Mkuu umechukua gari la mwaka 47 lazima lishindwe kukufikisha au ulipewa bure!!!
hahahahhahahahah lol
daahh haya bwana nilidhani utaniruka
mmhh
haya pole
kwa nini usitafute lingine
au kodisha mmmhh
maana kila mahali hili unalijutia
next time kabla hujapanda gari,angalia cc zake.Usikute mafuta uliweka lita 1 ili hali gari ina cc4700,aina hiyo ya magari yanaendeshwa na wakubwa tu.Usilaumu gari bana,rudi kwenye bajaji ,mafuta uliweka kidogo hayo yana wenyewe.
Yaani balaa ile iliyonikuta kweli ningepata nguvu ya kukodisha lingine, mmh na hata kukodisha lingine sidhani kama ni good idea
embu nidokeze kidogo
akili imechoka sana leo
hapa tunaongelea toyota haswa
au ni reverse physiology..
Hahaha AD bana, hebu rudia tena kusoma......... Umeniacha hoi, reverse physiology
Mwenzenu nilitamani, gari kulisafiria
Laonyesha la thamani, kwa nje na ndani pia
Kiumbo li wastani, mfano wa gari KIA
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Gari hili lavutia, kwa hilo nakubalia
Rangi yake kahawia, machoni imetulia
Wengi wanaliwazia, na sifa kulisifia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Kilitazama kwa mbele, pembeni limetanuka
Utapatwa na vipele, mwilini kusisimka
Natetemekwa vidole, nikipanda sita shuka
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Kwa nyuma linapendeza, napenda wake mbinuko
Na mwendo likiongeza, lapepea kama puto
Ni kweli sijalikweza, gari hili moto moto
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Muda nilipo patia, gari hili nilipanda
Tena nikashikilia, katikati nikatanda
Kelele nilisikia, ila gari halikwenda
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Gari lilikakamaa, lilishindwa nifikisha
Pale nilipo tazama, mafuta linavujisha
Si kama nalisakama, mashineni kulitisha
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Nimebaki na majuto, gari limekinaisha
Sina tena ule moto, wa gari kulipaisha
Mwili bado umzito, bora nisinge liwasha
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Bora kupanda bajaji, popote wajipitia
Hazina mwingi mtaji, injini ni ndogo pia
Beteri ukisha chaji, wajitambia na njia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
KLORO na SPRINI, mwaonaje hii hoja
SHOSI naye WAKIJIJI, mchango wenu nangoja
MAGULU uko kundini, LIZZY pia tupamoja
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Na wote nisowataja, msiache kuchangia
Nipeni nyingi faraja, hoja sitapuuzia
Safari niloipanga, katu haikutimia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Malenga wenu
Sindano ya ganzi (Local anaesthesia)
dahhh
itabidi nikaukumbatie
mto wangu kwanza mmhh
ni recharge hii battery halafu ntarudi.
Nisije kujibu majibu amaboyo hayajachujika
vizuri akilini..
Mashairi yamekua yananivutia siku zinavyozidi kwenda....mmmh
nikazane kujifunza...
i guess the car should be recalled as it seems to have manufacturer's defects!
Mwenzenu nilitamani, gari kulisafiria
Laonyesha la thamani, kwa nje na ndani pia
Kiumbo li wastani, mfano wa gari KIA
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Gari hili lavutia, kwa hilo nakubalia
Rangi yake kahawia, machoni imetulia
Wengi wanaliwazia, na sifa kulisifia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Kilitazama kwa mbele, pembeni limetanuka
Utapatwa na vipele, mwilini kusisimka
Natetemekwa vidole, nikipanda sita shuka
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Kwa nyuma linapendeza, napenda wake mbinuko
Na mwendo likiongeza, lapepea kama puto
Ni kweli sijalikweza, gari hili moto moto
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Muda nilipo patia, gari hili nilipanda
Tena nikashikilia, katikati nikatanda
Kelele nilisikia, ila gari halikwenda
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Gari lilikakamaa, lilishindwa nifikisha
Pale nilipo tazama, mafuta linavujisha
Si kama nalisakama, mashineni kulitisha
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Nimebaki na majuto, gari limekinaisha
Sina tena ule moto, wa gari kulipaisha
Mwili bado umzito, bora nisinge liwasha
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Bora kupanda bajaji, popote wajipitia
Hazina mwingi mtaji, injini ni ndogo pia
Beteri ukisha chaji, wajitambia na njia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
KLORO na SPRINI, mwaonaje hii hoja
SHOSI naye WAKIJIJI, mchango wenu nangoja
MAGULU uko kundini, LIZZY pia tupamoja
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Na wote nisowataja, msiache kuchangia
Nipeni nyingi faraja, hoja sitapuuzia
Safari niloipanga, katu haikutimia
Gari hili gari gani, najuta kulipandia
Malenga wenu
Sindano ya ganzi (Local anaesthesia)
Khaaaa! magari mabovu bana!
Pole kwa hili janga, dereva yakuonea
Hiki kweli ni kisanga, kilichokuelemea
Heri hukula mzinga, njiani na abiria
Gari lipige mnada , halifai nakwambia
Magari ya siku hizi, rangi yanametameta
Nje jina Mitsubishi, injini yake toyota
Mengine nayo ya wizi, Polisi wayatafuta
Gari lipige mnada, halifai nakwambia.
Gari ukilichagua, ni vyema uwe makini
Mengine yasuasua, mithili mkokoteni
Kuna yanayocheuwa, katikati safarini
Gari lipige mnada, halifai nakwambia.
Raha ya gari ujue, ni dhamana ya safari
Utakapo ikutue , hii ndio yake siri
Maji ndio yapungue, hii wala si dosari
Gari lipige mnada, halifai nakwambia
Gari bovu lasumbua, heri wende kwa miguu
Mimi fundi nayajua, ya manjano na buluu
Gamba bora ungevua, katafute brand nyuu
Gari lipige mnada, halifai nakwambia
Hongera sindano ya ganzi.....aiseee mistari yako imetulia sana............ keep it up!
Wow...Yakuonea naona umechukua fani nzima nzima!!
Zaidi ya hapo sichangii maana mimi sio mtaalamu wa magari!