Najuta kulipandia........

next time kabla hujapanda gari,angalia cc zake.Usikute mafuta uliweka lita 1 ili hali gari ina cc4700,aina hiyo ya magari yanaendeshwa na wakubwa tu.Usilaumu gari bana,rudi kwenye bajaji ,mafuta uliweka kidogo hayo yana wenyewe.
 
Yaani balaa ile iliyonikuta kweli ningepata nguvu ya kukodisha lingine, mmh na hata kukodisha lingine sidhani kama ni good idea

hahahahhahahahah lol
daahh haya bwana nilidhani utaniruka
mmhh

haya pole
kwa nini usitafute lingine
au kodisha mmmhh

maana kila mahali hili unalijutia
 
Hili gari mafuta lilikuwa linavujisha lenyewe, haya bana nitapanda bajaji maans injini yake pis kiduuchu

next time kabla hujapanda gari,angalia cc zake.Usikute mafuta uliweka lita 1 ili hali gari ina cc4700,aina hiyo ya magari yanaendeshwa na wakubwa tu.Usilaumu gari bana,rudi kwenye bajaji ,mafuta uliweka kidogo hayo yana wenyewe.
 
Yaani balaa ile iliyonikuta kweli ningepata nguvu ya kukodisha lingine, mmh na hata kukodisha lingine sidhani kama ni good idea

embu nidokeze kidogo
akili imechoka sana leo
hapa tunaongelea toyota haswa
au ni reverse physiology..
 
Hahaha AD bana, hebu rudia tena kusoma......... Umeniacha hoi, reverse physiology

dahhh
itabidi nikaukumbatie
mto wangu kwanza mmhh
ni recharge hii battery halafu ntarudi.

Nisije kujibu majibu amaboyo hayajachujika
vizuri akilini..
 
Mwenzenu nilitamani, gari kulisafiria
Laonyesha la thamani, kwa nje na ndani pia
Kiumbo li wastani, mfano wa gari KIA
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Gari hili lavutia, kwa hilo nakubalia
Rangi yake kahawia, machoni imetulia
Wengi wanaliwazia, na sifa kulisifia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Kilitazama kwa mbele, pembeni limetanuka
Utapatwa na vipele, mwilini kusisimka
Natetemekwa vidole, nikipanda sita shuka
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Kwa nyuma linapendeza, napenda wake mbinuko
Na mwendo likiongeza, lapepea kama puto
Ni kweli sijalikweza, gari hili moto moto
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Muda nilipo patia, gari hili nilipanda
Tena nikashikilia, katikati nikatanda
Kelele nilisikia, ila gari halikwenda
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Gari lilikakamaa, lilishindwa nifikisha
Pale nilipo tazama, mafuta linavujisha
Si kama nalisakama, mashineni kulitisha
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Nimebaki na majuto, gari limekinaisha
Sina tena ule moto, wa gari kulipaisha
Mwili bado umzito, bora nisinge liwasha
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Bora kupanda bajaji, popote wajipitia
Hazina mwingi mtaji, injini ni ndogo pia
Beteri ukisha chaji, wajitambia na njia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

KLORO na SPRINI, mwaonaje hii hoja
SHOSI naye WAKIJIJI, mchango wenu nangoja
MAGULU uko kundini, LIZZY pia tupamoja
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Na wote nisowataja, msiache kuchangia
Nipeni nyingi faraja, hoja sitapuuzia
Safari niloipanga, katu haikutimia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia


Malenga wenu

Sindano ya ganzi (Local anaesthesia)

i guess the car should be recalled as it seems to have manufacturer's defects!
 
Ukiweka nia utaweza, mimi nilikuwa napenda sana mashairi lkn sikuwahi kuandika shairi hata siku moja, like 3 weeks ago klorokwini alitoa shairi from me to u, and that was my turning point nilijaribu kuandika beti chache, magulumangu nae akaja kutoa shairi dear mama, nae pia nilijaribu kumjibu, suddenly nimejikuta so much in love na haya mashairi, everything has happened in a space of 3 weeks

Mashairi yamekua yananivutia siku zinavyozidi kwenda....mmmh
nikazane kujifunza...
 
