black abdu
Senior Member
- Dec 2, 2022
- 152
- 208
Wanakamati, hadi muda huu ikiwa timu zote zinazoshiriki Kombe la Mapinduzi licha ya kupigiwa promo sana ni mechi mbili pekee zimejaza uwanja, Mechi iliyochezwa na Yanga na nyingine ni mechi ya jana iliyochezwa na Simba na JKU. Hii inatupa ujumbe gani?
Tutakubali kuwa Simba na Yanga zinabeba mpira wa Tanzania kwenye mashindano yote zinazoshiriki, ya ndani na nje. Azam na Singida Fountain Gate licha ya ukubwa wao mechi zao hazikuwa na watazamaji wengi, hata hii inayoendelea sasa ya Azam na Vitalo uwanja ni mtupu kabisa.
Mechi zinapigiwa Zenji na hata zimecheza timu za Zenji pia watazamaji walikuwa wachache.
Kuna msemaji mmoja wa Timu moja hupenda kujipachika kundini, lakini hebu sasa aone nafasi yao halisi kwenye vichwa na mioyo ya wapenzi wa Kandanda.
Tusiogope kuzipa maua yao Simba na Yanga na tuzitambue kama utambulisho wa mpira wa Tanzania. Yaani hata ile mtu ukiwa Morocco unaweza kujitambulisha kuwa unatoka Tanzania inakotoka Simba Sports Club!
Tutakubali kuwa Simba na Yanga zinabeba mpira wa Tanzania kwenye mashindano yote zinazoshiriki, ya ndani na nje. Azam na Singida Fountain Gate licha ya ukubwa wao mechi zao hazikuwa na watazamaji wengi, hata hii inayoendelea sasa ya Azam na Vitalo uwanja ni mtupu kabisa.
Mechi zinapigiwa Zenji na hata zimecheza timu za Zenji pia watazamaji walikuwa wachache.
Kuna msemaji mmoja wa Timu moja hupenda kujipachika kundini, lakini hebu sasa aone nafasi yao halisi kwenye vichwa na mioyo ya wapenzi wa Kandanda.
Tusiogope kuzipa maua yao Simba na Yanga na tuzitambue kama utambulisho wa mpira wa Tanzania. Yaani hata ile mtu ukiwa Morocco unaweza kujitambulisha kuwa unatoka Tanzania inakotoka Simba Sports Club!