SI KWELI Mzazi akipata mimba wakati bado ananyonyesha hudhoofisha afya ya mtoto anayenyonya

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Mimi ni mmoja wa watoto waliotungwa mimba wakati mzazi bado ananyonyesha, bahati mbaya aliyenitangulia alifariki dunia kabla sijazaliwa. Hivyo wakati nakua niliambiwa na majirani kuwa kutungwa kwangu mimba kulisababisha afya ya dadangu kudhoofu na kupelekea kifo.

Hili suala ni kweli au vihoja na vijambo vya walimwengu.

RIP dada yangu Koku.

1708896761972.jpeg

 
Tunachokijua
Kunyonyesha ni ulishaji wa watoto wadogo kwa maziwa kutoka kwenye titi la mama. Wataalamu wa afya wanapendekeza kunyonyesha kuanzia saa ya kwanza ya maisha ya mtoto na kuendelea, mara nyingi na kwa kadiri mtoto anavyotaka.

Inashauri mtoto kunyonya miezi 6 ya kwanza bila kupewa chakula au kinywaji kingine na baada ya hapo anyonye huku anapewa vyakula vingine kwa takriban miaka 2. Wataalam wa afya wanasisitiza kunyonyesha maziwa ya mama, kuwa yana faida kubwa ya virutubisho ambavyo kwenye maziwa ya fomula hakuna.
330px-Breastfeeding_infant.jpg
Hata hivyo huenda wakati mama ananyonyesha yawezekana akapata ujauzito mwingine kabla ya mtoto anayenyonya kufikia muda wa kuachishwa kunyonya. Kutokana na hali hiyo imekuwa ikisemwa kuwa mtoto anatakiwa kuachishwa kunyonya kwa kuwa atadhoofika kiafya.

Jamiicheck imefuatilia iwapo ni kweli mama anayenyonyesha akipata mimba mtoto hudhoofu kiafaya.

Uchunguzi wa kitaalamu unaonyesha kwamba hakuna madhara kwa mwanamke kuendelea kumnyonyesha mtoto mchanga iwapo atajikuta amepata ujauzito

Pia Jamiicheck tumezungumza na mtaalamu wa afya, Dkt. Godfrey Chale, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake ambaye ameeleza kuwa:-

Mama anayenyonyesha akipata ujauzito anaweza kuendelea kumnyonyesha mtoto kama kawaida na Mtoto anayenyonya hatapata madhara yoyote kiafya, muhimu ni mjamzito kuzingatia lishe nzuri ili mazima yaendelee kutoka.

Miaka ya zamani Wanawake wengi walikuwa wananyonyesha Watoto muda mrefu hadi wanapofikisha miaka miwili tofauti na sasa hivi, hivyo Wazee wetu waliwaaminisha watu kuwa Mwanamke anayenyonyesha akipata ujauzito basi mtoto anayenyonya afya yake itadhoofika, hilo si kweli kitaalam.

Nadhani waliwaambia hivyo ili kutengeneza mazingira ya Wamama kupata muda wa kupumzika na mwili kujijenga vizuri kabla ya kupata ujauzito mwingine.

Kitaalamu mjamzito anaweza kuendelea kunyonyesha kama kawaida hadi miezi mitatu ya mwisho, ukifika muda huo akaacha, maziwa yatakata kisha yataanza kujitengeneza upya kwa ajili ya mtoto anayetarajiwa kuzaliwa akute yakiwa ‘fresh’.


Kutokana na wataalau wa afya kuthibitisha kutokuwepo kwa madhara kwa mtoto atakaeendelea kunyonya wakati mama yake akiwa na hali ya ujauzito ni muhimu mtoto anyonyeshwe ili anedelee kupata virutubisho muhimu kwa mtoto vinavyopatikana ndani ya maziwa ya mama huku mama akiendelea kupata lishe boora ili kulinda afya yake na ya mtoto
Hiyo sio mpya ni kweli. Kwa sababu maziwa yanajitengeneza kwa namna ya kusubiri mtoto anayekuja na sio ambaye amesha zaliwa
 
Hata kama hakuna madhara, bora mama anayenyonyesha ajitahidi kutobeba mimba, kusudi amtunze mtoto wake kwanza. Akimaliza kunyonyesha, basi apate mimba nyingine. Mama naye anahitaji kuwa na fya na kupumzika, siyo huku ananyonyesha, huku anatapika shauri ya mimba na madhira mengine yanayoendana na mimba!
 
Hii ilikuwa "misemo" ya wahenga iliyolenga kuweka hofu ili kuzuia uzazi holela.
 
Mimi ni mmoja wa watoto waliotungwa mimba wakati mzazi bado ananyonyesha, bahati mbaya aliyenitangulia alifariki dunia kabla sijazaliwa. Hivyo wakati nakua niliambiwa na majirani kuwa kutungwa kwangu mimba kulisababisha afya ya dadangu kudhoofu na kupelekea kifo.

Hili suala ni kweli au vihoja na vijambo vya walimwengu.

RIP dada yangu Koku.

Kweli.
 
Mimi ni mmoja wa watoto waliotungwa mimba wakati mzazi bado ananyonyesha, bahati mbaya aliyenitangulia alifariki dunia kabla sijazaliwa. Hivyo wakati nakua niliambiwa na majirani kuwa kutungwa kwangu mimba kulisababisha afya ya dadangu kudhoofu na kupelekea kifo.

Hili suala ni kweli au vihoja na vijambo vya walimwengu.

RIP dada yangu Koku.

Ukweli utabaki kuwa ni ukweli kwamba mama akiwa katika kipindi cha kunyonyesha halafu akapata ujauzito; mtoto anayenyonya hatadhurika kiafya directly kwa kuendelea kunyonya maziwa ya mama yake ambaye tayari ni mjamzito. Ila tuzingatie kwamba:

1. Mwili wa huyo Mama mjamzito unajiandaa kwa kuanza tena kumlisha mtoto mwingine. Hizo ni kazi mbili - kuzalisha maziwa(Lishe) kwa mtoto anayenyonya na tena kujishughulisha na kazi ya ukuaji mimba ili kuanza tena kazi ya kuzalisha maziwa fresh ya mtoto mwingine. Ni mzigo mkubwa kwa mama huyo.

2. Ukuaji mimba unapelekea ukuaji wa upendo i.e. mwili unaji-tune kisaikolojia kwa mtoto atakayezaliwa, lakini wakati huo huo yupo mtoto tayari anayeoneshwa upendo wa mama wakati wa kunyonyeshwa. Je, unabalance vipi hayo mawili kwa wakati mmoja kwa mama huyo (Hormonal balance)? Kumbuka pia kwamba mama huyo huyo anamajukumu mengine ya kifamilia. Huko ni kum-Overwork na Ndo mana wazee na watu wa busara wakashauri sio vyema.

Hilo hutumika kwa Mifugo e.g. ng'ombe anabebeshwa mimba nyingine baada ya siku 40-60 baada ya kuzaa (post partum ) na hukaushwa mwezi wa saba wa mimba hiyo ili awe na miezi 2 ya kujiandaa(Mapumziko) ili ajijenge kiafya na kuanza tena kunyonyesha au kukamuliwa.

Lakini kwa binadamu utaratibu huo sio muafaka kwani ng'ombe jike anafananishwa na mashine/kiwanda cha kuzalisha maziwa. Je, tunataka binadamu naye awe ni kiwanda cha kuzalisha watoto kivile? Kwani kuna shida gani kutulia hiyo miaka 2 - 2.5 bila ujauzito?
 
Ukweli utabaki kuwa ni ukweli kwamba mama akiwa katika kipindi cha kunyonyesha halafu akapata ujauzito; mtoto anayenyonya hatadhurika kiafya directly kwa kuendelea kunyonya maziwa ya mama yake ambaye tayari ni mjamzito. Ila tuzingatie kwamba:
Lengo la post ni kuonesha ukweli kuwa hakuna madhara mtoto akinyonya kama ambavyo wengi walikuwa wanadai sijui mtoto anadhoofu ikiwemo kuharisha na walikuwa wanamtaka mama kumwachishwa mtoto kunyonya iwapo mama kabeba mimba bila kukusudia wakati akinyonyesha.

Japo ni kweli kwa ajili ya afya ya mama ni vyema kusubiri miaka 2 kabla a kubeba ujauzito mwingine
 
Lengo la post ni kuonesha ukweli kuwa hakuna madhara mtoto akinyonya kama ambavyo wengi walikuwa wanadai sijui mtoto anadhoofu ikiwemo kuharisha na walikuwa wanamtaka mama kumwachishwa mtoto kunyonya iwapo mama kabeba mimba bila kukusudia wakati akinyonyesha.

Japo ni kweli kwa ajili ya afya ya mama ni vyema kusubiri miaka 2 kabla a kubeba ujauzito mwingine
Sawa kabisa mkuu.
 
Hii iende pamoja na ule uongo wa kusema mama akiwa na mtoto mchanga haruhusiwi kusex na mume wake au na mwanaume mwingine ety atakuwa amembemenda mtoto.
 
Hii iende pamoja na ule uongo wa kusema mama akiwa na mtoto mchanga haruhusiwi kusex na mume wake au na mwanaume mwingine ety atakuwa amembemenda mtoto.
Ni kwa Imani tuu lakini hakuna ukweli wowote. Ni kuwatisha au kuwaogopesha wahusika ili wawe watulivu na waweze kupata nafasi ya kumlea mtoto wao vizuri zaidi.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom