Nahodha Kanunuliwa Na SMT?

Junius

JF-Expert Member
Mar 11, 2009
3,181
139
WAZIRI Kiongozi, Shamsi Vuai Nahodha amesema kwamba mjadala wa mafuta na gesi asilia hakuhitajiki jazba katika kufikia ufumbuzi wa suala hilo iwapo lipakie aktika orodha ya mambo ya muungano au liondolewe na kusimamiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Nahodha aliyasema hayo wakati akiakhirisha kikao cha Baraza la Wawakilishi jana, ambapo alisema jambo hilo linahitaji busara zaidi kuliko jabza.
Msimamo huo wa Waziri Kiongozi unaonekana kwenda kinyume na hoja nyingi za wajumbe wa baraza la wawakilishi ambao mara kwa mara wamekuwa wakisisitiza kwamba uamuzi wa kuliondoka suala hilo katika orodha ya mambo ya muungano halihitaji mjadala zaidi ya utekelezaji.
Tayari baraza la wawakilishi pamoja na baraza la mapinduzi limeamua kuliondoa suala hilo katika muungano, lakini maamuzi hayo yanaonekana kupingana na hutuba ya waziri kiongozi.
Nahodha alisema kamwe suala hilo halitaachwa kuweza kusababisha kuvuruga amani na utulivu uliopo ambao kwa muda mrefu serikali ya Tanzania iansifikana kwa kuwa na hali ya mani ya utulivu katika bara la afrika.
Waziri Kiongozi alisema suala hilo halitaweza kusababisha mgogoro kiasi ya kuigawa nchi na kwamba Serikali ipo makini kuona ufumbuzi wake unapatikana kwa njia za amani.
“Waheshimiwa Wajumbe, napenda kuwajulisheni kuwa katika kulipatia ufumbuzi suala la mafuta na gesi asilia tutatumia busara katika kufikia ufumbuzi…Serikali italisimamia hilo” Alisisitiza Nahodha.
Katika uamuzi wake baraza la wawakilishi lilisisitiza ni lazima serikali ya mapinduzi Zanzibar iwasilishe sera katika baraza hilo ya nishati na gesi asilia ikiwa ni mchakato wa kuunda shirika la maendeleo ya petroli Zanzibar.
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Baraza la Mapinduzi wameamua kuwa suala la mafuta na gesi asilia liondolewe kwenye orodha ya mambo ya Muungano.
Wawakilishi hao walisema kwamba uamuzi huo ni wa wananchi wote wa Zanzibar na kamwe si utashi wa mtu mmoja ambapo walisema ni busara kuyaondoa kwa maslahi ya kulinda na kudumisha Muungano.
Tangu kuanza kupatikana kwa gesi asilia Zanzibar imekuwa hainufaiki na mapato ya nishati hiyo licha ya suala hilo kuwa ni la Muungano na badala yake upande mmoja wa Tanzania Bara ndio umekuwa ukinufaika.
Katika uamuzi wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar (BLM) limetoa maamuzi matano juu ya suala la mafuta na gesi asilia sasa liondolewe katika orodha ya masuala yanayojadiliwa na Kamati ya kujadili kero za Muungano iliyo chini ya Makamu wa Rais.
Maamuzi hayo ambayo ni pamoja na masuala yote yanayohusiana na mafuta na gesi asilia yatolewe kwenye orodha ya Muungano, usimamizi na udhibiti wa rasilimali hiyo katika maeneo yote ya ardhi na baharini pamoja na eneo la ukanda maalum wa kiuchumi ubaki kuwa chini ya SMZ peke yake.
Uamuzi wa tatu wa BLM ni Wizara husika imeagizwa kuanisha katika sera ya udhibiti wa rasilimali ya mafuta na gesi asilia kwa maeneo ya Zanzibar kama ilivyoelezwa katika mapendekezo ya Baraza la Wawakilishi.
Uamuzi mwengine wa BLM ni kuwa Wizara husika iandae mikakati ya kutayarisha sheria ya mafuta na gesi asilia Zanzibar ambayo inafuatiwa na kuanzishwa kwa Taasisi zitakazosimamia sekta hiyo Visiwani hapa.
Uamuzi wa mwisho wa SMZ kuwa ni taarifa ya maamuzi ya SMZ yawasilishwe katika kikao kinachofuata cha kujadili kero za Muungano ambapo kwa sasa kazi inayofuata ni utekelezaji wa maelekezo ya Baraza la Mapinduzi ili kuhakikisha kuwa SMZ inasimamia na kudhibiti sekta ya mafuta na gesi asilia kwa maslahi ya Wazanzibari.



