Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Katika hali ambayo yaonyesha Mwanasheria Mkuu ni kibaraka wa mwajiri wake JK na CCM yake ameona ni sahihi kabisa kutochunguza matukio yote ya uvunjaji sheria za uchaguzi lakini kuichafua Chadema kwa kauli za uchochezi na kusababisha vurugu kwenye kampeni!
Mwanasheria Mkuu angelikuwa ana busara angelijua ya kuwa NEC yenyewe haina ubavu wa kusimamia sheria ya uchaguzi kama jana ilivyojigonga kwa CCM na kuionya tu kwa mikutano yake kuzidi muda uliopangwa.
Ni dhahiri NEC hiyohiyo itakuwa na wakati mgumu kuichukulia Chadema hatua yoyote hata kama wakiona ina makosa kwa kuelewa adhabu walioipa CCM ilikuwa ya onyo tu na kwa kufahamu CCM ndiyo mhimili mkuu wa vurugu na matusi kwenye kampeni hizi
Mwanasheria Mkuu angelikuwa ana busara angelijua ya kuwa NEC yenyewe haina ubavu wa kusimamia sheria ya uchaguzi kama jana ilivyojigonga kwa CCM na kuionya tu kwa mikutano yake kuzidi muda uliopangwa.
Ni dhahiri NEC hiyohiyo itakuwa na wakati mgumu kuichukulia Chadema hatua yoyote hata kama wakiona ina makosa kwa kuelewa adhabu walioipa CCM ilikuwa ya onyo tu na kwa kufahamu CCM ndiyo mhimili mkuu wa vurugu na matusi kwenye kampeni hizi