Nani zaidi?

Ustaadh

JF-Expert Member
Oct 25, 2009
413
19
Nauliza.....nani zaidi?

  • Hayati Mwl. Nyerere alipigania uhuru na kujaribu kutekeleza siasa ya ujamaa na kujitegemea. Kuna wanaodai alijitahidi kwa kiasi kikubwa kuinua pato la mwananchi wa kawaida na kupunguza tofauti ya kipato kati ya aliye nacho na asiye nacho. Aidha, alifanikiwa kutokomeza ukabila, udini na kuhakikisha taifa kwa kiasi kikubwa linaunganishwa kwa lugha moja. Pamoja na mafanikio, wapo wanaodai kuwa sera zake zimewafanya watanzania kubweteka na kutokuwa na uwezo wa kupigania haki zao. Aidha, kuna wanaodai kuwa aliingiza nchi katika vita na nchi jirani kwa lengo la kumrejesha swahiba yake aliyepinduliwa katika nchi hiyo. Mwishoni mwa utawala wake, sera zake hazikuendana na hali halisi na zimebakia katika maandiko bila utekelezaji. Alipachikwa majina mengi mfano "Mchonga", "Musa", "Haambiliki" n.k.
  • Alhaj Ali Hassan Mwinyi aliruhusu soko huria - ilikuwa kama sandakalawe - mwenye kupata alipata, wengine hawakuambulia. Kuna wanaodai kuwa sera zake kwa kiasi fulani zilichangia kuporomoka kwa uchumi. Aidha, kuna wanaodai kuwa aliwekwa makusudi na Rais wa kwanza ili atumike kama "remote control". Amebaki na jina la "Mzee Ruksa" kwa "kufungua" milango ya uchumi.
  • Bw. Benjamin William Mkapa: Anasifika kwa kuimarisha uchumi na serikali kupata mapato zaidi yatokanayo na kodi.Inadaiwa alifanikiwa kuboresha miundo mbinu (hasa barabara). Hata hivyo anatuhumiwa kuendesha biashara Ikulu na kujiuzia baadhi ya rasilimali za taifa. Aidha wakati wa utawala wake nchi illingia katika mikataba ya uchimbaji madini ambayo kuna madai kuwa inawanufaisha zaidi wawekezaji wa kigeni kuliko taifa. Aliwahi kuitwa "Mr. Clean" ingawa jina hilo limefifia haraka.
  • Luteni-Kanali mstaafu Jakaya Kikwete: Anakaribia kumaliza ngwe ya kwanza kwa mujibu wa "utaratibu wa CCM", na anatarajiwa kupewa kipindi kingine cha miaka mitano. Inasemekana amewezesha nchi kunufaika na misaada mingi kutokana na ziara zake nchi za nje. Kuna wanaomtuhumu kwa kutoshughulikia masuala yanayolididimiza taifa kama ufisadi, mikataba mibovu na uwajibikaji. Pia anatuhumiwa kudidimiza juhudi za kumchukulia hatua Rais mstaafu Mkapa na wahujumu uchumi. Majina aliyowahi kupachikwa ni pamoja na "handsome boy" na mwanzoni mwa utawala wake yeye na aliyekuwa Waziri Mkuu (Edward Lowassa) walibatizwa jina la "Boyz to Men".
Nauliza....nani zaidi?
 
Nani zaidi kwa nini? Kwanza Mwinyi sio aliyeanzisha soko huria? Angalia facts zako.
 
Nyerere kama kiongozi alikuwa na mapungufu yake mengi tu, lakini kamwe hawezi kulinganishwa na Viongozi kama Mwinyi, Mkapa au Kikwete. Katika utendaji, kuweka maslahi ya nchi mbele, kuipenda Tanzania na Watanzania. kutokuwa na uroho wa kutumia dhamana ya uongozi aliokabidhiwa na Watanzania ili kujitajirisha yeye, familia yake ndugu, jamaa na marafiki na siku zote kuwa mkweli kwa Watanzania. Hata wenzetu katika nchi mbali mbali za Kiafrika wanamkumbuka sana Nyerere kama kiongozi shupavu na aliyeipenda nchi yake na watu wake kwa moyo wake wote.
 
Nyerere kama kiongozi alikuwa na mapungufu yake mengi tu, lakini kamwe hawezi kulinganishwa na Viongozi kama Mwinyi, Mkapa au Kikwete. Katika utendaji, kuweka maslahi ya nchi mbele, kuipenda Tanzania na Watanzania. kutokuwa na uroho wa kutumia dhamana ya uongozi aliokabidhiwa na Watanzania ili kujitajirisha yeye, familia yake ndugu, jamaa na marafiki na siku zote kuwa mkweli kwa Watanzania. Hata wenzetu katika nchi mbali mbali za Kiafrika wanamkumbuka sana Nyerere kama kiongozi shupavu na aliyeipenda nchi yake na watu wake kwa moyo wake wote.
Bubu,
Je kukaa madarakani kwa miaka 23 siko kulikompeleka Mwlm KOMBO?
 