SOURCE: ZANZIBAR YETU BLOG.
 
Nahodha yeye ameapa kulinda sheria za Znz na kuitetea SMZ na kuhakikisha Muungano unadumu. Sasa anaona haya mambo anapelekea kuvunja muungano ndio maana anajikomba.


Aha siasa bwana lazima uwe ndumilakuwili
 
Hongera sana Nahodha, jazba kweli hazijengi! Tukae, tuzungumze ili hayo mafuta hewa yabaki kwa wenyewe! Wakija kugundua hayapo na Tanzania Bara ikagundua mafuta ndio wataanza kuwa wapole na kuomba Muungano udumu! Si unajua ile sera ya 'changu changu, chako changu'? Mungu ibariki JMT na Watu Wake!
 
Mhe. Nahodha hajanunuliwa. Kwa mujibu wa makubaliano ya hati ya muungano, upande mmoja wa muungano hauwezi kujibadilishia mambo ya muungano bila kushirikisha upande mwingine. Kama BMZ na SMZ wengekuwa na nia ya dhati ya kuondoa swala la mafuta na gesi kwenye mambo ya muungano, basi wangefuata utaratibu wa hoja na kuipeleka kwenye Bunge la Jamhuri. Pia jinsi hali ilivyo sasa hivi sidhani kama yupo kiongozi wa ngazi ya juu ambaye angependa yeye awe ndio chanzo cha kuhatarisha uvunjifu wa muungano.


sakauyek
 
Mhe. Nahodha hajanunuliwa. Kwa mujibu wa makubaliano ya hati ya muungano, upande mmoja wa muungano hauwezi kujibadilishia mambo ya muungano bila kushirikisha upande mwingine. Kama BMZ na SMZ wengekuwa na nia ya dhati ya kuondoa swala la mafuta na gesi kwenye mambo ya muungano, basi wangefuata utaratibu wa hoja na kuipeleka kwenye Bunge la Jamhuri. Pia jinsi hali ilivyo sasa hivi sidhani kama yupo kiongozi wa ngazi ya juu ambaye angependa yeye awe ndio chanzo cha kuhatarisha uvunjifu wa muungano.


sakauyek
Kwa mujibu wa mktaba huo huo wa muungano ni kuwa sheria yoyote itakayotungwa na bunge kwa madhumuni ya kutumika katika Jamhuri ya Muungano lazima, ikeshapitishwa na bunge, iridhiwe na BARAZA LA WAWAKILISHI(BUNGE LA ZANZIBAR, UKIPENDA USIPENDE), kama mafuta yameingizwa katika mambo ya muungano bila ya utaratibu huo kufanyika sheria hiyo inakuwa ni batili kutumika Zanzibar. Kwa taarifa yako tu, siyo masuala ya gesi tu, yapo mambo kadhaa yameingizwa bila ya Kuridhiwa na BLW kama mkataba wa muungano unavyosema, na hayo ndiyo Zanzibar wanayoyalalamikia kuwa yanawaumiza kwa maslahi ya wachache(upande mmoja) Utakumbuka karibuni tu imeelezwa sheria ya chombo cha kusimamia mawasiliano imepitishwa na bunge na inatumika bila kuridhiwana BLW, utakumbuka kataka sheria ya Tume ya Haki za Binaadamu(In Liue of Ombudsman) ilivyopigwa danadana kutumika visiwani kwa kuwa tu utaratibu huo haukufuatwa na BLW haijaridhia. Mafuta yalipoingizwa mwaka 1968, hakukuwa na chombo cha kutunga sheria Zanzibar wala BLM halijakaa kuridhia, hivyo hata kama Bunge limepitisha sheria hiyo au kipengele hicho kilichoingiza kina kuwa void ab initio(asili yake hakikuwapo) kwa kuwa nchi hizi hazikuungana kwa katiba bali mkataba, mkataba ndio utakaotazamwa bila shaka hata Mahakama ya kimataifa wanaanzia hapo.
 
Kwa mujibu wa mktaba huo huo wa muungano ni kuwa sheria yoyote itakayotungwa na bunge kwa madhumuni ya kutumika katika Jamhuri ya Muungano lazima, ikeshapitishwa na bunge, iridhiwe na BARAZA LA WAWAKILISHI(BUNGE LA ZANZIBAR, UKIPENDA USIPENDE), kama mafuta yameingizwa katika mambo ya muungano bila ya utaratibu huo kufanyika sheria hiyo inakuwa ni batili kutumika Zanzibar. Kwa taarifa yako tu, siyo masuala ya gesi tu, yapo mambo kadhaa yameingizwa bila ya Kuridhiwa na BLW kama mkataba wa muungano unavyosema, na hayo ndiyo Zanzibar wanayoyalalamikia kuwa yanawaumiza kwa maslahi ya wachache(upande mmoja) Utakumbuka karibuni tu imeelezwa sheria ya chombo cha kusimamia mawasiliano imepitishwa na bunge na inatumika bila kuridhiwana BLW, utakumbuka kataka sheria ya Tume ya Haki za Binaadamu(In Liue of Ombudsman) ilivyopigwa danadana kutumika visiwani kwa kuwa tu utaratibu huo haukufuatwa na BLW haijaridhia. Mafuta yalipoingizwa mwaka 1968, hakukuwa na chombo cha kutunga sheria Zanzibar wala BLM halijakaa kuridhia, hivyo hata kama Bunge limepitisha sheria hiyo au kipengele hicho kilichoingiza kina kuwa void ab initio(asili yake hakikuwapo) kwa kuwa nchi hizi hazikuungana kwa katiba bali mkataba, mkataba ndio utakaotazamwa bila shaka hata Mahakama ya kimataifa wanaanzia hapo.

Maneno sawia kabida.

Nakupa hongera kuweka wazi hilo kwani wengi haalijui na hata wakijua wanajifanya kusahau ili yao Yapite
 
Kwa mujibu wa mktaba huo huo wa muungano ni kuwa sheria yoyote itakayotungwa na bunge kwa madhumuni ya kutumika katika Jamhuri ya Muungano lazima, ikeshapitishwa na bunge, iridhiwe na BARAZA LA WAWAKILISHI(BUNGE LA ZANZIBAR, UKIPENDA USIPENDE), kama mafuta yameingizwa katika mambo ya muungano bila ya utaratibu huo kufanyika sheria hiyo inakuwa ni batili kutumika Zanzibar. Kwa taarifa yako tu, siyo masuala ya gesi tu, yapo mambo kadhaa yameingizwa bila ya Kuridhiwa na BLW kama mkataba wa muungano unavyosema, na hayo ndiyo Zanzibar wanayoyalalamikia kuwa yanawaumiza kwa maslahi ya wachache(upande mmoja) Utakumbuka karibuni tu imeelezwa sheria ya chombo cha kusimamia mawasiliano imepitishwa na bunge na inatumika bila kuridhiwana BLW, utakumbuka kataka sheria ya Tume ya Haki za Binaadamu(In Liue of Ombudsman) ilivyopigwa danadana kutumika visiwani kwa kuwa tu utaratibu huo haukufuatwa na BLW haijaridhia. Mafuta yalipoingizwa mwaka 1968, hakukuwa na chombo cha kutunga sheria Zanzibar wala BLM halijakaa kuridhia, hivyo hata kama Bunge limepitisha sheria hiyo au kipengele hicho kilichoingiza kina kuwa void ab initio(asili yake hakikuwapo) kwa kuwa nchi hizi hazikuungana kwa katiba bali mkataba, mkataba ndio utakaotazamwa bila shaka hata Mahakama ya kimataifa wanaanzia hapo.

Maneno sawia kabida.

Nakupa hongera kuweka wazi hilo kwani wengi haalijui na hata wakijua wanajifanya kusahau ili yao Yapite
 
Back
Top Bottom