Mwacheni Gaddafi ana idea nzuri

rosemarie

JF-Expert Member
Mar 22, 2011
6,887
3,412
Pamoja na kwamba viongozi wa africa wanampa kisogo gadafi kwa mambo yanayomkuta naomba ulaya na marekani wamwache gadafi kwa sababu ndiye kiongozi pekee aliyabakia anayeona umuhimu wa kuiunganisha africa,hawa viongozi wengine akiwemo mkweree wetu wanajifanya kunyamaza kwa sababu ya ubinfsi wa kuendelea kushika madaraka,ni jambo baya sana na litaongeza matatizo makubwa sana hapa duniani!!!!!!!!!!!!!aghhhhhhh
 
Ghadaff ni kamanda wa ukweli ni yeye tu amebaki hapa Afrika amegom kuyapigia magoti haya mambwa ya kimarekani...hata yakimuua atakua shujaa wa Afrika sio muoga kama hawa matapeli wa AU..
 
Alivyoleta hoja ya kuunganisha africa viongozi wa africa walikaa kimya waliona watakosa nafasi zao!!!!!!ovyoooooooooo sana
 
inawezekana hayo makombora anayorushiwa ni kutokana na hiyo idea,labda hao jamaa mizungu iliona akiendeleza hiyo hoja ya africa kuwa moja tutaamka!!!!!!!!!hii mijitu hapa kwetu haioni mbali yenyewe yanaangalia leo leo wakati wenzao wanajua nini kitatokea miaka 10 ijayo,anghhhhhhhhhhh
 
ukiuliza hii mijitu hapa kwetu kuna vita kubwa inaandaliwa na hiyo mizungu itakuambia haijui,lakini kuna vita kubwa inakuja tukipona hapo ni bahati
 
Acheni kujidanganya Gaddaf ni msanii tu hana lolote si chochote kama kweli ni shujaa angehifadhi mamilioni marekani na ulaya tena kwa jina lake,Angewagawa watu wa libya kwa misingi ya ukabila huku kabila linaloishi tripoli likila bata lile la bengaz likiishi kama jehanamu hawana ajira na matatizo chungu mzima.Kashindwa kuwa unganisha walibya angeweza kuiunga nisha Afrika ambayo ina matatizo chungu nzima.Tatizo Afrika haijawah pata viongoz shupavu wote waliopo leo ni wa sanii tu.Mandela pamoja na kuteswa bado alipo pata madaraka aliruhusu demokrasia akakaa madarakani miaka mitano tu.Je demokrasia libya ipo wapi? Acheni kujidanganya!!
 
Kwanza tufahamu kwamba:-
1. Demokrasia si kuondoka madarakani baada ya miaka mitano, kumi au kumi na tano [Helmundt Korl wa Ujerumani alikaa madarakani miaka 18].
2. Sio sahihi kuamini kuwa nchi za magharibi ndiyo zenye demokrasia na usawa! [huenda sisi Waafrika hasa Watanzania tuna usawa wa hali ya juu kulika hao wa-magharibi! tofauti yetu na wao ni kwamba wenyewe wana vyombo vya habari vinavyoeneza propaganda dunia nzima]

Menny Terry:- Mabepari wamekwisha kukuingizia propaganda zao za uongo na kukuaminisha kuwa Gadaffi ni Dikteta. Ni jambo la kusikitisha sana unapokuwa mzalendo kisha ukatekwa na utumwa wa ki-magharibi.
Hao jamaa wakishamuondoa gadaffi itakuwa ni mchezo kwamba kila kiongozi atakayepingana nao watamtishia kwa reference ya Gadaffi. Nchi za Magharibi hawana nia njema na Africa hata kidogo. Wanarudisha utumwa na Ukoloni kwa mlango wa nyuma. Hebu fikiria hili: Baada ya vita vya peninsula mwaka 1953. Marekani na Japan ilipeleka misaada Korea kusini [misaada ya technolojia]. leo hii Korea ni miongoni mwa nchi tishio kiuchumi. Afrika tangu tupate uhuru tumepokea misaada na mikopo ambayo hadi leo watoto ambao hatujazaa wanadaiwa. Mikopo hiyo yooooote haikulenga kutuendeleza bali kutuingiza Kifungoni!! Ndiyo maana mkapa alipoingia madarakani alianza kupambana nao hadharani [Kumbuka hotuba yake aliyoitoa mwaka 1996 Tokyo Japan].
Ndugu Yangu Menny Terry:- Ni kudra za mwenyezi mungu kupata viongozi wenye silka za akina Mkwawa ndiyo watatuondoa kwenye hii minyororo ya Mabepari maana hawa mabepari wameshatudumaza kwa kupandikiza rushwa miongoni mwetu hadi kwamba mambo hayaendi.
Kwa Kumalizia Tafakari haya mawazo matatu ya Gadaffi ambayo aliyatoa kwa viongozi wa Afrika:-
1. Nchi za Kiafrika zikatae kulipa madeni zinayodaiwa na nchi za Magharibi kwa sababu westerns waliiba mali asili ya Afrika
2. Afrika tuwe na setillite yetu ya mawasiliano ili kuondokana na propaganda za vyombo vya habari vya Magharibi [Wachina walifanikiwa hili kwa kupiga marufuku vyombo vya habari vya magharibi. hivi sasa wanakula matunda ya mkakati wao]
3. Gadaffi alipendekeza Afrika iungane ili tuwe na sauti moja itakayotuwezesha kujilinda. [Libya wana mafuta gas na maliasili nyingine kiasi kwamba hawahitaji msaada wa nchi yeyote ya Kiafrika. Lakini wakapendekeza tuchangie hayo yote.

NINASHAWISHIKA KUKUBALIANA NA HOJA YA ROSEMARIE!!!
 
Hivi Babu Nelson Mandela ni kwamba haruhusiwi kuangalia taarifa za habari?? manake amekaa kimya kama vile hakuna kinachoendelea Libya.

Mnadela pekee ndiye angekuwa n uwezo wa kutoa tamko halafu NATO, USA na wavamizi wengine wangemsikiliza, manake wanaompinga Ghadafi ni waasi wachache wakisidiwa na Westerners wanaotaka mafuta ya Libya. Sio nguvu ya umma.

Sioni umuhimu wa kumuenzi Babu Mandela kama wakati wa shida kama ya Libya anakaa kimya na kushirikiana na wazungu as if nothing has happened.
 
Basi mwombe awapigie magoti wanachi wake kwani ndio wa kwanza kumtaka aachie madaraka. Moto umewashwa na Walibya wenyewe, wengine wamepata sababu tu.
 
Basi mwombe awapigie magoti wanachi wake kwani ndio wa kwanza kumtaka aachie madaraka. Moto umewashwa na Walibya wenyewe, wengine wamepata sababu tu.

Inaelekea husomi posts zote. Kuna mjumbe ametuambia kuwa westeners wana resources or tools to make us believe through propaganda that the problrms started by Libyans, but I doubt it and you need to prove it. Sijawahi kusikia duniani waasi wana ndege za kivita ndiyo kwanza Libya!!
 
Kwanza tufahamu kwamba:-
1. Demokrasia si kuondoka madarakani baada ya miaka mitano, kumi au kumi na tano [Helmundt Korl wa Ujerumani alikaa madarakani miaka 18].
2. Sio sahihi kuamini kuwa nchi za magharibi ndiyo zenye demokrasia na usawa! [huenda sisi Waafrika hasa Watanzania tuna usawa wa hali ya juu kulika hao wa-magharibi! tofauti yetu na wao ni kwamba wenyewe wana vyombo vya habari vinavyoeneza propaganda dunia nzima]

