BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 423
- 1,050
Bora niseme na jamii ijue kinachoendelea, taarifa ni kuwa kuna taarifa za watu kuuawa kwa sumu katika Kijiji cha Nakatuba, Wilaya ya Bunda Mkoa wa Mara.
Pia kuna matukio yameshamiri yakihusisha imani za kishirikina na kuuana katika kijiji hicho hadi kusababisha baadhi ya vijana kukimbia na kuhama kabisa hapo kijijini.
Mbali na hapo kuna baadhi ya familia zimekimbia kwa maana ya kuhama wakihofia kuuliwa kwa sumu pamoja na imani za kishirikina.
Kwa ufupi Kijiji cha Nakatuba imekuwa ni kama eneo la kuzika ndugu zetu na kuondoka, nimetoka hapo katika hicho kijiji leo hii na ninajua ninachokizungumza.
Natoa wito kwa Serikali na Jeshi la Polisi na vyombo vinbine vya Ulinzi na Usalama kufanya jambo, la sivyo hali inaelekea kuwa mbaya.
Pia kuna matukio yameshamiri yakihusisha imani za kishirikina na kuuana katika kijiji hicho hadi kusababisha baadhi ya vijana kukimbia na kuhama kabisa hapo kijijini.
Mbali na hapo kuna baadhi ya familia zimekimbia kwa maana ya kuhama wakihofia kuuliwa kwa sumu pamoja na imani za kishirikina.
Kwa ufupi Kijiji cha Nakatuba imekuwa ni kama eneo la kuzika ndugu zetu na kuondoka, nimetoka hapo katika hicho kijiji leo hii na ninajua ninachokizungumza.
Natoa wito kwa Serikali na Jeshi la Polisi na vyombo vinbine vya Ulinzi na Usalama kufanya jambo, la sivyo hali inaelekea kuwa mbaya.