Greenwhich
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 1,337
- 968
Nadhani kuna uchaguzi wa Vijiji na vitongoji kadhaa jimboni Iramba mwaka huu.Nawashauri Chadema waanze na hili iwe kama Trailer kwa Mwigulu kumuonyesha vita sasa inapiganwa mlangoni mwake.
Nimeipenda strategy ya wafuasi wa Chadema wanafanya kama Wamarekani kwamba mfuate adui huko huko aliko ukamchakaze na usimpe nafasi ya kutoka nyumbani kwake.
Nawashauri viongozi wa Kanda ya Kati wachukulie maombi haya ya wafuasi wa Chadema kwa umakini na umuhimu mkubwa.Wanachotakiwa ni kuratibu zoezi husika.Kwa kweli mamilioni yatachangwa endapo wakifungua akaunti maalum kama maombi ya wanachama yanavyosema.
Pia namshauri Kitila Mkumbo apokee kwa unyenyekevu mkubwa heshima hii ya wanachama waliyoonyesha kwake.Awaongoze kuhakikisha Chadema inakuwa na nguvu Iramba kama ilivyo katika jimbo la Arusha mjini kwa Godbless Lema.
Nimeipenda strategy ya wafuasi wa Chadema wanafanya kama Wamarekani kwamba mfuate adui huko huko aliko ukamchakaze na usimpe nafasi ya kutoka nyumbani kwake.
Nawashauri viongozi wa Kanda ya Kati wachukulie maombi haya ya wafuasi wa Chadema kwa umakini na umuhimu mkubwa.Wanachotakiwa ni kuratibu zoezi husika.Kwa kweli mamilioni yatachangwa endapo wakifungua akaunti maalum kama maombi ya wanachama yanavyosema.
Pia namshauri Kitila Mkumbo apokee kwa unyenyekevu mkubwa heshima hii ya wanachama waliyoonyesha kwake.Awaongoze kuhakikisha Chadema inakuwa na nguvu Iramba kama ilivyo katika jimbo la Arusha mjini kwa Godbless Lema.
Last edited by a moderator: