Mwaka 1995 Nyerere alitabiri kuanguka kwa CCM!

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,174

Kwenye Mkutano Mkuu wa CCM wa mwaka 1995 wa kumpitisha Mkapa kugombea uraisi, Nyerere alisema haya ambayo leo ninaona ni kero kwangu sijui kwenu na wala sikubaliani naye kwenye hilo hata kidogo.

Alisemaje? Hapa ninamnukuu:-

Kiongozi anaweza kutoka popote pale lakini kiongozi bora wa kutumainiwa na taifa atatoka ndani ya CCM.

Mimi sikubaliani naye kwa sababu nimemwona JK jinsi ambavyo yupo beneti na mafisadi na anakula nao sahani moja na ndiyo maana na hata Bw. Kifimbo hapo nionavyo alichemsha.

Lakini Nyerere ana busara sana kwenye hotuba hiyo hiyo alinena yafuatayo ambayo yanagusa sasa kudondoka kwa JK na timu yake ya watafunaji wa fedha za umma. Na ninamnukuu:-

Watanzania wakikosa uongozi bora ndani ya CCM watautafuta nje ya CCM..

Si sasa yametimia………………….GO DR. SLAA...GO TO STATE HOUSE
 

Kwenye Mkutano Mkuu wa CCM wa mwaka 1995 wa kumpitisha Mkapa kugombea uraisi, Nyerere alisema haya ambayo leo ninaona ni kero kwangu sijui kwenu na wala sikubaliani naye kwenye hilo hata kidogo.

Alisemaje? Hapa ninamnukuu:-



Mimi sikubaliani naye kwa sababu nimemwona JK jinsi ambavyo yupo beneti na mafisadi na anakula nao sahani moja na ndiyo maana na hata Bw. Kifimbo hapo nionavyo alichemsha.

Lakini Nyerere ana busara sana kwenye hotuba hiyo hiyo alinena yafuatayo ambayo yanagusa sasa kudondoka kwa JK na timu yake ya watafunaji wa fedha za umma. Na ninamnukuu:-


Si sasa yametimia………………….GO DR. SLAA...GO TO STATE HOUSE


Kwa wakati huo naweza sema walikuwepo lakini wakati huu ambao hata yeye Mwl.Nyerere hayupo hao viongozi ni watapingwa kwa hali na mali kuhakikisha wasiwepo hata kwenye safu ya uongozi ni wachache kama wakina maghufuli hata ukiwapa wizara gana atarudi pale pale hatelemki bali una mpandisha nadhani this time magufuli awe waziri wa maliasili na utarii mwone hata kakakuona watajulikana ni wangapi na hiyo barabara haitopita huko mbugani


Kumpata kiongozi nje ya CCM lawezekana kabisa ila hao walioko ndani ya system na CCM wao lao ni mmoja katu hawatokubali hiyo hali iwatokee kwanini wanajua watahadhilika huko mbeleni na tena kwa pilato na ndio maana hata jeshi lina toa tamko hii inamaanisha kuwa viongozi waliopo ni kuwa hawakubaliki na watanzania kwa nini hilo wasilione kwanini waweke vitisho na asilimia kubwa ni CCM wao kwa wao ndio wanaopisha huko majimboni na ndio wanao jua mfumo mzima wa kuhesabu kura then wanajua mchezo mchafu unavyo chezwa leo hii Jeshi mwaingizwa huku kwenye siasa na mwakubali maficha nini huko kwenye siasa??

 
Jethro hukumu ya safari hii twaitoa kwa Kikwete na vibaraka wake wote. CCM twahitaji ijijenge upya, ikiwaondoa wote ofcourse we includes hao wanajeshi. Hatujali nani alikuwa nani tunajali mabadiliko tu. Mabadiliko ni lazima hakuna kurudi nyuma.
CHAGUA CHADEMA KWA MAENDELEO YA NCHI HII. CHAGUA DR SLAA AENDE IKULU
 
Hata hao wanajeshi wana kashfa ya meremeta ndo maana wanaanza kuogopa jamaa akichukua nchi itakuwaje
 
JK, & SHIMBO. Nchi Hii sio ya kwenu. Wala nyie sio Miungu wa Tanzania kwanza hamna ubavu wa kumwaga damu yetu kunguru wakubwa nyie, Mtatoka kwa sanduku la Kura. Jeuri ya kupambana na Watanzania 40,000,000 Hmna. Mnaturingishia Amani ya Kinafki, ni sisi wenyewe ambao tumeamua kutulia kwa amani ila ninyi hakuna chochote ambacho mmeleta zaidi ya madudu. Kwanza mna nini cha ajabu ambacho hapa duniani hatujawai kukiona labda tuwaogope. Kwa Taarifa yenu na familia zenu Ikifika 31/10 Hamtaamini macho na masikio yenu.
 
