Just a person
JF-Expert Member
- May 16, 2022
- 964
- 1,187
Nitulie sasa
Pole mkuu achana nao, tusonge mbele tupe uhondoHaya mambo yakuchokozwa na kutukanwa na baadhi ya members humu halafu mimi nikimjibu nakula BAN sidhani kama imekaa sawa.Haiwezekani mtu anatoka huko anakokujua yeye anaanza kuniporomoshea matusi mazito halafu nimuangalie tu!.
Bado sijafikia kiwango hicho cha Utakatifu,kama ni nginja acha iwe nginja.
Wengine hatujaumbwa kuwa watukanaji,mimi nipo kuwaburudisha na kuwaelimisha hadhira yangu na umma wa watanzania wengi wanaojitambua,sasa anatokea mtu anaanza kukuporomoshea matusi ya nguoni kisa tu alikuja Inbox akaomba jambo fulani ukamnyima,ukimjibu kidogo tu anapelekea na wewe kufungiwa,hii siyo sawa moderators,wengine mnatuonea bila sababu ya msingi.
Kama nyuzi zangu zinakupa kero na huzipendi kwanini usipite ukatazame nyuzi zinazokufurahisha?,Kila mtu hapa anasoma anachoona kwake kina manufaa na anachokipenda,kama unaona hutaki usumbufu una-Block au Una - Ignore unaendelea na mishe zako,waachieni watu wanaotaka kujifunza na kuburudika wasome nyuzi zangu.
Hadhira yangu kwa muda wa siku zisizopungua 5 imeshindwa kupata simulizi nzuri na yenye mafunzo kwasababu tu ya watu fulani wajinga ambao hawataki kuniheshimu na kuanza kuniporomoshea matusi mazito,mimi kuwajibu imekuwa nongwa,hili halikubaliki hata kidogo moderators!.
Kuna muda tunachokozwa na kupandishwa hasira na wajinga kadhaa humu JF,sasa ajabu ni kwamba,mtu anapokutukana mara ya kwanza unamripoti hakuna hatua anayochukuliwa,mara ya pili pia ni vivyo hivyo,akikutukana mara ya tatu uzalendo unakushinda unamjibu,ukisha mjibu tu hapo ndipo Moderators wanakuja kuwaadhibu,wanashindwa kumuadhibu toka awali ulipomripoti wao wanakuja kumuadhibu ulipomjibu ambapo wanawaadhibu wote wanashindwa kumuadhibu mtoa matusi au muanzilishi wa matusi,hili halikubariki na nitaendelea kulipigia kelele.
Nimewahi kutoa mapendekezo kwenye uzi wangu mmoja uko kwenye Jukwaa la COMPLAINTS, APPRECIATION AND ADVICE(TO JF) nikasema tuwekeeni Blocking Button yenye nguvu na siyo hiyo Ignore iliyopo sasa,kwasababu kama nikishaona mtu ananitukana nitampiga Block ili aende akawatukane wazazi wake huko kwasababu wao ndiyo walimfundisha ujinga huo.
Aisee nimesikitishwa sana kupigwa BAN kwakosa ambalo limesabishwa na moja ya wapumbavu hapa JF.Wengine tunakiuka taratibu kwasababu ya kuchokozwa na siyo kwamba taratibu hatuzijui!.
Mimi ni mwema na nitaendelea kuwa mwema ila nikitukanwa lazima nijibu mapigo,kama ni kufungiwa nitafungiwa sana na nipo tayari kwa hilo!.
NIMESHINDWA KUSIMULIA STORI KWA SABABU YA WAJINGA KADHAA HAPA JF,HILI HALIKUBALIKI HATA KIDOGO NA NAUMIA SANA.
Huu ni ujumbe wenu Moderators najua uzi huu mnaupitia.
Ni hayo tu.
Achana nae huyo mkuu mim nimekuamini ulipotaja majina ya pepo zinazopatikana ziwa Tanganyika.Mkuu hili nalo kabisa unaandika uko serious!
Hapo si unaona tu ni typing error
📌📌Pole mkuu UMUGHAKA story hii inaonekana ni nzuri kuliko zote ulizowahi kuleta. HAO WANAOKUJIBU ACHANA NAO USI-COMMENT KITU WEWE WEKA UZI JUU YA UZI WAPUUZE NA SISI TUNAWAPUUZA, TUSONGE MBELE. Jitahidi sana usiwajibu wala usisome comments wewe chapa mwendo tu.
Ungekufa tu mkuu maana si kwa akili hizo za kukubali kubali kila ujingaBaada ya kuona hali inakuwa mbaya,kuna jamaa ambao walikuwa na mizigo yao kwenye ile boti walianza kuvua nguo wakabaki na kaptura pekee kisha wakaanza kupiga kelele ya kwamba wanaume wote tuingie chini tukasaidie kutoa maji kwa nguvu zote kupitia ndoo zilizokuwa huko kwasababu ile mashine iliilemewa.
Kwa hyo na wewe unaamini jamaa n bodabodaTuendelee master, baadae tuuze riwaya tuachane na bodaboda
Itakuwa Hanson choice au K vantMwezi wa pili tumezika jamaa angu alienda congo DR kutafuta utajiri inasemekana alipewa dawa Kali ilioathiri utumbo na maini