Kwa kumbukumbu zangu hiyo picha ni ya wakati wa kampeni mwaka 2010. Mleta maana amejifanya kama ameiona mwenyewe leo ilihali amkopi kutoka kwa wenzie. Hii ni mbinu ambayo CCM walishaitumia mwaka 2010 na bado hawakupata kura za kutosha huko Kigoma.Sikuwa nina nia ya kuchangia leo lakini hii imenisukuma kutoa machache niliyo nayo.Binafsi hii naiona kama changamoto kwa wapiganaji wa CHADEMA kuzidi kuwawashia moto hawa jamaa wa chama tawala,tangazo kama hili linaonesha wazi kuwa wameishiwa na sera na uwezo wa kutatua kero za wananchi kiasi cha kufikia kubuni mbinu za kuwahonga watu mchele na sukari kwa kisingizio cha punguzo la bei.Kama kawaida yao walivyokuwa wakitoa ubwabwa wakati wa kampeni,wameona waanze kuwarubuni wananchi mapema.Ni aibu kwa chama kilichokuwa madarakani zaidi ya miaka 35 kuja kwa wananchi na sera kama hizi.Kwa wapiganaji wa CHADEMA hii ni nafasi nzuri kwenu,kwani huu ni mtaji mzuri endapo mtaweza kuutumua kwa kuwaelemisha wananchi juu ya kushindwa kwa watawala waliopo madarakani hadi kufikia kwenye siasa za nyanya na vitunguu sokoni,Kila la kheri wapiganaji..