Nani huyu Angellah Jasmine Kairuki

Status
Not open for further replies.
Mkuu swali kwamba ana watoto wangapi na umri wake una relevance gani kwa kazi yake ya Unaibu Waziri? La maana hapa la kufahamu ni elimu yake. Kwa mujibu wa tovuti ya Bunge mheshimiwa huyu ni Mwanasheria, ni Wakili wa Mahakama Kuu, na kabla ya uteuzi wake alikuwa ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala.

Ukiachilia mbali michango yake mingi Bungeni inayohusu utetezi wa haki na maslahi ya wafanyakazi (malipo ya pensheni ya wafanyakazi wa Tazara, waalimu waliosimamishwa Chuo cha Ustawi wa Jamii, wafanyakazi wazalendo wa migodini wanaolipwa kipato tofauti na wageni kule Barick) mheshimiwa huyu aliongoza debate ya maoni ya wadau kuhusu muswada wa sheria ya Katiba kule Dodoma....pale ndipo alipo display skills za hali ya juu,kwa ku accomodate mawazo ya pande zote pasipo ushabiki.

Mpaka anateuliwa nafasi ya naibu Waziri wa Katiba na Sheria, alikuwa ni Katibu Mkuu wa Tanzania Women Parliamentarian Group (TWPG) inayojumuisha wabunge wanawake kutoka vyama vyote, pia alikuwa Mmoja wa wawakilishi wa Bunge la Tanzania katika Interparliamentarian Union (IPU) ambapo alichaguliwa na taasisi hiyo kuwa Mjumbe wa Kamati ya Haki za Binadamu.


- CV nzito nilidhani ni ya Rais mpya wa Ufaransa maana zinafanana fanana eti, saafi sana Waziri anakuwa kwenye kiwango cha elimu yake, sasa muacheni dada yetu afanye kazi ya taifa.


William.
 
Bachelor of Laws (LLB Hons) University of Hull, UK; Pgd in Legal Practise-Stafordshire University; Level 3 Certificate in French Language-university of Nantes,France

Professional qualifications: Commissioner for Oath and High Court advocate, Anti-money laundering (AML) specialist, Certificate in Legislative Drafting-Ghana Law school, Certificate in Altenative Dispute Resulution and Arbitration-UNiTAR, Certificate of Labour Law-Tanzania Labour College-mbeya, Qualified Arbitrator-


Pia mwaka jana alikuwa miomgoni mwa vijana wachache katika jumuiya ya Afrika ya Mashariki waliochaguliwa kushiki kwenye Programu ya Leadership for Change in Africa.....details zaidi zipo hapa Home - Team Web Site


 
Ni mtoto wa aliyekuwa bodigadi wa Mama Mkkapa ambaye kwasasa kapewa ulaji (Ester Mkwizu)
 
- CV nzito nilidhani ni ya Rais mpya wa Ufaransa maana zinafanana fanana eti, saafi sana Waziri anakuwa kwenye kiwango cha elimu yake, sasa muacheni dada yetu afanye kazi ya taifa.
William.
Mbona Ma CV kama haya CCM siyo tatizo? yapo mengi Lakini yote yamegeuka kutumika kwaajili ya wizi wa mali za umma Chenge ana CV nzito lakini bonge la fisadi halafu bungeni hana mchango lakini Mnyika ana Elimu ya wastani yenye ufanisi wa hali ya juu ha! ha! ha!
 
Ni kweli ni mdada mwenye uwezo mkubwa na vipaji lukuki.

Lakini ni kweli pia kuwa ni mtoto wa Esther Mkwizu aliyekuwa mshauri wa Rais Ben wa mambo ya uchumi. Kama sikosei bado ni mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation. Kwahiyo anatoka kwenye familia iliyojikita kwenye system.

Ukiacha hilo ni mke wa msaidizi mkuu wa rais Ndugu Mberwa Kairuki ambaye amekuwa msaidizi wake tangu foreign.

Nionavyo mimi ni kuwa pamoja na advantage zote hizo bado Angela ni mtu mwenye uwezo na anastahili hapo alipo!
 
Mkuu swali kwamba ana watoto wangapi na umri wake una relevance gani kwa kazi yake ya Unaibu Waziri? La maana hapa la kufahamu ni elimu yake. Kwa mujibu wa tovuti ya Bunge mheshimiwa huyu ni Mwanasheria, ni Wakili wa Mahakama Kuu, na kabla ya uteuzi wake alikuwa ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala.

Ukiachilia mbali michango yake mingi Bungeni inayohusu utetezi wa haki na maslahi ya wafanyakazi (malipo ya pensheni ya wafanyakazi wa Tazara, waalimu waliosimamishwa Chuo cha Ustawi wa Jamii, wafanyakazi wazalendo wa migodini wanaolipwa kipato tofauti na wageni kule Barick) mheshimiwa huyu aliongoza debate ya maoni ya wadau kuhusu muswada wa sheria ya Katiba kule Dodoma....pale ndipo alipo display skills za hali ya juu,kwa ku accomodate mawazo ya pande zote pasipo ushabiki.

Mpaka anateuliwa nafasi ya naibu Waziri wa Katiba na Sheria, alikuwa ni Katibu Mkuu wa Tanzania Women Parliamentarian Group (TWPG) inayojumuisha wabunge wanawake kutoka vyama vyote, pia alikuwa Mmoja wa wawakilishi wa Bunge la Tanzania katika Interparliamentarian Union (IPU) ambapo alichaguliwa na taasisi hiyo kuwa Mjumbe wa Kamati ya Haki za Binadamu.
good explanation
 
Ana elimu na uzoefu wa kutosha. Tatizo ni chama chake! Ukipata uongozi wa aina yeyote kupitia ccm, ubongo unaruka, akili zinakutoka, na ujajikuta na akili alizozungumzia Msaburi!
 
Naona JK kampatia uwaziri Angela Kairuki kutokana na zile ziara za mwaka jana za Kamati ya Wabunge kwenda UK kudai pesa za rada zirudishwe hazina, ambapo hatimaye walifanikiwa. Kwa mtazamo wangu, Angela Kairuki alionekana akizungumza kwa machungu makubwa na hasira wakati akiweka wazi msimamo wa Serikali mbele ya Wabunge wa UK kwenye taswira na video zilizotolewa wakati huo

Hivi huyu mdada ni chotara, na ana wasifu gani kwa maana ya umri, elimu, marital status, na kadhalika?

Mkuu katika hoja hii nilielewa kuwa unahoja unataka kuitoa, sasa ilikuwa vigumu kufanya hivyo bila taarifa za ziada kama ulivyozihitaji. Kwa kuwa sasa umezipata za kutosha hata za ziada kuliko mahitaji yako tunaomba sasa wasilisha hoja yako mezani. AU imepotea ghafla?
 
Ni kweli ni mdada mwenye uwezo mkubwa na vipaji lukuki.

Lakini ni kweli pia kuwa ni mtoto wa Esther Mkwizu aliyekuwa mshauri wa Rais Ben wa mambo ya uchumi. Kama sikosei bado ni mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation. Kwahiyo anatoka kwenye familia iliyojikita kwenye system.

Ukiacha hilo ni mke wa msaidizi mkuu wa rais Ndugu Mberwa Kairuki ambaye amekuwa msaidizi wake tangu foreign.

Nionavyo mimi ni kuwa pamoja na advantage zote hizo bado Angela ni mtu mwenye uwezo na anastahili hapo alipo!

Mbelwa Kairuki ni mume wa Angella Kairuki. Mbelwa Kairuki amekuchua nafasi ya January Makamba Ikulu ya mwandishi wa habari wa Rais ni mtoto wa mwisho wa Marehemu Prof Herbet Kairuki mwenye Mikocheni Hospital. Kwa taaluma Mbelwa naye ni mwanasheria kutoka chuo kimoja Uingereza. Nafikiri walikutana na Angella masomoni UK.

Angella ana uwezo mkubwa tusubiri kupima utendaji wake ingawa kweli amekulia kwenye system ambayo hatuwezi kupuuza kwamba imemsaidia kumbeba.
 
Ni mtoto wa aliyekuwa bodigadi wa Mama Mkkapa ambaye kwasasa kapewa ulaji (Ester Mkwizu)

Pwitoooo,

Tufanye ulikuwa unatania tu. Mama Mkwizu hajawahi kuwa bodyguard wa Mama Mkapa, Mama huyu sio mwepesi kiivyo. Alikuwa Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya EOTF. Isitoshe kama ni kuhusu kuteuliwa kwake kwenye Tume ya Katiba utapenda kufahamu tu Mama huyo ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Private Sector Foundation. Is unajua kuwa Rais aliomba taasisi zipeleke majina ya wanaopendekezwa kwenye Tume?TPSF ndio waliompendekeza, au usingependa Sekta Binafsi iwakilishwe kwenye Tume?
 
cv imetulia tunamuombea kila la kheri katika utendaji wake na MUNGU amsaidie,pia amesoma Kilakala sekondari
 



Bachelor of Laws (LLB Hons) University of Hull, UK; Pgd in Legal Practise-Stafordshire University; Level 3 Certificate in French Language-university of Nantes,France

Professional qualifications: Commissioner for Oath and High Court advocate, Anti-money laundering (AML) specialist, Certificate in Legislative Drafting-Ghana Law school, Certificate in Altenative Dispute Resulution and Arbitration-UNiTAR, Certificate of Labour Law-Tanzania Labour College-mbeya, Qualified Arbitrator-


Pia mwaka jana alikuwa miomgoni mwa vijana wachache katika jumuiya ya Afrika ya Mashariki waliochaguliwa kushiki kwenye Programu ya Leadership for Change in Africa.....details zaidi zipo hapa Home - Team Web Site



- Duh! jamani imetossha sasa maana this is simply overqualified, sasa tuwe objective na openminded kama watu tulioenda shule somo kama hili tunatakiwa tulinganishe, hebu huko upande wa pili leteni CV ya Mwenyekiti ili tukate mzizi wa fitina, ni maoni yangu tu! ha! ha! ha!


William.
 
Ana wasifu mzuri ambao kwa serikali zinazotumia potentials huyo atatusaidia kusogeza mambo,issue ni je sisiem huwa wanajua kutumuia vipaji kwa manufaa yetu?.genius wetu mzee Balali wa BOT alitufikisha wapi..?kwa serikali yetu ni vigumu sana kuweka matarajio makubwa katika aspect yoyote manake waweza kufa kwa stress......!ukistaajabu ya musa...
 
- Duh! jamani imetossha sasa maana this is simply overqualified, sasa tuwe objective na openminded kama watu tulioenda shule somo kama hili tunatakiwa tulinganishe, hebu huko upande wa pili leteni CV ya Mwenyekiti ili tukate mzizi wa fitina, ni maoni yangu tu! ha! ha! ha!


William.

ndiyo maana ulikosa ubunge wa africa mashariki
 
Mkuu katika hoja hii nilielewa kuwa unahoja unataka kuitoa, sasa ilikuwa vigumu kufanya hivyo bila taarifa za ziada kama ulivyozihitaji. Kwa kuwa sasa umezipata za kutosha hata za ziada kuliko mahitaji yako tunaomba sasa wasilisha hoja yako mezani. AU imepotea ghafla?

Well, more power to Angellah. Lakini pamoja na elimu yake yote, kwa kiasi fulani amebebwa na connections zake za kifamilia kupitia mamake na mumewe kama Wachangiaji wengine walivyogusia hapo juu. Huo ndiyo ukweli uliojidhihirisha, na umuhimu wa thread niliyoanzisha haukuwa haba. Wengi tumefahamu tuliyokuwa hatuyajui.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom