Mwanamke huyu anadaiwa kuwa nyuma ya mafanikio ya Dokta Cheni

Nifah

JF-Expert Member
Feb 12, 2014
31,531
65,303
IMG_4480.jpeg


Mafanikio ni mafanikio, haijalishi njia zilizotumika kuyafikia… mwisho yataitwa mafanikio bila kujali kama ni kwa njia halali au kupitia njia haramu.
Na daima mafanikio hutukuzwa, na waliofanikiwa hupewa heshima!

Muigizaji mkongwe, mfanyabiashara na mshereheshaji maarufu Mahsein Awadhi ‘Dr. Cheni ’ yeye mafanikio yake yamepitia kwa mwanamke, ndio vijana huita 'mishangazi '!

Si huwa wanasema mwanaume aliyefanikiwa nyuma yake kuna mwanamke? Ndivyo ilivyokuwa kwa Dr. Cheni… mwanamke aliyekuwa katika mafaniko yake sio mwanamke wa mchezo mchezo, ni mwanamke wa shoka kwelikweli!
Ukisikia mabalaa yake utabaki mdomo wazi, sio mwanamke, ni chuma!

NI SALMA MTAMBO!

96d08adf-01d6-4150-909a-2b66c300861a.jpeg

Bibie Salma Mtambo ni tapeli wa kupindukia. Akitapeli vijana kwa wazee, wanaume kwa wanawake.
Utapeli wa magari na kughushi nyaraka kwake ni jambo dogo na la kawaida kama kufumba na kufumbua macho!

Licha ya yote hayo, hakuna mkate mgumu mbele ya chai!
Bibie alikufa na kuoza kwa Dr. Cheni! Nini hakumpa Dr. Cheni? Mapenzi alimpa na mtaji wa biashara ya magari ambayo imemtajirisha sana Dr. Cheni alimpa yeye!
Kifedha na kwa kumpa baadhi ya magari yake mengi yaliyopatikana katika utapeli wake aanzie biashara hiyo.

Licha ya tofauti kubwa iliyokuwepo baina yao kiumri, haikuweza kuzuia mapenzi hayo mazito baina yao.
Kila mmoja akinufaika kwa namna yake, kimapenzi na kifedha!
Mapenzi yao yalikuwa mazito na yaliyojaa kufuru ya hela kutokana na utajiri wa kupindukia wa Salma!

ZA MWIZI AROBAINI…
Hakuna marefu yasiyo na ncha! Penzi la Dr. Cheni na ‘rich auntie’ Salma liliingia mdudu mara baada ya mfululizo wa kesi zilizomuandama Salma kutokana na ‘mission’ zake zilizomuweka mjini na kumpa heshima kubwa kutokana na ukwasi aliokuwa akiumiliki.

Ifahamike kwamba, utapeli wa Salma ulianzia miaka ya 90! Hivyo alikuwa na ‘Misala’ kibao!

Tamati ilifikia September 18 mwaka 2019 alipohukumiwa miaka 99 jela baada ya kupatikana na hatia katika mashtaka 17 ikiwemo kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu!

SALMA ALIA GEREZANI!
Baada ya Salma kupewa hukumu hiyo Dr. Cheni alipotelea kusikojulikana na Salma! Hakuwahi kuonekana kokote wala kumtembelea gerezani!

Salma anaumia zaidi kwa kuona kijana aliyempenda kwa moyo wote na kumpa kila kitu ikiwemo kushiriki katika ujenzi wa jumba la kifahari la Dr. Cheni akimtelekeza wakati alipokumbwa na matatizo!

Lakini, kesi za Salma ni mbaya na ni hatari zaidi kwa mtu maarufu na sasa mfanyabiashara mkubwa kujihusisha nae moja kwa moja.
Pengine ndio maana Dr. Cheni ameamua ‘kula kona’.

Hivyo basi, kama ilivyo ada ya muosha huoshwa na mshahara wa dhambi ni mauti… ndiyo yanayomsibu Salma! Anachuma aliyoyapanda kwa dhulma!

Ni yuleyule ripota kutokea JF mwenye chanzo chake nyeti…

Nawatakia sikukuu njema ya Krismasi,

Nifah

Nimeambatanisha baadhi ya nyaraka za kesi zilizokuwa zikimkabili Salma Mtambo.

Screenshot 2023-12-25 at 07.17.54.png

Screenshot 2023-12-25 at 07.18.43.png


Na hii

Screenshot 2023-12-25 at 07.15.11.png

Screenshot 2023-12-25 at 07.16.06.png
 

Attachments

  • Asha Mwinyimvua vs Salama Issa Mtambo (PC Civil Appeal 49 of 2010) 2010 TZHC 2 (16 September 2...pdf
    237.5 KB · Views: 7
  • Zahoro Salum Zahoro vs Salma Issa Mtambo (Being The Administratrix of the Estate of the Late K...pdf
    862.6 KB · Views: 4
Ila Dr cheni alikuwa ameshajipata zamani.

