Mwigulu Lameck Nchemba, Is The Most Genuine So Far!-Can Make The Best President!-Nimeguswa!

Mwigulu amebeba dhamira ya kweli tatizo ni mfumo uliopo ndani ya chama chake ataweza kuufuta.

Chama kipi kisicho na mfumo wa kufumuliwa?Mwigulu ana ambitions na energy ya kuyafanya hayo.

Kumbuka vyama vyote vina mifumo ya umiliki wa watu fulani, inahitajika mtu mpya kuufumua.
 
Amekuwa gumzo kutokana na mabango aliyojiandika nchi nzima nadhani.
Tanzania will be lead by one President EL
 
Tatizo hapo sio mtu. Tatizo ukiwa ndani ya CCM ni kansa tayari. Kazi kubwa iliyopo ni kuitoa CCM madarakani. CCM ni system ambayo IMEOZA. Lazima system hiyo iondolewe kwanza. Gari likiwa na MATAIRI MABOVU, hata kama una DEREVA mzuri toka NIT, Haizuii kupata pancha njiani. Ondoa kwanza TAIRI hizo mbovu, weka mpya.Gari litafika mbali bila pancha!!!


Wanabodi,

Tuweke ushabiki pembeni, kati ya watangaza nia watatu kati ya jana na leo, Mwigulu Lameck Nchemba is the most bonafide genuine mgombea so far, ukimuangalia huku unamsikiliza, utaiona his genuinety kutoka moyoni mwake 'to practice what he preach' kwa aliyoyasema yanaonekana kabisa yametoka moyoni mwake, tofauti na hawa wengine wawili waliyoyatamka yametoka tuu midoni mwao, hivyo kiukweli kabisa wa nafsi yangu, nadhani kwa kati ya hawa watangaza nia watatu so far, naamini Mwigulu can make the best president this country has e has ever had tangu Mwalimu Nyerere!.

Jee wewe mwenzangu ulibahatika kumsikia, unamuonaje?!.

NB: Ku make the best president ni jambo moja, lakini kuchaguliwa na chama kuwa mgombea ni jambo jingine!.

Kati wa watangaza nia hawa watatu, kuna mgombea anayependwa sana na watu na huyu sii mwingine bali ni ni Edward Lowassa, jee ni kwa nini Edward Lowassa anapendwa sana, sababu zinajulikana!, ila kama urais ni kupendwa basi rais wetu ni Lowassa!.

Kuna mgombea ambaye ni the most experieced so far, huyu ni Stephen Wasira, yeye ana uzoefu toka enzi za Nyerere alikuwa mbunge wa CCM, akahama CCM na kuwa mbunge wa upinzani, na kisha kurejea CCM, hivyo kama urais ni uzoefuu, then rais wetu ni Wasira.

Kati ya hawa watangaza nia watatu wa mwanzo wa CCM, Mwigulu Nchemba kwenye aspect ya originality na genuinety, Mwigulu ndio the most real, the most original na the most genuine!.

Mwigulu ameonyesha yuko real and down to earth kwa kuonyesha ametoka familia masikini, sio mtu wa makuu ya kujionyesha ili just to impress people kwa mbwembwe zozote kwenye uzinduzi, set yake ilikuwa simple, ameongelea background yake ya kimasikini na kuthibitisha kuwa yeye ni best brain tangu alikopita mpaka hapa alipo lakini kamwe hajasahau alikotoka!, hivyo huyu ndio mfano halisi wa Mtanzania wa kawaida, anaonyesha anawajua Watanzania, anaijua Tanzania, anawajua Watanzania wanataka nini, na anaijua Tanzania inatakiwa ifanye nini kutoka hapa tulipo twende kwenye the next level!.

Ukiangalia speech za wengine ni za kuandikiwa wa na mtu akisoma speech ya kwake mwenyewe aliyoiandika mwenyewe, utamjua, mtu akisoma speech aliyoandikiwa kisha aka kremu na kuja kusoma utamjua, na mtu akiandika speech yake mwenyewe na kuisoma mwenyewe, utamjua!, Mwingulu ndio was the most original, amekuja na talking notes too kama Nyerere na vitu vyote kutoka kichwani!.

Hivyo kwa maoni yangu, so far, ni Mwigulu ndio can make the best president this country can ever had, ila kwa sababu watia nia wanaendelea nitaendelea kuwapatia uchambuzi wangu kidogo kidogo kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa!.

Wakati tukielekea kumpata rais wetu wa 2015, kwa vile CCM ndio chama tawala, hatuwezi kukwepa kuuzungumzia mtindo wa uchaguzi wa kumpata mgombea wa CCM kwa sababu za kihistoria ya hii miaka 50 ya uhuru wetu, mgombea wa CCM ndie rais wa nchi, unless kama mwaka huu historia itabadilika!.

Tukiuchukulia mchakato wa 2005 wakati JK alipochaguliwa, kama reference, assuming hawa watatu ndio wameingia tatu bora, Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wakipewa choice ya kuchagua between "the most loved", "the most experienced" and the "the best president", watachagua mtu 'anayependwa na watu', mtu 'atakayechagulika' kwa urais kwa lengo la kuwapatia ushindi, na baada ya kumpitisha mbinu nyingine zote safi na chafu hutumika kwa sababu lengo ni ushindi, na ukiishapatikana zile mbinu zilizotumika zinakuwa justified na the end results.

Hivi ndivyo JK alivyochaguliwa ile 2005 kwa sababu kwenye the finalist watatu, JK was never the best, kulikuwa na "the most experienced" Dr. Salim, "The best Brain", Prof. Mwandosya, na "the good looking" Jakaya Kikwete, akapitishwa JK kwa hoja kuwa 'ni mwenzetu' ndiye 'anayependwa na watu', as if mapenzi ya watu ndio uongozi wa nchi!. Matokeo ya kumchagua rais 'mwenzetu' na sifu kuu ni 'kupendwa na watu' ili kukiletea chama ushindi wa kishindo, ndio haya ya kuunda serikali ya kishikaji yenye madudu kibao!, watu wakiboronga ni kuhamishia tuu, kwa sababu ni 'wenzetu', jee kwa 2015 Watanzania wanahitaji rais 'mwenzetu' tena, au this time tunahitaji the best?!.

JF has a role to play kupitia ma great thinkers wa jf, tutangulize mbele maslahi ya taifa kwa kuyaweka pembeni mahaba niue ya wapendwa wetu, na kujitolea kuwaelimisha wananchi wetu nchi hii inahitaji nini na kuongozwa na mtu wa aina gani, ili waweze kufanya informed decisions kwenye choice of president, ili ifike mahali chaguo la mgombea wa CCM sio lazima ndio automatikally awe rais wa nchi, kama CCM wakituletea ule ujinga ujinga kama wa 2005, tunapiga tuu chini CCM only if huko kungine kuna the better alternative!.

Ushauri wangu wa kwanza kwa wana JF, huyu Mwingulu Nchemba sio mtu wa kubezwa hata kidogo, he is a man to keep a close watch seriously, if the best is what we are looking for!.

NB. Kwa walionidhania mimi Pasco wa jf, niko kambi fulani, naomba tena kuwathibitishia kuwa Pasco wa jf, hana chama, hana kambi, hana mtu, ila kuna watu anawakubali akiwemo yule 'jamaa yetu', lakini linapokuja suala la kuchagua kati ya mapenzi binafsi kwa watu na maslahi ya taifa, nitatanguliza maslahi ya taifa mbele!, hivyo sitarajii kuulizwa kama nimehama kambi kwa sababu sijawahi kuwepo kambi yoyote!.

Hivyo kati ya hawa watatu wa mwanzo, kiukweli mimi Pasco wa jf, nimeguswa na Mwigulu Nchemba!.

Vipi wewe?.

Pasco


NB. Kutokana na kuwa bize na mambo mengi, sitaweza kuchangia uzi huu, wala kujibu hoja au swali lolote hivyo nitakushukuru kama utasoma tuu bila kuniuliza chochote!.
 
Mtoa mada umeainisha kuwa gumzo hilo limechanganya wale wanaomkosoa na wale wanaomuunga mkono . How comes uulize juu ya ishara? Tupe uwiano wa hao wanaomkosoa na wanaomuunga mkono tuweze kukupa mtazamo wetu. Otherwise na hii mada yako inaongezea tu idadi ya mada zinazomzungumzia Mwigulu na sio tathmin
 
hivi 1961 nyerere alikuwa na umri gani?
Red Giant latu huwezimlinganisha Nyererr na Mwigulu.... uthubutu wao ni tofauti kabisa. Nyerere aliyethubutu kuwaface wakoloni na masilaha yao... na huyu ambaye hata kutamka atawashughulikiaje watuhumiwa wa Escrow, EPA na mafisadi wengine ndani ya chama chake ameshindwa ndio tumlinganishe na Nyerere wa wakati ule?
 
Last edited by a moderator:
ati maisha bora kwa kila mtanzania mh!! ilitakiwa iwekwe wazi maisha bora kila fisadi full stop.
subirini butwaa DR HUSSEIN MWINYI ndio atakayemrithi jk.
 
mimi nadhani Mwigulu hakujua kama atakuja kumbea urais hadi alipojiona ni maarufu ghafla,

1. angejua asingekuwa anaropoka au kutoa kauli chafu tena kana kwamba sio msomi.
mfano ccm ni ng'ombe wananchi ni ndama. mkikataa kutujagua udiwani mtakufa maana tutagoma kuwanyonyesha. Ni kazi ya srikali kumuudumia kila mwananchi bila kujali dini wala itikadi. ulitereza hapo mkuu.

2. Kama raia mwema kudai kuwa anaushahidi wa ugaidi huku akishindwa kuupeleka polisi, tena hata polisi kumuhoji ni udhaifu na kutafuta umaarufu mwepesi wa kisiasa.

3. kama Mwanasiasa mzarendo hakupaswa kuongea yale ambayo huwa anayapinga kisa kutetea ccm hashindwi kutetea mafisadi akiwa rais. Kigeugeu.

4. Herikopta ya msukuma ndio aliitumia kujitafutia umaarufu kule moro, wakati huohuo huyo jamaa ni mfuasi mkubwa wa EL. inanipa picha kuwa kuna uwezekano hawa lao ni moja.

5. Bingwa wa siasa chafu, Kutembea na Mtu aliyemwagiwa tindikali ili kuwatisha wananchi ubaya wa wapinzani wakati alipaswa kuwaeleza nini SERA zake na atatekeleza vipi.

6. Kama ukiwa na elimu ya Masters ulishindwa kubuni njia ya kisomi ya kujipatia Kipato (labda kama ulisoma elimu mbaya) ukaenda kubeba zege, nilitegemea labda ufanye kazi ya kuandika proporsals, projects, au hata kutafuta nafasi ya kufundisha ktk mamia ya shule hapo jijini,. utawezaje kubuni miradi au mawazo ya kuondoa umasikini kwa graduates hususani kipindi ambacho hata kupata internship ni kazi.(msoni ni yule anayetumia elimu yake kujikwamua kimaisha kwa mtazamo wangu mimi ambaye sijaenda shule)

7. Siku moja ukiwa umejaa jazba bungeni ulitamani kupata japo nafasi ya urais ili uwashughulikie wapinzani na watu waliokuwa na mawazo tofauti na yako. Hadi ukasiema usingekuwa waziri ungeongea maneno mabaya zaidi(jinsi nilivyokuelewa). Sasa ilinitisha kidogo kwa jaribu dogo tu lilikutoa kwenye mstari, je ukikabidhiwa nchi?? You need time to convince people that you are new Mwigulu.

Maoni yangu: Mwigulu wa leo sio kama wa miaka iliyopita. Unaonekana unakuja kama mkombozi lakni inabidi upate muda tujiridhishe vizuri kama kweli umebadilika au unatumia sifa mbaya ya USAHAULIFU wa wachache kutimiza malengo yako kisiasa.

yote kwa yoe, Nakupongeza kwa kutangaza lakini fanya marekebisho, kama unafaa siku ikifika utakuwa.
 
Red Giant latu huwezimlinganisha Nyererr na Mwigulu.... uthubutu wao ni tofauti kabisa. Nyerere aliyethubutu kuwaface wakoloni na masilaha yao... na huyu ambaye hata kutamka atawashughulikiaje watuhumiwa wa Escrow, EPA na mafisadi wengine ndani ya chama chake ameshindwa ndio tumlinganishe na Nyerere wa wakati ule?
kuna theory ya history make the man. inasema mwigulu angekuwepo 1961 angepambana na wakooloni na Nyerere angekuwepo leo asingeweza pambana na mafisadi.
unajua sasa anatafuta kupita kura za maoni akianza kuwachokonoa EPA na ESCROW ataharibu kila kitu. mafisadi wata retaliate. mi nafikiri kuongoza na umri ni vitu tofauti. watu wenye uzoeefu kwenye serikali na umri mkubwa ndiyo wametufikisha hapa.
 
Kuajiliwa BoT sio kazi ndogo. Ukishapewa offer sio cgini ya miezi mitatu kumaliza process including vetting. Kama huna pesa utaishije miezi yote hiyo kama hujabeba zege. Tafuteni uongo wa kweli sio huo.
 
Mwigulu ni opportunistic populist tu.
I am glad someone else could see through Mwigulu, Mwigulu uses the people agenda as his main speech, however he needs to stay consistent and tell us his strategy, so far he has only been telling us ACTION PLANS, well you cant make president if you talk of action plan, that level is not for presidents, that's for DIWANI NA MBUNGE, lets talk US politics, when Obama went out to the mass with his message, it was CHANGE, , he stayed consistent with his message, but it was not built on action plans, rather long term strategies , I will await for others to see , we need to be able to draw a line between.............................1. STRATEGIES 2. INITIATIVES 3. ACTION PLANS
 
nimewaeleza watu wakabisha sana. mimi nimekaa pale Idara ya Uchumi, UDSM. najua mtu akisomeshwa masters na BoT (yeye amesomeshwa masters baada ya kuongoza GPA), anapata ajira moja-kwa-moja hata kabla hajamaliza. lakini cha kushangaza eti anasema alibeba zege. watu nao wanakubali, wanampigia makofi.

Duuh, Nakumbuka alisema pia kuwa alikuwa anamsaidia mke wake kazi ya "mama ntilie", nadhani angeitwa yeye mwenyewe atoe ufafanuzi maana mimi mwenyewe napata mashaka. Nimesoma UDSM pia na nafahamu that system ya "kubakizwa idarani" kwa wanaongoza kimasomo katika idara na ajira kwao huo ni moja kwa moja hapo hapo chuoni (Tutorial Assistant for 1st degree holder). How come waalimu waliokufundisha wakudai cheti wakati wa kukuajiri huku wanakujua nje ndani kitaaluma. Anyway, majibu ya hakika atakuwa nayo Mwigulu tumuite atuptie ufafanuzi wa hoja yake.
 
Mwigulu Nchemba aliyesuka kesi ya Ugaidi dhidi ya Lwakatare wa CHADEMA. Leo hii tumpe uraisi? Kuch nehii!
 
Hii inawezekana tanzania tu,"alisema tena bugeni anao ushahidi wa bomu kwenye mkutano wa chadema Arusha,viwanja vya soweto",mbona mpaka leo ajautoa hadharani?sembuse kuojiwa na polisi?Aiwezekani gaidi kuwa rais wa Tanzania jamani tuache maigizo,Eti kila kona ni gumzo!!kona zipi,huku niliko ata awamjui ila ukiwaambia ni yule jamaa kwenye kampeni za uchaguzi mdogo arumeru alikuwa kila akipanda jukwaani ni kuporomosha matusi tu,Ahaa ndio wanamkumbuka,sasa wanashangaa eti naye awe rais
 
Watu walimkaataa hata Yesu wakaona bora Baraba achiwe...! Sishangai kuona watu wakishabikia mgawa fedha EL nakuacha watu safi..!
Tuombe MUNGU...!
 
Pasco,

Kwa maneno ya Mwingulu Nchemba na ambavyo amekuwa akibehave na ambavyo anaonyesha nia ya kutenda mambo, anajaribu kujionyesha kuwa anafaa kuwa rais wa nchi hii. Ila kwa bahati mbaya sana, nia yake, mawazo na matendo yake yanaonekana ni mtu atakayetaka kufanya kazi na wachapakazi na wanaojielewa. Kwa bahati mbaya mawazo na nia yake vitamfanya asivuke hata ngazi ya kamati kuu.
Hata hivyo huwa simuamini Nchemba maana CCM hakuna hata mmoja anayeaminika. Tumesikia maneno mazuri sana toka CCM kama maisha bora kwa kila mtanzania, rushwa ni adui wa haki nk lakini Mh!
 
Back
Top Bottom