Kwa Mtazamo wangu mimi hakuna hata mmoja aliyekuwa mbele karibu wote wako sawa Baba wa Taifa Mwalimu nyerere Alishindwa kwa Ujamaa wake matokeo yake akapigana na Nduli IDD Amin Dada Matokeo yake Nchi imekuwa Masikini mpaka leo. Mzee wa (Rukhsa) Rais wa pili Ally Hassan Mwinyi nae Umasikini alioucha Babawa Taifa nae akaja Mzee Mwinyi kuuendeleza nae akapiga Miaka 10 bila ya Mafanikio yoyote. Na aliyefuatia Rais Wa Tatu Mzee Mkapa nae aliwabana wananchi kwa kodi lakini naye Mkapa hakuweza kuondowa umasikini watu wanaoishi mijini hawana Umeme, Maji safi hakuna basi Matatizo yamezidi kila kukicha na huyo tuliyekuwa nae Luteni-Kanali mstaafu Jakaya Kikwete kazi yake ni kutembea kila nchi kwa lugha ya kizungu tunaweza kumwita ni Tourist wa kuomba Misaada kwa wafadhili na hakuna cha maana mpaka sasa tutategemea Misaada ya wafadhili kutoka nje ya Nchi mpaka lini? Nchi imejaa Ufisadi,Rushwa,Wizi Wa Mali ya Umma,Umasikini,Maradhi,hatuna Maendeleo yoyote Mpaka sasa kila kukicha Matatizo yanazidi Tuamke Watanzania Tuijenge nchi yetu jamani tunashindwa na nchi za jirani kama Uganda,Malawi,na Kenya? tuko bado Usingizini tuamkeni jamani. (MIAFRIKA BWANA NDIVYO ILIVYO)
 
Kwa Mtazamo wangu mimi hakuna hata mmoja aliyekuwa mbele karibu wote wako sawa Baba wa Taifa Mwalimu nyerere Alishindwa kwa Ujamaa wake matokeo yake akapigana na Nduli IDD Amin Dada Matokeo yake Nchi imekuwa Masikini mpaka leo. Mzee wa (Rukhsa) Rais wa pili Ally Hassan Mwinyi nae Umasikini alioucha Babawa Taifa nae akaja Mzee Mwinyi kuuendeleza nae akapiga Miaka 10 bila ya Mafanikio yoyote. Na aliyefuatia Rais Wa Tatu Mzee Mkapa nae aliwabana wananchi kwa kodi lakini naye Mkapa hakuweza kuondowa umasikini watu wanaoishi mijini hawana Umeme, Maji safi hakuna basi Matatizo yamezidi kila kukicha na huyo tuliyekuwa nae Luteni-Kanali mstaafu Jakaya Kikwete kazi yake ni kutembea kila nchi kwa lugha ya kizungu tunaweza kumwita ni Tourist wa kuomba Misaada kwa wafadhili na hakuna cha maana mpaka sasa tutategemea Misaada ya wafadhili kutoka nje ya Nchi mpaka lini? Nchi imejaa Ufisadi,Rushwa,Wizi Wa Mali ya Umma,Umasikini,Maradhi,hatuna Maendeleo yoyote Mpaka sasa kila kukicha Matatizo yanazidi Tuamke Watanzania Tuijenge nchi yetu jamani tunashindwa na nchi za jirani kama Uganda,Malawi,na Kenya? tuko bado Usingizini tuamkeni jamani. (MIAFRIKA BWANA NDIVYO ILIVYO)

Humtendei haki kabisa kwa kutoa kauli kwamba Mwalimu yuko sawa na Mwinyi, Mkapa na Kikwete. Na si kweli kwamba umaskini wa Tanzania ulisababishwa na vita vya kumtoa nduli ndani ya mipaka yetu. Mwalimu aling'atuka miaka 25 iliyopita tukaingia katika sera za ubinafsishaji ambazo Watanzania wengi hawakuona manufaa yake, tukaingia mikataba ya uchimbaji wa madini yetu mbali mbali ikiwemo dhahabu ambayo hadi hii leo Watanzania hatujaona manufaa ya mikataba hiyo kutokana na kuambulia 3% tu ya mapato yote. Tukaona jinsi nchi ilivyovamiwa na mafisadi wa Kiwira, Rada, Ndege ya rais, Richmond, Meremeta, Mwananchi Gold na hadi hii leo hakuna hata mmoja aliwajibishwa.

