DOKEZO Mwanza ni Jiji la pili kwa ukubwa na wingi wa watu lakin Barabara ya Kenyatta ni mbovu na haina hadhi kabisa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

KONK MASTER

JF-Expert Member
Jan 31, 2023
1,225
511
Ninamasikitiko sana ingawa Mwanza ni Jiji la pili baada ya Dar lakini barabara ya Kenyata ni mbovu sana kuliko barabara zote kuu za Tanzania.

Serikali inatakiwa iiangalie hii barabara kwa jicho la kipekee, barabara inatakiwa ifumuliwe yote kuanzia Mwanza mjini hadi Shinyanga boarder km 104 na iijenge upya kabisa kwa viwango vikubwa.

Inatakiwa ijengwe njia sita kutoka mjini hadi Usagara, njia nne Usagara had Mwanangwa - Misungwi kupunguza foleni kubwa iliyopo na ambayo itakuja baada ya kukamilika kwa daraja la JPM.

Pia barabara za mitaa Nyegezi ni mbovu kweli hata gari kuendesha unapata shida kwani ni kweli viongozi hamlioni hili?

Barabara iendayo machinjioni ni huzuni sana na inamfikirisha kwa kuona barabara inayoelekea machinjio ya Jiji lakini imejaa makorongo na viongozi wanapita tu wala hawajali kabisa, miaka kadhaa haijengwi kwa lami wakati ni fupi kama mita 400.

Barabara ya Kishiri ni mbovu mno, sometime mvua zikizidi hatupati huduma ya magari maana barabara haipitiki na viongozi mpo tu.

Naomba viongozi mtekeleze hili maana najua mnajua sana na mnatupuuza kama vile hatulipi Kodi. 🧐
 
Shinyanga road iyo,ipo kwenye mpango wa upanuzi lakini mpaka sasa naona kimya kingi.

mradi wa maji Sahwa ya chini mbunge Mabula alisema utaanza kazi January mwaka huu lakini kimya.

stendi mpya nyegezi imekwisha ka barabara kafupi sana kakuingia ndani ya stendi sijui katamaliza mwaka ndo stendi ifunguliwe,sijui!

uwanja mpya wa ndege imekua story miaka nenda miaka rudi,how!
 
Shinyanga road iyo,ipo kwenye mpango wa upanuzi lakini mpaka sasa naona kimya kingi.

mradi wa maji Sahwa ya chini mbunge Mabula alisema utaanza kazi January mwaka huu lakini kimya.

stendi mpya nyegezi imekwisha ka barabara kafupi sana kakuingia ndani ya stendi sijui katamaliza mwaka ndo stendi ifunguliwe,sijui!

uwanja mpya wa ndege imekua story miaka nenda miaka rudi,how!
Yaaan uhuni na usanii mwingi lakin mbona dsm wakikohoa TU tayr washapewa bajet ila sisi tukiomna utaskia mradi upo katka feasibility study Leo miaka Saba na huku tunatoa Kodi tena zaidi Sasa si Bora kama hawawez iwepo serikali ya majimbo this is madness
 
Back
Top Bottom