Mwenzenu nilitamani, gari kulisafiria
Laonyesha la thamani, kwa nje na ndani pia
Kiumbo li wastani, mfano wa gari KIA
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Gari hili lavutia, kwa hilo nakubalia
Rangi yake kahawia, machoni imetulia
Wengi wanaliwazia, na sifa kulisifia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Kilitazama kwa mbele, pembeni limetanuka
Utapatwa na vipele, mwilini kusisimka
Natetemekwa vidole, nikipanda sita shuka
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Kwa nyuma linapendeza, napenda wake mbinuko
Na mwendo likiongeza, lapepea kama puto
Ni kweli sijalikweza, gari hili moto moto
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Muda nilipo patia, gari hili nilipanda
Tena nikashikilia, katikati nikatanda
Kelele nilisikia, ila gari halikwenda
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Gari lilikakamaa, lilishindwa nifikisha
Pale nilipo tazama, mafuta linavujisha
Si kama nalisakama, mashineni kulitisha
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Nimebaki na majuto, gari limekinaisha
Sina tena ule moto, wa gari kulipaisha
Mwili bado umzito, bora nisinge liwasha
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Bora kupanda bajaji, popote wajipitia
Hazina mwingi mtaji, injini ni ndogo pia
Beteri ukisha chaji, wajitambia na njia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

KLORO
na SPRINI, mwaonaje hii hoja
SHOSI naye WAKIJIJI, mchango wenu nangoja
MAGULU uko kundini, LIZZY pia tupamoja
Gari hili gari gani, najuta kulipandia

Na wote nisowataja, msiache kuchangia
Nipeni nyingi faraja, hoja sitapuuzia
Safari niloipanga, katu haikutimia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia


Malenga wenu

Sindano ya ganzi (Local anaesthesia)

Khaaaa! magari mabovu bana!

Pole kwa hili janga, dereva yakuonea
Hiki kweli ni kisanga, kilichokuelemea
Heri hukula mzinga, njiani na abiria
Gari lipige mnada , halifai nakwambia

Magari ya siku hizi, rangi yanametameta
Nje jina Mitsubishi, injini yake toyota
Mengine nayo ya wizi, Polisi wayatafuta
Gari lipige mnada, halifai nakwambia.

Gari ukilichagua, ni vyema uwe makini
Mengine yasuasua, mithili mkokoteni
Kuna yanayocheuwa, katikati safarini
Gari lipige mnada, halifai nakwambia.

Raha ya gari ujue, ni dhamana ya safari
Utakapo ikutue , hii ndio yake siri
Maji ndio yapungue, hii wala si dosari
Gari lipige mnada, halifai nakwambia

Gari bovu lasumbua, heri wende kwa miguu
Mimi fundi nayajua, ya manjano na buluu
Gamba bora ungevua, katafute brand nyuu
Gari lipige mnada, halifai nakwambia


Hongera sindano ya ganzi.....aiseee mistari yako imetulia sana............ keep it up!
 
Wow...Yakuonea naona umechukua fani nzima nzima!!
Zaidi ya hapo sichangii maana mimi sio mtaalamu wa magari!
 
you are the reason behind this, shairi lako 'from me to you' was my turning point, much respect


Vipi nipige mnada, kwa gari lisilo langu
Nilitaka tu kupanda, linifikishe mwenzangu
Kwa miguu sitakwenda, sitaki kizungu zungu
Gari hili sio langu, siwezi piga mnada

vipi ningelijulia, kama ni gari makini
Waweza nisaidia, mwenzio sikubaini
Mafuta livujishiwa, sikuiona injini
Gari hili sio langu, siwezi piga mnada

Khaaaa! magari mabovu bana!

Pole kwa hili janga, dereva yakuonea
Hiki kweli ni kisanga, kilichokuelemea
Heri hukula mzinga, njiani na abiria
Gari lipige mnada , halifai nakwambia

Magari ya siku hizi, rangi yanametameta
Nje jina Mitsubishi, injini yake toyota
Mengine nayo ya wizi, Polisi wayatafuta
Gari lipige mnada, halifai nakwambia.

Gari ukilichagua, ni vyema uwe makini
Mengine yasuasua, mithili mkokoteni
Kuna yanayocheuwa, katikati safarini
Gari lipige mnada, halifai nakwambia.

Raha ya gari ujue, ni dhamana ya safari
Utakapo ikutue , hii ndio yake siri
Maji ndio yapungue, hii wala si dosari
Gari lipige mnada, halifai nakwambia

Gari bovu lasumbua, heri wende kwa miguu
Mimi fundi nayajua, ya manjano na buluu
Gamba bora ungevua, katafute brand nyuu
Gari lipige mnada, halifai nakwambia


Hongera sindano ya ganzi.....aiseee mistari yako imetulia sana............ keep it up!
 
Back
Top Bottom