Mwalimu alikuwa na sera nzuri sana isipokuwa watekelazaji wake walikuwa hawako makini. Angalia kama sera ya kuhakikisha elimu bure kuanzia shule ya msingi hadi Varsity matokeo yake mpaka kesho kutwa yanainemeesha dunia na si Tanzania tu maana wasomi wengi wa Kitanzania walio nje ni matunda ya sera nzuri za Mwalimu katika elimu kuhakikisha kwamba watoto wote wa Kitanzania wanapata elimu mpaka ya juu bila kujali kipato cha wazazi wao. Je, ulitaka Mwalimu asipigane ile vita na kumuacha nduli aiteke Kagera? :confused:
 
Humtendei haki kabisa kwa kutoa kauli kwamba Mwalimu yuko sawa na Mwinyi, Mkapa na Kikwete. Na si kweli kwamba umaskini wa Tanzania ulisababishwa na vita vya kumtoa nduli ndani ya mipaka yetu. Mwalimu aling'atuka miaka 25 iliyopita tukaingia katika sera za ubinafsishaji ambazo Watanzania wengi hawakuona manufaa yake, tukaingia mikataba ya uchimbaji wa madini yetu mbali mbali ikiwemo dhahabu ambayo hadi hii leo Watanzania hatujaona manufaa ya mikataba hiyo kutokana na kuambulia 3% tu ya mapato yote. Tukaona jinsi nchi ilivyovamiwa na mafisadi wa Kiwira, Rada, Ndege ya rais, Richmond, Meremeta, Mwananchi Gold na hadi hii leo hakuna hata mmoja aliwajibishwa.

Mwalimu alikuwa na sera nzuri sana isipokuwa watekelazaji wake walikuwa hawako makini. Angalia kama sera ya kuhakikisha elimu bure kuanzia shule ya msingi hadi Varsity matokeo yake mpaka kesho kutwa yanainemeesha dunia na si Tanzania tu maana wasomi wengi wa Kitanzania walio nje ni matunda ya sera nzuri za Mwalimu katika elimu kuhakikisha kwamba watoto wote wa Kitanzania wanapata elimu mpaka ya juu bila kujali kipato cha wazazi wao. Je, ulitaka Mwalimu asipigane ile vita na kumuacha nduli aiteke Kagera? :confused:

Mwalimu Nyerer Ana Makosa yake Yeye ndiyo aliyoanzisha Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea Matokeo yake aliwafukuza Matajiri, mwaka 1967 alipoanzisha azimio la Arusha matokeo yake Nchi ikawa Masikini,Matajiri walipoondoka Nchini kisha akapigana na Nduli idd Amin Matokeo yake akasema tujiandae kwa miezi 18 kwakukabiliana na hali mbaya ya kiuchumi Matokeo yake sio miezi ni Miaka 18 au zaidi mpaka leo nchi yetu imekuwa na Umasikini umeona Ya Mugabe nchi yake inavyokwenda mpaka sasa?kawfukuza Wazungu Matokeo yake wananchi wake ndiowanaopata tabu Nchi imekwisha hakuna chakula njaa tupu pesa haina dhamani ya Zimbabwe kwa hiyo hakuna tofauti kati ya Mwalimu nyerere ,Mwinyi,Mkapa na kiongozi wetu wa Sasa itabidi CCM iondoke kwenye uongozi tunataka Maendeleo bwana sio kumsifia mtu kwa jina upo na mimi BUbu Atakapokusema?
 
