Nahofia uhakika wa Takwimu Sensa Hii.Tufanye nini tuokoe Jahazi?

Nicholas

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
25,260
7,195
Duh.. katik pita pita yangu iliyonipitisha miji kama mitatu hivi nimeguja gundua kuwa watu hawapo tayari kwa sensa,pia nilibahatika scan kidogo mahiojiano ya ATN na raia mitaani.Hofu yangu ni kwamba hili si kwa waislam tuu ndugu zangu.Kweli kuna idadi kubwa ya waislam wasiokuwa tayari kufanya hivyo,ila pia kuna watu kutoelewa sana, na pia watu kutokuwa na nia kabisa.

Hofu yangu ni kwamba hata kama sheria ipo je itatekelezeka kama nusu ya nchi hawatashiriki?Watawekwa magereza yapi, na watashikwa na askari au hata migambo wangapi?Na watasafirishwa na magari yapi?Kuna uwezekano wakahesabiwa watu chini ta walioandikishwa katika kupiga kura katik uchaguzi uliopita, kama watazidi basi watazidi kwa idadi ya watoto wadogo na si watu wazima. katika pitapita yangu nimegundua kwanza watu hawajui umuhimu wa sensa na hivyo kutojianda kwa lolote.

Kati ya hao wasiojua wapo waliodanganyana kwa kuambiwa kuwa mafisadi wanataka watumie majina kujipatia hela toka kwa wafadhili.Wapo wengine wanahofu kwanini ianze usiku?na wanahofu kuwa na wezi wanaweza wagongea kwa style hiyohiyo.Wapo watu mjini kabisa wenye imani zao toka vijijini wanaamini kuhesabiwa ni vibaya kwani watakufa.Na kuna wengi wanalalamika kuwa kuhesabu pamoja na mifugo ni dharau, kwamba nao ni wanyama.Wengine wanasema kuwa mifugo yao inahesabiwa ili ije chukuliwa na serikali ya mafisadi... Hayo yote kwa msomi si vigezo sana ila in reality si yakuchezea.

Katika pita pita yangu ,nimegundua kuwa katika vigenge vyote hivyo vilikuwa vikiongozwa na watu wenye ushawishi na kuaminika katika circle zao ingawa nao ama si waelewa ama wanadhamiria.Na pengine palikuwa na wazee ambao wanawaangalia hawa jamaa kama waelewa na kukubalina nao kwani sehemu nyingine nimesikia wakichangia kwa kauli kama "mbona zamani hatukuhesabiwa na tuliishi", wengine wanasema "hii ni janja ya wazungu kutuua kwa vile CCM wanahongeka" na mengine mengi sana. Hofu yangu ni kwamba serikali haikufanya vizuri sana katik kujihakikishia hadi siku moja kabla watu zaidi ta 99% wapo tayari na wanafikika,ili watakaobaki kama wanaleta za kuletwa basi waadhibiwe huku data zao zikitolewa na mtu mwingine.

Serikali haikuwa na 2-ways channel ya kuwasiliana na wananchi na wananchi kuwasiliana na serikali. Kwa muda tuliofikia ni vigumu kubadili tarehe, na vigumu serikali kukaa na kurekebisha hali,ila NI RAHISI wananchi kuelimishana,kuhimizana kuhesabiwa na hata kukumbushana na kutoana hofu kuwa watoe majibu sahihi bila kudanganya.Kwani sensa siku hizi ni zaidi ya kuhesabu idadi. Pamoja na kuwa tunahimizana kushiriki na kutoa majibu sahihi bado serikali inabidi iwe flexible katika kupokea taarifa na kuzifanyia kazi haraka na kwa uwazi ili mwisho wa zoezi pasiwe na mashaka ya makosa makubwa.Wajaribu fanya namna ya kuwafikia watu wa jamii za wafugaji ambao huhama hama katika mapori nao wakipewa habari potofu kuwaona ni kukimbizana katikati ya wanyama pori,kitu kinachoweza washawishi makarani kuishia chini ya mti n akujiandia wajuavyo.

Hakuna muda wa kulaumu tena serikali ingawa hali ni very citical zaidi ya kila mtu kuwa mwalimu.Kwa wale wana campaign wa vyama hapa ndipo kwa kufanyia mazoezi ya 2015. Mungu Ibariki TZ, Mungu ibariki Africa.
 
