Huyo Sitta na Maembe ni nani kama hukumu imeshatolewa? ni kupoteza muda na kutaka longo longo tu. Cha msingi wahusika waliotufikisha hapo ndio wanatakiwa kutiwa kitanzi. Hata kama siyo leo lakini huko tuendako lazima ipo siku atakuja mkuru 'mwendawazimu'. It is just the matter of time. Kama watu walilazimika kujiuzuru nyadhifa zao kwa kashfa ya Richmond iliyozaa Dowans, iweje watu hao waendelee kula bata mitaani huku sisi tukikibebeshwa mzigo wa kulipa tozo hili la mabilioni? Je, pesa hizo hizo si watakazotumia kununua uongozi ili wafikie malengo yao ya kuimaliza kabisa raslimali za nchi hii?. Eti leo baadhi yao wanajifanya wema na kutoa misaada makanisani. Pesa hizo hazitokani na kodi zetu? Tutakuja kushtuka kuvuta blanketi wakati kumeshakucha.
Kaskazini, mashariki na kusini kuzunguka nje ya uzio wa Ikulu kuna idadi kubwa ya Askari FFU na vifaa vya kazi. Ni idadi kubwa kuliko siku zingine.
Upande wa baharini mahali ambapo ni eneo la kuegesha magari kukiwa na sherehe kubwa ikulu, kuna gari ya maji ya washawasha, defender nne na FFU wamebeba bunduki na mabomu ya machozi.