Mpendwa,
Salamu natuma kwako, naomba uzipokee
Nauliza hali yako, nataka nikujulie
Barua hii ni yako, ujumbe uusikie
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Binti Msemaovyo, mwenziyo unanikosha
Siropoki hovyohovyo, na hilo nakujulisha
Nasema ujue hivyo, sikwamba nimechemsha
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Kwa maumbile na pozi, kiroho chaniripuka
Nashindwa kufanya kazi, kichwani wanizunguka
Nauomba ukimbizi, kwa weye uloumbika
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Ningali bado kijana, m-bichi nisiyeoa
Tuli nimetulizana, ni mwenza natafutia
Usiku pia mchana, nikweli nakuwazia
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Pia tena mcha mungu, huyo huyo wako wewe
Naomba tena kwa mungu, niweze kupata wewe
Dini yako ndiyo yangu, nasema bila kiwewe!
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Msomi ki kweli kweli, kijana miye nasema
Shahada ya uzamili, nimemaliza si zama
Ki pesa nipo kamili, nimejaliwa karama
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Nitawacha ukapera, na hilo nasisitiza
Kijana sina papara, nashinda nikikuwaza
Nitakufanya kinara, uweze kuniongoza
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Nane nasema tamati, kwako uliye umbika
Hakuna ambayo nyeti, kwangu yaliyofichika
Ni mimi mtanashati, nakuagia waraka
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Wakatabahu waraka,
Kijana Bin Mbichi .
Salamu natuma kwako, naomba uzipokee
Nauliza hali yako, nataka nikujulie
Barua hii ni yako, ujumbe uusikie
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Binti Msemaovyo, mwenziyo unanikosha
Siropoki hovyohovyo, na hilo nakujulisha
Nasema ujue hivyo, sikwamba nimechemsha
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Kwa maumbile na pozi, kiroho chaniripuka
Nashindwa kufanya kazi, kichwani wanizunguka
Nauomba ukimbizi, kwa weye uloumbika
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Ningali bado kijana, m-bichi nisiyeoa
Tuli nimetulizana, ni mwenza natafutia
Usiku pia mchana, nikweli nakuwazia
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Pia tena mcha mungu, huyo huyo wako wewe
Naomba tena kwa mungu, niweze kupata wewe
Dini yako ndiyo yangu, nasema bila kiwewe!
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Msomi ki kweli kweli, kijana miye nasema
Shahada ya uzamili, nimemaliza si zama
Ki pesa nipo kamili, nimejaliwa karama
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Nitawacha ukapera, na hilo nasisitiza
Kijana sina papara, nashinda nikikuwaza
Nitakufanya kinara, uweze kuniongoza
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Nane nasema tamati, kwako uliye umbika
Hakuna ambayo nyeti, kwangu yaliyofichika
Ni mimi mtanashati, nakuagia waraka
Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!
Wakatabahu waraka,
Kijana Bin Mbichi .