Economy Main articles: Economy of Tanzania, Transport in Tanzania, and Microfinance in Tanzania A market near Arusha. The economy is mostly based on agriculture, which accounts for more than half of the GDP, provides 85 percent (approximately) of exports, and employs approximately 80 percent of the workforce. Topography and climate, though, limit cultivated crops to only 4 percent of the land area. The nation has many resources including gold and natural gas. Extraction of natural gas began in the 2000s. Gas is drawn into the commercial capital, Dar Es Salaam and exported to various markets overseas. Lack of overall development has hampered the extraction of these various resources, and even up to the present there has been effort to develop the natural resource sector but no major quantifiable results. Industry is mainly limited to processing agricultural products and light consumer goods. Tanzania has vast amounts of natural resources including gold, diamonds, coal, iron ore, uranium, nickel, chrome, tin, platinum, coltan, niobium and other minerals. It is the third-largest producer of gold in Africa after South Africa and Ghana. Tanzania is also known for the Tanzanite gemstones. Tanzania has dozens of beautiful national parks like the world famous Serengeti and the Ngorongoro Conservation Area, that generate income with a large tourism sector that plays a vital part in the economy. Growth from 1991 to 1999 featured a pickup in industrial production and a substantial increase in output of minerals, led by gold. Commercial production of natural gas from the Songo Songo island in the Indian Ocean off the Rufiji Delta commenced 2004,[17] with natural gas being pumped in a pipeline to the commercial capital Dar es Salaam, with the bulk of it being converted to electricity by the public utility and private operators. A new gas field is being brought on stream in Mnazi Bay. Recent public sector and banking reforms, and revamped and new legislative frameworks have all helped increase private-sector growth and investment. Short-term economic progress also depends on curbing corruption and cutting back on unnecessary public spending.[18] Prolonged drought during the early years of the 21st century has severely reduced electricity generation capacity (some 60 percent of Tanzania's electricity supplies are generated by hydro-electric methods).[19] During 2006, Tanzania suffered a crippling series of "load-shedding" or power rationing episodes caused by a shortfall of generated power, largely because of insufficient hydro-electric generation. Plans to increase gas- and coal-fueled generation capacity are likely to take some years to implement, and growth is forecast to be increased to seven per cent per year, and perhaps eight or more.[20] There are 3 major airlines in Tanzania, the Air Tanzania Corporation, Precision Air which provide local flights (Arusha, Kigoma, Mtwara, Mwanza, Musoma, Shinyanga, Zanzibar) and regional flights to Kigali, Nairobi, Mombasa routes and a third one that provides local flights only. There are also several charter aeroplane firms. There are two railway companies: TAZARA caters for service between Dar-es-Salaam and Kapiri Mposhi, a district of the Central Province in Zambia. The other one is the Tanzania Railways Corporation, which provides services between Dar-es-Salaam and Kigoma, a town on the shores of Lake Tanganyika and between Dar-es-Salaam and Mwanza, a city on the shores of Lake Victoria. There is also a service across the Indian Ocean between Dar-es-Salaam and Zanzibar by several modern hydrofoil boats. Tanzania is part of the East African Community and a potential member of the planned East African Federation.
 
Mwalimu Nyerer Ana Makosa yake Yeye ndiyo aliyoanzisha Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea Matokeo yake aliwafukuza Matajiri, mwaka 1967 alipoanzisha azimio la Arusha matokeo yake Nchi ikawa Masikini,Matajiri walipoondoka Nchini kisha akapigana na Nduli idd Amin Matokeo yake akasema tujiandae kwa miezi 18 kwakukabiliana na hali mbaya ya kiuchumi Matokeo yake sio miezi ni Miaka 18 au zaidi mpaka leo nchi yetu imekuwa na Umasikini umeona Ya Mugabe nchi yake inavyokwenda mpaka sasa?kawfukuza Wazungu Matokeo yake wananchi wake ndiowanaopata tabu Nchi imekwisha hakuna chakula njaa tupu pesa haina dhamani ya Zimbabwe kwa hiyo hakuna tofauti kati ya Mwalimu nyerere ,Mwinyi,Mkapa na kiongozi wetu wa Sasa itabidi CCM iondoke kwenye uongozi tunataka Maendeleo bwana sio kumsifia mtu kwa jina upo na mimi BUbu Atakapokusema?

Nchi yeyote ni lazima imiliki uchumi wake badala ya kumilikiwa na wageni. Mwalimu aliliona hilo na ndiyo maana akataifisha mali zile ili uchumi uwe mikononi mwa Watanzania. Na kuhakikisha makampuni yale na mengine mapya yanaongozwa na Watanzania akawapeleka Watanzania wengi kusoma nchi za nje na pia kujenga UDSM, IDM na kadhalika ili kuhakikisha Tanzania inazalisha wasomi wake wenyewe wa kushika nafasi mbali mbali za juu na za kati. Akaanzisha makampuni chungu nzima na kujenga viwanda mbali mbali ambavyo vilichangia katika uchumi wa Taifa na kucreate ajira chungu nzima.

Mwalimu nimesema na narudia tena kama kiongozi alikuwa na mapungufu yake mengi tu lakini mazuri yake yanashinda mapungufu yake kwa kiasi kikubwa kabisa. Mwalimu kang'atuka miaka 25 iliyopita hao waliomfuata akina Mwinyi, Mkapa na Kikwete kipi kilichowashinda kunyanyua maisha ya Watanzania walio wengi ukilinganisha na ilivyokuwa wakati wa Mwalimu!? Kwa mara nyingine tena uamuzi wa Mwalimu wa kumtoa nduli ndani ya mipaka yetu uliungwa mkono na Watanzania walio wengi kabisa na si kweli kwamba vita ile ndiyo chanzo cvha umaskini wa nchi yetu.

Na kwa taarifa yako Tanzania si nchi maskini, tumejaaliwa rasilimali chungu nzima kama Almasi, Dhahabu, Uranium n.k. Tuna viongozi wabovu wanaosaini mikataba ambayo haina maslahi kabisa na nchi yetu hili ndilo tatizo letu kubwa na pia utawala wa sheria hakuna kabisa watu wataiba mabilioni lakini kwa sababu walitoa mabilioni ya mchango kwenye kampeni za mkuu basi wanakuwa hawaguswi kabisa na mkono wa sheria.
 
Back
Top Bottom