Uchaguzi 2020 Mwigulu Nchemba Vs Kiltila Mkumbo jimbo la Iramba Magharibi

Kanywe uji wa mihogo.
Sinywagi uji.
umetumwa na Yule anayechoraga mawe mkoa wa singida.
Sijui kama umesoma posti kwa umakini,

Rudia kusoma hii sehemu...

"...Maendeleo hayaletwi na mwanasiasa, maendeleo yako yataletwa na wewe mwenyewe. ."

Ungekua na akili ungejua hapa sio tu nimegusa kitila bali nimegusa mpaka huyo mwigulu wako.

Tafadhali soma vizuri mada kabla ya kukimbilia kujibu ujinga.

Narudia tena huo muda unaotumia kutafutia watu chakula ungeutumia kusaidia bibi yako kule kijijini, huyo mwigulu au kitila wakishapata ubunge hutawaona tena mpaka 2025 tena!!

Acha ujinga kijana.
 
Rais 2020
 

Attachments

  • FB_IMG_15867997808272711.jpg
    FB_IMG_15867997808272711.jpg
    34 KB · Views: 1
Kwakweli hakuna mgombea mwenyw nguvu iramba kama Prof,hali ya Mqigulu imekuwa tete mmno hasa baada yankuonekana dhahiri anautaka urais na kuvunja kanuni za ccm,Anashirikiana na familia mmoja kubwa na wafanyabiashara akiamini anaweza kuwa Raid jambo ambalo kamwe haliwezi kutokea
Labda kura ipigiwe jf na WhatsApp, Ila kwa Iramba, akipata hata nusu ya kura zangu nawambia Chama changu wamtangaze kuwa ndio mshindi. "NI HESABU MBAYA SANA KUPAMBANA NA MAMBA KWENYE KINA KIREFU CHA MAJI"
 
Labda kura ipigiwe jf na WhatsApp, Ila kwa Iramba, akipata hata nusu ya kura zangu nawambia Chama changu wamtangaze kuwa ndio mshindi. "NI HESABU MBAYA SANA KUPAMBANA NA MAMBA KWENYE KINA KIREFU CHA MAJI"
Umepanic Sana wewe dogo, JIMBO Huna
Umeaminiwa Ktk sehem nyingi serikalin
Umeenda kuwa mwiz tuu
Kwanini Jpm alikutumbia?
 
Labda kura ipigiwe jf na WhatsApp, Ila kwa Iramba, akipata hata nusu ya kura zangu nawambia Chama changu wamtangaze kuwa ndio mshindi. "NI HESABU MBAYA SANA KUPAMBANA NA MAMBA KWENYE KINA KIREFU CHA MAJI"
Nyie madokta na maprofesa wa nchi ni wajinga kweli yani mnatia aibu.

Profesa/dokta mzima badala ya kukaa kuja mawazo ya kuisaidia hii nchi kutoka kwenye UMASKINI ambao chama chenu kimesababisha mnakaa kuanza utafuta teuzi na kubishana kama watoto!!

Hivi ni lini mtakua na akili?

Shilingi inashuka, uchumi mbovu nyie mpo tu! ajira hakuna, viwanda hoi....yani mmekaa kaa tu mnawaza madaraka!

Sasa PhD zenu zina msaada gani kwenye hii nchi maskini kusini mwa afrika?

Jifunzeni hata kwa wenzenu basi!! Angalieni wanavyo saidia nchi zao!

Kwa kweli sio wewe tu, hata kitila, mnatia aibu sana.
 
Jimbo la Iramba limekuwa na vita vikali kati ya Mwigulu Nchemba (Mbunge wa sasa aliyewahi kuwa Waziri pia) na Katibu Mkuu wa sasa Wizara ya Maji Prof. Kitila Mkumbo. Wasomi hawa wamekuwa na msigishano wa hapa na pale na kufanya Jimbo sasa kuangalia zadi watu waofaa badala ya kuangalia nini kinapaswa kufanyika kwenye Jimbo letu la Iramba.

Hivi karibuni kulitokea msiba wa mtu maarufu Dr. Mwigulu akiwa njiani kuelekea katika msiba huo baada ya kuambiwa kuwa Prof. kitila kishafika kule yeye akaghairi kwenda. Ajabu sana!

Sasa hawa watu wawili wameunda Timu zao za kutaka Jimbo na tayair wameshalalamikiana kufanyiana hujuma. Inashanagaza wanaangalia nafasi badala ya nini wanapaswa kukifanya kwa manufaa ya Jimbo.

Mwigulu ameunda timu abayo inaongozwa na Diwani wa kwenye Kata yake na yule Diwani wa Kinampanda. Mwigulu pia ametengeneza mtandao unaohusisha watu kama Richard Mkumbo - Mchumi mwenzie yupo Ofisi ya Makamu wa Rais, Kanali Mstaafu wa Jeshi Kitundu, Katibu Mkuu wa Wizara aliyejiudulu hivi karibuni yule Kingu. Mwigulu pia anaungwa mkono na Mbunge Viti maalum Martha Mlata na pia anafanya mawasiliano ya karibu na Mwanasheria Kitandu Ugula ambaye wapo naye Chamani na wanatoka Kata moja. Huyu anategemewa katika kuongoza mikakati ya kisheria katika kampeni zake.

Kundi la Prof. Kitila linaoenekana kujipanga zaidi kwani wale walioumizwa na Dr. Mwigulu wakati akigombea Mwaka 2015 wanaungana naye ili kuhakikisha wanamtoa kwenye ubunge. Kundi hili linajumuisha watu kama kina David Jairo (Katibu Mkuu wa zamani Madini na Nishati), Timothy Lyanga, Jumbe Katala, Jesca Kishoa (ambaye inadaiwa anasubiri Prof. Kitila alianzishe naye ahamaie CCM kumfuata muwe wake Kafulila). Kuna pia ambao wanaonekana kutokuwepo upande wowote, kwa mfano kuna Eng. William Shila ambaye anapanga mikakati mikali ya kuchukua Jimbo akifanya mawasiliano ya karibu na Diwani wa Ulemo nyumbani kwao Engineer huyu.

Kuna pia akina Juma Kilimba mwenyekiti wa CCM mkoa ambaye wanapambana kivyao na kuhakikisha wanachukua jimbo, Kilimba anadaiwa ana mtandao mkubwa Kitaifa.
Kundi la Prof. Kitila lina mikakati mizuri lkn limekuwa likikwama kidogo kupenya kwa WanaCCM kwa sababu ya Jimbo husika kuonekana lina UCCM mwingi....

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii niliwahi kuileta mimi kwa title ingine - du kumbe JF kuna watu wanachukua threads za wenzao!
 
Labda kura ipigiwe jf na WhatsApp, Ila kwa Iramba, akipata hata nusu ya kura zangu nawambia Chama changu wamtangaze kuwa ndio mshindi. "NI HESABU MBAYA SANA KUPAMBANA NA MAMBA KWENYE KINA KIREFU CHA MAJI"
Mayu na Mimi naomba kazi kwenye timu yako!
 
"NI HESABU MBAYA SANA KUPAMBANA NA MAMBA KWENYE KINA KIREFU CHA MAJI"
Mkuu Mhe. Mwigulu Nchemba, maadam wewe ni kada mzoefu wa CCM ambaye ni born and breed, unajua fika the determinant ya mgombea wa CCM sio kura za maoni za wana CCM!, huna sababu ya ya kutumia maneno ya mipasho ya kwenye kanga kutishia watu.

Kitu cha muhimu sana kwako kwa sasa Mhe. Mwigulu, ni kuendelea kujibu hoja kama hizi kule kwenye like bandiko lako hili
Ana kwa ana na Mwigulu Nchemba: Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020 - JamiiForums

Zitakusafishia njia, na sio kujibu kimipasho humu.
Ni ushauri tuu!
P
 
Back
Top Bottom