Sensa sensa sensa kila kona,tunataka tujue gharama iliyotumika isije ikawa changa la macho kama ile miaka50 ya uhuru kumbe mradi wa watu kupata kujaza akount zao ili figure za account zao zisomeke Trillion maana kama majumba,magari,mashamba na kila anasa wanayo iliyobaki ni kupamba Account zao na tarakimu zisomekazo Trillion!
 
Hapo hujagusia suala zima la makarani kutowezeshwa ipasavyo/kwa viwango tofauti, watendaji wa serikali za mitaa kutofikiriwa kabisa licha ya majukumu mazito watakayobeba siku hiyo, upungufu wa vifaa etc
 
...Serikali itazipika namba na kila kitu kitakuwa shwari....na hizi takwimu zitakazopatikana zitawekwa kwenye mabakrasha na kupigwa na vumbi kwa miaka chungu nzima kama ilivyotokea katika takwimu zilizopatika katika miaka ya nyuma.

Hakuna lolote litakalofanyika kutumia takwimu hizo eti kuleta maendeleo kwa Watanzania. Hii Serikali ilivyo kigeugeu...miezi michache iliyopita iliwaambia madakatari na walimu kwamba haina uwezo wa kuwalipa mishahara na marupurupu mazuri ili kukidhi upandaji wa kutisha wa gharama za maisha...leo inageuka na kudai takwimu za sensa zitatumika eti kuleta maendeleo kwa Watanzania!! maendeleo ambayo yameshindwa kupatikana katika miaka 50 ya uhuru wa Tanzania!!! sijui huo uwezo wa kuleta maendeleo utapatikana kutoka wapi hasa ukitilia maanani Kikwete alishatamka "Serikali haina uwezo."
 
Hapa tusidanganyane, kama ni mwendo huu basi sensa 2012 imeshaharibika. na takwimu zitakazokuja hazitakuwa kamili. hivyo basi ni jukumu la serikali kujipanga upya na kuangalia wapi ilipojikwaa kisha kuja na sensa nyingine 2014.
 
Wewe Pia kwenye hiyo PITA PITA yako UNATULETEA HAPA ni DODOSO la KUENDELEZA hiyo STATUS-QUO; Haujatuelimisha

Chochote...

Tatizo lilianzia kwa serikali kuu wakati wa UCHAGUZI wa RAIS; Mheshimiwa Rais wakati wa Campaign zake kujitofautisha

Na chama kikuu cha Upinzani 2010 - CHADEMA; alitumia DINI kama karata ya kukidhalilisha CHADEMA kuwa sio CHAMA

kinachofaa kuongoza nchi; Wakati anakiongelea CHADEMA wakati huo alikuwa anamaanisha kuwa kilikuwa hakifanyi

Mikakati kama CCM kukaribisha Wananchi wa DINI mbalimbali hasa DINI ya KIISLAMU kugombea Madaraka ndani ya CHADEMA

hii ilizua MTAFAKURU mkubwa sana... MOJA ya CHADEMA kutokuwa na WAWAKILISHI Sehemu nyingine ni BAJETI na pia

Wawakilishi ilikuwa VIGUMU kuwapata wengine ilikuwa ni RAHISI kuhongwa na chama tawala CCM na kukimbia VITUO VYAO

na CCM iliwalima haswa CHADEMA... na UDINI CARD; iliwasaidia CCM kwenye MAENEO YA PWANI kupata KURA NYINGI...

WALAKINI... HAWAKUJUA KUWA KAMA WAKISHINDA WALITAKIWA KURUDI MAENEO HAYO NA KUHUBIRI AMANI NA UPENDO NA

KUWA HAKUNA KITU KAMA UDINI; RAISI JAKAY KIKWETE kama kawaida yake alipuuza SUALA hili kama anavyopuuza MAUALA

MUHIMU YANAYOIKABILI NCHI HII; NYERERE alisha sema KIONGOZI IMARA NI YULE ANAYEONA MBALI; na alisha sema

JAKAYA MRISHO KIKWETE SI KIONGOZI IMARA ANAYE ONA MBALI; HAKUJUA SENSA INAKUJA.... HAKUONA MBALI...

SENSA sio kufuatilia Mambo ya DINI hata kidogo sensa ni ya maendeleo; watu wangapi sasa wapo kwenye KATA au TARAFA au

WILAYA oh WANASTAHILI Hospitali, UMEME, Uwanja wa MPIRA, SHULE za MSINGI NGAPI, Secondary au Vyuo Vya Elimu au UFUNDI

na SIO Ma-Askofu au Ma-Sheikh inaangalia HEAD-COUNT... sio Idadi ya DINI...

Sasa Raisi Wetu kagonga chini... Hawezi hata kujaribu kulizungumzia sababu; hajui aanzie wapi; CCM - Taifa ni Dhaifu

Rais Wa NCHI hawezi kuishi Maisha ya Uwalakini...

Sasa Mwana HOJA; HII NDIO SABABU ya UDINI na sio Unachoongelea... ilianzia serikalini toka kwa Mheshimiwa Raisi

na aliwaamsha WAISLAMU ambao hawakuwa na MPANGO WOWOTE; na kuwapa kete... Sasa ndio hii inayotupata Sasa

NA TUSIPOANGALIA... ITAKUWA ndio MWANZO WA GENOCIDE... kama MTU MWENYE HEKIMA kama za Mwl. Nyerere hatatokea
 
Hapa tusidanganyane, kama ni mwendo huu basi sensa 2012 imeshaharibika. na takwimu zitakazokuja hazitakuwa kamili. hivyo basi ni jukumu la serikali kujipanga upya na kuangalia wapi ilipojikwaa kisha kuja na sensa nyingine 2014.

No sweat, ije tu, akina mwaalimu waendelee kupiga mpunga kwa kwenda mbele.
 
vyombo vya habari vinaendelea kuivuruga sensa. ishaurin serikali itatue mzozo na waislam kwanza na si kuchochea.
 
Habari zenu wadau,

Natoa masikitiko yangu juu ya hali inayojitokeza katika mfululizo mzima wa kuelekea kwenye zoezi muhimu sana kwa mustakabari wa nchi yetu,ninamini hakuna familia,ukoo na nchi kwa ujumla ambalo linaweza kupanga mambo ya kimaendeleo bila kujua idadi kamili ya watu wake.Kama sijakosea zoezi la sensa limewakuta maraisi wote wa awamu zote nne na sina kumbukumbu sahihi ambazo zinanieleza kuwa huko nyuma kuliwahi kujitokeza upinzani kama huu unaojitokeza hivi sasa.Kwa namna moja au nyingine naweza sema kuwa inatokana na kubadilika kwa fikra za watu ama utandawazi uliopo kipindi hiki tofauti na huko nyuma.Ngoja nijaribu kuviangalia vikwazo tulivyonavyo na jinsi gani serikali imechukua hatua.

1. KIPENGELE CHA DINI KTK DODOSO ZA SENSA.
Hili limeonikana kuwa jambo kubwa sana hasa Kwa watanzania wenye imani ya dini ya kiislam,hapa nawezasema kuwa ni suala dogo sana la utashi wa kisiasa ambao umesababisha huu mkanganyiko.Maandalizi ya sensa yalitakiwa yawepo muda mrefu ikiwa ni pamoja na kuiandaa jamii(dini zote) kifikra juu ya jambo hili.Serikali yetu haina dini ila imekuwa ikinadi siku zote kuwa inatambua kuwa watu wake wana dini na hii sensa inawahusu watu hivyo hakuna ambacho hakitakiwi kujulikana toka kwa hao watu na kama inavyosisitiza kuwa hizo taarifa ni siri.Kama ni kweli serikali haina aja na dini za wananchi wake basi ilitakiwa itoe amri ya kufuta kipengele cha dini ktk mambo yote yanayowahusu wananchi serikalini,ukiandikishwa shule ya msingi moja ya swali utakaloulizwa ni Dini yako ni ipi?,ukienda sekondali utaulizwa swali hili,chuo kikuu utaulizwa swali hili na mbaya zaidi ata unapoingia mikataba mbalimbali ya kazi iwe na serikali au sekta binafsi ili swali linakuwepo,iweje lionekane gumu kwenye zoezi la sensa?.Kama unahitaji kujua idadi ya walemavu,watoto,wazee,idadi ya nyumba ikiwemo makanisa na misikiti kwa nini ionekana ngumu kujua ni idadi gani ya watu wanayatumia hayo makanisa/misikiti?.Katika mitaa yetu kuna sehemu maalum za wazi kwa ajili ya mapumziko na michezo lakini kuna sehemu maalum kwa ajili ya kuabudu.Sehemu za ibada zilitakiwa ziwepo kulingana na uwiano wa watu katika sehemu husika na sio kurundika utitiri wa misikiti na makanisa katika sehemu ambayo haina uhitaji na kusababisha majengo hayo kugeuzwa sehemu za wahuni na kuleta kero ktk mtaa husika.Hivyo ktk hili serikali inapaswa kulaumiwa ama kwa kupuuza au kutosoma alama za nyakati ktk hili.

