Elections 2010 Mwanasheria Mkuu aiburuta Chadema kwa NEC

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,174
Katika hali ambayo yaonyesha Mwanasheria Mkuu ni kibaraka wa mwajiri wake JK na CCM yake ameona ni sahihi kabisa kutochunguza matukio yote ya uvunjaji sheria za uchaguzi lakini kuichafua Chadema kwa kauli za uchochezi na kusababisha vurugu kwenye kampeni!

Mwanasheria Mkuu angelikuwa ana busara angelijua ya kuwa NEC yenyewe haina ubavu wa kusimamia sheria ya uchaguzi kama jana ilivyojigonga kwa CCM na kuionya tu kwa mikutano yake kuzidi muda uliopangwa.

Ni dhahiri NEC hiyohiyo itakuwa na wakati mgumu kuichukulia Chadema hatua yoyote hata kama wakiona ina makosa kwa kuelewa adhabu walioipa CCM ilikuwa ya onyo tu na kwa kufahamu CCM ndiyo mhimili mkuu wa vurugu na matusi kwenye kampeni hizi
 
Ruta;

Post yako haina details za kwa nini Mwanasheria Mkuu anaishtaki CHADEMA NEC. Au ulikuwa una maana CCM ndo imeshtaki? Au Mwanasheria kaishtaki Mahakamani?
 
na bado.. wiki hizi mbili zilizobakia mtaona watu wanatiwa pingu.. ukishindwa hoja tumia vitisho..!!! Wakati huu ndio bendera za Chadema zinahitaji kupatikana kwa wingi kuonesha defiance!!!
 
Katika hali ambayo yaonyesha Mwanasheria Mkuu ni kibaraka wa mwajiri wake JK na CCM yake ameona ni sahihi kabisa kutochunguza matukio yote ya uvunjaji sheria za uchaguzi lakini kuichafua Chadema kwa kauli za uchochezi na kusababisha vurugu kwenye kampeni!

Mwanasheria Mkuu angelikuwa ana busara angelijua ya kuwa NEC yenyewe haina ubavu wa kusimamia sheria ya uchaguzi kama jana ilivyojigonga kwa CCM na kuionya tu kwa mikutano yake kuzidi muda uliopangwa.

Ni dhahiri NEC hiyohiyo itakuwa na wakati mgumu kuichukulia Chadema hatua yoyote hata kama wakiona ina makosa kwa kuelewa adhabu walioipa CCM ilikuwa ya onyo tu na kwa kufahamu CCM ndiyo mhimili mkuu wa vurugu na matusi kwenye kampeni hizi

Kwa kawaida wewe ni mwandishi mzuri sana, lkn hapa umechemsha maana heading na content haviendani
 
*

Mwanasheria Mkuu ajitosa

?

Oktoba 13, 2010

?

Mwandishi Wetu




MGOMBEA Urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, wameshitakiwa wakidaiwa kufanya uchochezi kwa kutoa kauli za kuishutumu Serikali kuhusika kukibeba Chama Cha Mapinduzi (CCM), Raia Mwema, limebaini.

Habari zilizothibitishwa na CHADEMA zimeeleza kwamba, Dk. Slaa na Mbowe wameshitakiwa kwenye Kamati ya Maadili ya Taifa, chini ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), wakidaiwa kutoa kauli zinazoitwa za uongo kwa nia ya kusababisha chuki dhidi ya serikali.

Mwenyekiti wa Kampeni za CHADEMA, Profesa Mwesiga Baregu, amelithibitishia Raia Mwema kwamba tayari wanasheria wa chama hicho wanalifanyia kazi suala hilo kabla ya kujibu tuhuma zilizoelekezwa kwa viongozi hao.

Habari zilizolifikia gazeti hili zinaeleza hoja zilizotumiwa na Serikali ‘kuwashitaki’ viongozi hao wa CHADEMA ni viongozi wao kutoa lugha za uzushi, uongo na zenye mwelekeo wa kuchochea chuki dhidi ya Serikali na Taifa.

Viongozi hao wanatuhumiwa kutoa kauli hizo za uchochezi katika mkutano wao na vyombo vya habari katika ofisi za CHADEMA, Kinondoni Septemba 28, mwaka huu na kuripotiwa na vyombo vya habari.

Tuhuma ambazo zinaelezwa kutolewa na Dk. Slaa na Mbowe na ambazo Serikali imezieleza kwamba ni za uongo na zenye kuhatarisha amani ni pamoja na madai kwamba Serikali imewatuma na kuwasambaza nchi nzima maofisa wa Usalama wa Taifa ili kuhakikisha kuwa mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete anashinda.

Katika maelezo yao viongozi hao wa CHADEMA walidai kwamba wanao waraka waliodai kuwa umeandikwa na Serikali na kupelekwa kwa Wakuu wa Usalama wa Taifa wa Mikoa yote, Wakuu wa Mikoa yote, Wakuu wa wilaya zote na Wakurugenzi Watendaji wa Wilaya zote nchini wakielekezwa kuhakikisha CCM inashinda kwa gharama zozote.

Tuhuma nyingine ambazo zimeelekezwa kwa Serikali zilizoripotiwa na vyombo vya habari ni kwamba Serikali imetuma maofisa wake nje ya nchi kuchapisha karatasi za kupigia kura ambazo ni nje ya zile zilizoandaliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Katika maelezo yake Serikali imekanusha tuhuma hizo ikisema kwamba hazina ukweli wowote na viongozi wa chama hicho wanatakiwa kutoa uthibitisho (kama kweli wanao) la sivyo hatua stahili zichukuliwe dhidi yao.

Akizungumzia mashitaka hayo ya Serikali, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema wiki hii hakutaka kwenda katika undani akisema ni busara zaidi kuacha mamlaka zilizoandikiwa barua hiyo kutimiza wajibu wake.

Katika mazungumzo hayo Jaji Werema alisema; “Ni vizuri ukawauliza vyombo vilivyofikishiwa hayo malalamiko. Mimi na wewe (mwandishi) lengo letu ni kuendelea kuwa na nia nzuri na nchi yetu. Natumaini hata Watanzania karibu wote wana nia hiyo. Kwa hiyo kama malalamiko yamewasilishwa naamini wahusika watapewa fursa ya kujibu.”

Uchunguzi zaidi unabainisha kuwa barua ya mashitaka hayo iliandikwa Septemba 30, mwaka huu na ikawasilishwa Tume Oktoba mosi, mwaka huu.

Hata hivyo, licha ya barua hiyo kufikishwa tume Oktoba mosi, ilichukua siku takriban saba kuifikisha kamati ya maadili.

Inadaiwa kuwa barua hiyo ilifikishwa hapo Oktoba 8, mwaka huu na baadhi ya wajumbe wamekuwa wakihoji sababu za kukwama au kukwamishwa barua hiyo kufika sehemu iliyokusudiwa kwa wiki nzima.

Kwa mujibu wa kanuni za kamati hiyo ya maadili mtu au chama kinachotuhumiwa au kulalamikiwa kinapaswa kuandikiwa barua rasmi na kutakiwa kutoa majibu ndani ya saa 48.

Raia Mwema ilizungumza pia na Kaimu Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika, ambaye pia ni mgombea ubunge kwa tiketi ya chama hicho Jimbo la Ubungo, ambaye alisema bado chama chake hakijafikishwa rasmi malalamiko husika.

“Kanuni zinataka anayelalamikiwa kuletewa malalamiko hayo rasmi na kuyajibu ndani ya saa 48. Kama hayo malalamiko yapo hayajatufikia rasmi kama taasisi. Ni kweli tunaye mjumbe wetu kama ilivyo vyama vingine kwenye kamati hiyo lakini huyu siye anayelalamikiwa.

“Wanaostahili kufikishiwa malalamiko ni wahusika moja kwa moja au chama kama ndicho kinalalamikiwa. Hata hivyo, binafsi kwa niaba ya chama nimechukua hatua za tahadhari, nimeandikia barua kwenda Tume ya Taifa ya Uchaguzi kujua rasmi masuala haya.

“Kama kweli watatuandikia kulalamika basi nasi tuko tayari kujibu kwa mujibu wa kanuni. Na hapa ukweli ni kwamba hiki wanachozungumza kinafanyika na kutolewa matamko baada ya kufanyika upotoshaji wa makusudi.

“Yaani watu wamekaa wakafanya upotoshaji, na matamko yakatolewa juu ya msingi wa upotoshaji. Ukweli ni kwamba, watu wanahangaika kufanyia kazi upotoshaji wa makusudi,” alisema Mnyika.

Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Rajabu Kiravu, naye alishindwa kuzungumzia suala hili akieleza kuwapo katika kikao.

Tathmini ya hivi karibuni ya kampeni za Uchaguzi Mkuu zinabainisha kuwa CHADEMA kwa sasa ndicho chama kinachoonekana kutoa changamoto kubwa ya kisiasa dhidi ya chama tawala-CCM, ikielezwa kuwa mgombea wake, Dk. Willibrod Slaa ndiye kinara wa changamoto hizo.

Source: Raia Mwema - Muungwana ni Vitendo, Mwanasheria Mkuu ajitosa
?
 
Sasa kule Hai na Tarime mbona CCM waliamua kuact kabisa kwa kumwaga damu.
Uyu nae kibaraka tuu hana lolote.
Mwaka huu CCM mtabana mtaachia
 
Mimi ninachoona hapa ni porojo za kuchafuana ambazo hazina wa msingi wowote. Maana kama kuna msingi wa kulaumu/kutuhumu sidhani kama hawa mabwana wangesubiri muda woote huo bila kuyafanyia kazi malalamiko yao. Hivyo basi inatupasa kuliangalia hili kwa jicho la uchonganishi zaidi kuliko hivi lilivyowekwa, maana sidhani kama kuna busara inayohitajika kuliona hili la kuleta tuhuma zisizo msingi mbele ya tume ambayo nayo kwa woga wake baada ya kukosa uhalisia/uzito ama ushahidi wa kutosha wakashindwa kulitupilia mbali.

TUFUNGUKE MACHO SASA
 
CHURA ANAPENDA MAJI.....LAKINI SIYO YA MOTO. (Mwenye akili aelewe)
 
ninyi hamjui kwa nini serikali iliamua kukata rufaa dhidi ya mgombea binafsi? Ni serikali hiyohiyo ambayo inaongozwa na chama tawala imeonesha ukiukwaji mkubwa wa kusimamia maadili ya uchaguzi kwa kuruhusu matukio ya kifisadi na matendo ya kishetani ya wafuasi wa ccm na pia wameshindwa kumwondoa kikwete kwenye kinyang'anyiro kwa kuvunja mara kadhaa sheria alizosaini yeye mwenyewe.

Serikali ndiyo iliyoibiwa fedha kwenye akaunti za EPA na ikafunga bakuli mpaka wasio serikalini walipoamua KUROPOKA ukweli. je niamini kwamba serikali inajifitini yenyewe? hakina ufalme unaojifitini hautasimama kamwe.

AG ni mtumishi wa serikali mwenye utashi wa kisiasa ndo maana post yake haithibitishwi na bunge bali only aliyemteua. na kama mjuavyo
 
Ruta;

Post yako haina details za kwa nini Mwanasheria Mkuu anaishtaki CHADEMA NEC. Au ulikuwa una maana CCM ndo imeshtaki? Au Mwanasheria kaishtaki Mahakamani?

Kwenye Magazeti ya leo ipo hii habari. hata kwenye hiyo taarifa iliyotolewa na NEC hawaelezea details.
Hii ni propaganda na ni mchoro umbao umeshachongwa ili kuichafua CHADEMA. Both NEC na Mwanasheria Mkuu wanahusika. Wameshindwa kusema ni kwa jinsi gani CHADEMA wametishia uvunjifu wa Amani. Je hadi sasa ni nani aliyevunja amani kama sio CCM? Je viongozi wa CCM wanaposema LAZIMA washinde uchaguzi sio uvunjifu wa Amani? na Je Mwanasheria mkuu ana madaraka gani juu ya kauli za wanasiasa kama sio kujipendekeza?
Ni dhahiri sasa kuwa kuingoa CCM madaraka ni kazi kubwa sana, mana vyombo vyote viko wazi kwa Upendeleo.
Mi naona kabisa NEC waliitisha kikao na waandishi wa habari sio kutoa ufafanuzi wa mambo ya kampeni, bali walitaka tu kuiweka hiyo issue ili kuichafua CHADEMA! kwa nini hawakuongelea vurugu wanazofanya CCM?
 
Kwenye Magazeti ya leo ipo hii habari. hata kwenye hiyo taarifa iliyotolewa na NEC hawaelezea details.
Hii ni propaganda na ni mchoro umbao umeshachongwa ili kuichafua CHADEMA. Both NEC na Mwanasheria Mkuu wanahusika. Wameshindwa kusema ni kwa jinsi gani CHADEMA wametishia uvunjifu wa Amani. Je hadi sasa ni nani aliyevunja amani kama sio CCM? Je viongozi wa CCM wanaposema LAZIMA washinde uchaguzi sio uvunjifu wa Amani? na Je Mwanasheria mkuu ana madaraka gani juu ya kauli za wanasiasa kama sio kujipendekeza?
Ni dhahiri sasa kuwa kuingoa CCM madaraka ni kazi kubwa sana, mana vyombo vyote viko wazi kwa Upendeleo.
Mi naona kabisa NEC waliitisha kikao na waandishi wa habari sio kutoa ufafanuzi wa mambo ya kampeni, bali walitaka tu kuiweka hiyo issue ili kuichafua CHADEMA! kwa nini hawakuongelea vurugu wanazofanya CCM?
AG na Makame wapo ofisini wakisubiri kuambiwa cha kufanya. hawana jipya hao

 
AG Werema ni mwanachama wa CCM, kama Alivyokuwa Andrew Chenge - MZee wa Vijisenti na Ajali za kugonga pikipiki!!!

Andrew Chenge alikuwa mwanasheria wa Serikali na hapo hapo mwanachama wa CCM, ndo maana akaja kugombea ubunge kwa ticketi ya CCM.

Nimesoma Habari yote, AG anataka CHADEMA wapeleke ushahidi kuwa UWT na Wakuu wa mikoa/wilaya wameagizwa na JK wahakikishe kuwa CCM ishinde kwa gharama yoyote.

Huo waraka kwenda kwa wakuu wa Mikoa/Wilaya hata kama CHADEMA wana Nakala, wasiupeleke NEC.

Kama CHADEMA wakiamua kupeleka Ushahidi, wapeleke kwa Masharti yafuatatayo.

-Ikidhibitika ni Ukweli waraka umesambazwa, NEC na AG wajiuzulu.

AG na NEC wakubali kwa maandishi kuwa Chadema ikipeleka nakala ya Waraka, Watajiuzulu. Vinginevyo Wao AG na NEC watafute Ushahidi wao wenyewe.

AG na NEC wana uwezo wa kuhoji UWT na Wakuu wa Mikoa/Wilaya.

Kwa hiyo Chadema tuwe strong tafadhali. Tusitoe document kirahisi
 
Back
Top Bottom