Menny Terry:- Mabepari wamekwisha kukuingizia propaganda zao za uongo na kukuaminisha kuwa Gadaffi ni Dikteta. Ni jambo la kusikitisha sana unapokuwa mzalendo kisha ukatekwa na utumwa wa ki-magharibi.
Hao jamaa wakishamuondoa gadaffi itakuwa ni mchezo kwamba kila kiongozi atakayepingana nao watamtishia kwa reference ya Gadaffi. Nchi za Magharibi hawana nia njema na Africa hata kidogo. Wanarudisha utumwa na Ukoloni kwa mlango wa nyuma. Hebu fikiria hili: Baada ya vita vya peninsula mwaka 1953. Marekani na Japan ilipeleka misaada Korea kusini [misaada ya technolojia]. leo hii Korea ni miongoni mwa nchi tishio kiuchumi. Afrika tangu tupate uhuru tumepokea misaada na mikopo ambayo hadi leo watoto ambao hatujazaa wanadaiwa. Mikopo hiyo yooooote haikulenga kutuendeleza bali kutuingiza Kifungoni!! Ndiyo maana mkapa alipoingia madarakani alianza kupambana nao hadharani [Kumbuka hotuba yake aliyoitoa mwaka 1996 Tokyo Japan].
Ndugu Yangu Menny Terry:- Ni kudra za mwenyezi mungu kupata viongozi wenye silka za akina Mkwawa ndiyo watatuondoa kwenye hii minyororo ya Mabepari maana hawa mabepari wameshatudumaza kwa kupandikiza rushwa miongoni mwetu hadi kwamba mambo hayaendi.
Kwa Kumalizia Tafakari haya mawazo matatu ya Gadaffi ambayo aliyatoa kwa viongozi wa Afrika:-
1. Nchi za Kiafrika zikatae kulipa madeni zinayodaiwa na nchi za Magharibi kwa sababu westerns waliiba mali asili ya Afrika
2. Afrika tuwe na setillite yetu ya mawasiliano ili kuondokana na propaganda za vyombo vya habari vya Magharibi [Wachina walifanikiwa hili kwa kupiga marufuku vyombo vya habari vya magharibi. hivi sasa wanakula matunda ya mkakati wao]
3. Gadaffi alipendekeza Afrika iungane ili tuwe na sauti moja itakayotuwezesha kujilinda. [Libya wana mafuta gas na maliasili nyingine kiasi kwamba hawahitaji msaada wa nchi yeyote ya Kiafrika. Lakini wakapendekeza tuchangie hayo yote.

NINASHAWISHIKA KUKUBALIANA NA HOJA YA ROSEMARIE!!!


Nilitamani kuwa na mengi sana ya kusema, ila baada ya kusoma post yako hapo naona mkuu wangu umemaliza kila kitu.
Labda mi niseme kitu kidogo tu kuwa sisi waafrika (hasa wasomi) tumekuwa mabingwa wa ushabiki wa siasa za magharibi,
Hili limekuwa ni tatizo sana miongoni mwetu, sababu tunakuwa carried away kirahisi na propaganda zao.....
Marabaada ya Gadaff kuja na hiyo hoja ya itikadi mpya ya siasa za "africansm" viongozi wetu vilaza tayari kwa kupitia kwa redio mbao za mabepari wakawa weshaanza kufikiria urais wa wa hiyo "united states of africa" wakaanza kumsema kuwa Gadaf anataka kuwapiga bao katika kiti hicho.
Kumdhoofisha Gadaf, kunakofanywa saiv na NATO na washirika wengine, sio msiba wa walibya, bali ni msiba wa taifa kubwa la "united states of africa". Ambapo sioni kiongozi mwenye hiyo ndoto tena waliobaki ni wachumia tumbo tu.
 
Jamani. Pamoja mambo aliyo ongea PAPA D, kuna hili pia ambalo ni kubwa zaidi; KUNA MPANGO MAHAHUSUSI WA SIRI(conspiracy) wa kutaka DUNIA KUWA NA SERIKALI MOJA(one world government). Mpango huu umepewa jina la NEW WORLD ORDER. Ili mpango huo utimie ni pamoja na kuhakikisha kuwa hakuna raisi yeyeto atakeye kuwa anaupinga mpango huu(taarifa zinaonyesha kuwa GADAFI ni mmoja kati ya maraisi wanaoupinga au wanaweza kutoboa siri kuhusu mpango huu). Na ndio maana western countries(nato ikiwa ndio military base yao wanafanya kila njia kuhakikisha kuwa hawa watu wanaopinga huu mpango wanatoweka duniani). Moja ya njia rahisi ya kufikia mpango huo ni kwa kupromote democracy(mahala ambako kuna upinzani na huu mpango) ili waweze kuwapachika vibaraka wao. Hii one world government itafikiwa baada ya vita kuu ya tatu ya dunia ambayo kwa sasa maandalizi yako hatua za mwishomwisho. (hizi arab states unrest(ondoa misri na tunisia) ni moja ya utekelezaji wa huu mpango). Kwa maana hiyo basi.
1. nashanga sana kuona kwa sababu ya waafrika kukosa taarifa,wanasupport gadafi kung'oka madarakani.
2. Naomba tujitahidi kusoma vitabu vitakatifu(ufunuowa yohana kwa wakristo) ili ujue kuwa lazima hii conspiracy iwepo ili unabii utimie.
3, kwa wanaotaka kujua zaidi hebu tembelea WW3: How Will World War Three Affect You? Learn How To Prepare - Free Newsletter (huku utaweza kupata some facts about this conspiracy).
4. Nasikitika kuona tunaendelea kuwa manipulated na propaganda za nchi za magharibi kwa kupitia vyombo vyake vya habari.
 
America empire is falling!. greedy, deception, lies, have engulfed this country and so by those evils, the empire is crumbling!.
How can a country seek revenge for a man said to kill 3000 Americans for ten years, while it has itself caused the death of 1 Million people in Iraq!.

How can the country respect human rights, while it has caused the death of more than 5 million people in Vietnam!.
How can a country respect "life, liberty and pursuit of happiness", while it has Killed more than 200000 people with An Atomic bomb in Japan

How can a country respect " humanity", while it has killed more than 2500 innocent people with drone attacks and call it collateral damage!.
How can a country defend civilians while it participate in the mission that target civilian targets in Libya.
 
Waafrika tungekuwa na uadilifu ingewezekana kuunda USA, lkn kwa hali ilivyo mi naona Ghadafi alikuwa anaota, kwanza huo muungano ungewasaidia raia au watawala? Maana kama serikali zetu zimejaza wezi hiyo usa ingewatoa wapi watendaji waaminifu. Kiasili kama mnigeria hawezi kuwafanyia mema watu wa kwao hawezi kuja kuwafanyia mema say watu wa Malawi na vice vesa.
 
wakuu haya maneno yamenifanya nilie kumbe bob marley aliona mbali
They don't want to see us unite:
All they want us to do is keep on fussing and fighting.
They don't want to see us live together:
All they want us to do is keep on killing one another.

 
inawezekana hayo makombora anayorushiwa ni kutokana na hiyo idea,labda hao jamaa mizungu iliona akiendeleza hiyo hoja ya africa kuwa moja tutaamka!!!!!!!!!hii mijitu hapa kwetu haioni mbali yenyewe yanaangalia leo leo wakati wenzao wanajua nini kitatokea miaka 10 ijayo,anghhhhhhhhhhh
Tembelea hizi links.Bofya.
Saving the world economy from Gaddafi – Gold Dinar (Video) : Deadline Live With Jack Blood

https://alexandravaliente.wordpress...y-that-would-be-the-death-of-the-fiat-system/

Gaddafi & Africa

http://www.africanews.com/site/Ethiopia_Gaddafi_is_new_AU_chairman/list_messages/22955Posted
 
Waafrika tungekuwa na uadilifu ingewezekana kuunda USA, lkn kwa hali ilivyo mi naona Ghadafi alikuwa anaota, kwanza huo muungano ungewasaidia raia au watawala? Maana kama serikali zetu zimejaza wezi hiyo usa ingewatoa wapi watendaji waaminifu. Kiasili kama mnigeria hawezi kuwafanyia mema watu wa kwao hawezi kuja kuwafanyia mema say watu wa Malawi na vice vesa.
Mkuu.
Gaddafi anaota..wewe hata ndoto huna?

USA au nchi za Europe hazikufika katika hali ambazo unaziona leo kwa miujiza au kama mchawi anayefunika kijiwe kitambaa cheupe na kutoka njiwa.
Wamedhulumu sana, wameua na kuuana sana,wamefanya watu watumwa na wameunda systems za kuendelea kuitawala dunia kifedha,kiuchumi na hata kutawala mawazo na fikra za watu, na yeyote anaejaribu kuzipinga au kuzipiga vita systems zao basi ataitwa mad man, dictator.

Kwa hiyo, ndugu hizi serikali zetu,jamii zetu hazitakuwa safi, hazitapata watendaji waadilifu,hazitakosa wezi kama hatutakuwa tayari kujenga check and balaces ndani ya systems zetu,ndani ya taasisi zetu, ndani ya serikali zetu lakini tuelewe haya hayafanyiki over night!! Wakati nchi zetu zina miaka 50,40,30 tokea kupata uhuru, nchi za west na US zina zaidi ya miaka 100,200 ya uhuru wao na ujenzi wa systems zao ambazo pia wanazilazimisha kwetu.Lakini hata wao wanafanya "madudu".

Ifike wakati tuamini kuwa sisi pia kama tungeamua kila kitu wenyewe basi tungechukua muda mfupi kufikia lengo la uhuru wa kweli kwa kila mwafrika, hali ya dunia na uchumi unaoendeshwa na wababe wa dunia hautupi nafasi hiyo. Tukilielewa hili, basi tutaanza kuwekana sawa na kuzi-reforms taasisi zetu ili tupate watu waadilifu, viongozi wa aina ya Gaddafi kwa yale mazuri yake.
Tanzania, Afrika bila viongozi wizi na wasio waadilifu inawezekana,tekeleza sehemu ya jukumu lako.

Unapoona tatizo na kama unaelewa dawa yake usisiste kuuamsha umma wa Afrika.
Hakuna mwananchi wa kiafrika anaetaka kiongozi mwizi au asiye muadilifu, wengine wanahitaji kufunzwa vipi watawapata viongozi waadifu na wasio wezi.

Demokrasia ya West na USA hazikuota kama uyoga ,ni matokea ya ujenzi wa taasisi za umma zenye check and balance kwa miaka mingi.

Kuna tangazo la HEDEX, maumivu ya kichwa huanza pole pole.....na hivyo hivyo, tunaweza kuzijenga Taasisi zetu hapa Afrika pole pole,iko siku zitafikia hatua tutakayoridhika nayo.
Kutokuwa na taasisi hizo ni hasara zaidi. Tuzianzishe huku tunazipiga msasa.

Wasahili husema "ukiona vyaelea, vimeundwa!"
Tafakari, mkuu.
 
Gadafi ndiye haswa anapaswa kuwa rais wa africa, nimeuona uzalendo wake kwa Afrika, bahati mbaya wenzake wamempa kisogo sabau ya uoga wao. Museveni hafai kuwa hata rais wa east african federation kwa kuwa uzalendo wake kwa afrika ulikwisha zamani, na sasa ni dictator tu wa uganda kama amini, poleni waganda. Rais wa Afrika ni Colonel Gadaffi, Makamu wa rais wa Afrika ni Robert Mugabe, na Waziri Mkuu wa Afrika ni Bingo Mutharika.
 
Waafrika tungekuwa na uadilifu ingewezekana kuunda USA, lkn kwa hali ilivyo mi naona Ghadafi alikuwa anaota, kwanza huo muungano ungewasaidia raia au watawala? Maana kama serikali zetu zimejaza wezi hiyo usa ingewatoa wapi watendaji waaminifu. Kiasili kama mnigeria hawezi kuwafanyia mema watu wa kwao hawezi kuja kuwafanyia mema say watu wa Malawi na vice vesa.

mimi siamini uchawi,kama upo waje tuloge wezi wote serikalini wabakie watu wema peke yao
 
Ataiunganisha kwa vigezo gani? lugha tofauti, fedha tofauti, uwiano ulio mbali wa uchumi wa nchi za africa hata watu wetu bado wanapenda kujitofautisha, waarabu wanapenda watambuliwe hivyo na sio waafrica, muungano wa tanganyika na zanziber unatushinda EAC inasuasua, je kama kwa hizi jumuia ndogo tunashindwa tutaweza kuwa na muungano wa africa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom