- Thread starter
- #21
Bobby pole kwa maumivu ila ni jambo la kawaida kuumia pale unapoona jambo la kuumiza tena hasa mahali ambapo huna maelezo ya kutosha.Ni vizuri pia umeomba kujuzwa katika jukwaa hili.Safari afanyazo JK katika kampeni zake zimeandaliwa na chama chake katika kitu ambacho kila chama kinacho,namaanisha "mkakati wa kampeni na ushindi".Ndani ya hili kuna fundraising,kuna savings (kumbuka CCM imekuwepo toka 1977,kwa taasisi kuwa na akiba si jambo la ajabu),michango ya wanachama na mapato toka miradi ya chama.Hivi vyote vinakipa chama nguvu ya kusonga mbele kikampeni.Katika nchi kama Ghana,labda tu nikukumbushe kwamba hata waziri wa serikali anaporesign bado anabaki kuwa former member of cabinet.Kama mtu wa aina hii alifanya kazi vizuri,uwezekano wa kupata support ya umma kifedha na kimkakati hadi kupata ushindi ni mkubwa.Kupata vyema ninalosema jaribu kufikiri bila kadi ya chama mfukoni,it will affect ur judgement.
Mungu Ibariki Tanzania.
Nos, sikuomba theory niliomba practical answers. Umenisikitisha, umenisononesha na umenifadhaisha kwa kiasi kisicho na mfano. Umetoa majibu ya kitoto as if unaongea na mtoto wa nursery. Siamini kwamba unaamini hayo uliyosema kitheory mimi siyajuwi. Hivi unayo taarifa kwamba billboards zote za ccm zimelipwa kwa kodi zetu? Swali lilikuwa nani anauthibitisho kwamba kwa mfano ndege anayoitumia mwenyeketi wa ccm sasa kwa kampeni ambayo ndio hiyo hiyo huwa anaitumia kwa safari za kiserikali kwa sasa inalipiwa na ccm na si ikulu? Ninahitaji pia mtu aje na uthibitisho kwamba posho za safari ikiwemo yake mwenyewe rais na ujumbe wake wote (mind you size ya msafara na aina ya watu ni wale wale anaowatumia siku zote) zinalipiwa na ccm na si kutoka ikulu inayoendeshwa kwa kodi za watanzania wote? Nahitaji uthibitisho sihitaji kuambiwa vile ambavyo inapaswa kuwa kwani ninafahamu hayo yote already. Next time Nos, sitahitaji theories kwenye maswali practical.