Miaka ya 2010 mpaka 2017. Dr cheni ndie alikuwa Mc namba moja Tanzania kwa kupata kazi nyingi.. Mc Garab ndie aliekuja kumpora Dr Cheni hiyo nafasi mwaka 2017.

Swala la kipato cha milioni 20 kwa mwezi. DR cheni amepata zamani sana kwenye dili zake tu za u mc

DR cheni ameanza kujipata zamani sana kiuchumi. Amepiga sana hela kwenye U MC.

Kama instagram isingeruhusu kupost Video. Mpaka leo Garab mwenyewe angekuwa bado nyuma ya Dr cheni.

Garab kajua kuitumia instagram ilivyoruhusu video kwa kucheza na video nzuri za matukio ya harusi yake. Wakati huo Dr cheni amelalala anafanya kazi kwa mazoea anaiona insta ya watoto
 
View attachment 2851623

Mafanikio ni mafanikio, haijalishi njia zilizotumika kuyafikia… mwisho yataitwa mafanikio bila kujali kama ni kwa njia halali au kupitia njia haramu.
Na daima mafanikio hutukuzwa, na waliofanikiwa hupewa heshima!

Muigizaji mkongwe, mfanyabiashara na mshereheshaji maarufu Mahsein Awadhi ‘Dr. Cheni’ yeye mafanikio yake yamepitia kwa mwanamke, ndio vijana huita mishangazi!

Si huwa wanasema mwanaume aliyefanikiwa nyuma yake kuna mwanamke? Ndivyo ilivyokuwa kwa Dr. Cheni… mwanamke aliyekuwa katika mafaniko yake sio mwanamke wa mchezo mchezo, ni mwanamke wa shoka kwelikweli!
Ukisikia mabalaa yake utabaki mdomo wazi, sio mwanamke, ni chuma!

NI SALMA MTAMBO!

View attachment 2851628
Bibie Salma Mtambo ni tapeli wa kupindukia. Akitapeli vijana kwa wazee, wanaume kwa wanawake.
Utapeli wa magari na kughushi nyaraka kwake ni jambo dogo na la kawaida kama kufumba na kufumbua macho!

Licha ya yote hayo, hakuna mkate mgumu mbele ya chai!
Bibie alikufa na kuoza kwa Dr. Cheni! Nini hakumpa Dr. Cheni? Mapenzi alimpa na mtaji wa biashara ya magari ambayo imemtajirisha sana Dr. Cheni alimpa yeye!
Kifedha na kwa kumpa baadhi ya magari yake mengi yaliyopatikana katika utapeli wake aanzie biashara hiyo.

Licha ya tofauti kubwa iliyokuwepo baina yao kiumri, haikuweza kuzuia mapenzi hayo mazito baina yao.
Kila mmoja akinufaika kwa namna yake, kimapenzi na kifedha!
Mapenzi yao yalikuwa mazito na yaliyojaa kufuru ya hela kutokana na utajiri wa kupindukia wa Salma!

ZA MWIZI AROBAINI…
Hakuna marefu yasiyo na ncha! Penzi la Dr. Cheni na ‘rich auntie’ Salma liliingia mdudu mara baada ya mfululizo wa kesi zilizomuandama Salma kutokana na ‘mission’ zake zilizomuweka mjini na kumpa heshima kubwa kutokana na ukwasi aliokuwa akiumiliki.

Ifahamike kwamba, utapeli wa Salma ulianzia miaka ya 90! Hivyo alikuwa na ‘Misala’ kibao!

Tamati ilifikia September 18 mwaka 2019 alipohukumiwa miaka 99 jela baada ya kupatikana na hatia katika mashtaka 17 ikiwemo kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu!

SALMA ALIA GEREZANI!
Baada ya Salma kupewa hukumu hiyo Dr. Cheni alipotelea kusikojulikana na Salma! Hakuwahi kuonekana kokote wala kumtembelea gerezani!

Salma anaumia zaidi kwa kuona kijana aliyempenda kwa moyo wote na kumpa kila kitu ikiwemo kushiriki katika ujenzi wa jumba la kifahari la Dr. Cheni akimtelekeza wakati alipokumbwa na matatizo!

Lakini, kesi za Salma ni mbaya na ni hatari zaidi kwa mtu maarufu na sasa mfanyabiashara mkubwa kujihusisha nae moja kwa moja.
Pengine ndio maana Dr. Cheni ameamua ‘kula kona’.

Lakini, kama ilivyo ada ya muosha huoshwa na mshahara wa dhambi ni mauti… ndiyo yanayomsibu Salma!

Ni yuleyule ripota kutokea JF mwenye chanzo chake nyeti…

Nawatakia sikukuu njema ya Krismasi,

Nifah
KUNA KITU NITACHANGIA ILA NITATUMIA CODE......
BAADAE KIDOGO 🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom