Muundo wa Utawala/Muungano hauwezi kuwa Sera au Ilani ya Chama cha Siasa

Getstart

JF-Expert Member
Oct 13, 2012
6,658
2,235
Kumekuwa na mjadala na ubishani wa kimtazamo katika suala la muundo siyo tu wa kiutawalawa dola (Serkali) lakini pia muungano wetu. Kwa kweli mambo haya mawilihayawezi (muundo wa utawala na muundo wa muungano) kutenganishwa.

Kwa upande wa muundo wa utawala kuna ambao wanapendekeza mfumo wa majimbo ambao utatoa mwanya kwa watu kujitawala na kujiamulia mambo yao ya kimaendeleo ikiwemo ya kijamii na uchumi. Serkali kuu ikibaki na masuala muhimu ya kitaifa na pia kuratibu maendeleo ya jumla kwa nchi nzima. Ninakumbuka hii ilijaribiwa miaka ya sabini (wakati wa Chama kimoja) katika mfumo wa sasa kwa sera za madaraka mikoani ingawa haikufanikiwa sana.

Lakini wapo watu wanaofikiria kuwa mfumo huu utaligawa taifa na hivyo kupigia chepuo muudo wa sasa ambao unagawa nchi katika mikoa, wilaya, tarafa, kata na vijiji lakini utawala ukiendelea kuongozwa kupitia Serkali kuu (Dar es Salaam) kwa mambo yote.

Kwenye muungano kuna maoni tofauti ya mfumo wake. Kuna wanaowaza kuwa tuendelee na mfumo wa Serkali mbili kama ilivyo sasa lakini tutatue kero zinazoonekana kuzaliwa ndani ya mfumo huu. Lakini pia katika mfumo huu kuna wanaofikiria kuwaSerkali hizi mbili (ya Muungano na ya Zanzibar) zinatakiwa kuwa na hadhi sawa na maraisi wake wawe na mamlaka yanayoligana! Ukitekeleza maoni haya unatengeneza tatizo lingine kwamba Muungano unalingana na upande mmoja (na kwa bahati mbaya upande ambao ni mdogo siyo tu kwa eneo bali hata kwa idadi ya watu) wakati upande mwingine hauko waziwazi – umemezwa na muungano!

Pia wapo wanaofikiria kuwa muungano wetu unatakiwa uwe wa Serikali tatu, yaani ya muungano, ya Zanzibar na ya Tanganyika (Tanzania bara). Hii nayo ina changamoto zake na hasa ya mgawanyo wa madaraka na jinsi ya uendeshaji wa Serkali ya muungano. Isipowekwa vyema itapelekea kuvunjika muungano mapema mno kuliko matarajio ya wengi. Kuna wanaodai muungano wa mkataba (na mara kadhaa wametolea mfano wa Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki). Sijui hasa wanachokitaka katika hili lakini nafikiri katika mfumo huu hakutakuwa na muungano. Lakini wapo wachache wanaofikiria kuwa muungano wetu sasa unatakiwa upelekwe katika daraja lingine la Serikali moja yenye mamlaka kamili katika nchi moja.

Kwa bahati mbaya tofauti hii ya mawazo ya mifumo ambayo inapelea tofauti ya muundo wetu wa utawala na muungano imekuwa ikichukuliwa kuwa ni sera za vyama vya siasa. Lakini inashangaza zaidi vyama hivi vinapodai kuwa mifumo hii ni ilani zao za uchaguzi na kuwa wanaposhinda wanaweka mkataba na watanzania jinsi ya kutawaliwa.

Hii si sahihi kwani haisaidii taifa letu kuwa endelevu. Fikiria tu chama kikishinda na ilani yake inataka muungano wa Serkali tatu na au hata wa mkataba na wakafanikiwa kuweka mfumo huu. Laknini baada ya miaka mitano Chama chenye sera na ilani yaSerikali mbili kikashinda uchaguzi, wakafumua tena na kutengeneza muundio wa Serikali mbili! Itakuwa vurugu tu ambayo haisaidii kuleta utulivu. Halikadhalikahii pia ni kwa mfumo wa utawala – wa majimbo au wa utawala wa Serikali Kuu kufanya kila kitu.

Ndiyo maana ni maoni yangu kuwa mfumo wa utawala na muungano haviwezi kuwa sera au ilani ya chama cha siasa. Haya ni masuala ya msingi ya uwepo wa taifa letu na wote tukubaliane ni lazima yawe ndani ya Katiba yetu ya nchi. Lakini haiwezi kuwekwa hivi hivi bila kujenga muafaka wa kitaifa. Tunapaswa kuyajadili nakufikia muafaka wa mfumo tuutakao na baada ya hapo kuuweka katika Katiba. Kinyume chake kwenda na mtiririko huu wa kivyama vya siasa itatuwia vigumu kuufikia huomuafaka na itatugawa. Tuache vyama vishindane kwa kutueleza katika ilani zao ni jinsi gani ya kuendesha Serkali kwa gharama ndogo katika mfumo tuliokubaliana.
 
1. Kwa jinsi ilivyo Visiwani hawana uwezo kuchangia Muungano.. wenyewe wanasema na maskini na ni wachache! Bara wanabeba gharama zote za Muungano!

2. Bora Ufe.. huu Muungano na Zanzibar.. kila Mmoja ajiunge na EAC kila mmoja kivyake...hii ina maslahi zaidi ya kiuchumi kwa Bara na Visiwani watakuwa na uhuru zaidi kuamnua mambo yao!

3. Bara iitwe Tanzania Bara au Azania! Visiwani watakuwa huru kuja Bara kama ilivyo Kenya au Uganda.

4. Azania igawanywe majimbo saba (states) ili kurahishisha utawala!
 
1. Kwa jinsi ilivyo Visiwani hawana uwezo kuchangia Muungano.. wenyewe wanasema na maskini na ni wachache! Bara wanabeba gharama zote za Muungano!

2. Bora Ufe.. huu Muungano na Zanzibar.. kila Mmoja ajiunge na EAC kila mmoja kivyake...hii ina maslahi zaidi ya kiuchumi kwa Bara na Visiwani watakuwa na uhuru zaidi kuamnua mambo yao!

3. Bara iitwe Tanzania Bara au Azania! Visiwani watakuwa huru kuja Bara kama ilivyo Kenya au Uganda.

4. Azania igawanywe majimbo saba (states) ili kurahishisha utawala!

ukivunja muungano kwa sababu hiyo maanake baadaye hata hiyo Tanzania Bara au Azania unayoipigia chepuo haitasalimika. Mkoa au jimbo litakaloshindwa kuchangia mapato ya kuendesha Serikali itafukuzwa? Suala hapa tusifanye muundo wa utawala na muungano kuwa sera na Ilani ya vyama vya siasa.
 
Huu ujinga ulianzishwa na CCM chini ya hayati Baba wa Taifa JKN. Kwamba sera ya CCM ni serikali mbili kuelekea Serikali moja. Nafikiri mawazo ya CCM na Nyerere wakati ule ilikuwa ni kwamba CCM itatawala MILELE. Ajabu ni kwamba hata vyama vya upinzani vimeingia kwenye mtego huu wa Panya wa CCM. Sasa tunasikia CDM nao wanasema sera yao ni Serikali tatu, CUF wao wanasema sera yao ni Muungano wa Mkataba, DP wao wanasema sera yao ni Kuvunja MUUNGANO. Sijui NCCR, TLP, UDP wao wanasimamia wapi.

Suala la muundo wa muungano ni suala la KIKATIBA. Na si ILANI (Manifesto) ya chama cha SIASA na katika katiba mpya tunataka litamkwa waziwazi, hata muundo wa wizara zetu, madaraka mikoani/sera za majimbo. Haiwezekani kila chama kinachoingia madarakani kuja na muundo wake wa Muungano. Huu ni uwendawazimu, hata Banana republic huwezi kupata UJINGA wa aina hii.

Suluhisho la matatizo ya muungano wetu ni wa aina mbili tu. Haya mengine ni kuzunguka mbuyu.
  1. Tuwe na nchi moja, serikali moja, Rais mmoja, Unguja na Pemba iwe mikoa ya 31 na 32 ya JMT.
  2. Kama hilo haliwezekani basi tuvunje Muungano kila nchi (Tanganyika na Zanzibar zijijue)

That are the only practical solution.
 
sawa mkuu. sina hakika kama jaji warioba ameliona lakini huu ndo muda wake. tunataka majimbo. wanaosema majimbo mengine yatakuwa maskini, umaskini unaletwa na uvivu. ninachokiona hapa tz ni kuwa ile mikoa watu wanasema iko nyuma kimaendeleo, kiini chake ni uvivu wa mtu mmoja mmoja na uvivu wa kitaasisi. suluhu la uvivu wanalo wahusika. hakuna sababu hata moja kwa nini watu waxembe wanufaike sawa na wachapa kazi. ujamaa haupo tena, tusiogope sera ya majimbo. itatuwezesha kuyabana majizi yanayotuibia. kila jimbo litajipangia kiwango cha mshahara kulingana na kipato chake.
 
Kuhusu serekali tatu, sidhani kuwa zitafanya muungano uvunjike kama unavyofikiria, mimi nadhani ndio utakaoufanya muungano uimarike zaidi. Na kama utavunjika, sio tatizo zaidi. Tatizo ni kuwepo kwenye muundo wa muungano ambapo mwananchi haupendi kila mmoja akifikiri kuwa anaonewa.
 
Kumekuwa na mjadala na ubishani wa kimtazamo katika suala la muundo siyo tu wa kiutawalawa dola (Serkali) lakini pia muungano wetu. Kwa kweli mambo haya mawilihayawezi (muundo wa utawala na muundo wa muungano) kutenganishwa.

Kwa upande wa muundo wa utawala kuna ambao wanapendekeza mfumo wa majimbo ambao utatoa mwanya kwa watu kujitawala na kujiamulia mambo yao ya kimaendeleo ikiwemo ya kijamii na uchumi. Serkali kuu ikibaki na masuala muhimu ya kitaifa na pia kuratibu maendeleo ya jumla kwa nchi nzima. Ninakumbuka hii ilijaribiwa miaka ya sabini (wakati wa Chama kimoja) katika mfumo wa sasa kwa sera za madaraka mikoani ingawa haikufanikiwa sana.

Lakini wapo watu wanaofikiria kuwa mfumo huu utaligawa taifa na hivyo kupigia chepuo muudo wa sasa ambao unagawa nchi katika mikoa, wilaya, tarafa, kata na vijiji lakini utawala ukiendelea kuongozwa kupitia Serkali kuu (Dar es Salaam) kwa mambo yote.

Kwenye muungano kuna maoni tofauti ya mfumo wake. Kuna wanaowaza kuwa tuendelee na mfumo wa Serkali mbili kama ilivyo sasa lakini tutatue kero zinazoonekana kuzaliwa ndani ya mfumo huu. Lakini pia katika mfumo huu kuna wanaofikiria kuwaSerkali hizi mbili (ya Muungano na ya Zanzibar) zinatakiwa kuwa na hadhi sawa na maraisi wake wawe na mamlaka yanayoligana! Ukitekeleza maoni haya unatengeneza tatizo lingine kwamba Muungano unalingana na upande mmoja (na kwa bahati mbaya upande ambao ni mdogo siyo tu kwa eneo bali hata kwa idadi ya watu) wakati upande mwingine hauko waziwazi – umemezwa na muungano!

Pia wapo wanaofikiria kuwa muungano wetu unatakiwa uwe wa Serikali tatu, yaani ya muungano, ya Zanzibar na ya Tanganyika (Tanzania bara). Hii nayo ina changamoto zake na hasa ya mgawanyo wa madaraka na jinsi ya uendeshaji wa Serkali ya muungano. Isipowekwa vyema itapelekea kuvunjika muungano mapema mno kuliko matarajio ya wengi. Kuna wanaodai muungano wa mkataba (na mara kadhaa wametolea mfano wa Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki). Sijui hasa wanachokitaka katika hili lakini nafikiri katika mfumo huu hakutakuwa na muungano. Lakini wapo wachache wanaofikiria kuwa muungano wetu sasa unatakiwa upelekwe katika daraja lingine la Serikali moja yenye mamlaka kamili katika nchi moja.

Kwa bahati mbaya tofauti hii ya mawazo ya mifumo ambayo inapelea tofauti ya muundo wetu wa utawala na muungano imekuwa ikichukuliwa kuwa ni sera za vyama vya siasa. Lakini inashangaza zaidi vyama hivi vinapodai kuwa mifumo hii ni ilani zao za uchaguzi na kuwa wanaposhinda wanaweka mkataba na watanzania jinsi ya kutawaliwa.

Hii si sahihi kwani haisaidii taifa letu kuwa endelevu. Fikiria tu chama kikishinda na ilani yake inataka muungano wa Serkali tatu na au hata wa mkataba na wakafanikiwa kuweka mfumo huu. Laknini baada ya miaka mitano Chama chenye sera na ilani yaSerikali mbili kikashinda uchaguzi, wakafumua tena na kutengeneza muundio wa Serikali mbili! Itakuwa vurugu tu ambayo haisaidii kuleta utulivu. Halikadhalikahii pia ni kwa mfumo wa utawala – wa majimbo au wa utawala wa Serikali Kuu kufanya kila kitu.

Ndiyo maana ni maoni yangu kuwa mfumo wa utawala na muungano haviwezi kuwa sera au ilani ya chama cha siasa. Haya ni masuala ya msingi ya uwepo wa taifa letu na wote tukubaliane ni lazima yawe ndani ya Katiba yetu ya nchi. Lakini haiwezi kuwekwa hivi hivi bila kujenga muafaka wa kitaifa. Tunapaswa kuyajadili nakufikia muafaka wa mfumo tuutakao na baada ya hapo kuuweka katika Katiba. Kinyume chake kwenda na mtiririko huu wa kivyama vya siasa itatuwia vigumu kuufikia huomuafaka na itatugawa. Tuache vyama vishindane kwa kutueleza katika ilani zao ni jinsi gani ya kuendesha Serkali kwa gharama ndogo katika mfumo tuliokubaliana.
Kwa upande wa zanzibar tayari tushatoa maoni ya katiba,tunataka muungano wa mkataba, asilimia 65 ya wazanzibar ambao wanaotaka mkataba, serikali mbili am,bazo ziwe na mamlaka sawa , ni asilimia 31 wengine kama tupumue asilimia 1 ,na serikali moja 0.

Badu hamjafahamu kuwa muundo gani unatakiwa wa muungano ? Munataka mjadala gani ? Suala la muungano naona lingepigwa vita kutokuwa sera na badala yake liwe chini ya maamuzi ya wananchi, na suala la muungano lisiingizwe katika katiba ispokuwa muungano wowote ambao serikali inataka kuingia lazima wananchi wapige kura ya maoni kama vile wazanzibari walivyo piga kura kuunda serikali ya umoja wa kitaifa.

Chukulia mfano muungano wa EAC, serikali imeingia katika muungano moja kwa moja bila ya kuwashirikisha wananchi, jee hamuoni kuwa hiyo ni hasara kubwa kwa taifa ? Sasa hivi wana hofu na mali zao na rasilimali zao pamoja ajira ?

Hivi watanzania milioni 44 ambao wenye ajira ni wangapi na wasio kuwa na ajira ? Wasomi na wasio wasio wasomi ? Angali vipato vya wananchi, ? Angalia wakulima ambao uwezo wao ni mdogo ? Wote hao wana hofia rasilimali zao.

Ukija katika suala la ardhi, nchi za eac kila mtu anaiyangalia tanzania katika suala hilo, makazi hali kadhalika ? serikali imejipanga vipi ? Hawa viongozi hawakufikiria hilo, wanacho jaribu wao kung'ang'ania madaraka tu, huku mbunge wa tanzania huku mbunge wa EAC, wengine huku mbunge huku waziri waziri wa EAC, wao wanatafuta kila njia ya ulaji, na sio kutafuta njia za kuwakomboa wananchi ?

Leo hii mchakato wa katiba ukiangalia wanao toa maoni utacheka, mtua anatoa maoni eti vbijana wasivae suruali magotini, sijui sketi, mchakato wa katiba umenifumbua kuwa kuna idadi kubwa ya wananchi ambao hawana elimu hata ile ya secondari, nafikiri serikali ingejikita zaidi pia katika elimu, iwalazimishe ambao wasikuwa na ajira kupatiwa elimu na kuwapa welfare ili kuweza kuwapeleka katika daraja jengine.

Nilitegemea kuona maoni ya katika nchi kama Tanganyika yenye rasilimali kubwa ,kuona wananchi wanaoa maoni kwa mfano, serikali iweke welfare benefit kwa wale wasikuwa na ajira,wazee kupatiwa malipo pamoja na watoto, serikali kuwajengea makazi wananchi na kuwapa bure au kulipia fedha kidogo sana, katika huduma hizi fedha zitoke katika rasilimali za nchi, kwa silimia kuanzia 30 hadi 50.

Elimu iwe bure, na elimu iboreshwe, mfumo wa elimu ubadilishwe uwendane na wa kimataifa, mtu hata akiwa hana secondary akitaka kusoma hata awe na umri wa zaidi wa maika 20 aweze kurudi kusoma apate alimu hadi ya juu.

Nilitegemeo kuona wananchi wakisema kuwa rais asiwe ndio amiri jeshi mkuu wa nchi, ili vyombo vya ulizi kutojishirikisha kisiasa kwa kuwaonea wananchi.

Nilitegemea kuona wananchi wakitoa maoni wakisema kuwa jeshi la police liwe halina haki ya kumpiga mwananchi au kumnyanyasa kwa njia ya yoyote ile ! kAMA vile nchi za wenzetu, tunaona wananchi wanaandana japokuwa maandamano yanakuwa yako kivyume lakini police hathubutu kumpiga mwananchi,m badala yake wanawakamata tu nakuwapeleka wanako husika.
 
Suala la muuungano au lolote la taifa ,liwe chini ya mikono ya wananchi na sio sera ya chama chochote, wananchi ndio wanaumia kwa athari zozote za taifa,wao wapewe fursa kujadili, ili kwa kongamano ,au njia yoyote ya maoni, na mwisho kura ya maoni.
 
Suala la muuungano au lolote la taifa ,liwe chini ya mikono ya wananchi na sio sera ya chama chochote, wananchi ndio wanaumia kwa athari zozote za taifa,wao wapewe fursa kujadili, ili kwa kongamano ,au njia yoyote ya maoni, na mwisho kura ya maoni.

Hapa umenena, ndiyo maana inahitajika mjadala na mwisho wake kura ya maoni kukubaliana mfumo ambao utaingizwa katika Katiba.
 
Kwa upande wa zanzibar tayari tushatoa maoni ya katiba,tunataka muungano wa mkataba, asilimia 65 ya wazanzibar ambao wanaotaka mkataba, serikali mbili am,bazo ziwe na mamlaka sawa , ni asilimia 31 wengine kama tupumue asilimia 1 ,na serikali moja 0.

Badu hamjafahamu kuwa muundo gani unatakiwa wa muungano ? Munataka mjadala gani ? Suala la muungano naona lingepigwa vita kutokuwa sera na badala yake liwe chini ya maamuzi ya wananchi, na suala la muungano



lisiingizwe katika katiba ispokuwa muungano wowote ambao serikali inataka kuingia lazima wananchi wapige kura ya maoni kama vile wazanzibari walivyo piga kura kuunda serikali ya umoja wa kitaifa.

Chukulia mfano muungano wa EAC, serikali imeingia katika muungano moja kwa moja bila ya kuwashirikisha wananchi, jee hamuoni kuwa hiyo ni hasara kubwa kwa taifa ? Sasa hivi wana hofu na mali zao na rasilimali zao pamoja ajira ?

Hivi watanzania milioni 44 ambao wenye ajira ni wangapi na wasio kuwa na ajira ? Wasomi na wasio wasio wasomi ? Angali vipato vya wananchi, ? Angalia wakulima ambao uwezo wao ni mdogo ? Wote hao wana hofia rasilimali zao.




Ukija katika suala la ardhi, nchi za eac kila mtu anaiyangalia tanzania katika suala hilo, makazi hali kadhalika ? serikali imejipanga vipi ? Hawa viongozi hawakufikiria hilo, wanacho jaribu wao kung'ang'ania madaraka tu, huku mbunge wa tanzania huku mbunge wa EAC, wengine huku mbunge huku waziri waziri wa EAC, wao wanatafuta kila njia ya ulaji, na sio kutafuta njia za kuwakomboa wananchi ?

Leo hii mchakato wa katiba ukiangalia wanao toa maoni utacheka, mtua anatoa maoni eti vbijana wasivae suruali magotini, sijui sketi, mchakato wa katiba umenifumbua kuwa kuna idadi kubwa ya wananchi ambao hawana elimu hata ile ya secondari, nafikiri serikali ingejikita zaidi pia katika elimu, iwalazimishe ambao wasikuwa na ajira kupatiwa elimu na kuwapa welfare ili kuweza kuwapeleka katika daraja jengine.

Nilitegemea kuona maoni ya katika nchi kama Tanganyika yenye rasilimali kubwa ,kuona wananchi wanaoa maoni kwa mfano, serikali iweke welfare benefit kwa wale wasikuwa na ajira,wazee kupatiwa malipo pamoja na watoto, serikali kuwajengea makazi wananchi na kuwapa bure au kulipia fedha kidogo sana, katika huduma hizi fedha zitoke katika rasilimali za nchi, kwa silimia kuanzia 30 hadi 50.

Elimu iwe bure, na elimu iboreshwe, mfumo wa elimu ubadilishwe uwendane na wa kimataifa, mtu hata akiwa hana secondary akitaka kusoma hata awe na umri wa zaidi wa maika 20 aweze kurudi kusoma apate alimu hadi ya juu.

Nilitegemeo kuona wananchi wakisema kuwa rais asiwe ndio amiri jeshi mkuu wa nchi, ili vyombo vya ulizi kutojishirikisha kisiasa kwa kuwaonea wananchi.

Nilitegemea kuona wananchi wakitoa maoni wakisema kuwa jeshi la police liwe halina haki ya kumpiga mwananchi au kumnyanyasa kwa njia ya yoyote ile ! kAMA vile nchi za wenzetu, tunaona wananchi wanaandana japokuwa maandamano yanakuwa yako kivyume lakini police hathubutu kumpiga mwananchi,m badala yake wanawakamata tu nakuwapeleka wanako husika.

Hivi kulikuwa na kura ya maoni Zanzibar ya aina ya muungano?
 
Nani kakwambia?Acha assumptions zisizo na mshiko.
ukivunja muungano kwa sababu hiyo maanake baadaye hata hiyo Tanzania Bara au Azania unayoipigia chepuo haitasalimika. Mkoa au jimbo litakaloshindwa kuchangia mapato ya kuendesha Serikali itafukuzwa? Suala hapa tusifanye muundo wa utawala na muungano kuwa sera na Ilani ya vyama vya siasa.
 
Serikali moja na utawala wa majimbo ndo suluhisho
Serikali moja? Hii ilishindikana mwanzoni kabisa wakati waasisi wapo madarakani sembuse wakati huu, tatu tu ndo muarobaini. Mbili ni kuendeleza matatizo na kudumaza maendeleo ya nchi ila kwa watakao teuliwa kutatua matatizo watakuwa wananeemeka tu.
 
Mie naamini wale wanaotetea muundo huu wa serikali mbili wanafaidika nao kimaslahi kuliko sie wananchi haswa tunaotaka kuuboresha.
 
Kumekuwa na mjadala na ubishani wa kimtazamo katika suala la muundo siyo tu wa kiutawalawa dola (Serkali) lakini pia muungano wetu. Kwa kweli mambo haya mawilihayawezi (muundo wa utawala na muundo wa muungano) kutenganishwa.

Ndiyo maana ni maoni yangu kuwa mfumo wa utawala na muungano haviwezi kuwa sera au ilani ya chama cha siasa. Haya ni masuala ya msingi ya uwepo wa taifa letu na wote tukubaliane ni lazima yawe ndani ya Katiba yetu ya nchi. Lakini haiwezi kuwekwa hivi hivi bila kujenga muafaka wa kitaifa. Tunapaswa kuyajadili nakufikia muafaka wa mfumo tuutakao na baada ya hapo kuuweka katika Katiba. Kinyume chake kwenda na mtiririko huu wa kivyama vya siasa itatuwia vigumu kuufikia huomuafaka na itatugawa. Tuache vyama vishindane kwa kutueleza katika ilani zao ni jinsi gani ya kuendesha Serkali kwa gharama ndogo katika mfumo tuliokubaliana.

Huu ujinga ulianzishwa na CCM chini ya hayati Baba wa Taifa JKN. Kwamba sera ya CCM ni serikali mbili kuelekea Serikali moja. Nafikiri mawazo ya CCM na Nyerere wakati ule ilikuwa ni kwamba CCM itatawala MILELE. Ajabu ni kwamba hata vyama vya upinzani vimeingia kwenye mtego huu wa Panya wa CCM. Sasa tunasikia CDM nao wanasema sera yao ni Serikali tatu, CUF wao wanasema sera yao ni Muungano wa Mkataba, DP wao wanasema sera yao ni Kuvunja MUUNGANO. Sijui NCCR, TLP, UDP wao wanasimamia wapi.

