Nadharia Tete: Bila Ujumbe NEC, Urais Haiwezekani

Wakuu mpaka sasa kuna vigezo vya kimaandishi vya nani anayetakiwa kuwa kiongozi katika ngazi mbalimbali za Chama na kuwa kiongozi wa ngazi mbalimbali za seriklai kwa tiketi ya chama. Na kuna vision na manifesto ya chama ambayo wanaogombea nafasi yoyote ile wanatakiwa kuwa na jukumu la kuitekeleza. Lakini kuna vigezo vingine ambavyo havipo kiimaandishi ndio vinaangaliwa na kuzingatiwa kabla ya kuruhusu mtu kupewa nafasi ya kuwa mgombea wa nafasi uongozi, inawezekana hivyo ndio vina nguvu zaidi kuliko vile vilivyoandikwa. It is a matter of having those unwritten qualities and mimick the written ones. So we have official criteria and real criteria, the official one ni ya kuwadanganya watu, na real one is the one which actually work .

Inasikitisha sana kuona kuwa kiongozi anasema wazi kuwa ana msimamo huu kuhusu jambo hili na ana mtazamo ule kuhusu jambo lile, lakini ukiangalia utendaji wake na vitendo vyake huwezi kuamini kinachofanyika. So the idea that we should judge them on their statements and views on policies, budget and how they will work around them is questionable. There is plenty of evidence that what they say and what they actually do, are two different things. Umetoa mfano mzuri sana wa "maisha bora kwa kila mtanzania", angalia nani alileta maisha bora kwa mtanzania, at least aliyejaribu. JK au BM?

Ni vizuri ku-strengthen institutions na kuwapima watu kwa walichofanya kutekeleza kile kilichoandikwa kwenye katiba ya chama, manifesto ya chama na katiba ya serikali na malengo ya kuiboresha Tanzania. Nadhani kuna haja ya kuwa na uniformity kwenye katioba za vyama vyote inapokuja kwenye mambo ya kugombea nafasi za urais. Sasa hivi techinically kuna uwezekano wa any party to win presidency, kwa hiyo ni vizuri kuwe na utaratibu wa kitaifa wa kuscreen wanaotaka kwenda kugombea urais.

NEC yenyewe (hata ya Chadema na vyama vingine) ukiangaza ndani yake unaweza kuona ni chombo chenye jina kubwa lakini kuna members ndani yake ambao are worse than you and me who are not in there. Pamoja na kuwa kweli katiba haisemi mgombea Urais awe mjumbe wa NEC, lakini huo ndio ukweli. Na kama ukiweza kurally support ndani ya NEC kwanza (kwa ulaghai au ukweli) unakuwa na nafasi nzuri kuteuliwa kuwa mgombea urais. Hiyo ni weakness kubwa sana ya real unwritten Constitution of CCM.

Naona kizuri ni kuimarisha miondo na taasisi iliziwe na nguvu zaidi ya kuwabana wanaogombea nafasi waweze kudeliver baada ya kuchaguliwa. sasa hakuna.

Nakubaliana na wewe. Hoja zako kuhusu utendaji wa kazi wa viongozi, sera, kauli mbiu n.k, zimeniacha na maswali kadhaa, kwa mfano, kwa mujibu wa katiba ya CCM, moja ya majukumu ya NEC ni: "Kuandaa Ilani ya CCM ya Uchaguzi na kutoa msukumo wa utekelezaji wa Ilani hiyo". Je, nini ni Key Performance Indicators ya Rais, Waziri Mkuu na Mawaziri? Ni utekelezaji wa ilani ya CCM? Au hizi indicators zipo ndani ya vikao vya baraza la mawaziri? Je, zina compliment au pingana na Ilani ya CCM? Na matakwa ya donors yanaingiaje katika mchakato wote huu? Do we have a standardised way of measuring performance ya executive branch - cabinet kwa mfano, au what we have ni kwamba, Aggrey Mwanri kwa mfano anapimwa kivyake, Magufuli kivyake, Pinda nae kivyake n.k, n.k? Nakumbuka miaka ya mwanzio ya 2000, Mkapa alitamka nadhani akiwa mkoani Pwani kwamba JK na Lowassa na sijui nani mwingine ndio mawaziri wake wachapa kazi, sijui alikuwa ana base on what indicators, wadau mnalionaje hili, any ideas juu ya uwepo wa hizi indicators ambazo umma hauna taarifa nazo?
 
Mimi naweza kusema hivi; haijalishi mabadiliko ambayo CCM inafanya kwa sababu yamechelewa na kwa kweli kabisa ni cosmetic zaidi kuliko substantial. CCM bila kuvunjika haiwezi kuokoleka kwa sababu matatizo yake ni zaidi ya vikao na watu wanavyochaguliwa baadhi ya matatizo yake (naamini makubwa zaidi) ni ideological and structural. Vinginevyo wataendelea kubadilishana badilishana rangi tu lakini asili iko pale pale. Nimefikia hitimisho kuwa hakuna mabadiliko ambayo yanaweza kuigeuza CCM isiwe CCM.
 
a. ukiangalia mfumo wetu wa vyama vya siasa, si rahisi kwa wanachama kumchagua mgombea urais directly. Kwa mfano, ni rahisi mno kwa mwanachama wa CCM mkoa wa Dar es salaam, kwenda kupiga kura morogoro au Pwani. Hata kama watapiga kura siku moja, itakuwa vigumu sana kuitambua "franchise" ya CCM na kuicontrol (ni rahisi kuhujumu). Pia, pamoja na gharama kuwa kubwa, visiwani hawatawakilishwa proportionally.... au mikoa migine ambayo haina wanachama wengi wa CCM. Kwa hiyo NEC itafaa kwa sababu itakuwa inawakilisha chama proportionally based on the citizenry and not party affilliation.

b.Kwa Tanzania, chama cha siasa kinasimamia hoja. Unlike US, wagombea wa republicans wanaweza kuwa na hoja inayokinzana na chama chao na bado wakashinda uchaguzi. Kwa Tanzania hiyo haiwezekani. Kama unataka serikali tatu..... unaenda CDM etc.. Kama kuna chama kinataka kufanya huu mtindo kifanye,ila nadhani kutakuwa na ngonjera nyingi tu, na wagombea wataonekana kuwa tofauti na imani za vyama vyao.

c. a na b nadhani zinaelezea c kwa sababu vyama ndio vinavyoongoza nchi ndiyo maana hakuna mgombea binafsi.

Kuchagua wajumbe wa NEC kutoka wilayani ni jambo la busara, kwa sababu matawi na kata ndiyo zitakazoshindanisha ujumbe wa NEC... if you can penetrate that deep, then you definately deserve to be a presidential candidate. Mabo ya kuhonga wajumbe wa mkutano mkuu yatakuwa yamekatiliwa mbali. This is the best way kama CCM inataka kuwashirikisha wanachama wake kwenye maamuzi.

Ni kweli, chini ya mabadiliko haya, sasa chama kimesogea zaidi kwa wanachama, kwani wanachama wapo kwenye matawi/kata, sio mkoani au wilayani. Kwa wajumbe hawa 221 maana yake ni kwamba kila jimbo litakuwa na mjumbe wa NEC, na kama tunavyofahamu, majimbo hutengenezwa na kata. Lakini tunabakia kusubiri kuona iwapo wajumbe hao watakuwa wanawatumikia wananchi wa maeneo yao au watajikita zaidi katika siasa za kitaifa kama ilivyo sasa. Ni muhimu tukaona job description mpya ya wajumbe wa NEC kama ipo, vinginevyo chini ya katiba ya sasa, job description ya mjumbe wa NEC haina lolote muhimu kwa wananchi wa ngazi za chini moja kwa moja.

Hoja kwamba ukitaka serikali tatu basi uende CDM, nadhani hata CCM wenyewe hoja hii haikwepeki. Kolimba na Malecela walikosana na Mwalimu kwa hoja hii tu, hakuna lingine. Wao walimshauri Mwinyi kwamba suala la serikali tatu halikwepeki, jambo ambalo mwalimu alilipinga, na kupelekea viongozi hawa kutolewa katika nafasi zao za uongozi kwa 'kumpa Rais na Mwenyekiti wa CCM ushauri mbaya'. Kati ya mambo machache ambayo kwa kweli Mwalimu Nyerere hakuwa na logic ni suala la kupinga muungano wa serikali tatu. Inawezekana serikali tatu zitadhoofisha muungano, lakini serikali mbili zitatuletea machafuko.
 
Mimi naweza kusema hivi; haijalishi mabadiliko ambayo CCM inafanya kwa sababu yamechelewa na kwa kweli kabisa ni cosmetic zaidi kuliko substantial. CCM bila kuvunjika haiwezi kuokoleka kwa sababu matatizo yake ni zaidi ya vikao na watu wanavyochaguliwa baadhi ya matatizo yake (naamini makubwa zaidi) ni ideological and structural. Vinginevyo wataendelea kubadilishana badilishana rangi tu lakini asili iko pale pale. Nimefikia hitimisho kuwa hakuna mabadiliko ambayo yanaweza kuigeuza CCM isiwe CCM.

Hivi kwa mtazamo wako, unadhani kwanini CCM inaogopa sana kuvunjika katika vipande viwili wakati ukweli ulio wazi ni kwamba hiyo ndio njia pekee ya kupona na kubakia katika siasa za ushindani?
 
Kitendo cha kumfanya rais na mwenyekiti wa CCM kuwa na nguvu ya kuteuwa mrithi wake (technically) ndicho kilichoiuwa KANU nchini Kenya na mpaka sasa KANU imebaki historia tu ndani ya Kenya. Kikwete akumbuke kuwa mfumo huu kama Mzee Mkapa angeutumia kwake wala leo asingekuwa magogoni. Inafamika wazi Kikwete hakuwa chagua la Mkapa, bali nguvu kubwa ya Mwinyi, Kawawa na Wazee wa Zanzibar ndio iliyobadisha upepo. Hilo rungu analolisaka na kuwachagulia CCM mgombea anayekuja alitumie vizuri la sivyo 2016 watu wanaanza kufungia maandazi mafail ya CCM
 
Hivi kwa mtazamo wako, unadhani kwanini CCM inaogopa sana kuvunjika katika vipande viwili wakati ukweli ulio wazi ni kwamba hiyo ndio njia pekee ya kupona na kubakia katika siasa za ushindani?

kuvunjika kwa CCM kunatisha kwa sababu moja kubwa - kunaondoa a comparative advantage ambayo CCM inayo dhidi ya vyama vingine hasa mahali ambapo kuna chama ambacho kinaonekana kukua zaidi in this case CDM. CCM ikivunjika sasa hivi katika udhaifu wake utakuwa ni mwisho wa kuweza kusimama; ni bora ivunjike baada ya kupata nguvu kidogo. Mabadiliko ya CCM yanajaribu kutengeneza cushion ya mpasuko huo mkubwa.

Kwa mfano, baada ya mabadiliko haya na matendo kadha wa kadha ya kujivua "gamba" wachache ambao walikuwa na nguvu watajikuta wanapoteza hoja kubwa ndani ya chama; watakosa support. HIvyo, hata wakija kutoka baadaye - say in 2013 au baada ya uchaguzi wa CCM kwa vile watakosa nafasi hawatokuwa na hoja kubwa sana kwani wataonekana ni sore losers.

Lakini jambo jingine linalotisha ni kuwa ikivunjikaa sasa nchi na chama kinaweza kisipone tena mpasuko wa namna hiyo. Umeona ilivyo ngumu kwa KANU ya kenya kureconstitute au hata ZANU-PF.
 
Kitendo cha kumfanya rais na mwenyekiti wa CCM kuwa na nguvu ya kuteuwa mrithi wake (technically) ndicho kilichoiuwa KANU nchini Kenya na mpaka sasa KANU imebaki historia tu ndani ya Kenya. Kikwete akumbuke kuwa mfumo huu kama Mzee Mkapa angeutumia kwake wala leo asingekuwa magogoni. Inafamika wazi Kikwete hakuwa chagua la Mkapa, bali nguvu kubwa ya Mwinyi, Kawawa na Wazee wa Zanzibar ndio iliyobadisha upepo. Hilo rungu analolisaka na kuwachagulia CCM mgombea anayekuja alitumie vizuri la sivyo 2016 watu wanaanza kufungia maandazi mafail ya CCM

Kwa mtazamo wako, je unadhani kiti cha mwenyekiti wa CCM taifa na Rais vikitenganishwa havitapelekea nchi kuyumba? Kwani tofauti na nchi kama marekani na kwingineko ambako mwenyekiti wa Chama ngazi ya taifa mara nyingi wala huwa hana interest ya kuwania urais, kwetu sisi, ukimpa uenyekiti hata mtu ambae alikuwa hajui na hapendi siasa, tayari utakuwa umemfungulia mlango wa kuwania urais, na atawachachafya sana wagombea wengine. Nadhani kuna umuhimu wa kutenganisa kofia hizi mbili lakini sio kwa kasi ambayo wengi wanaitaka, inabidi kukuna vichwa hasa ili kubaini jinsi gani tunaweza vitenganisha. Kwa mfano, mwenyekiti wa CCM taifa asiruhusiwe kugombea Urais mpaka muda wake wa uenyekiti uishe?

Je, ni yepi kati ya haya ndiyo yanampa mwenyekiti nguvu alizonazo na nini kifanyike kumpunguza nguvu hizi?
Katiba inasema hivi kuhusu mwenyekiti wa CCM Taifa;

  • Ndiye msemaji mkuu wa CCM.
  • Atachaguliwa na mkutano mkuu wa ccm taifa na atakuwa katika nafasi hiyo ya uongozi kwa muda wa miaka mitano, lakini anaweza kuchaguliwa tena baada ya muda huo kumalizka.
  • Anaweza kuondolewa katika uongozi kwa azimio litakalopitishwa katika mkutano mkuu wa CCM taifa na kuungwa mkono na theluthi mbili za wajumbe kutoka bara na theluthi mbili za wajumbe kutoka visiwani.
  • Atakuwa mwenyekiti wa mkutano mkuu wa CCM taifa, halmashauri kuu wa CCM taifa na kamati kuu ya halmashauri kuu ya taifa.
  • Katika mikutano anayoiongoza zaidi ya kuwa na kura yake ya kawaida, mwenyekiti atakuwa pia na kura ya uamuzi endapo kura za wajumbe wanaoafiki na wasioafiki zitalingana.
 
Ni kweli, chini ya mabadiliko haya, sasa chama kimesogea zaidi kwa wanachama, kwani wanachama wapo kwenye matawi/kata, sio mkoani au wilayani. Kwa wajumbe hawa 221 maana yake ni kwamba kila jimbo litakuwa na mjumbe wa NEC, na kama tunavyofahamu, majimbo hutengenezwa na kata. Lakini tunabakia kusubiri kuona iwapo wajumbe hao watakuwa wanawatumikia wananchi wa maeneo yao au watajikita zaidi katika siasa za kitaifa kama ilivyo sasa. Ni muhimu tukaona job description mpya ya wajumbe wa NEC kama ipo, vinginevyo chini ya katiba ya sasa, job description ya mjumbe wa NEC haina lolote muhimu kwa wananchi wa ngazi za chini moja kwa moja.

Hoja kwamba ukitaka serikali tatu basi uende CDM, nadhani hata CCM wenyewe hoja hii haikwepeki. Kolimba na Malecela walikosana na Mwalimu kwa hoja hii tu, hakuna lingine. Wao walimshauri Mwinyi kwamba suala la serikali tatu halikwepeki, jambo ambalo mwalimu alilipinga, na kupelekea viongozi hawa kutolewa katika nafasi zao za uongozi kwa 'kumpa Rais na Mwenyekiti wa CCM ushauri mbaya'. Kati ya mambo machache ambayo kwa kweli Mwalimu Nyerere hakuwa na logic ni suala la kupinga muungano wa serikali tatu. Inawezekana serikali tatu zitadhoofisha muungano, lakini serikali mbili zitatuletea machafuko.
Nakubaliana na wewe ila serikali mbili au moja ndiyo msingi wa CCM kukaa madarakani. Binafsi siushabikii sana muungano ila najua muungano ndiyo unaoiweka CCM madarakani.

Kuhusu job description, wajumbe wa NEC waliopo sasa hivi hawawezi kubanwa na wanachama ngazi ya tawi na kata kwa sababu hawawarepresent. Huwezi kupata taarifa yeyote kutoka jimbo la kigamboni au Uzini kuhusu matatizo ya wanachama kwenye majimbo hayo simply because concentration imekuwa kimkoa na hususan kitaifa zaidi. Kwa hiyo mfumo huu mpya unaondoa hiyo kiaina.
 
Nd. Mchambuzi,

Unasema, " Mwaka huu ni muhimu sana kwangu kuhusu maamuzi magumu." Kwanza sisi vijana wa nchi hii ili tuendelee inabidi tuachane na "siasa za maji taka" kama utumiaji wa maneno vague na meaningless kama mfano "maamuzi magumu" , "Kujivua gamba" etc. Hii misemo inatugharimu sana kama Taifa. Tujiulize ni nguvu kazi kiasi gani imepotea kwa wananchi kudiscuss maana ya hii misemo?

Wewe kama young professional tunayekutegemea kwanza inabidi utuambie unategemea mabadiliko gani pindi ikifikia Dec2012? Kama mategemeo yako yasipotimizwa (yote au baadhi), utaamua kuachana/kujiondoa kwenye CCM? Maana sijaona mahali ulipoweka wazi kuwa a,b,c ... zisipotimia basi ni time ya kuondoka CCM. Otherwise kama unaendelea kuongea kwa kutumia lugha za viongozi wako nawe utakuwa huna tofauti nao. Yaani unakuwa unaitumia JF kama platform ya kujijenga ndani ya CCM as "a Young turk" wakukumbuke kwani unajua bigwigs wa CCM wanategemea JF for reliable political news. Mwanakijiji amekusaidia kuweka wazi kabisa jinsi gani hizo changes zilivyo shallow na sijaona CCM diehards hata mmoja aliyejitokeza kuja kumpinga kuwa hajui political reality ya TZ kwa kuwa yupo Nje. Naona tunajadili jinsi gani ya kuzuia inevitable yaani pending kifo cha CCM similar to KANU. Unasubiria kuachana nacho pale tu daktari atakapo declare kuwa kimekufa, huoni kuwa CCM imeshapoteza dira, moral authority? Binafsi thinking hiyo ya kusubiria naifananisha na watu wanaoitwa "Political Opportunists" ambao daima ni hatari sana kwani leadership skills zao kikomo chao huwa kipo chini, mfano hai ni Dr, Baba Mwanaasha, Vasco D-G, Msanii na mengineyo....hayo majina yote yametokana na mapungufu makubwa aliyonayo kiongozi wenu.
Ni hayo tu ndugu yangu, siasa njema.
Angalizo: Sijakushauri ujiunge na chama chochote kwani natambua unaouwezo wa kupima vilivyopo kama vinafaa au la, na pia unaweza kuanzisha cha kwako.
 
Mkuu, mchambuzi analysis yako nzuri na post zako kuhusu chama chako ziko deep na only active members ndio wataelewa. Hatuoni members wa vyama vingine wakifanya haya au kunena haya, wengi ni kama wanaburutwa tu, mbele wamezibwa, nyuma wamesahau kushoto na kulia kuna ushabiki

when it come to dream party for kids, CCM inaongoza...I mean kama mtoto anaona kuwa rais leo hii ni rahisi kusema na kufanya hivyo kupitia CCM na sio chama kingine chochote.

though I stand with my signature, lets me give u thump up to stand like this!
 
kuvunjika kwa CCM kunatisha kwa sababu moja kubwa - kunaondoa a comparative advantage ambayo CCM inayo dhidi ya vyama vingine hasa mahali ambapo kuna chama ambacho kinaonekana kukua zaidi in this case CDM. CCM ikivunjika sasa hivi katika udhaifu wake utakuwa ni mwisho wa kuweza kusimama; ni bora ivunjike baada ya kupata nguvu kidogo. Mabadiliko ya CCM yanajaribu kutengeneza cushion ya mpasuko huo mkubwa.

Kwa mfano, baada ya mabadiliko haya na matendo kadha wa kadha ya kujivua "gamba" wachache ambao walikuwa na nguvu watajikuta wanapoteza hoja kubwa ndani ya chama; watakosa support. HIvyo, hata wakija kutoka baadaye - say in 2013 au baada ya uchaguzi wa CCM kwa vile watakosa nafasi hawatokuwa na hoja kubwa sana kwani wataonekana ni sore losers.

Lakini jambo jingine linalotisha ni kuwa ikivunjikaa sasa nchi na chama kinaweza kisipone tena mpasuko wa namna hiyo. Umeona ilivyo ngumu kwa KANU ya kenya kureconstitute au hata ZANU-PF.

Mwanakijiji tukitaka kuwa wakweli tuseme wazi kabisa kwamba CCM ya sasa ni nightmare kwa Tanzania, if it continues to exist in it's current shape, chances that Tanzania will change for better are extremely slim. Huu ni ukweli ambao kila mtanzania mwenye akili timamu anaujua. Kuibadilisha Tanzania ya sasa kunahitaji a major overhaul of whole political system, KATIBA is just one of them.

Comparative advantage ya CCM (over other ruling parties like ZANU-PF or former KANU, not over CDM or CUF) ni kuwa support base yake ni wanyonge (kielimu), na kuwa watu bado wafirikiri CCM 2010 au ile ya 2015 ni sawa na ile ya mwaka 1977, ndio maana bado wanendelea kuipigia kura. Wangekuwa na elimu ya kujua ukweli wa CCM ya sasa inavyofanya wawe na maisha magumu, wasingeipigia kura. CCM ya sasa ni chama tofauti kabisa na CCM ya mwaka 1977, na kamwe haitarudi kuwa CCM ile ya wakulima na wafanyakazi, no matter what is being done.

Unajua wengine wanadhani kuwa kuvunjika kwa CCM ndio kutakuwa miwsho wa CCM, i really do not think so. Inawezekana ikivunjika ndio ikawa na nguvu kubwa zaidi kuliko sasa. Kwa kuwa lengo la kuleta vyama vingi lilikuwa kupunguza nguvu ya CCM lakini sasa CCM ndio ina nguvu zaidi, serikali na chama walikubali ili kuirubuni jumuiya ya kimataifa kuwa we are multiparty democracy, kwa kuwa walijua watatumia usalama wa mataifa na mbinu nyingine ku-keep de-facto status quo, ambayo mpaka sasa inaendelea. CCM ya sasa ikipasuka na kuwa CCM A na CCM B, haitakuwa na tofauti yoyote na full CCM, it will take long time kuwa na mabadiliko. Hali ya Kenya na Zimbabwe ambako ukabilla una nguvu ni tofauti sana na Tanzania.

Kumbuka kuwa tulipo-introduce vyama vingi vya siasa lengo lilikuwa ni kuifanya CCM isiwe na ukiritimba wa madaraka, isiwe corrupt na isiwe na officials ambao ni corrupt. Look at where we are now compared with one party rule, ufisadi kwa sasa unalindwa kiwaziwazi. Siku hizi ukiwa mwizi, muuza dawa za kulevya, fisadi etc as long as uko CCM na ukaitwa "mmoja wetu", unapeta. Ukiwa smart, clean na visionary ukiwa upinzani, au ukiwa ndani ya CCM na uwa si mmoja wao huna maana. This is fact. Sasa hivi tuna mifano mingi ya CCM B, vyama vingine si opposition ispokuwa ni position tu ya CCM in opposition. Kumbuka siku Mabere marando alivyopigiwa kura kuwa mbunge wa bunge la Afrika mashariki, that was a very clear message kwamba hakuna opposition in opposition, ni sasa Chadema at least wanapnesha kiasi, na CUF imeshamezwa na kufa kwenye trap ya mwafaka. Usitegemee kama CCM ikivunjika kwa katiba yetu ya sasa na kwa level ya uelewa wa watanzania wa sasa, kutakuwa na mabadiliko yoyote ya maana.
 
Mkuu, mchambuzi analysis yako nzuri na post zako kuhusu chama chako ziko deep na only active members ndio wataelewa. Hatuoni members wa vyama vingine wakifanya haya au kunena haya, wengi ni kama wanaburutwa tu, mbele wamezibwa, nyuma wamesahau kushoto na kulia kuna ushabiki

when it come to dream party for kids, CCM inaongoza...I mean kama mtoto anaona kuwa rais leo hii ni rahisi kusema na kufanya hivyo kupitia CCM na sio chama kingine chochote.

though I stand with my signature, lets me give u thump up to stand like this!

Mkuu the point here is, regardless of your party Tanzania must come first. Sisi ni watanzania kwanza, ni wana CCM, Chadema na CUF baadaye, kuna vyama hivyo kwa sababu kuna Tanzania. We must speak for Tanzania first. Vijana tukifanya hivi Tanzania inaweza kubadilika. Ukweli utabaki kuwa ukweli ragardless umesimama juu ya meza gani.
 
Huu sio utaratibu wa CCM ni wa vyama vyote kwenye mchakato wa kutafuta wagombea kupitia vyama vya siasa. Utaratibu huu unatumika sehemu kubwa duniani tukiondoa wagombea binasi.
 
1. Ingawa mgombea Urais kwa tiketi ya CCM halazimiki atoke miongoni mwa wajumbe wa NEC na pia suala hili halipo kikatiba, Chama Cha Mapinduzi hakina utamaduni wa kuteua wagombea wake wa Urais ambao sio miongoni mwa wajumbe wa NEC.

...................CCM ilitoka kwenye mfumo wa chama kushika hatamu, wagombea wake kutoka NEC si jambo la ajabu. Katika hali ya kawaida mgombea wenye sifa na vigezo bora kuwa nje ya NEC kisiasa ni jambo ambalo sio rahisi sana. Mwanachama bora hawezi kuachwa na chama nje ya mfumo wa NEC ingawa kwa nadra inaweza kutokea.

II. Ili mwana CCM awe na nafasi nzuri ya kuteuliwa kubeba bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, inamlazimu mwanachama huyu, agombee na ashinde uchaguzi wa wajumbe wa NEC kwenye uchaguzi wa ndani wa CCM mwaka huu wa 2012. Kwa kufanya hivyo, mwana CCM huyo atakuwa ni mjumbe wa NEC-CCM ifikapo mwaka wa uchaguzi mkuu, 2015, hivyo kuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kuteuliwa kubeba bendera ya CCM mwaka 2015.

.........................Nadharia yako sio kweli, angalia hata chadema waliowahi kugombea wote hawakuwahi kuwa nje ya vikao vya juu vya chama. CCM wakati ukufika akaonekana mtu safi kabisa nje ya vikao vikuu vya chama nina hakika hawawezi kumtupa.

III. Wanachama wa CCM wenye malengo ya kugombea Urais kupitia CCM mwaka 2015, ambao kwa sasa wanashikilia nafasi mbili kwa pamoja – yani ubunge na ujumbe wa NEC, chini ya mabadiliko ya katiba ya CCM ya hivi karibuni, itawalazimu aidha waachie nafasi zao za ubunge na kubakia wajumbe wa NEC, au waendelee na Ubunge na waachane na ujumbe wa NEC, huku wakisubiri Baraka za Mwenyekiti wa CCM Taifa za kuwateua kuwa wajumbe wa NEC, kupitia zile nafasi kumi, miezi michache kabla ya mchakato wa kutafuta mgombea Urais kupitia CCM, ili mwanachama huyo awe katika nafasi nzuri zaidi ya kushinda katika kinyang'anyiro hicho.

.........................Nape amekanusha hili na hata Jk wabunge wataendelea kuwa wajumbe wa NEC wakati huo huo ni wabunge. Umepata wapi hii taarifa ya uongo?

IV. Kwa maana hii, Mchezo wote wa kinyang'anyiro cha Urais kupitia CCM mwaka 2015, umebadilika kutokana na mabadiliko ya katiba ya CCM, hivyo tutarajie majina mapya kutawala mbio hizi baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa CCM Novemba mwaka huu wa 2012, majina ambayo wengi hatukuyatarajia.

..................Rais aliyoko madarakani anamaliza kipindi chake hakuna ubishi majina mapya tutayaona wengi wakitaka kuchukua kiti cha Rais. Hii haitakuwa kwa CCM tu bali hata chadema na CUF vyama pinzani. Kimsingi, mabadiliko ya katiba ya CCM nimeona kwa ujumla wake ni mazuri. Kelele zinazopigwa ni hofu ya mabadiliko hayo. Binadamu hapendi mabadiliko kama yanagusa maslahi yake binafsi.
 
Binafsi nilitarajia pamoja na mabadiliko hayo ambayo hayana msaada sana wafanye yafuatayo:
-Miiko na maadili ya UONGOZI iimarishwe na kusisitizwa katika kila ngazi ya chama.
-Maisha binafsi ya wagombea yawekwe wazi zaidi. Wagombea waeleze wazi UKWASI wao wameupataje.
-Matumizi mabaya ya pesa yadhibitiwe ikiwa na pamoja na kuweka wazi wanaomchangia mgombea.
-Vyombo vingine vya DOLA vihusishwe tangu mwanzo wa michakato hii.
Walichofanya NEC ya CCM juzi ni kuleta mabadiliko ambayo kimsingi yanawalenga watu au kundi fulani la watu ambalo lina nguvu nyingi kuliko CCM yenyewe kama taasisi. Wamechelewa. Hata huko wilayani mtandao wao mafisadi ni mkubwa sana. Umasikini wa watu wetu unawakubali sana hawa jamaa.
 
Uchambuzi wako ni kama umetumwa na Lowassa au ni mfuasi wake. Hii ndio kambi yenye hofu kupita kiasi lakini bila sababu za msingi.
 
Watafanikiwa kweli kwa njia hii badala ya kuendeleza utamaduni ule ule wa kujaribu wakubalike ndani ya chama kwanza? Maana ni jadi kwa viongozi wa CCM wenye ubunifu na wachapa kazi kuonekana hawafai; ni kawaida kupigwa majungu na kumalizwa kisiasa, hata kama wanachofanya kina maslahi kwa taifa.

Hapa ni madon wachache wanataka kustaafu vizuri na walinde walichochuma na familia zao...yaani Rais wa Tanzania toka CCM kuanzia chaguzi ijayo atakua anawekwa na kakikundi ka watu kwa maslahi yao binafsi na si ya Tz....
 
Mkuu Mchambuzi,

Nimekusoma sana kwa kweli una hoja za msingi sana sikutarajia CCM bado ina wanachama wa aina yako wenye uwezo wa kutafakari na kubaini chama kinapoelekea.
 
Mchambuzi nakupa thumb up, najifunza mengi toka post zako hapa jukwaani........ Keep it up Bro. wadogo zako tunajifunza sana huku mavumbini....
 
Mkuu the point here is, regardless of your party Tanzania must come first. Sisi ni watanzania kwanza, ni wana CCM, Chadema na CUF baadaye, kuna vyama hivyo kwa sababu kuna Tanzania. We must speak for Tanzania first. Vijana tukifanya hivi Tanzania inaweza kubadilika. Ukweli utabaki kuwa ukweli ragardless umesimama juu ya meza gani.

Mkuu uko sahihi kabisa,vijana wa Kitanzania ni wakati wetu sasa kufanya maamuzi kwa ajili ya taifa letu badala ya kuhangaika na vyama ambavyo haviweki maslahi ya taifa mbele. Kuna mchangaiji amesema ccm hata ifanye mabadilko kiasi gani haiwezi kuwa kama ile ya 1977 nami nakubaliana naye kabisa kwani kwa sasa uadilifu umepungua sana na ndio unaifanya ccm kuwa mbali na wananchi kwani watu wako bize kujijenga kimaslahi na kiutawala badala ya kushughulikia kero za wananchi.
 
Back
Top Bottom