2.KUDAI NYAMA/MCHELE ILI KUHESABIWA.

Hapa suala ni lile lile la kuonyesha fikra kuwa hili zoezi ni la serilakali zaidi na sio la wananchi,kama wananchi wangeelimishwa vizuri mambo kama haya yasingetokea,lakini bado serikali inaendelea kuonyesha mtindo wake wa kufanya jambo kwa msukumo wa migomo na mambo mengine,watu wanasoma haya na kutafuta sehemu ya kutekelezewa mambo yao ambayo yalikuwa yanapuuzwa muda mrefu,kama mtu haoni msaada wowote wa serikali ktk maisha yake ya kila siku kwa maana yy hajawahi ata kumuona kiongozi yeyote wa serikali kwa nn aache shughuli zake kwa siku kadhaa eti kwa sababu serikali inataku kumuhesabu huku haoni faida yake?.Kutimiza dai hili ni udhaifu mwingine unaoonekana kwa serikali pia.

3.KUDAI MJUSI ALIYEPELEKWA UJERUMANI KWA UTAFITI KAMA SHARTI LA KUHESABIWA.

Hii ni changamoto iliyojitokeza mkoa wa Lindi na somo ambalo serikali inatakiwa kutokanalo hapa ni kutofanya siri mambo yanayowahusu wananchi,taarifa ni muhimu ktk kila hatua ya kila jambo linalohusiana na jamii.Ktk halmashauri kuna idara ya maliasili iliyotakiwa kuwa na taarifa sahihi ya hili jambo na moja kwa moja kutoa taarifa kwa wanachi ktk kila hatua inayofikia.Kukaa kimya kwa wananchi msichukulie kuwa hawayajui yale yanayoendelea ktk maeneo yao.Lkn hapa serikali ilipaswa kufurahia kuwa watu sasa wana uchungu na nchi yao na kufanya taratibu za kurudisha huyo mjusi nchini au kupeleka watanzania wakaone ni nn kinaendelea ktk uchunguzi huo.

4.DAI LA KUTOHESABIWA MPAKA WAKULIMA WA KOROSHO WALIPWE MALIPO YA BONUS.

Hii haina tofauti na wale jamaa zetu wa mjusi kwani taarifa na vikwazo vya kiutendaji vinatakiwa viwe open kwa kila hatua inayofikia ili kuepusha wanachi kutumia mambo muhimu yanayowahusu kama bakora ya kujichapia wenyewe.

5.MABALOZI WA NYUMBA KUDAI POSHO ILI WASIMAMIE ZOEZI LA SENSA.

Hili ni tatizo kuwa la kiutendaji ambalo serikali haipaswi kujitetea kama halikujua madhara yake.Wakati wa kufanya kazi kwa wito ulishapita zamani,mabalozi ni wanachi wanaofanya kazi za serikali bila malipo yoyote na huku wakijishughulisha na mambo yao ilikujipatia riziki yao ya halali.suala la kumwambia aache shughuli zake kwa kipindi fulani ili kusimamia zoezi ambalo lina watu maalumu ambao tayari wamesapewa mafunzo tofauti na wao ni uonevu.Ilitakiwa serikali ktk mpango wake wa kutoa ajiara ya muda na mafunzo ya sensa iwafikilie mabalozi wa sehemu husika ili kutoa hamasa kwa hawa viongozi wetu.

Kuna mengine madogo madogo ambayo nayo yanaingia ktk kudhoofisha zoezi hili ambayo serikali ama kwa kutojua ama ubinafsi wa watu wachache umeigharimu.Kuwaengua walimu walio wengi ktk zoezi hili wakati walipewa ahadi ya muda mrefu kuwa wao ndio watatumika kwa kiasi kikubwa kunaweza kuleta hujuma kwa watu hao.Hapa sababu inaonekana ni kutokana na wao kuingia ktk mgomo dhidi ya serikali ingawa serikali haitaki kukubaliana na hili.
Yangu ni hayo tu wadau na hii ni kwa mustakabari wa nchi yangu ila mwisho kabisa napenda kuwasihi makundi yote ya wanachi kuoondoa tofauti zetu na kushirki ktk zoezi hili muhimu kwetu kwa maendeleo yetu na nchi yetu.

MUNGU IBARIKI TANZANIA,MUNGU IBARIKI AFRIKA.

Nawasilisha.
 
Inanishangaza serekali ya ccm ikiwahadaa watanzania kwa kuwaambia kuwa wajitokeze kuhesabiwa ili waletewe maendeleo,,,,je,kwa muda wa miaka 50 mmeshindwa kumtoa mtanzania kwenye lindi la umasikini kwa kuwa hamjui idadi yao?,,nahitaji majibu
 
Vyombo vya habari ktk hili vimechemka ile mbaya. Yaani hamjaisaidia kabisa serikali. Wanausalama nao ndio ima walikusudia kwa makusudi sensa ifeli au waliifanya kazi kwa hisia za itikadi zao nakuwa influenced na misimamo ya makanisa na kuificha serikali ukweli. Sensa mpaka dakika hii imefeli kupita maelezo. Hii itakuwa nchi yakwanza duniani kushindwa zoezi la sensa.
 
Habari zenu wadau,

Natoa masikitiko yangu juu ya hali inayojitokeza katika mfululizo mzima wa kuelekea kwenye zoezi muhimu sana kwa mustakabari wa nchi yetu,ninamini hakuna familia,ukoo na nchi kwa ujumla ambalo linaweza kupanga mambo ya kimaendeleo bila kujua idadi kamili ya watu wake.Kama sijakosea zoezi la sensa limewakuta maraisi wote wa awamu zote nne na sina kumbukumbu sahihi ambazo zinanieleza kuwa huko nyuma kuliwahi kujitokeza upinzani kama huu unaojitokeza hivi sasa.Kwa namna moja au nyingine naweza sema kuwa inatokana na kubadilika kwa fikra za watu ama utandawazi uliopo kipindi hiki tofauti na huko nyuma.Ngoja nijaribu kuviangalia vikwazo tulivyonavyo na jinsi gani serikali imechukua hatua.

1. KIPENGELE CHA DINI KTK DODOSO ZA SENSA.
Hili limeonikana kuwa jambo kubwa sana hasa Kwa watanzania wenye imani ya dini ya kiislam,hapa nawezasema kuwa ni suala dogo sana la utashi wa kisiasa ambao umesababisha huu mkanganyiko.Maandalizi ya sensa yalitakiwa yawepo muda mrefu ikiwa ni pamoja na kuiandaa jamii(dini zote) kifikra juu ya jambo hili.Serikali yetu haina dini ila imekuwa ikinadi siku zote kuwa inatambua kuwa watu wake wana dini na hii sensa inawahusu watu hivyo hakuna ambacho hakitakiwi kujulikana toka kwa hao watu na kama inavyosisitiza kuwa hizo taarifa ni siri.Kama ni kweli serikali haina aja na dini za wananchi wake basi ilitakiwa itoe amri ya kufuta kipengele cha dini ktk mambo yote yanayowahusu wananchi serikalini,ukiandikishwa shule ya msingi moja ya swali utakaloulizwa ni Dini yako ni ipi?,ukienda sekondali utaulizwa swali hili,chuo kikuu utaulizwa swali hili na mbaya zaidi ata unapoingia mikataba mbalimbali ya kazi iwe na serikali au sekta binafsi ili swali linakuwepo,iweje lionekane gumu kwenye zoezi la sensa?.Kama unahitaji kujua idadi ya walemavu,watoto,wazee,idadi ya nyumba ikiwemo makanisa na misikiti kwa nini ionekana ngumu kujua ni idadi gani ya watu wanayatumia hayo makanisa/misikiti?.Katika mitaa yetu kuna sehemu maalum za wazi kwa ajili ya mapumziko na michezo lakini kuna sehemu maalum kwa ajili ya kuabudu.Sehemu za ibada zilitakiwa ziwepo kulingana na uwiano wa watu katika sehemu husika na sio kurundika utitiri wa misikiti na makanisa katika sehemu ambayo haina uhitaji na kusababisha majengo hayo kugeuzwa sehemu za wahuni na kuleta kero ktk mtaa husika.Hivyo ktk hili serikali inapaswa kulaumiwa ama kwa kupuuza au kutosoma alama za nyakati ktk hili.

2.KUDAI NYAMA/MCHELE ILI KUHESABIWA.

Hapa suala ni lile lile la kuonyesha fikra kuwa hili zoezi ni la serilakali zaidi na sio la wananchi,kama wananchi wangeelimishwa vizuri mambo kama haya yasingetokea,lakini bado serikali inaendelea kuonyesha mtindo wake wa kufanya jambo kwa msukumo wa migomo na mambo mengine,watu wanasoma haya na kutafuta sehemu ya kutekelezewa mambo yao ambayo yalikuwa yanapuuzwa muda mrefu,kama mtu haoni msaada wowote wa serikali ktk maisha yake ya kila siku kwa maana yy hajawahi ata kumuona kiongozi yeyote wa serikali kwa nn aache shughuli zake kwa siku kadhaa eti kwa sababu serikali inataku kumuhesabu huku haoni faida yake?.Kutimiza dai hili ni udhaifu mwingine unaoonekana kwa serikali pia.

3.KUDAI MJUSI ALIYEPELEKWA UJERUMANI KWA UTAFITI KAMA SHARTI LA KUHESABIWA.

Hii ni changamoto iliyojitokeza mkoa wa Lindi na somo ambalo serikali inatakiwa kutokanalo hapa ni kutofanya siri mambo yanayowahusu wananchi,taarifa ni muhimu ktk kila hatua ya kila jambo linalohusiana na jamii.Ktk halmashauri kuna idara ya maliasili iliyotakiwa kuwa na taarifa sahihi ya hili jambo na moja kwa moja kutoa taarifa kwa wanachi ktk kila hatua inayofikia.Kukaa kimya kwa wananchi msichukulie kuwa hawayajui yale yanayoendelea ktk maeneo yao.Lkn hapa serikali ilipaswa kufurahia kuwa watu sasa wana uchungu na nchi yao na kufanya taratibu za kurudisha huyo mjusi nchini au kupeleka watanzania wakaone ni nn kinaendelea ktk uchunguzi huo.

4.DAI LA KUTOHESABIWA MPAKA WAKULIMA WA KOROSHO WALIPWE MALIPO YA BONUS.

Hii haina tofauti na wale jamaa zetu wa mjusi kwani taarifa na vikwazo vya kiutendaji vinatakiwa viwe open kwa kila hatua inayofikia ili kuepusha wanachi kutumia mambo muhimu yanayowahusu kama bakora ya kujichapia wenyewe.

5.MABALOZI WA NYUMBA KUDAI POSHO ILI WASIMAMIE ZOEZI LA SENSA.

Hili ni tatizo kuwa la kiutendaji ambalo serikali haipaswi kujitetea kama halikujua madhara yake.Wakati wa kufanya kazi kwa wito ulishapita zamani,mabalozi ni wanachi wanaofanya kazi za serikali bila malipo yoyote na huku wakijishughulisha na mambo yao ilikujipatia riziki yao ya halali.suala la kumwambia aache shughuli zake kwa kipindi fulani ili kusimamia zoezi ambalo lina watu maalumu ambao tayari wamesapewa mafunzo tofauti na wao ni uonevu.Ilitakiwa serikali ktk mpango wake wa kutoa ajiara ya muda na mafunzo ya sensa iwafikilie mabalozi wa sehemu husika ili kutoa hamasa kwa hawa viongozi wetu.

Kuna mengine madogo madogo ambayo nayo yanaingia ktk kudhoofisha zoezi hili ambayo serikali ama kwa kutojua ama ubinafsi wa watu wachache umeigharimu.Kuwaengua walimu walio wengi ktk zoezi hili wakati walipewa ahadi ya muda mrefu kuwa wao ndio watatumika kwa kiasi kikubwa kunaweza kuleta hujuma kwa watu hao.Hapa sababu inaonekana ni kutokana na wao kuingia ktk mgomo dhidi ya serikali ingawa serikali haitaki kukubaliana na hili.
Yangu ni hayo tu wadau na hii ni kwa mustakabari wa nchi yangu ila mwisho kabisa napenda kuwasihi makundi yote ya wanachi kuoondoa tofauti zetu na kushirki ktk zoezi hili muhimu kwetu kwa maendeleo yetu na nchi yetu.

MUNGU IBARIKI TANZANIA,MUNGU IBARIKI AFRIKA.

Nawasilisha.

Yes kweli nimeona hilo, Sensa imeonekana kuwa ya serikali kuliko ya wananchi.Pia kutoaminika kwa CCM katika statistics.Kwanini hawakuyatumia haya yote kuelimisha watu?
 
Inanishangaza serekali ya ccm ikiwahadaa watanzania kwa kuwaambia kuwa wajitokeze kuhesabiwa ili waletewe maendeleo,,,,je,kwa muda wa miaka 50 mmeshindwa kumtoa mtanzania kwenye lindi la umasikini kwa kuwa hamjui idadi yao?,,nahitaji majibu

Hapo ndipo anaonyesha kuwa CCM haikuwa na moral authority ya kuendesha sensa.
 
...Serikali itazipika namba na kila kitu kitakuwa shwari....na hizi takwimu zitakazopatikana zitawekwa kwenye mabakrasha na kupigwa na vumbi kwa miaka chungu nzima kama ilivyotokea katika takwimu zilizopatika katika miaka ya nyuma.

Hakuna lolote litakalofanyika kutumia takwimu hizo eti kuleta maendeleo kwa Watanzania. Hii Serikali ilivyo kigeugeu...miezi michache iliyopita iliwaambia madakatari na walimu kwamba haina uwezo wa kuwalipa mishahara na marupurupu mazuri ili kukidhi upandaji wa kutisha wa gharama za maisha...leo inageuka na kudai takwimu za sensa zitatumika eti kuleta maendeleo kwa Watanzania!! maendeleo ambayo yameshindwa kupatikana katika miaka 50 ya uhuru wa Tanzania!!! sijui huo uwezo wa kuleta maendeleo utapatikana kutoka wapi hasa ukitilia maanani Kikwete alishatamka "Serikali haina uwezo."

Yeah...ila zingekuwa sahihi, basi hata watu wengine wangezitumia. Mfano makampuni yanaweza zitumia kujua mambo muhimu kuhusu soko wanalolilenga. Hii itaboost sector nyingi sana mbali na maendeleo ya serikali.Sasa tukipata sensa za kijinga kama idadi ya kura itolewayo na tume ya uchaguzi si vyema sana.Mbaya hata CCM hawajui usahihi wa sensa una umuhimu gani?Ndio maana wanhubiri kama vile wao ndio watazitumi kuletea nchi maendeleo na ndio maana haowaoni umuhimu huku ikizingatiwa CCM haina moral authority.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Sensa sensa sensa kila kona,tunataka tujue gharama iliyotumika isije ikawa changa la macho kama ile miaka50 ya uhuru kumbe mradi wa watu kupata kujaza akount zao ili figure za account zao zisomeke Trillion maana kama majumba,magari,mashamba na kila anasa wanayo iliyobaki ni kupamba Account zao na tarakimu zisomekazo Trillion!

...Serikali itazipika namba na kila kitu kitakuwa shwari....na hizi takwimu zitakazopatikana zitawekwa kwenye mabakrasha na kupigwa na vumbi kwa miaka chungu nzima kama ilivyotokea katika takwimu zilizopatika katika miaka ya nyuma.

Hakuna lolote litakalofanyika kutumia takwimu hizo eti kuleta maendeleo kwa Watanzania. Hii Serikali ilivyo kigeugeu...miezi michache iliyopita iliwaambia madakatari na walimu kwamba haina uwezo wa kuwalipa mishahara na marupurupu mazuri ili kukidhi upandaji wa kutisha wa gharama za maisha...leo inageuka na kudai takwimu za sensa zitatumika eti kuleta maendeleo kwa Watanzania!! maendeleo ambayo yameshindwa kupatikana katika miaka 50 ya uhuru wa Tanzania!!! sijui huo uwezo wa kuleta maendeleo utapatikana kutoka wapi hasa ukitilia maanani Kikwete alishatamka "Serikali haina uwezo."
Angalia coincidence ya mambo:
Mabilioni ya RADA
Mabilioni ya NDEGE YA RAISI
Mabilioni ya EPA
Mabilioni ya RICHMOND
Mabilioni ya KIKWETE
Mabilioni ya JKT
Mabilioni ya MIGODINI
Mabilioni ya benki za USWISI,bila ya kusahau
Mabilioni kwa mabilioni kwa matrilioni tusiyoyajua ya ufisadi katika mikataba feki na isiyozingatia faida kwa nchi bali 10% ambazo kikundi fulani inaingiza mfukoni.

Mabilioni yote hayo (matrilioni) ambayo tumeshudia yakibukanywa hivi hivi kama nchi haina wenyewe, kama kwamba nchi ni ya CCM peke yao na washirika wao (matajiri na wawekezaji).

Halafu serikali inakurupuka kitandani inawaambia wananchi washiriki katika Sensa, mbiu ikiwa SENSA KWA MAENDELEO. Bila ya kuona haya inasema serikali itatumia Bilioni 141 kwa Sensa ya Maendeleo. Hivi ni kuwadharau Watanzania na kuwafanyia mzaha - Tuacheni tupumue kidogo!

Binafsi sipingani na dhana ya sensa kwani ninaelewa umuhimu wake kwa maendeleo ya nchi, lakini napinga serikali kuendelea kutudanganya kama watoto wadogo. Sioni kama uamuzi wa kufanya sensa mwaka huu ulikuwa sahihi kutokana na hali mbaya ya kisiasa, kijamii na kiuchumi ya nchi.

Na ziadi, kama tutaangalia kumbukumbu, ambapo sensa baada ya uhuru zilifanyika miaka ya 1967, 1978, 1988, 2002, utaona kumbe inawezekana kuahirisha kufanya sensa na sio kila baada ya miaka 10 kama vile imeandikwa ndani ya Vitabu Vitakatifu. Serikali ingewez kuahirisha sensa miaka minne hadi 2016 au wakati wowote baada ya kutatua kero sugu za wafanyakazi wa kada zote. Ninachoona hapa ni kuwa serikali imekimbilia kufanya sensa ili "kuChukua Chao Mapema" kwa vile mwaka 2016 haina uhakika kama itakuwepo madarakani.

Pamoja na yote hayo niliyosema, mimi na familia yangu tayari tumeshahesabiwa, kwa hofu ya kuja kukosa maendeleo kumbe ni sisi wenyewe ndio tungeinyima serikali data za kutuletea maendeleo. SENSA OYEEE!
 
mammamia you are right...halafu makosa ya udini yameanza wa cost CCM,ila makosa ya sensa ndio yatawapeleka kaburini kabisa.Hawatakuwa na data sahihi za kuwasaidia kujipanga kwa 2015.
 
Kinondoni nao tayari kama kawa wamepiga panga hela za makarani.Kweli CCM wamelaaniwa.Kila kitu kinagoma.Anayway sisi tuhimizane kuhesabiwa, wao washindwe himiza makarani kuchukua data sahihi
 
Kweli kuna mushkeli kadhaa katika zoezi hili. Inaonekana uhamasishaji pia haukufanyika vya kutosha na pia tatizo la uhamasishaji unaofanyika haueleweki vizuri. Nadhani mambo yatakayoharibu hii sensa ni kama ifuatavyo:
1. Kuacha kutumia walimu na kuchuuwa watu holela na wengine kifisadi bila kuangalia qualification
2. Kutowaandaa viongozi wa mitaa na mabalozi ipasavyo
3. Kutowashirikisha vyama vya siasa katika maandalizi. Naamini serikali ingeshirikisha vyama kama CHADEMA na CUF tangu awali wangekuwa wakiwahamasisha wananchi wakati wa operesheni zao.
4. Kuendeshwa kwa programu muhimu kwa wakati mmoja. Wakati watu watu wakihamasishwa kushiriki ktk kutoa maoni ya katiba mpya, ghafla zoezi la vitambulisho vya taiofa vinaibuka tena bila kuandaa watu ipasavyo tena ghafla zoezi la sensa linaingia tena. Haya masuala yalitakiwa yapishanishwe. Mfano kwani baada ya kuona zoezi hili likiwa likisuasua wangeahirisha tu.
5. Maandalizi hafifu.
Pamoja na madhaifu hayo tuwasamehe tu wahusika na tushiriki kwa pamoja sensa. Maadamu itaendelea kwa wiki moja basi ni wakati wa kurekebisha mapungu yaliyojitokeza ili zoezi lifanikiwa.
 
Back
Top Bottom