Mwigulu Nchemba Utawaua bure Maafisa ktk Halmashauri mbalimbali hapa Nchini

NYACHA

JF-Expert Member
Dec 26, 2013
273
65
Wadau, maafisa wetu wa halmashauri mbalimbali hapa nchini wanalia! yaani wanatia huruma jamani! ni miezi miwili tu tangu Mh Mwigulu Nchemba alipookoa zaidi ya bilion 40-50 za wafanyakazi hewa; ambapo zoezi hili lilifanyika mishahara yote ya wafanyakazi kuingiziwa kwenye akaunti zao moja kwa moja kutoka hazina! huu mchakato wa Mwigulu Nchemba maarufu kama mtoto wa mfugaji umewaathiri sana kiuchumi maafisa wengi wa halmashauri mbalimbali ambao ndio waliokua wanufaikaji wakubwa wa hizi billion 40; kwasasa hawana tofauti na walimu kwenda kwa mangi kukopa; kumbi za starehe hawaonekani tena kama ilivyozoeleka kwa baadhi yao; hawa maafisa kwa sasa wameanza kuheshimu ndoa zao tofauti na kipindi cha nyuma kabla ya operation ya Mwigulu Nchemba. Wameanza kupaki magari yao nyumbani ; semina nazo zimepungua kwao. Jamani wanatia huruma maafisa wetu! Wafanyakazi wote wa serikali wanaanza kuwa sawa. Kwasasa wabunge ndo wamebaki wanasumbua mjini. Poleni sana maafisa, Mungu atawaidia. Ni maisha tu. MWIGULU NCHEMBA UMEKOMESHA.
 
Watanzania tujifunze kuacha kumsifia mtu anaetekeleza majukumu yake.

Hapo angefanya "beyond" aliyiagizwa ndio tungemsifia, but kama ni "within " his job descriptions basi kawaida tu!!
 
Kwa hili nampongeza. Huwez kuamini mwezi huu fedha tarehe 19, tayari ishaingizwa moja kwa moja kutoka hazina na siyo utumishi tena! Hapa namkubali jamaa ni jembe. Hata hivyo nampongeza tu kama mtu neutral mwenye fikra huru na nitampongeza yeyote bila kujali ni wa mrengo gani. Big up mh Nchemba, kwa hapa nakupongeza.
 
Huo ni ushabiki tu, nothing more!

Huo utafiti umeufanyia wapi?

Hao waliokuwa wanakula mabilioni kila mwaka ni marehemu? Mbona hatuoni huyo mwigulu akiwaweka hadharani? Huyo anataka nafasi ya Sada Mkuya tu opportunist huyo.
 
inaelekea mmejipanga Leo kumsifia kwa nini isiwe na mawaziri wenzie
 
Hoja ya kijinga hii. Kama mtu ameokoa kiasi cha ela, na alikuwa na uhakika kuwa zilikuwa zinaliwa, sasa hao waliokuwa wanakula ni kina nani, na amewachukulia hatua gani.

Usanii mtupu..!!
 
Watanzanixa tujifunze kuacha kumsifia mtu anaetekeleza majukumu yake.

Hapo angefanya "beyond" aliyiagizwa ndio tungemsifia, but kama ni "within " his job descriptions basi kawaida tu!!
Shakir sijui una elimu gani lakini kitu muhimu cha kufanya mtu afanye zaidi, aoungeze juhudi ni kumpa hamsa/motivate and ndio hivyo kwa wachezaji wa soka ndio maana kila siku Ronaldo akifunga bao/goal anashangiliwa na mashabiki na anapongezwa na wachezaji wenzake ingawa ndio kazi yake na analipwa hela nyingi kwa kazi hiyo. Hivyo hakuna la ajabu kwa Mwigulu Nchemba.
 
Last edited by a moderator:
Watanzania tujifunze kuacha kumsifia mtu anaetekeleza majukumu yake.

Hapo angefanya "beyond" aliyiagizwa ndio tungemsifia, but kama ni "within " his job descriptions basi kawaida tu!!


Ni kwa sababu wanamwona yupo juu ya mnazi, ngoja si muda mrefu watasikia ladha ya tembo atakalowaletea akishuka,

Wanasahau kuwa huyo ni mgema
 
Watanzania tujifunze kuacha kumsifia mtu anaetekeleza majukumu yake.

Hapo angefanya "beyond" aliyiagizwa ndio tungemsifia, but kama ni "within " his job descriptions basi kawaida tu!!

lakini kweli
 
Hoja ya kijinga hii. Kama mtu ameokoa kiasi cha ela, na alikuwa na uhakika kuwa zilikuwa zinaliwa, sasa hao waliokuwa wanakula ni kina nani, na amewachukulia hatua gani.

Usanii mtupu..!!
Pole mkurugenzi.
 
zoezi hili lilifanyika mishahara yote ya wafanyakazi kuingiziwa kwenye akaunti zao moja kwa moja kutoka hazina!
Unapoingiza hela kwenye akaunti moja kwa moja unatibu vipi tatizo?

Kama kuna binadamu hewa hakuwezi kuwa na akaunti hewa?
 
Watanzania tujifunze kuacha kumsifia mtu anaetekeleza majukumu yake.

Hapo angefanya "beyond" aliyiagizwa ndio tungemsifia, but kama ni "within " his job descriptions basi kawaida tu!!
Shakir, unayosema ni sawa. Hatahivyo mimi sioni ubaya kumpongeza aliyeweza kutekeleza majukumu yake kwa kiwango cha kuridhisha. Kama watu wanapongezwa kwa kutimiza tu umri fulani(Birthday), kitu ambacho hawana dhamana nacho hata kidogo, seuze kazi nzuri!
 
Last edited by a moderator:
Kwa hili nampongeza. Huwez kuamini mwezi huu fedha tarehe 19, tayari ishaingizwa moja kwa moja kutoka hazina na siyo utumishi tena! Hapa namkubali jamaa ni jembe. Hata hivyo nampongeza tu kama mtu neutral mwenye fikra huru na nitampongeza yeyote bila kujali ni wa mrengo gani. Big up mh Nchemba, kwa hapa nakupongeza.

Uko sawa nivema kwa mtu yeyote anapofanya jambo zuri ni vyema kupongezwa, ili kumpa moyo aendele kufanya vizuri zaidi.
 
Shakir sijui una elimu gani lakini kitu muhimu cha kufanya mtu afanye zaidi, aoungeze juhudi ni kumpa hamsa/motivate and ndio hivyo kwa wachezaji wa soka ndio maana kila siku Ronaldo akifunga bao/goal anashangiliwa na mashabiki na anapongezwa na wachezaji wenzake ingawa ndio kazi yake na analipwa hela nyingi kwa kazi hiyo. Hivyo hakuna la ajabu kwa Mwigulu Nchemba.

Wewe ndio Elimu yako haieleweki. Unachoongea nacho hakieleweki. Unatoa mifano isiyoendana. Si lazima kila mfungaji/mshambuliaji afunge goli.

Ndio maana kuna kufungwa na sare. Na sio kila mechi lazima iishe kwa magoli. Na wala mshambuliaji asipofunga haina maana hakatimiza majukumu yake kwa 100%, wala sio pia lazima afunge yeye!!!

Sasa kwa huyo Mwigulu ni jukumu lake kuhakikisha mianya yote ya ulaji inazibwa pia kubuni vyanzo vingine vya mapato, na sio ombi au msaada, ni WAJIBU.

Na akifanya hivyo ndio inaelekea kua perform kwa 100%, hakuna cha ziada cha kusifia hapo!!
 
Last edited by a moderator:
Shakir, unayosema ni sawa. Hatahivyo mimi sioni ubaya kumpongeza aliyeweza kutekeleza majukumu yake kwa kiwango cha kuridhisha. Kama watu wanapongezwa kwa kutimiza tu umri fulani(Birthday), kitu ambacho hawana dhamana nacho hata kidogo, seuze kazi nzuri!

Ni wajibu wa Baba kuleta hela ya chakula nyumbani familia ile ishibe, na Baba anapofanya hivyo haitajiki kusifiwa kwa kufanya kitu ambacho ni jukumu lake.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom