Habari wana JF!
Sorry, kuna kitu kinanisumbua kidogo. Nimejaribu kufuatilia safari za jk kwa ajili ya kampeni sijaona tofauti yeyote kimuundo na kigharama kati ya safari za kawaida anapokuwa rais na hizi za sasa anaposafiri kwa ajili ya kampeni kama mwenyekiti na mgombea wa urais kwa ticketi ya ccm. Mfano ni safari ya Mwanza ambayo picha zinaonyesha ni ndege ya serikali ilitumika, swali ni nani alilipa gharama za hiyo ndege kwenda Mwanza na gharama zinginezo kwa ajili ya kampeni za ccm? Je ni kodi zetu watanzania kwa maana ya wana CUF, CHADEMA, TLP au wanachama wa chama chochote na hata wale wasio na vyama zinatumika kumnadi mgombea wa ccm?
Mtu yeyote mwenye akili timamu atakubaliana na mimi kwamba hakuna hata safari moja ya kampeni yenye manufaa kwa Taifa, safari zote ziko meant kuomba ridhaa ya watanzania kuendelea "kuitawala" nchi hii. Nionavyo mimi ni makosa kwa kodi za watanzania kutumika kwenye kampeni za chama chochote kile iwe ccm au chama kingine chochote. Nina mifano ya nchi kadhaa Africa, Ghana ni miongoni mwao ambao wamefanikiwa kutofautisha kampeni na shughuli zingine za rais. Kwa Ghana kwa mfano, endapo waziri anateuliwa kugombea urais anatakiwa kuresign kwenye nafasi kama waziri ili aweze kushiriki kwenye kampeni. So ni kitu kinachowezekana kama tukiamua. Hapa kwetu sivyo, jk aliendelea kuwa waziri mwaka 2005 pamoja na kwamba hakufanya kazi kwa zaidi ya miezi miwili kwa ajili ya kampeni. Wajuvi kwenye hili naomba mnisaidie, inanikera tena sana kwa kodi yangu kutumika visivyo kwenye kampeni ya kupeana tshirts ili hali tumboni nina njaa ya siku mbili an mm si mwanachama wa chama chochote kile nchini.
Sorry, kuna kitu kinanisumbua kidogo. Nimejaribu kufuatilia safari za jk kwa ajili ya kampeni sijaona tofauti yeyote kimuundo na kigharama kati ya safari za kawaida anapokuwa rais na hizi za sasa anaposafiri kwa ajili ya kampeni kama mwenyekiti na mgombea wa urais kwa ticketi ya ccm. Mfano ni safari ya Mwanza ambayo picha zinaonyesha ni ndege ya serikali ilitumika, swali ni nani alilipa gharama za hiyo ndege kwenda Mwanza na gharama zinginezo kwa ajili ya kampeni za ccm? Je ni kodi zetu watanzania kwa maana ya wana CUF, CHADEMA, TLP au wanachama wa chama chochote na hata wale wasio na vyama zinatumika kumnadi mgombea wa ccm?
Mtu yeyote mwenye akili timamu atakubaliana na mimi kwamba hakuna hata safari moja ya kampeni yenye manufaa kwa Taifa, safari zote ziko meant kuomba ridhaa ya watanzania kuendelea "kuitawala" nchi hii. Nionavyo mimi ni makosa kwa kodi za watanzania kutumika kwenye kampeni za chama chochote kile iwe ccm au chama kingine chochote. Nina mifano ya nchi kadhaa Africa, Ghana ni miongoni mwao ambao wamefanikiwa kutofautisha kampeni na shughuli zingine za rais. Kwa Ghana kwa mfano, endapo waziri anateuliwa kugombea urais anatakiwa kuresign kwenye nafasi kama waziri ili aweze kushiriki kwenye kampeni. So ni kitu kinachowezekana kama tukiamua. Hapa kwetu sivyo, jk aliendelea kuwa waziri mwaka 2005 pamoja na kwamba hakufanya kazi kwa zaidi ya miezi miwili kwa ajili ya kampeni. Wajuvi kwenye hili naomba mnisaidie, inanikera tena sana kwa kodi yangu kutumika visivyo kwenye kampeni ya kupeana tshirts ili hali tumboni nina njaa ya siku mbili an mm si mwanachama wa chama chochote kile nchini.