Mwenzako anaweza kuondoka bila kuaga?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,997
Kuna watu katika nahusiano wanaamini jatika kuagana. Wengine hawaamini katika hilo. Siyo katika kuaga tu bali pia katika kuulizana. Kwa mfano, mtu akitaka kutoka anaweza kukuuliza "unakwenda wapi" au kama anarudi unaweza kumuuliza "unatoka wapi au ulienda wapi". Na upande mwingine wa hilo unajisikiaje kama mwenzio anakuuliza hivyo. Anakuona unajiandaa na anajua utamwambia lakini anashindwa kujizuia "unakwenda wapi tena?" anauliza.

Au kuna kiwango gani cha kuulizana kinaruhusiwa? Kwa mfano, kama unaenda "dukani mara moja" unahaja ya kumwambia mwenzio? Ni mipaka gani ipo kwenye suala la kuagana na kuulizana kabla halijawa kero na kuanza kuleta kisirani?
 
Kwasababu sipendi kuulizwa/uliza "unatoka wapi" napenda tuagane. Hata kama hayupo nyumbani na unatoka kwa zaidi ya saa moja unaweza ukamtext tu kwamba "natoka kidogo, ntakurudi nyumbani baada ya muda fulani". Hivyo hata akifika akakukosa hatokua na maswali ya wapi ulipo, wakati gani uliondoka na wakati gabi utarudi. Na swala la kusubiria eti mpaka mmoja ajipare au avae ndio aseme 'natoka' sio zuri sana. Ni vizuri mkaambiana mapema ,let say kabla ya kuingia bafuni ili kama mwenzako nae alikua na mipango mingine hata kama haikuhusishi (huhitajiki kujumuika nae) ujue na yeye ajue yako kisha mkubaliane kama kuna cha kukubaliana.

Hata "naenda dukani mara moja", "namuona fulani hapo nje" ni muhimu, you never know what might happen. Unaweza ukakabwa kabari nje au hata ukaanguka mwenzio asijue na wala asiwe na wasiwasi maana anajua utakua jikoni tu au uko humo humo ndani unahangaika na mambo yako.
 
Hapo ni kuetegemeana na hesabu za kapo hiyo
Kama ujuavyo, social life haina marking scheme
Na wala haina formula kwamba tutafuata 'MAGAZIJUTO'

ni convinience ya wawili hao
Mfani kwa mtazamo wangu, sitajali mtu kaaga au hakuaga kama anaondoka ili mradi hajasafiri na simu yake iko ON na ana tabia ya kupokea simu akipigiwa.
 
Kuondoa maswali kama ulienda wapi mbona hujanambia au ujataka twende wote bora uage yaishe.
 
Hapa watu hutofautiana sana katika mahusiano, wengine wanatoa nafasi ya kutotaka kuulizwa ili wawe huru, wengine hupenda kuuliza kama aina fulani ya udhibiti wa nyendo zisizo za lazima.Lakini katika mahusiano ya mke na Mume ni lazima ujue safari za mweza wako na wakati mwingine kunaweza kuwa hamna ulazima wa safari mtu akataka kasafiri.Mimi Binafsi toka yangu nyumbani mara nyingi ina usumbufu, ukitaka kutoka wakati mwingine unaombwa utoke na watoto, ukiuliza unaambiwa na wao watembee kidogo! kweli? kama dukani utasikia kwanini usitume mtoto! Namna hiyo, kwahiyo nimejifunza kuwa ninapokuwa nyumbani My wife wangu hapendi nitoke toke na huwa najitahidi kutokuwa na vijisafari.
 
Sijali wala sichukii kuulizwa,
lakini mimi asiponiaga kwa kweli inakua ngumu kumuelewa.
Sijawahi kuishi pamoja na mwenzi lakini sio sababu ya kutoniaga/kunijulisha safari zako.
 
Kama siishi nae, asiniongezee stress ya kujua safari zake, nami nampunguzia kwa kutomwambia zangu
 
Kama tunaishi pamoja ni vizuri kuagana ila ishu ya kutoa maelezo wala haina umuhimu labda mtuaapende mwenyewe kujieleza alikoenda au anakotaka kwenda,

Km hatuishi pamoja wala sina haja ya kuagwa wala kujua chochote kuhusu safari zake,Ila mie najisikia aman zaidi nikimuaga yeye na kumfahamisha safari zangu au mizunguko yangu,

Labda km anasafiri ni lzm aniage, lkn mizunguko tu ya mjini wala sihitaji kujua as long as kuna mawasiliano likitokea lolote tutafahamishana.
 
Back
Top Bottom