Muswada wa Marekebisho katika Sheria ya Vyama vya Siasa: Tunahitaji mjadala mpana (Sehemu ya Kwanza)

Aug 31, 2010
9
13
Serikali imewasilisha Bungeni kwa mara ya kwanza muswada wa marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa. Muswada huu unahitaji mjadala mpana ukiwashirikisha wadau wote ili tuweze kutataua baadhi ya changamoto zilizojitokeza katika uwanja wa siasa, na muhimu zaidi tuweze kusonga mbele na kuimarisha demokrasia nchini.

Muswada huu una mapendekezo machache mazuri, lakini kwa kiwango kikubwa una mapendekezo ambayo yatafifisha demokrasia iwapo mapendekezo haya yatapitishwa na Bunge.

Dhumuni la andishi hili ni kujaribu kuainisha baadhi tu ya mapungufu makubwa ambayo yanaweza kupelekea kuua mfumo wa vyama vingi ambao tumekuwa tukiendelea kuujenga na kuuimarisha.

Ni muhimu tukumbuke kuwa jukumu la kujenga demokrasia ya vyama vingi, ni jukumu la Watanzania, na si la nchi wahisani wala wafadhili na wala watawala. Ni sisi ndio tuna wajibu wa kupiga kelele pale tunapoona misingi ya demokrasia na utawala bora inaminywa.

Kama ambavyo tuna matatizo katika sheria nyingine, mapendekezo ya mabadiliko ya sheria hii yanampa madaraka makubwa sana Msajili wa vyama vya siasa.

Nitajaribu kueleza. Ila kabla ya kueleza, tujiulize maswali yafuatayo: Hivi ni kweli ana madaraka makubwa? Na je kuna ubaya gani kumpa mtu mmoja madaraka makubwa sana? Kuna athari gani kwa Msajili wa Vyama Siasa kuwa na madaraka makubwa sana? Na swali linguine muhimu, je Msajili tuliye naye anapatikana vipi? Je, anakubalika na wadau wote wanaoshiriki katika siasa? yupo huru na haegemei au kupendelea upande wowote? Je, tunaweza sote tukasema bila unafiki kuwa Msajili tuliye naye ni ‘neutra’, ‘impartial’? na independent?

Nianze na swali la kwanza : Kwa mujibu wa mapendekezo haya, ni maoni yangu kuwa Msajili wa vyama vya siasa amepewa madaraka makubwa sana. Katika kifungu cha nne kwa mfano, kinapendekeza kurekebishwa ili kubainisha majukumu ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa. Kipengele ‘C’ kinasema kuwa Msajili ataangalia chaguzi za ndani za vyama na mchakato wa uchaguzi. Haya ni madaraka makubwa sana na yanaingilia uhuru wa vyama vya siasa katika kuendesha mambo yao ya ndani kwa mujibu wa katiba zao. Itakuwa ni vyema sana tukipata ufafanuzi ya mantiki na faida za kumpa Msajili madaraka haya. Tunataka tupate matokeo gani? Ni jambo gani jema litapatikana kwa kumpa Msajili madaraka haya?

Ni sababu zipi zilizopelekea Msajili wa Vyama kupewa jukumu hili? Unaweza kusema labda ni kwa sababu chaguzi nyingi za baadhi ya vyama vya siasa hugubikwa na mizengwe, ukiukaji wa sheria, kanuni na katiba za vyama. Hili si jukumu la Msajili, bali ni jukumu la wanachama husika kuhakikisha kuwa chama chao kinafuata katiba na kanuni za uchaguzi walizojiwekea. Na Msajili ana mamlaka ya kuingilia kuona haki inatendeka pale wanachama wa chama cha siasa wanapohitaji Msajili kuingilia kati mgogoro uliopo ndani ya chama na kutoa haki. Kazi ya kulinda katiba, kanuni na kuhakikisha kuwa chaguzi zinafanyika kwa mujibu wa katiba na kanuni na uchaguzi ni wa haki na huru, ni kazi na wajibu wa wanachama wenyewe na sio Msajili wa Vyama vya Siasa. Mathalani, ni jukumu la wana CCM kuhakikisha kuwa utaratibu wa kura za maoni za kuwapata wagombea wa nafasi mbalimbali ama za Ubunge au Udiwani, zinafuatwa kwa mujibu wa katiba ya chama chao na kanuni zao.

Lipo swali la msingi sana: Je, Ofisi ya Msajili itaangalia chaguzi za vyama katika chaguzi za ngazi zote? Kama jibu ni ndio, je Ofisi hii ina rasilimali watu na fedha za kutosha kuweza kuangalia chaguzi zote za vyama vyote katika ngazi zote? Na kama jibu ni hapana, labda wataangalia chaguzi za ngazi ya Kitaifa, au Mkoa au Wilaya, je kuna faida gani kufanya hivyo na kuacha chaguzi katika ngazi za chini?

Kipengele ‘D’ kinampa Msajili mamlaka makubwa sana ya kusimamia utoaji wa elimu ya uraia kwa vyama vya siasa. Aidha kinaendelea kusema kuwa mtu yeyote au taasisi yoyote ya ndani au nje ambayo inataka kutoa elimu ya uraia au kujenga uwezo kwa chama cha siasa, kabla ya kufanya hivyo, mtu au taasisi hiyo italazimika kumtaarifu kwa maandishi Msajili na kueleza malengo na aina ya mafunzo, washiriki katika mafunzo hayo, zana za kufundishia (teaching aids) na matokeo tarajiwa.Msajili akipokea taarifa hiyo anaweza kukataa kutolewa mafunzo hayo au program yoyote ya kuwajengea uwezo na kutoa sababu.

Taasisi au mtu yeyote atakayekiuka kifungu hiki atahukumiwa, kupigwa faini sio chini ya milioni moja lakini isizidi milioni tano au kwenda jela sio chini ya miezi sita lakini isizidi miezi kumi na mbili au vyote viwili.Kipengele hiki kitaleta ugumu sana kwa vyama vyenye mashirikiano (sister parties) kutoka katika nchi mbalimbali kuweza kuwa na program za kujengeana uwezo, na kuendesha mafunzo kwa watendaji wake.

Piaasasi mbalimbali, wafadhili nao watakumbana na kikwazo katika kuendesha programu za mafunzo kwa vyama vya siasa. Kinachotia mashaka zaidi ni adhabu zinazotolewa kwa kuendesha mafunzo bila kibali cha Msajili wa Vyama. Hapa tena tunaona madaraka makubwa sana ambayo amepewa Msajili ya ama kukubali au kukataa utoaji wa elimu ya uraia na chama cha siasa ama kupata au kutopata mafunzo. Madaraka haya yamewekwa kwa mtu mmoja. Na maamuzi yake ni ya mwisho!

Kipengele 5B kinampa mamlaka Msajili kuwa anaweza kudai kupewa taarifa na kiongozi wa chama cha cha siasa au mwanachama kama zitakavyohitajika. Iwapo Kiongozi wa chama au mwanachama atakiuka kifungu hiki basi naye atakuwa ametenda kosa na atapewa adhabu ambazo nazo zimetajwa ikiwa ni pamoja na faini au kifungu au vyote viwili. Kipengele hiki kinaminya uhuru wa chama cha siasa, kwani baadhi ya taarifa zinaweza kuwa zinahusiana na masuala ya binafsi ya kichama ambayo chama husika wanaweza kuwa wasipende kuitoa kwa Msajili. Katiba yetu ya sasa inatambua haki ya faragha na usiri. Matahalani, taarifa iliyosheheni mikakati halali ya kupata ushindi kwa chama cha siasa, taarifa hii inaweza kuwa sio muafaka kwa chama husika kuiwasilisha kwa Msajili na hasa katika mazingira haya ambayo uhuru wa Ofisi ya Msajili bado unahojiwa na mazingira ya kutoaminiana katika medani ya siasa.

Yawezekana kuwa kipengele hiki kimependekezwa kulenga taarifa za fedha na hasa misaada ya fedha ambayo vyama hupokea kutoka kwa wafadhili wa ndani na nje nchi. Kuna uoga kuwa misaada hii yawezekana huwa inaliwa na wajanja wachache ndani ya vyama vya siasa au baadhi ya wafadhili wanaweza kutumia fedha zao ili tu kuondoa utangamano uliopo nchini. Hivyo, ni vyema kuwabaini ni kina nani hao wanaotoa fedha kwa vyama vya siasa na kwa malengo gani. Yawezekana kipengele hiki kinajaribu kuziba mwanya huu.

Kwa mfano, iwapo CCM imepokea msaada wa fedha kutoka China, kwa mfano, Msajili ana mamlaka ya kudai kupewa hizi taarifa kutoka kwa Mwenyekiti au Mwanachama na endapo wawili hao hawatatoa taarifa hizo basi wakabiliwe na adhabu kali kabisa.Nadhani hili ndio lengo ambalo si baya, ila tu kinachokosekana hapa ni kuaminiana. Swali la kujiuliza : Je, Msajili ataweza kutenda haki na sawasawa kwa chama tawala na vyama vya upinzani? Je, Vyama vya upinzani vina imani na Msajili? Vyama vya upinzani vina sababu za msingi kuamini kuwa Msajili anaweza asitende haki.

Kama ni hivyo, basi tutafute utaratibu wa kumpata Msajili ambaye atakubalika na kuonekana miongoni mwa wadau wote kuwa ana uhuru na hawezi kuegemea upande wowote. Pia kama lengo ni kuwa na uwazi kuhusiana na vyanzo vya mapato vya vyama, basi tuweke utaratibu wa kuwa timu maalum ya wakaguzi wa mahesabu ambao miongoni mwao watoke katika vyama vya siasa, kwa maana chama tawala na vyama vya upinzani. Aidha hali hii inaoyesha umuhimu mkubwa wa kukamilisha suala zima la kukamilisha mchakato wa kuandika katiba mpya na kuzipitia upya baadhi ya sheria kadhaa kama vile sheria ya gharama za uchaguzi n.k.


Itaendelea… hapa Muswada wa Marekebisho katika Sheria ya Vyama vya Siasa: Tunahitaji mjadala mpana (Sehemu ya Mwisho) - JamiiForums
 
Huwezi kusema unahitaji mjadala mpana bila kututajia mazuri ya muswada...yaani unataka kuukataa muswada wa vipengele vitatu tu? C D na B?
Mkuu,

Kuna sehemu imeandikwa kuwa tuukatae muswada? Umesoma kilichoandikwa kwa undani? Utaona kuwa kuna maeneo napongeza nia ya waandaaji lakini na mapendekezo yamewekwa. Mapendekezo yanaletwa kwa nia njema.

Kama wewe ni miongoni mwa waandaaji, natarajia utasoma kwa kina na kuona hoja ni nini badala ya kufikiria kuwa tunapinga tu.
 
Tatizo ni mswada wote au baadhi ya vipengele?Hamtaki muswada wote au Vipengele baadhi?
Huwezi kusema unahitaji mjadala mpana bila kututajia mazuri ya muswada...yaani unataka kuukataa muswada wa vipengele vitatu tu? C D na B?
Jadili muswada.

Nikikupa juice ya lita moja kisha nikatia ndani yake kipande kidogo cha kinyesi cha binadamu utakunywa? Ulivyomjinga unaangalia uchache wa vipengele huangalii uzito wake! Sishangai kwa sababu ni fisiem lazima utetee bila kufikiria.

Hata ingekuwa kipengele kimoja tunahaki ya kujadili, Quality ni muhimu zaidi kuliko Quantity.
 
Tatizo ni mswada wote au baadhi ya vipengele?Hamtaki muswada wote au Vipengele baadhi?
Huwezi kusema unahitaji mjadala mpana bila kututajia mazuri ya muswada...yaani unataka kuukataa muswada wa vipengele vitatu tu? C D na B?
MTU anashindwa kuleta mswada wote analeta vipengele hasivyovipenda yeye
 
Tatizo ni mswada wote au baadhi ya vipengele?Hamtaki muswada wote au Vipengele baadhi?
Huwezi kusema unahitaji mjadala mpana bila kututajia mazuri ya muswada...yaani unataka kuukataa muswada wa vipengele vitatu tu? C D na B?
Ni muhimu ujifunze kusoma kwa makini, hakuna sehemu yoyote ambapo mleta mada kasema anaupinga mswada mzima
 
Tatizo ni mswada wote au baadhi ya vipengele?Hamtaki muswada wote au Vipengele baadhi?
Huwezi kusema unahitaji mjadala mpana bila kututajia mazuri ya muswada...yaani unataka kuukataa muswada wa vipengele vitatu tu? C D na B?
Huwezi kupuuza umuhimu wa kuwa na mjadala mpana hata kama muswada ungekuwa ni mzuri kiasi gani. Umuhimu wa mjadala mpana upo pale pale. Unless kama mnaamini au unaamini kuwa nynyi ndio mnajua kila kitu na nyinyi ndio mna mawazo mazuri. Wengine hatuna mawazo.

Na kama unaamini hivyo basi ni hatari. Naomba uelewe kuwa hiyo ni sehemu ya kwanza, sehemu itakayofuata, itakayoendelea, itajadili kwa kuvieleza vifungu vyote vyenye mapungufu. Pia itaeleza vile vifungu vichache vizuri. Lengo ni kuamsha mjadala.

Nategemea kutoka kwako uni challenge kwa hoja na uje na mtazamo wako ambao si sawa na wangu, kwa hoja. Inaweza ikawa hujusoma hata muswada wenyewe. Nakushauri nenda kasome muswada, pia soma makala yangu YOTE kwa utulivu halafu tujadili.

Nikupe angalizo tu: Vipengele vile vibaya vina defeat purpose nzima na vinaufanya muswada wote usio na maana hata vile vipengele vichache vizuri vinakuwa havina maana tena. Vitakuwa na maana gani iwapo Msajili ana mamlaka makubwa namna ile ya hata kukifuta chama?!!!! na hakuna mahali ambapo maamuzi yake yanaweza kuwa challenged?!!
 
Tatizo ni mswada wote au baadhi ya vipengele?Hamtaki muswada wote au Vipengele baadhi?
Huwezi kusema unahitaji mjadala mpana bila kututajia mazuri ya muswada...yaani unataka kuukataa muswada wa vipengele vitatu tu? C D na B?
jingalao wewe kwako haiwezi tokea ukao ubovu wa yale yaliotendwa na selikali badala yake wewe ni kupiga vigeregere hata Kama jiwe kajamba ua sio jingajinga
 
Ushirikishwaji katika suala lolote lenye maslahi kwa pande zote ni wa lazima. Hivyo ni muhimu kutumia majukwaa yaliyopo katika kujadili suala hili ili liwe na rejelea / kumbukumbu ya kutosha pale itakapokuwa inahitajika.

Kuhusu chaguzi ndani ya vyama, msajili anayo haki ya kujua zinavyoendeshwa / zilivyofanyika ili zisikiuke katiba ya vyama hivyo na kuleta mizozo ndani ya vyama. Hili nalo lina shida gani? Mbona wakati wa usajili lazima mpeleke katiba zenu kwa Msajili?
Hata hivyo, sioni ni kwa vipi chama kilete watu kutoka nje kuja kuwajengea uwezo kwani kwa kufanya hivyo, unaweza ukajikuta mnatoa mianya kwa wenye nia ovu kwa taifa letu, kujipenyeza!

Aidha, tunavyo vyuo ambavyo, kama tutahitaji kuwawezesha viongozi na wanachama wetu, vinaweza kutoa elimu hiyo. Kutumia watu kutoka nje wasiojua utamaduni, mila na desturi zetu ni hatari!

Kuhusu misaada kwa vyama, kuna shida gani msajili akijua makusudio yake? Ikitokea ikawa na maksudi mabaya kwa usalama wa taifa letu?

Kumbukeni kuwa, Msajili wa Vyama vya Siasa ndiye mlezi wa vyama na hivyo sio rahisi, jicho lake litenganishwe na vyama!
 
Ushirikishwaji katika suala lolote lenye maslahi kwa pande zote ni wa lazima. Hivyo ni muhimu kutumia majukwaa yaliyopo katika kujadili suala hili ili liwe na rejelea / kumbukumbu ya kutosha pale itakapokuwa inahitajika.

Kuhusu chaguzi ndani ya vyama, msajili anayo haki ya kujua zinavyoendeshwa / zilivyofanyika ili zisikiuke katiba ya vyama hivyo na kuleta mizozo ndani ya vyama. Hili nalo lina shida gani? Mbona wakati wa usajili lazima mpeleke katiba zenu kwa Msajili?
Hata hivyo, sioni ni kwa vipi chama kilete watu kutoka nje kuja kuwajengea uwezo kwani kwa kufanya hivyo, unaweza ukajikuta mnatoa mianya kwa wenye nia ovu kwa taifa letu, kujipenyeza!

Aidha, tunavyo vyuo ambavyo, kama tutahitaji kuwawezesha viongozi na wanachama wetu, vinaweza kutoa elimu hiyo. Kutumia watu kutoka nje wasiojua utamaduni, mila na desturi zetu ni hatari!

Kuhusu misaada kwa vyama, kuna shida gani msajili akijua makusudio yake? Ikitokea ikawa na maksudi mabaya kwa usalama wa taifa letu?

Kumbukeni kuwa, Msajili wa Vyama vya Siasa ndiye mlezi wa vyama na hivyo sio rahisi, jicho lake litenganishwe na vyama!

Ahsante kwa maoni yako. Nakushukuru. Lakini rejea moja ya paragraph katika andiko langu na hasa linalozungumzia uhuru wa Msajili wa Vyama vya Siasa. Nimeuliza na naomba nikuulize na wewe: Je Msajili wa vyama yupo huru? Yupo neutral na impartial? Hoja ni kuwa Msajili amepwa madaraka makubwa sana. na Msajili anavyopatika ni kuwa anateuliwa na Rais ambaye Rais pia ni Mwenyekiti wa CCM.

Hoja hapa ni kuwa Msajili anaweza kukipendelea chama tawala na kukandamiza vyama vya upinzania na hasa chama kikuu cha upinzani kama tunavyoona msimamo wa Msajili katika suala la mgogoro wa CUF.

Hivyo basi kuna ubaya kumpa Msajili madaraka makubwa msajili ambaye anaegemea upande wa chama tawala. Hilo wewe hulioni?!! Hivi kwanini mna wasiwasi Ndio maana Tume ya Warioba ilipendekeza utaratibu mzuri wa kumpata Msajili ambaye atakubalika na pande zote na sio yule tu anaykubalika na wale waliomteua.

Na taasisi za nje? hivi zote zina nia ovu? kwa nini mna wasiwasi sana?

Bado sijapata hoja ya msingi. Hivi kwa nini kibali cha kufanya kuwafundisha madiwani wa chama 'A' kitolewe na Msajili? kwa nini yeye tu ndio awe na mamlaka ya ama kuruhu au kutoruhusu civc education kutolewa?

Hivi kuna mantiki gani kusema kuwa chama kisiwe kama presuure group ya ku influence jamii?

Kuna mantiki gani ya kusema kuwa ukitaka kuandikisha chama lazima uwe na miaka 21? je kama nina miaka 20? kuna tofauti gani?
 
Ushirikishwaji katika suala lolote lenye maslahi kwa pande zote ni wa lazima. Hivyo ni muhimu kutumia majukwaa yaliyopo katika kujadili suala hili ili liwe na rejelea / kumbukumbu ya kutosha pale itakapokuwa inahitajika.

Kuhusu chaguzi ndani ya vyama, msajili anayo haki ya kujua zinavyoendeshwa / zilivyofanyika ili zisikiuke katiba ya vyama hivyo na kuleta mizozo ndani ya vyama. Hili nalo lina shida gani? Mbona wakati wa usajili lazima mpeleke katiba zenu kwa Msajili?
Hata hivyo, sioni ni kwa vipi chama kilete watu kutoka nje kuja kuwajengea uwezo kwani kwa kufanya hivyo, unaweza ukajikuta mnatoa mianya kwa wenye nia ovu kwa taifa letu, kujipenyeza!

Aidha, tunavyo vyuo ambavyo, kama tutahitaji kuwawezesha viongozi na wanachama wetu, vinaweza kutoa elimu hiyo. Kutumia watu kutoka nje wasiojua utamaduni, mila na desturi zetu ni hatari!

Kuhusu misaada kwa vyama, kuna shida gani msajili akijua makusudio yake? Ikitokea ikawa na maksudi mabaya kwa usalama wa taifa letu?

Kumbukeni kuwa, Msajili wa Vyama vya Siasa ndiye mlezi wa vyama na hivyo sio rahisi, jicho lake litenganishwe na vyama!
Nami sioni mantiki ya wafadhili ambao most yao ni wazungu waje watujengee uwezo wa kuendesha siasa zetu.
Kwa kifupi umedadavua vizuri mzee naungana nawe
 
Vipengele vyote vya muswaada ni sawa kabisa kwa sababu shughuli za vyama vya siasa kimsingi zilitakiwa ziwe wazi kwa uma. Umemalizia vizuri kuwa utaratibu wa kumpata Msajili pia uwe democratic ili apatikane msajili neutral asiyependelea upande mmoja
 
Mimi nadhani kuwa jambo moja kubwa sana ni kufanya mabadiliko ya namna ya kumpata msajiri wa vyama. Ningetaka mtu huyu awe na mamlaka na wadhifa kama wa jaji kuhusu uendeshaji wa shughuli zake; vile vile itasaidia kuwapo kwa haki iwapo ofisi hii itahamishwa kutoka kwenye executive branch na kuwekwa kwenye judiciary branch.
 
Back
Top Bottom