Suala la muundo wa muungano ni suala la KIKATIBA. Na si ILANI (Manifesto) ya chama cha SIASA na katika katiba mpya tunataka litamkwa waziwazi, hata muundo wa wizara zetu, madaraka mikoani/sera za majimbo. Haiwezekani kila chama kinachoingia madarakani kuja na muundo wake wa Muungano. Huu ni uwendawazimu, hata Banana republic huwezi kupata UJINGA wa aina hii.

Suluhisho la matatizo ya muungano wetu ni wa aina mbili tu. Haya mengine ni kuzunguka mbuyu.
  1. Tuwe na nchi moja, serikali moja, Rais mmoja, Unguja na Pemba iwe mikoa ya 31 na 32 ya JMT.
  2. Kama hilo haliwezekani basi tuvunje Muungano kila nchi (Tanganyika na Zanzibar zijijue)

That are the only practical solution.
Shirikisho la Afrika mashariki.

Mchakato wa Kuiunganisha Afrika Mashariki (uk. 90-92)

Miongoni mwa mambo mengine, kamati hiyo ilitengeneza ratiba iliyotaka mambo yafuatayo:

a. Rasimu ya katiba ya shirikisho la Afrika Mashariki ifikapo Desemba 2007
b. Kupitishwa katiba na mkutano wa Wakuu wa Nchi mwezi Januari 2009
c. Kura ya maoni kuhusu katiba ifikapo Desemba 2009
d. Shirikisho la kisiasa lenye urais wa mzunguko ifikapo 2010 na uchaguzi wa rais ifikapo 2013
Mkutano wa Wakuu wa Nchi Usio wa Kawaida uliofanyika Dar es Salaam mwezi Mei 2005 ulielekeza kuundwa kwa utaratibu wa mashauriano ya kitaifa kukusanya maoni kutoka kwa Waafrika Mashariki juu ya Shirikisho la Afrika Mashariki na kuharakisha mchakato huo.
Michakato ya mashauriano ya kitaifa ilizinduliwa mwezi Oktoba nchini Tanzania, Kenya na Uganda na mwaka 2008 nchini Rwanda na Burundi.

Waafrika Mashariki walikubaliana kwa kauli moja juu ya shirikisho la kisiasa.

Yalitolewa pia mawazo ya kupinga uharakishwaji. Wasiwasi mmoja uliojitokeza kutokana na mchakato wa mashauriano nchini Tanzania ulikuwa ni suala la kuitenga Zanzibar kabisa, chini ya serikali ya Muungano katika serikali ya shirikisho.

Link kituochakatiba

Kwa kweli hata kesho Nchi za Afrika ya Mashariki zikiamua kuungana, na Tanzania ikawa ni mshiriki, naamini kuwa ni rahisi zaidi kushirikisha Tanzania yenye Serikali Mbili - ya Zanzibar na ya Tanganyika - kuliko Tanzania yenye Serikali Mbili, ya Tanzania na ya Zanzibar.Uk 11-12 link Uongozi Wetu Na Hatma Ya Tanzania (by Nyerere)

(ii) Pendekezo la kugeuza mfumo wa Muungano wa Serikali Mbili, na kuleta mfumo wa Shirikisho la Serikali Tatu uk 1

Wakawaambie wabunge wahusika kwamba hoja yao ya kutaka Serikari Tatu ni kinyume cha sera ya chama chao, na ina hatari ya kuigawa na kuiangamiza Nchi yetu uk 13

Muundo wa Muungano, pamoja na kwamba hatutaki uwe ukitibuliwa tibuliwa mara kwa mara, ni suala la sera, si amri ya Mungu. Vyama vya siasa mbali mbali vinaweza vikawa na maoni mbali mbali kuhusu muundo unaofaa kwa Katiba ya nchi yetu.uk 18

Basi na tutafute mfumo ambao utaiondolea Zanzibar hofu hii ya kumezwa, bila kuibebesha Tanganyika mzigo wa kuendesha Serikali mbili zenye uzito unaolingana uk 11

Mzizi wa tatizo kuu la muungano unabainishwa hapa Link https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/334649-tundu-lissu-na-kiini-macho-cha-muungano.html


Tume ya Warioba ndio inamalizia kukusanya maoni, hujachelewa, tuma maoni yako kwa maandishi sasa. Au mfumo utabaki wa serikali mbili kama ulivyo sasa, hiyo ndio sera ya CCM. Serikali mbili kuelekea moja.

Kwa wanaotegemea kuwa uchaguzi mkuu wa 2015 utatumia Katiba mpya wanajidanganya. Haitapitishwa katika kura ya maoni. Bado madai ya tume huru ya uchaguzi na kubadilisha sheria za uchaguzi ni muhimu kabla 2014.

Katiba mpya "ploy" is another kiini macho cha CCM.

 
Solution ni kuvunja muungano na nchi za Tanganyika na Zanzibar zirudishwe kama zilivyokuwa kabla ya muungano. Mfumo wowote ule wa muungano hautatatua matatizo tunayoyapata sasa hivi ya kutoaminiana na ya kiuchumi. Hivi mlishawahi kusikia faida zozote au tathmini yoyote za/ya muungano katika kukuza uchumi wa nchi yetu?
 
Serikali moja? Hii ilishindikana mwanzoni kabisa wakati waasisi wapo madarakani sembuse wakati huu, tatu tu ndo muarobaini. Mbili ni kuendeleza matatizo na kudumaza maendeleo ya nchi ila kwa watakao teuliwa kutatua matatizo watakuwa wananeemeka tu.

Muundo wa Serkali moja haukusindikana kwani haukujaribiwa. Ni bahati mbaya Nyerere aliukataa kwa sababu ya kuogopa kuimeza Zanzibar (kwa fikra tu). Je unafikiri Serkali tatu hazitazalisha matatizo na pengine makubwa kuliko ya sasa ya Serkali mbili?
 
Huu ujinga ulianzishwa na CCM chini ya hayati Baba wa Taifa JKN. Kwamba sera ya CCM ni serikali mbili kuelekea Serikali moja. Nafikiri mawazo ya CCM na Nyerere wakati ule ilikuwa ni kwamba CCM itatawala MILELE. Ajabu ni kwamba hata vyama vya upinzani vimeingia kwenye mtego huu wa Panya wa CCM. Sasa tunasikia CDM nao wanasema sera yao ni Serikali tatu, CUF wao wanasema sera yao ni Muungano wa Mkataba, DP wao wanasema sera yao ni Kuvunja MUUNGANO. Sijui NCCR, TLP, UDP wao wanasimamia wapi

Suala la muundo wa muungano ni suala la KIKATIBA. Na si ILANI (Manifesto) ya chama cha SIASA na katika katiba mpya tunataka litamkwa waziwazi, hata muundo wa wizara zetu, madaraka mikoani/sera za majimbo. Haiwezekani kila chama kinachoingia madarakani kuja na muundo wake wa Muungano. Huu ni uwendawazimu, hata Banana republic huwezi kupata UJINGA wa aina hii.

Suluhisho la matatizo ya muungano wetu ni wa aina mbili tu. Haya mengine ni kuzunguka mbuyu.
  1. Tuwe na nchi moja, serikali moja, Rais mmoja, Unguja na Pemba iwe mikoa ya 31 na 32 ya JMT.
  2. Kama hilo haliwezekani basi tuvunje Muungano kila nchi (Tanganyika na Zanzibar zijijue)

That are the only practical solution.

Hii pia ilichangiwa na jinsi tulivyoingia katika mfumo wa vyama vingi; hatukujiandaa na kuweka misingi iliyohitajika. Nakubaliana na wewe kabisa kwamba CCM walidhani wataendelea kutawala na hivyo kutoa sababu nyepesi kwa masuala mazito Kama haya. Ndiyo maana sasa tunasukumwa kutengeneza katiba bila kuafikiana vitu vya msingi Kama hivi vya muundo na muungano. Nina wasiwasi Kama tutafikia muafaka utakaotuvusha salama.
 
Hivi kulikuwa na kura ya maoni Zanzibar ya aina ya muungano?
Nimeongea kura ya maoni ya kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa, na katika uchukuwaji maoni, ukilinganisha maoni ya watoaji maoni ya katiba, wanao taka mkataba ni asilimia kubwa, hio ni kipima joto au upepo , kwa maana ya kwamba hata kama ingeletwa kura ya maoni basi aidha asilimia kubwa ingeanguka kukataliwa muungano au mkataba.
 
GHIBUU, Nguruvi3,

..Chadema wamependekeza kura ya maoni ktk kujitoa ktk muungano.

..kitu cha ajabu kabisa hawakupendekeza kura ya maoni ktk kuunda na muungano wa serikali 3.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom