Elections 2010 Nani kateua mhuni kampeni za CCM?

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Nani kateua mhuni kampeni za CCM?

Na Anthony Mayunga

Mtendaji Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba ametetea chama chake, kwamba hakihusiki na tukio la kufukuzwa kwa waandishi wa habari, wiki tatu zilizopita mjini Bukoba.

Alisema, “CCM ni chama makini, hakiwezi kufukuza waandiushi wa habari.”

Makamba alikuwa akijibu tuhuma kwamba chama chake kilishiriki katika kufukuza waandishi wawili wa habari wa magazeti ya Mwananchi na The Citizen.

Katika kutetea chama chake, Makamba alisema, “Ili uamuzi wa chama chake uwe wa chama, ni lazima ufikiwe na Kamati Kuu (CC), Halamashauri KUU ya Taifa (CCM-NEC), au aufanye katibu mkuu. Vikao hivi havikufanyika kokote na mimi katibu mkuu sijaagiza mtu awafukuze waandishi.”

Aliongeza, “Fuatilia vizuri habari yako, ni lazima utagundua kuwa yupo mhuni amekosana nao akawafukuza.”

Makamba hataki kumtaja huyo anayemwita mhuni ambaye ameongozana na mgombea wa chama cgake. Wala hataki kujadili hatua ambazo chama makini kitamchukulia mhuni anayetajwa kufukuza waandishi wa habari.

Aidha, Makamba hataki kueleza ulimwengu, kwa nini chama chake kimeteua mhuni na kumwingiza katika msafara wa mgombea urais.

Hataki kujadili kwa nini yeye na chama chake wameshindwa kumwondoa mhuni huyo. Hataki kueleza kwa nini chama kinachoelekea Ikulu kimebeba wahuni.

Ni kwa sababu, alichokisema Makamba sicho anachokiamini. Makamba anajua kuwa uhuni si sifa nzuri. Anayeitwa mhuni hafai kukaa na watu makini; hawezi kuruhusiwa kufanya kazi zao wala hawezi kuwasemea.

Kama afisa wa habari wa mgombea wa urais ni mhuni, habari zinazotoka zitawezaje kuaminika? Je, nani anaweza kuziamini? Kwa vigezo vipi?

Ni muhimu hili likafahamika. Kama mhuni yupo katika msafara wa mgombea urais, tena ambaye yuko madarakani, wahuni wengine wangapi wamejazana Ikulu? Akibahatika kushinda uchaguzi, atauynda serikali gani na iliyolenga kundi gani?

Je, mgombea ambaye amekusanya wahuni katika timu yake ya kampeni, atawezaje kuaminisha wananchi, kwamba serikali atakayounda haitajaa wahuni?

Kauli ya Makamba ni tata kwa ujumla wake na ina tafsiri nyingi kwa watu; maana haiwezewkani chama makini kinachoongoza serikali kuchukuwa mhuni na kumlipa fedha ili kuratibu waandishi wa habari.

Mtu aliyemtaja Makamba kwamba ni mhuni bado anaendelea na kazi yake. Anaendelea kufukuza waandishi. Amekabidhiwa fuko la fedha ambazo zimechangwa na wanachama.

Bila shaka Makamba anajua maana ya mhuni; ni kapera, mseja, mpora wake za watu, asiye na makzi maalum, mwizi, kibaka, mvunjaji wa sheria, mnyang’anyi, mchopozi na ambaye anaishi kihuni.

Kutokana na hali hiyo, Makamba anataka kuwaambia wanachama wake, kwamba amekosa watu makini wa kufanya kazi ya kuratibu vyombo vya habari. Ndiyo sababu amelazimika kuchukua mhuni kufanya kazi hiyo.

Vinginevyo, Makamba anataka kutuambia kuwa CCM yote imejaa “manyani” – wanaoweza kuruka pamoja….

Chanzo: Mwanahalisi, toleo la sasa.
 
Nani kateua mhuni kampeni za CCM?

Na Anthony Mayunga

Mtendaji Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba ametetea chama chake, kwamba hakihusiki na tukio la kufukuzwa kwa waandishi wa habari, wiki tatu zilizopita mjini Bukoba.

Alisema, "CCM ni chama makini, hakiwezi kufukuza waandiushi wa habari."

Makamba alikuwa akijibu tuhuma kwamba chama chake kilishiriki katika kufukuza waandishi wawili wa habari wa magazeti ya Mwananchi na The Citizen.

Katika kutetea chama chake, Makamba alisema, "Ili uamuzi wa chama chake uwe wa chama, ni lazima ufikiwe na Kamati Kuu (CC), Halamashauri KUU ya Taifa (CCM-NEC), au aufanye katibu mkuu. Vikao hivi havikufanyika kokote na mimi katibu mkuu sijaagiza mtu awafukuze waandishi."

Aliongeza, "Fuatilia vizuri habari yako, ni lazima utagundua kuwa yupo mhuni amekosana nao akawafukuza."

Makamba hataki kumtaja huyo anayemwita mhuni ambaye ameongozana na mgombea wa chama cgake. Wala hataki kujadili hatua ambazo chama makini kitamchukulia mhuni anayetajwa kufukuza waandishi wa habari.

Aidha, Makamba hataki kueleza ulimwengu, kwa nini chama chake kimeteua mhuni na kumwingiza katika msafara wa mgombea urais.

Hataki kujadili kwa nini yeye na chama chake wameshindwa kumwondoa mhuni huyo. Hataki kueleza kwa nini chama kinachoelekea Ikulu kimebeba wahuni.

Ni kwa sababu, alichokisema Makamba sicho anachokiamini. Makamba anajua kuwa uhuni si sifa nzuri. Anayeitwa mhuni hafai kukaa na watu makini; hawezi kuruhusiwa kufanya kazi zao wala hawezi kuwasemea.

Kama afisa wa habari wa mgombea wa urais ni mhuni, habari zinazotoka zitawezaje kuaminika? Je, nani anaweza kuziamini? Kwa vigezo vipi?

Ni muhimu hili likafahamika. Kama mhuni yupo katika msafara wa mgombea urais, tena ambaye yuko madarakani, wahuni wengine wangapi wamejazana Ikulu? Akibahatika kushinda uchaguzi, atauynda serikali gani na iliyolenga kundi gani?

Je, mgombea ambaye amekusanya wahuni katika timu yake ya kampeni, atawezaje kuaminisha wananchi, kwamba serikali atakayounda haitajaa wahuni?

Kauli ya Makamba ni tata kwa ujumla wake na ina tafsiri nyingi kwa watu; maana haiwezewkani chama makini kinachoongoza serikali kuchukuwa mhuni na kumlipa fedha ili kuratibu waandishi wa habari.

Mtu aliyemtaja Makamba kwamba ni mhuni bado anaendelea na kazi yake. Anaendelea kufukuza waandishi. Amekabidhiwa fuko la fedha ambazo zimechangwa na wanachama.

Bila shaka Makamba anajua maana ya mhuni; ni kapera, mseja, mpora wake za watu, asiye na makzi maalum, mwizi, kibaka, mvunjaji wa sheria, mnyang'anyi, mchopozi na ambaye anaishi kihuni.

Kutokana na hali hiyo, Makamba anataka kuwaambia wanachama wake, kwamba amekosa watu makini wa kufanya kazi ya kuratibu vyombo vya habari. Ndiyo sababu amelazimika kuchukua mhuni kufanya kazi hiyo.

Vinginevyo, Makamba anataka kutuambia kuwa CCM yote imejaa "manyani" – wanaoweza kuruka pamoja….

Chanzo: Mwanahalisi, toleo la sasa.



Huyo anayetajwa na Makamba kuwa ni mhuni si mwingine bali ni Muhingo Rweyemamu, Mlamba Viatu No. 1 wa Rostam Aziz (wa pili ni Balile na wa tatu ni Manyerere), mtetezi miubwa wa mafisadi, na pia ni Managing Editor (Mhariri Mkuu (sic)) wa magazeti yanayomilikiwa na RA.

Kazi hii ya Managing Editor amejitahidi kuifanya kwa kiwango ambacho amefanikiwa kuyabadili magazeti hayo kwa kuuzwa kwa kilo siku ya pili tu baada ya kuchapishwa, badala ya kuuza moja moja kwenye vibanda vya magazeti (newsstands).

Ni mwandishi ambaye ana matatizo makubwa ya maadili ya uandishi: Mwaka 2005 alipokuwa Mwananchi, alifukuzwa kwa kosa la kughushi picha ya Dr Salim na kuiweka kwenye gazeti ili kumdhalilisha mbele ya wananchi.

Hata hivyo pamoja na tukio hilo, alipewa kazi hiyo hiyo anayo sasa ya kuratibu waandishi katika kampeni za JK za mwaka huo.

Mtu anayemjua vizuri, hashangai kwa nini yeye ni mratibu wa waandishi katika msafara wa kampeni za JK – aliteuliwa na RA. JK mwenyewe, Makamba, Kinana etc hawakushirikishwa na sababu kubwa ni kwamba RA ndiye anayekiendesha chama hicho (na serikali pia) – hivyo his word is God's word! Hakuna kati ya wakubwa hao anayeweza kusema fyoko na kumpinga.

Hapo New Habari anajulikana kwa vitisho kwa waandishi wa habari wa kike ambao huajiriwa pale – kwa kuwataka afanye nao ngono tena bila ya kondom, ama sivyo huwatisha kuwafukuza kazi. Hii habari inajulikana sana pale na imesababisha waandishi wa kike wengi kuacha kazi kwa kumkataa, au yeye kuwafukuza kazi.

Malalamiko haya yalifika kwa Mwandishi mmoja mkongwe, Balinagwe Mwambungu ambaye aliteuliwa kama "Ombudsman" – yaani ofisa anayepokea na kushughulikia malalmiko kutoka kwa wasomaji na waandishi pia. Mwambungu alilifikisha suala hili kwa RA mwenyewe ingawa hakuna hatua yoyote aliyeichukua hadi sasa.

Hakika Makamba hakukosea kusema kwamba mtu huyo ni Mhuni, isipokuwa alichoshindwa kusema ni tu kwamba uteuzi wake ulilazimishwa na RA.



 
Huyu ni yule yule Muhingo Rweyemamu ambaye alitumwa na RA kwenda kwenye Mkutano Mkuu wa CUF mwaka jana ambako alitoa maneno ya kuiponda sana CCM -- kwamba viongozi wake (CCM) hawana kazi nyingine isipokuwa kugombana tu wenyewe kwa wenyewe.
 
Huyo mjamaa ni zero kabisa, kiuandishi na ki-maadili. hana maana yoyote kabisa!!!
 
Huyo anayetajwa na Makamba kuwa ni mhuni si mwingine bali ni Muhingo Rweyemamu, Mlamba Viatu No. 1 wa Rostam Aziz (wa pili ni Balile na wa tatu ni Manyerere), mtetezi miubwa wa mafisadi, na pia ni Managing Editor (Mhariri Mkuu (sic)) wa magazeti yanayomilikiwa na RA.

Kazi hii ya Managing Editor amejitahidi kuifanya kwa kiwango ambacho amefanikiwa kuyabadili magazeti hayo kwa kuuzwa kwa kilo siku ya pili tu baada ya kuchapishwa, badala ya kuuza moja moja kwenye vibanda vya magazeti (newsstands).

Ni mwandishi ambaye ana matatizo makubwa ya maadili ya uandishi: Mwaka 2005 alipokuwa Mwananchi, alifukuzwa kwa kosa la kughushi picha ya Dr Salim na kuiweka kwenye gazeti ili kumdhalilisha mbele ya wananchi.

Hata hivyo pamoja na tukio hilo, alipewa kazi hiyo hiyo anayo sasa ya kuratibu waandishi katika kampeni za JK za mwaka huo.

Mtu anayemjua vizuri, hashangai kwa nini yeye ni mratibu wa waandishi katika msafara wa kampeni za JK – aliteuliwa na RA. JK mwenyewe, Makamba, Kinana etc hawakushirikishwa na sababu kubwa ni kwamba RA ndiye anayekiendesha chama hicho (na serikali pia) – hivyo his word is God's word! Hakuna kati ya wakubwa hao anayeweza kusema fyoko na kumpinga.

Hapo New Habari anajulikana kwa vitisho kwa waandishi wa habari wa kike ambao huajiriwa pale – kwa kuwataka afanye nao ngono tena bila ya kondom, ama sivyo huwatisha kuwafukuza kazi. Hii habari inajulikana sana pale na imesababisha waandishi wa kike wengi kuacha kazi kwa kumkataa, au yeye kuwafukuza kazi.

Malalamiko haya yalifika kwa Mwandishi mmoja mkongwe, Balinagwe Mwambungu ambaye aliteuliwa kama "Ombudsman" – yaani ofisa anayepokea na kushughulikia malalmiko kutoka kwa wasomaji na waandishi pia. Mwambungu alilifikisha suala hili kwa RA mwenyewe ingawa hakuna hatua yoyote aliyeichukua hadi sasa.

Hakika Makamba hakukosea kusema kwamba mtu huyo ni Mhuni, isipokuwa alichoshindwa kusema ni tu kwamba uteuzi wake ulilazimishwa na RA.





Kwenye red: Umenikumbusha mabo ya New habari. Bootlicker mwingine alikuwa boniface Makene -- huyu aligombana na Muhingo na kamtimua. Lakini pia pale kulikuwako wanahabari makini ambao hawakutaka kulamba viatu vya huyo mdosi na katika kutunza heshima zao na maadili ya uandishi waliamua kujiondokea. Hawa ni Rosemary Mwakitwange, aliyekuwa CEO, ASttilio tagalile (aliyemtangulia Muhingo kama Mhariri Mkuu, Eric Anthony Mkuti, aliyekuwa Mhariri wa gazeti la Mtanzania Jumapili, Ray Naluyaga, mwandishi wa habari makini ambaye sasa yuko Mwananchi na ni mmojawapo aliyefukuzwa na huyo Muhingo kwenye msafara wa JK, na Hilal Sued, aliyekuwa Mhariri wa The Weekend African. Simeon Ileta aliyekuwa Mhariri wa The African alikatishwa mkataba wake kwani Muhingo alimhisi kuwa ni pandikizi la Mengi.
 
Back
Top Bottom