpelekeni mahakamani kwa makosa anayotenda,nina iman akifungwa itakuwa vizuri kidogo.Kuna mmoja alifungwa karud kanyooka.Pia ikiwezekana mbembeleze aende JKT ATARUD NA ADABU.
 
Hujasema status yako. ie single parent, divorced, married. Je ni mtoto nje ya ndoa au una m/watoto nje ya ndoa
. Huwezi kupata ushauri mzuri bila vitu hivi kufahmika pamoja na mambo mengine.
 
Eti waalimu wanadai kwa mtoto ni mlevi, anavuta bhange, anatoroka... Wazazi wengine bwana!
 
Pole sana; Kwanza muombee sana kwa Mungu.
Pili hope kwenu ni kijijini, mpeleke kijijini kama kuna baba yake mkubwa au mdogo au mjomba asiende kwa bibi/babu atawasumbua, akae huko kwa muda wa zaidi ya miezi mitatu na atakayekaa naye awe anaenda naye shamba kulima tena ampe shamba lake na alime na kupanda na kupalilia kila simu kasoro siku za ibada. Na hakikisha nyumba anayokwenda haina umeme wala anasa zozote za mjini.

Kama ulimnunulia simu mnyang'nye kipindi hiki atachokuwa kijijini
Mpeleke mwenyewe na umuachie hela kidogo sana zisizoweza kutosha nauli ya kurudia kijijini hadi hapo utakapomfuata.
Mpe masharti kwamba kama anapenda shule, basi akae hapo wakati unatafakari nini asome na unajipanga kifedha.
Mwambie ndg utakayempelekea mtoto wako kwamba ahakikishe anafanya kazi na siku za ibada anaenda kusali bila kukosa

Kama huwa anakusiliza, akikaa kijijini kwa muda huo, bila tv, umeme, simu, na kufanya kazi za shamba atabadilika ila atakayekaa naye awe strict kwa nidhamu na kazi.
Wakati yupo jijini muombe Mungu ambadilishe na asirudi hadi utapomfuata
All the best
 
POLE KWA MKASA.INGEKUWA VEMA KAMA UNGETUJUZA NANI ALIMLEA ALIPOKUWA MDOGO?JE ALIKUWA ANAADHIBIWA ALIPOKUWA ANAFANYA MAKOSA PINDI ALIPOKUWA MDOGO?ALIKWENDA SHULE AKIWA NA KIASI GANI CHA MATUMIZI?KULIKUWA KUNA UTARATIBU WA KUMSEMA ANAPOFANYA MAKOSA?NYUMBANI KUNA MALI INAYOMPA KIBURI?ANAVUTA BANGI?NIJIBU HAYO ILI NIKUPE MENGINE.TAFUTA MZEE WA HESHIMA AMBAYE ATAMPA DARASA LA KUTOSHA JUU YA MAISHA NA TARATIBU ZAKE.kuna uwezekano ujana unamsumbua!pia wakati mwingine jaribuni kutomjali ili ajue umuhimu wenu!Pia akileta utata mpelekeni mahakamani kwa makosa anayotenda,nina iman akifungwa itakuwa vizuri kidogo.Kuna mmoja alifungwa karud kanyooka.Pia ikiwezekana mbembeleze aende JKT ATARUD NA ADABU.

Ushauri wako umetulia, nimeupenda. Pia umeuliza maswali ya msingi sana
 
Pole sana kaka Moghaka, hata mimi nilipita katika kipindi cha nduguyo. Kikubwa ni kuwa anadhani ninyi mnashirikiana na walimu kumchukia, tayari ubongo wake umejijenga kwa hilo. Kuhusu balehe, NO, hakuna balehe ya 17+ siku hizi. Ushauri wangu ni kuwa, kwanza, punguza kumuonesha kuwa umemchoka, kijana kama huyo ukimhubiria kuhusu mapungufu yake mara nyingi unakuwa kama wimbo, anauzoea na haumpi tabu kabisa. Nadhani wewe ndio mlezi wake, tumia nafasi ya yeye kuomba fedha au privileji zingine kumueleza vile unakwazika na matendo yake, au mpotezee kwa muda mpaka ajistukie.
 
Eti waalimu wanadai kwa mtoto ni mlevi, anavuta bhange, anatoroka... Wazazi wengine bwana!
nlidhani ingekuwa busara kama ungetoa maoni yako kwa kumshauri na sii kwa kumkejeli we kama huna jibu sii ukae kimya tu.Yatakukuta na ww naona bado hujui nini maana ya uzazi.
 
POLE KWA MKASA.INGEKUWA VEMA KAMA UNGETUJUZA NANI ALIMLEA ALIPOKUWA MDOGO?JE ALIKUWA ANAADHIBIWA ALIPOKUWA ANAFANYA MAKOSA PINDI ALIPOKUWA MDOGO?ALIKWENDA SHULE AKIWA NA KIASI GANI CHA MATUMIZI?KULIKUWA KUNA UTARATIBU WA KUMSEMA ANAPOFANYA MAKOSA?NYUMBANI KUNA MALI INAYOMPA KIBURI?ANAVUTA BANGI?NIJIBU HAYO ILI NIKUPE MENGINE.TAFUTA MZEE WA HESHIMA AMBAYE ATAMPA DARASA LA KUTOSHA JUU YA MAISHA NA TARATIBU ZAKE.kuna uwezekano ujana unamsumbua!pia wakati mwingine jaribuni kutomjali ili ajue umuhimu wenu!Pia akileta utata mpelekeni mahakamani kwa makosa anayotenda,nina iman akifungwa itakuwa vizuri kidogo.Kuna mmoja alifungwa karud kanyooka.Pia ikiwezekana mbembeleze aende JKT ATARUD NA ADABU.

Tuko pamoja mkuu! Huruma hailei mwana.
 
umeyasababishwa mwenyewe mzaz....kuna shule moja iko kenya huko watot wakotrofi wote wako kule
 
Wakuu tafadhalini sana naomba msaada wenu, kijana mkorofi, mtukutu amemaliza f4-2010 matokeo ana D moja tu ya biology,veta hataki anataka kuunga certificate ya business, akaomba ali-sit mwaka huu 2011, shuleni fujo, walimu wanadai anakunywa pombe, sigara, kutoroka n.k wamemfukuza na malalamishi km hayo alikuwanayo akiwa f4, nimechoka sana, naomba msaada wenu wa kila hali niko tayari na ndio first born, je pana shule ya WATUKUTU kama hawa ?

mpeleke mombasa
 
Mwana umleavyo ndivyo akuavyo huyo kwa sasa ni maombi tu maana kila utakalomwambia anakuona umepitwa na wakati
 
Kuna shule moja kenya kama utahitaji jina lake ni PM.Mtoto unamkabidhi mwalimu hapa dar na haruhusiwi kurudi mwenyewe mpaka utakabidhiwa tena na mwalimu watakapofunga shule.Akifika shule haruhusiwi kutoka nje ya eneo la shule na haruhusiwi kuwa na simu.Ukitaka kuwasiliana nae utampigia matron au patron na mtoto wako utaongea nae.
Hii ilimsaidia jirani yangu ambaye binti yake alianza ukorofi wa ajabu alipofika form two alimpeleka huko na sasa amebadilika
Kumbadilishia mazingira na kampani inasaidia sana kwani yawezekana ana group baya la marafiki .
 
Pole ila hujanijibu maswali ambayo nilikuuliza mkuu.Au bado unampenda mwanao?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom