Uchaguzi 2020 Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa, John Pambalu malizana na mawakala wako huko Mwanza hasa hasa wale wa kule Buhongwa

Countrywide

JF-Expert Member
Mar 2, 2015
18,385
27,604
Uchaguzi umekwisha na matokeo yaneshatoka (yawe halali au sio hilo sio dhumuni la post hii).

Lakini kuna maeneo bado kuna manung'uniko makubwa, na hapa ntazungunzia kwa sehemu nilisikia na kuona. Siku moja kabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi nilikuwa Mwanza.

Na nisewe wazi nilijumuika na wana mwanza kwenye kushauriana kupata viongozi bora. Upepo wa John Pambalu ambaye alikuwa anagombea jimbo la nyamagana haukuwa mbaya sana, ila ndio kama tunavyojua mambo ya uchaguzi yalivyo.

Lakini kubwa zaidi lililonisikitisha ni hili la mawakala kutokupata pesa zao baada ya uchaguzi hapa nazungumzia kwa wale ambao nina ushahidi nao, huko kwingine sijui.

John Pambalu nakuomba upokee simu za hawa mawakala na umalizane nao, uwalipe pesa zao maisha yaendelee. Hili jambo linataka kukutia doa, kwa kuwa wapo waliopanga kwenda kulalamika kwa waandishi wa habari.

Lakini pia unaweza puuzia hili jambo na kukanusha na watu wa mitandaoni wakakuelewa, ila wale vijana utawaumiza sana mioyoni mwao kwa kuwa ukweli unaujua.

Ninakuomba sana kwa unyenyekevu mkubwa watafute umalizane nao, najua kwenye kampeni umetumia pesa nyingi lakini jitahidi kuongea nao na kumalizana nao kwa kuwa wale wana ndugu, jamaa na marafiki na wakisikia habari hizi unaweza kupoteza credibility uliyonayo.

Kwa nini nimekuja humu sababu hata simu zao hutaki kupokea na wakipiga kwa katibu wanaishia kuzungushwa tu wanaambiwa warudi kwako, leo ni siku ya 6 na bado muafaka wa pesa zao haujapatikana.

Nawasilisha
 
Uchaguzi umekwisha na matokeo yaneshatoka (yawe halali au sio hilo sio dhumuni la post hii)....
Sasa si ungemtumia tu SMS au email. Pia kuna mitandao mingine, mfano, ungeweza tu kum check huko WhatsApp badala ya kutujazia ujinga humu.
 
Acha hasira kama wengine tunawasemea humu na mambo yanakaa sawa basi hata hili mambo yatakaa sawa tu.
Sms na huko whatsapp hajibu, pengine kwa kuandika humu anaweza kuona aibu na kuwalipa pesa zao
Sasa si ungemtumia tu SMS au email. Pia kuna mitandao mingine, mfano, ungeweza tu kum check huko WhatsApp badala ya kutujazia ujinga humu.
 
Ukituma msg ya malalamiko hayo hajibu.

Humu itaonwa na watu wengi na pengine hao watu wataoona anawasikiliza hivyo inaweza saidia wale vijana kupata haki yao.

Jj mnyika yupo humu, makene yupo humu, na viongozi wengine.

Kama unabisha jaribu kucopy hii habari umtumie uone kama atajibu
Haya uliyoandika humu ungemtumia yeye message.
 
Yeye ndio alikuwa na jukumu la kuwalipa mawakala, wala sio chama. Na ndio alivyowaambia hapo kabla kuwa atawalipa
Sio kosa la Pambalu ni chama hakikua na fedha za ku finance uchaguzi hasa kwa wagombea wapya ambao hawakuwa na viinua mgongo vya ubunge.
 
Napokuona mnafiki ni pale unaposema upepo wa Pambalu "haukuwa mbaya sana" unajaribu kumshusha aonekane alishindwa kihalali, wakati ukweli km uchaguzi ungekuwa huru na haki Pambalu angeshinda kwa kura nyingi sana.

Halafu unakuja na malalamiko feki hapa kumchafua kwanini usimtafute huko jimboni au hamjui anapoishi?! wacha uchawi.
 
Uchaguzi umekwisha na matokeo yaneshatoka (yawe halali au sio hilo sio dhumuni la post hii).

Lakini kuna maeneo bado kuna manung'uniko makubwa, na hapa ntazungunzia kwa sehemu nilisikia na kuona. Siku moja kabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi nilikuwa Mwanza.

Na nisewe wazi nilijumuika na wana mwanza kwenye kushauriana kupata viongozi bora. Upepo wa John Pambalu ambaye alikuwa anagombea jimbo la nyamagana haukuwa mbaya sana, ila ndio kama tunavyojua mambo ya uchaguzi yalivyo.

Lakini kubwa zaidi lililonisikitisha ni hili la mawakala kutokupata pesa zao baada ya uchaguzi hapa nazungumzia kwa wale ambao nina ushahidi nao, huko kwingine sijui.

John Pambalu nakuomba upokee simu za hawa mawakala na umalizane nao, uwalipe pesa zao maisha yaendelee. Hili jambo linataka kukutia doa, kwa kuwa wapo waliopanga kwenda kulalamika kwa waandishi wa habari.

Lakini pia unaweza puuzia hili jambo na kukanusha na watu wa mitandaoni wakakuelewa, ila wale vijana utawaumiza sana mioyoni mwao kwa kuwa ukweli unaujua.

Ninakuomba sana kwa unyenyekevu mkubwa watafute umalizane nao, najua kwenye kampeni umetumia pesa nyingi lakini jitahidi kuongea nao na kumalizana nao kwa kuwa wale wana ndugu, jamaa na marafiki na wakisikia habari hizi unaweza kupoteza credibility uliyonayo.

Kwa nini nimekuja humu sababu hata simu zao hutaki kupokea na wakipiga kwa katibu wanaishia kuzungushwa tu wanaambiwa warudi kwako, leo ni siku ya 6 na bado muafaka wa pesa zao haujapatikana.

Nawasilisha
Mtafuteni Katibu mkuu John Mnyika ndie anashughulikia masuala ya malipo ya mawakala wa CHADEMA, huyo kijana mnamuonea bure
 
Wakati wa kudai katiba mpya pia tutadai ofsi ya msajiri wa vyama ndiyo ishughulikie malipo na uendeshaji wa vyama vyote.

Siyo Kama Sasa baadhi ya viongozi wa vyama wanajipangia tu mishahara minono huku wenye nafasi za chini ndani ya chama wakiambulia kulamba vumbi tu.
Na ukihoji unaambiwa msaliti na kufukuzwa kwenye chama.​
 
Hawa sio ndio wale mawakala walioahidiwa malipo yao yatakua teuzi
Na wao wakaamini kabisa wangekuja kuteuliwa ukurugenzi, ukuu wa wilaya na mikoa🤣🤣🤣🤣
Ila chadema Mungu anawaona na ndio maana wakapata malipo yao tarehe 28
 
Back
Top Bottom