Mwanza: Nimekutana na handsome balaa

Ironbutterfly

JF-Expert Member
Feb 5, 2023
3,044
8,165
Habari za asubuh wana ukumbi,

Mweh mweh mweh, nimeingia Mwanza juzi kikazi nikatimiza majukumu yangu. Nilipomaliza nikasema nikamwone kijana wangu anaishi Bwiru hapo kwa matajiri (kwa wakwe zangu).

Nikaishia ATM nitoe kasalio halafu nipande boda nimfate shule twende home, wakati naifata ATM nikapita sehemu jirani na mama ntilie mmoja, nikapiga jicho, nikamwona kijana shababi anakula ugali-mbogamboga, aliponiona akaniita we sista njoo, nikamwambia eeh, akanambia njoo, nikasema haya👌.

Nikaenda akanambia waitwa nani? Nikamjibu siongeagi na waume za watu, akanambia mi bachelor, nikamjibu ok ila mie siko singo, akasema usijali, waenda wapi? Nikamjibu namfata mtoto hapo shule niende naye nyumbani, ndio nimedondoka Nyegezi hapo.

Akasema ok nipe no yako, nikamwambia sitoi no kwa strangers, akachukua simu yangu akajibip, akanambia baada ya lisaa ntakuchek mchumba! Lol nikacheka nikaondoka zangu kuendelea na ratiba.

Nikampokea mwanangu, nikamfikisha home, nafika tu nasalimiana na baba mkwe, jamaa anapiga, nikaomba udhuru nikatoka nje, then nikapokea simu yake, akanambia ushampokea mtoto, nikamjibu yap na niko home, akanambia kamilisha ratiba afu unambie, akakata simu.

Sikumtafuta maana niko ukweni, kapigaa weeh sijapokea ila nimemwelewa, kumbe kuna Wasukuma mahandsome lol.🤣

Sema kutoka kipengele maana niko ukweni, natamani kukipambazuka nitunge safari nionane naye, anaonekana mtamu kwa bed au nitakuwa nazingua wana ukumbi?
 
Back
Top Bottom