Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,898
- 943
MWENYEKITI CCM (M) MARTHA MLATA KATIKA ZIARA YA RAIS SAMIA MKOA WA SINGIDA
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, Ndugu Martha Mlata ameambatana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ziara ya kukagua miradi na kuzindua miradi mbalimbali ndani ya Mkoa wa Singida
Ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan katika Mkoa wa Singida imeambatana na kuadhimisha miaka 60 ya kuzaliwa kwa Mkoa wa Singida uliozaliwa tarehe 16 Oktoba, 2023 tangu kuanzishwa kwake.
Rais Samia Suluhu Hassan amekagua na kuzindua miradi mbalimbali ya kimaendeleo mkoani Singida ikiwemo Ufunguzi wa Shule ya Msingi Imbele, mabweni ya madarasa ya Shule ya Sekondari Mwanamwema Shein; Kuweka jiwe la Msingi Ujenzi wa Barabara ya kiwango cha Lami kutoka Makongorosi-Rungwa-Noranga-Mkiwa sehemu ya Mkiwa-Itigi-Noranga km 56.9; Ufunguzi wa Jengo la Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Ikungi; Ufunguzi wa Daraja la Msingi lililopo Wilayani Mkalama.
Viongozi mbalimbali wamekula Keki kusherehekea miaka 60 tangu kuanzishwa kwa Mkoa wa Singida katika Uwanja wa Bombadia mkoani Singida leo tarehe 16 Oktoba, 2023 ambapo Mgeni rasmi katika maadhimisho haya ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan
Attachments
-
F8eiZJ9WAAAGZnn.jpg94.2 KB · Views: 4
-
F8hRStyXQAEI_w3.jpg80.4 KB · Views: 3
-
F8fCM0BXwAAUixX.jpg96.3 KB · Views: 3
-
F8kQ0dwWwAAY5XI.jpg265.2 KB · Views: 3
-
F8kQ0d1W0AADYcT.jpg235.3 KB · Views: 4
-
F8kSry0XkAASN6l.jpg97.2 KB · Views: 1
-
F8kDEESWYAA__FQ.jpg60.6 KB · Views: 2
-
F8jgc2nW8AAaEDQ.jpg85 KB · Views: 4