Nyerere pia alisema yafuatayo katika kitabu chake cha Uongozi wa Tanzania:

Nilisema awali kwamba kansa ya uongozi ndani ya Chama cha Mapinduzi isingekuwa ni jambo la kutisha sana kama tungekuwa tumeanza kuona Chama kizuri cha upinzani kinachoweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM. Ubovu wa uongozi ndani ya CCM ndio uliofanya nikapendekeza tuanzishe mfumo wa Vyama Vingi. Nilitumaini kuwa tunaweza kupata Chama kingine kizuri ambacho kingeweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM; au ambacho kingekilazimisha Chama cha Mapinduzi kusafisha uongozi wake, kwa kuhofia kuwa bila kufanya hivyo kitashindwa katika uchaguzi ujao. Lakini bado sijakiona Chama makini cha upinzani; na wala dalili zo zote za kuondoa kansa ya uongozi ndani ya CCM. Bila upinzani mzuri wa nje, na bila demokrasia halisi ndani ya Chama cha Mapinduzi, Chama hiki kitazidi kudidimia chini ya uzito wa uongozi mbovu. Kwa hali yetu ya kisiasa ilivyo nchini hili si jambo la kutarajia bila hofu na wasi wasi! (Ukurasa 66)
 
Wana wasiwasi kwelikweli. Hawaamini kuwa chama chao ndio kinaelekea kaburini muda si mrefu kitasahaulika kama KANU ilivyosahaulika huko kwa watani.
 

Kwenye Mkutano Mkuu wa CCM wa mwaka 1995 wa kumpitisha Mkapa kugombea uraisi, Nyerere alisema haya ambayo leo ninaona ni kero kwangu sijui kwenu na wala sikubaliani naye kwenye hilo hata kidogo.

Alisemaje? Hapa ninamnukuu:-



Mimi sikubaliani naye kwa sababu nimemwona JK jinsi ambavyo yupo beneti na mafisadi na anakula nao sahani moja na ndiyo maana na hata Bw. Kifimbo hapo nionavyo alichemsha.

Lakini Nyerere ana busara sana kwenye hotuba hiyo hiyo alinena yafuatayo ambayo yanagusa sasa kudondoka kwa JK na timu yake ya watafunaji wa fedha za umma. Na ninamnukuu:-


Si sasa yametimia………………….GO DR. SLAA...GO TO STATE HOUSE

Alikuwa sahihi kwa yote mawili. Hilo la kwanza alilisema akijua wakati huo kwamba CCM kilikuwa kimejaa wanachama na viongozi wazoefu ambao wangeliweza kuwania uongozi na kuliongoza taifa bila matatizo.

Halikadhalika, alikuwa sahihi kwa sababu hata Dk. Slaa anayesifika hivi sasa ametoka ndani ya CCM hiyo hiyo akaenda upinzani baada ya CCM kuengua jina lake katika kinyang'anyiro cha kugombea ubunge jimboni kwake Karatu. Akaingia CHADEMA na kumshinda mgombea wa CCM ambaye ndiye alipitishwa na vikao vya juu kuwa mgombea wa CCM badala ya Dr. Slaa ambaye wananchi walikuwa wakimtaka.

Kama kweli Dk. Slaa ama mgombea yoyote wa upinzani anaonyesha kuwa na nguvu sisi CCM tukubali tu kushindwa kuliko kulazimisha mambo. Lazima lazima yetu inaweza kutugharimu sana kama Taifa.

Hata hivyo, CCM (wenye uchungu na Taifa letu) Oyee!
 
Kwako Bibi ntilie

Alikuwa sahihi kwa yote mawili. Hilo la kwanza alilisema akijua wakati huo kwamba CCM kilikuwa kimejaa wanachama na viongozi wazoefu ambao wangeliweza kuwania uongozi na kuliongoza taifa bila matatizo.

Halikadhalika, alikuwa sahihi kwa sababu hata Dk. Slaa anayesifika hivi sasa ametoka ndani ya CCM hiyo hiyo akaenda upinzani baada ya CCM kuengua jina lake katika kinyang'anyiro cha kugombea ubunge jimboni kwake Karatu. Akaingia CHADEMA na kumshinda mgombea wa CCM ambaye ndiye alipitishwa na vikao vya juu kuwa mgombea wa CCM badala ya Dr. Slaa ambaye wananchi walikuwa wakimtaka.

Huu ni ushahidi CCM siku nyingi haikuwa na ungozi bora vinginevyo wangeliheshimu kura za maoni ndani ya CCM mwaka 1995



Tatizo hapo ni kuwa Nyerere aliwaona Mkapa na baadaye JK ni uongozi bora wakati siyo na hapo ndipo alipochemsha.
 
Nyerere pia alisema yafuatayo katika kitabu chake cha Uongozi wa Tanzania:

Nilisema awali kwamba kansa ya uongozi ndani ya Chama cha Mapinduzi isingekuwa ni jambo la kutisha sana kama tungekuwa tumeanza kuona Chama kizuri cha upinzani kinachoweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM. Ubovu wa uongozi ndani ya CCM ndio uliofanya nikapendekeza tuanzishe mfumo wa Vyama Vingi. Nilitumaini kuwa tunaweza kupata Chama kingine kizuri ambacho kingeweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM; au ambacho kingekilazimisha Chama cha Mapinduzi kusafisha uongozi wake, kwa kuhofia kuwa bila kufanya hivyo kitashindwa katika uchaguzi ujao. Lakini bado sijakiona Chama makini cha upinzani; na wala dalili zo zote za kuondoa kansa ya uongozi ndani ya CCM. Bila upinzani mzuri wa nje, na bila demokrasia halisi ndani ya Chama cha Mapinduzi, Chama hiki kitazidi kudidimia chini ya uzito wa uongozi mbovu. Kwa hali yetu ya kisiasa ilivyo nchini hili si jambo la kutarajia bila hofu na wasi wasi! (Ukurasa 66)

MNAFIKI MKUBWA. Alipokuwa yeye madarakani hakutaka wapinzani na alipiga marufuku vyama vya siasa, vyama vya wafanyakazi na akaleta sheria ya kutia watu ndani bila ya kuwafikisha mahakamani. Wakati wa utawala wake, jela zilikuwa zimejaa wafungwa wa kisiasa na huko ugenini badala ya wapiga boksi kulikuwa na wakimbizi wa kisiasa. Halafu anazungumzia upumbavu wa ubovu wa uongozi wa CCM ndiyo aliofanya apendekeze siasa za vyama vingi ama alisoma alama za ishara hasa baada kuona huko Poland na kwa rafiki yake Cauesescu wakichinjwa barabarani?

Acheni kumtukuza huyo mzee wakati alikuwa na mabaya yake mengi tu. :hand:
 



Kwa wakati huo naweza sema walikuwepo lakini wakati huu ambao hata yeye Mwl.Nyerere hayupo hao viongozi ni watapingwa kwa hali na mali kuhakikisha wasiwepo hata kwenye safu ya uongozi ni wachache kama wakina maghufuli hata ukiwapa wizara gana atarudi pale pale hatelemki bali una mpandisha nadhani this time magufuli awe waziri wa maliasili na utarii mwone hata kakakuona watajulikana ni wangapi na hiyo barabara haitopita huko mbugani


Kumpata kiongozi nje ya CCM lawezekana kabisa ila hao walioko ndani ya system na CCM wao lao ni mmoja katu hawatokubali hiyo hali iwatokee kwanini wanajua watahadhilika huko mbeleni na tena kwa pilato na ndio maana hata jeshi lina toa tamko hii inamaanisha kuwa viongozi waliopo ni kuwa hawakubaliki na watanzania kwa nini hilo wasilione kwanini waweke vitisho na asilimia kubwa ni CCM wao kwa wao ndio wanaopisha huko majimboni na ndio wanao jua mfumo mzima wa kuhesabu kura then wanajua mchezo mchafu unavyo chezwa leo hii Jeshi mwaingizwa huku kwenye siasa na mwakubali maficha nini huko kwenye siasa??


Huyo Nyerere ndiyo aliyeshiriki "kuchakachua" kura kule Zanzibar 1995. Pia alishiriki kuhamisha milingoti ya goli pale mgombea wake, Benjamin Mkapa aliposhika nafasi ya pili dhidi ya JK. Yote haya mnayajua lakini mnajitia wazimu msiokuwa nao. :hand:
 
Alikuwa sahihi kwa yote mawili. Hilo la kwanza alilisema akijua wakati huo kwamba CCM kilikuwa kimejaa wanachama na viongozi wazoefu ambao wangeliweza kuwania uongozi na kuliongoza taifa bila matatizo.

Halikadhalika, alikuwa sahihi kwa sababu hata Dk. Slaa anayesifika hivi sasa ametoka ndani ya CCM hiyo hiyo akaenda upinzani baada ya CCM kuengua jina lake katika kinyang'anyiro cha kugombea ubunge jimboni kwake Karatu. Akaingia CHADEMA na kumshinda mgombea wa CCM ambaye ndiye alipitishwa na vikao vya juu kuwa mgombea wa CCM badala ya Dr. Slaa ambaye wananchi walikuwa wakimtaka.

Kama kweli Dk. Slaa ama mgombea yoyote wa upinzani anaonyesha kuwa na nguvu sisi CCM tukubali tu kushindwa kuliko kulazimisha mambo. Lazima lazima yetu inaweza kutugharimu sana kama Taifa.

Hata hivyo, CCM (wenye uchungu na Taifa letu) Oyee!

Ni kawaida ya WANAJIMU kuzungumzia vitu ambavyo ni very obvious. Mwaka 1995 "Shekhe Yahaya" alitabiri mgombea mwenye "uwalaza" (siyo upara) atashinda uchaguzi. Mkapa, Lipumba, Mrema na Cheyo wote wana uwalaza. Sasa hapo kimetabiriwa kitu gani? Hivyo hivyo ndivyo alivyofanya Nyerere. It is obvious kuwa chama kitakachoshinda uchaguzi ni aidha CCM au chama cha upinzani, is there any other option?

Isitoshe ni muhimu pia tukakumbushana mbinu aliyokuwa anaitumia Nyerere. Nyerere alikuwa na mgombea wake aliyetaka ndiyo apitishwe. Kabla ya mchakato ule wa Dodoma aliwatishia CCM kuwa hatowapigia kura kama hawatomchagua mtu msafi kugombea urais. Na pale alipopita mtu wake baada ya kubadilisha milingoti ya goli in the middle of the game, alipita nchi nzima kumnadi mgombea wa CCM na akawa anamuita Mr. Clean. Na huyo u-Clean wa Mr. Clean wote tunaujua. Lakini :hand: usiniletee habari za sijui alianza ufisadi baada ya Nyerere kuondoka. Hivyo vioja huko huko. :hand:
 
Mhh kwa jinsi kampeni zinavyoendeshwa na vyombo mbalimbali dhidi ya Dr SLAA na jinsi navyowafahamu wengi wa watanzania, si rahisi DR SLAA kushinda uchaguzi huu pamoja na kuwa ana kila point ya kumfanya ashinde. Kama kuna alosikiliza jana usiku vipindi viwili kimoja cha redio moja ya kidini na kingine cha TV kinachorushwa kila jumapili mida ya saa nne usiku ndani ya channel ten, atanielewa nini maana yangu. KAtika vipindi hivyo hiyo jana kampeni kali dhidi ya DR Slaa ilikuwa ikiendeshwa na hasa juu ya suala la kashfa ya mchumba wake. Kwa maoni yangu ni muhimu saana kwa benchi la ufundi la Dr Slaa kuhakikisha suala hili la mchumba wake linawekwa sawa haraka iwezekanavyo. Vinginevyo nafikiri yalotokea kwa Mrema 1995, na Lipumba 2000 yatatokea tena kwa SLAA. Benchi la ufundi la Slaa likiongozwa na Marando, linatakiwa kulishughulikia suala hili haraka saana.
 
we need changes and goodluck tanzanians are ready to accept them let cooperate in fillfulling this task
 
Back
Top Bottom