Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,811
- 15,404
Kuachwa huwa kunauma sana, na hasa inapotokea uliyeachana naye ulizaa naye, na hapo ndipo unapojikuta ukilazimika kuwa na mawasiliano na bwana huyo kwa takriban miaka 18 hivi.
Hebu tuchukulie hujapata mwenza na huyo mpenzi wako amekwishaoa. Je Utayachukuliaje mafanikio ya huyo mzazi mwenzako katika maisha yake ya ndoa ……………..?
Je wewe ni aina ya wanawake ambao humudu kujenga uhusiano bora na bwana aliyeachana naye bila kuathiri maisha yake ya ndoa na mwenzi wake au ni aina ya wanawake ambao hutafuta kila namna kwa mawio na machweo ili kuhakikisha wanavuruga ndoa ya bwana waliyeachana ili kumkomesha………….?