Muongozo na ushauri kwa wanafunzi udahili vyuo vikuu 2015/16

Casuist

JF-Expert Member
Jul 23, 2014
1,179
2,940
Habari wakuu,

Kuna wadogo zetu walimaliza kidato cha sita na matokeo yao yametoka karibuni, kwa sasa wapo kwenye mchakato wa kujaza vyuo na uchaguzi wa shahada watazochukua. Ni ngwe muhimu sana kwenye maisha yao, kwa sababu ndio itayochagua awe nani baadae kitaaluma.

Shahada gani na chuo gani anaweza kwenda ni changamoto nyingine hasa kipindi hiki ambacho ushindani umekuwa mkubwa hadi kwa kozi za sayansi kinyume sana na kipindi cha nyuma. Kwa sasa kuna changamoto kubwa ya watu kwenda kusoma vitu wasivyotarajia dakika za mwisho na wengine kuahirisha kabisa masomo mpaka mwaka unaofata.

Hapa jukwaani kuna wanavyuo wengi ambao kwa sasa wanasoma vyuo na shahada ambazo wengine wangependa kwenda, kuna wahitimu wa hivyo vyuo na wanajua mazingira ya vyuo husika pia changamoto gani wamezipata kwenye hivyo vyuo na kuelekea kwenye ajira kulingana na shahada walizosoma.

Kwa pamoja naamini tunaweza kuwapa mwanga hawa wadogo zetu wapunguze idadi ya makosa yanayotokana na kutokuwa na ufahamu. Kwa heshima ningependa kuwaita LORDVILLE LISANDIME tzhumoally CDG Marco Polo mchepukomatope Chungu cha bibi na wengine wote katika kufikisha lengo la mada hii.

Karibuni!

Kitabu cha Mwongozo wa Vyuo na kozi cha TCU 2015/16
 
Mshaurini huyu tafadhali

Ni mtoto wa Jirani yangu Kamaliza 2013 PCM

Kapata C Maths, D Physics na S Chemistry
Je ataweza kupata corse gani kwa urahisi

Vyuo alivyopendekeza ni Ardhi, UDSM na DIT

Nimwemwuliza amesema anapenda civil engineering

Nawasilisha
 
Nadhani hayo matokeo sio ya BRN!! By the way simshaur aji limit kwenye vyuo hivyo tu. Itagemea na olevo alifaulu vipi...ila kwa ud kuna textile eng (kuna jamaa alikua na ufaulu wake akachaguliwa) ... kuna SUA (kama ni mla bata asijaze hiki chuo) ambapo anaeza jaza kozi za engineering...hata udom nao wana kozi za engineering ambazo anaeza pata... asisahau na MUST cha mbeya nako kuna koz ambazo zitamfaa pia!!! Na zaid ya yote muulize (japo unaeza uka ww ndio muhusika) yeye anapenda kozi zipi???
Mkuu nimwemwuliza amesema anapenda civil engineering
Civil hawezi kosa, aombe ardhi, MUST mbeya, asiache kuomba na DIT (kama akiweza aweke cha kwanza kabisa hiki), st joseph dar pangefaa sana ila shida yao ni ada!!!
 
Wanajamii mimi nilikuwa nahitaji msaada mwenye detail kuhusu joining instruction kwa waliopangiwa huko huwa zinatoka mda gani?
 
Ni mtoto wa Jirani yangu Kamaliza 2013 PCM

Kapata C Maths, D Physics na S Chemistry
Je ataweza kupata corse gani kwa urahisi

Vyuo alivyopendekeza ni Ardhi, UDSM na DIT

Nawasilisha

Wakuu kutokana na ushauri wenu jamaa kaweka hivi....

1. Civil Engineering (Ardhi University)
2. Civil Engineerin (UDSM)
3. Geomatics (Ardhi)
4. Irrigation Engineering (SUA)
5. Electrical Engineering (UDSM)

Naombeni mumshauri nini aweke na nini atoe kulingana na competition na matokeo yake
Ndugu LORDVILLE tzhumoally karibuni kwa ushauri

Ahsanteni.
 
Last edited by a moderator:
aombe geomatics au geoinfo ardhi university,udsm aombe hio textile kama alivyokuelekeza mdau hapo..udom wana environmental engineering,dit aombe civil au mechanical hizo course anaweza kupata na ni nzur sana tuu...

Ni mtoto wa Jirani yangu Kamaliza 2013 PCM

Kapata C Maths, D Physics na S Chemistry
Je ataweza kupata corse gani kwa urahisi

Vyuo alivyopendekeza ni Ardhi, UDSM na DIT

Nawasilisha

hio ya pili angeweka DIT nadhan maana udsm itakua ngumu sana kwake..kwa ushauri wangu geomatics angeweka first choice believ me hatoweza kuregret maisha yake yote..hio course ina ajira nyingi sana..even diploma holder wa hio course basi wanapeta mtaani(hio ni kwa ushauri wng)na jengine course za competition aanze kuweka juu kwa sababu kama hio electrical na irrigation akifika huko bas ujue pameshajaa..huku chini angeweka kama electrical ya MUST au geoinformatics ya UDOM
 
hio ya pili angeweka DIT nadhan maana udsm itakua ngumu sana kwake..kwa ushauri wangu geomatics angeweka first choice believ me hatoweza kuregret maisha yake yote..hio course ina ajira nyingi sana..even diploma holder wa hio course basi wanapeta mtaani(hio ni kwa ushauri wng)na jengine course za competition aanze kuweka juu kwa sababu kama hio electrical na irrigation akifika huko bas ujue pameshajaa..huku chini angeweka kama electrical ya MUST au geoinformatics ya UDOM

Nimekusoma mkuu,
Thanks.
 
Wakuu kutokana na ushauri wenu jamaa kaweka hivi....

1. Civil Engineering (Ardhi University)
2. Civil Engineerin (UDSM)
3. Geomatics (Ardhi)
4. Irrigation Engineering (SUA)
5. Electrical Engineering (UDSM)

Naombeni mumshauri nini aweke na nini atoe kulingana na competition na matokeo yake
Ndugu LORDVILLE tzhumoally karibuni kwa ushauri

Ahsanteni.
Kwanza hongera zakekwa kuwa na passion na engineering.
Kabla hajaendelea mbele je nyumbani mnajiweza/ada, maana hiyo geomatics sizani kama ni priority je what if akipangiwa huko alafu akakosa mkopo, je maisha ya chuo atayaweza??
Kwa ufaulu wake japo simkatishi tamaa ila khapo kwenye UDSM panatia shaka japo si mbaya pia akiweka!!

Kwa kozi ya irrigation, kama jamaa anapassion na kilimo na ujenzi kwa ujumla hapo ni pake (infact nna uzoefu nayo, hasa kwa pale SUA na kama atahitaji ufafanuzi wa hii kozi usisite kuuliza), incase akipata ana uhakika wa 100% maana nna uhakika bado ni priority.

Kutokana na matokeo yake na kama home mnajiweza basi aiache hiyo geomatic (sina hakika ni priority) japo tzhumoally katoa mapendekezo yake hapo juu!!! Pia ningependekeza aweke civil ya DIT kama mbadala wa hiyo geomatic
Naona angeeka hivi...
1. Civil Engineering (Ardhi University)
2.Civil engineering (DIT)
3.Irrigation and water resouces Engineering (SUA)
4.Architecture (ARDHI) au Civil ya UDSM (Kama mbadala wa geomatic)
5.Electrical Engineering (UDSM)

NB. Awe makini sana kwenye kuchagua vyuo ili kuepuka usumbufu wakati wa masomo yake.
Karibu.
 
Last edited by a moderator:
Kwanza hongera zakekwa kuwa na passion na engineering.
Kabla hajaendelea mbele je nyumbani mnajiweza/ada, maana hiyo geomatics sizani kama ni priority je what if akipangiwa huko alafu akakosa mkopo, je maisha ya chuo atayaweza??
Kwa ufaulu wake japo simkatishi tamaa ila khapo kwenye UDSM panatia shaka japo si mbaya pia akiweka!!

Kwa kozi ya irrigation, kama jamaa anapassion na kilimo na ujenzi kwa ujumla hapo ni pake (infact nna uzoefu nayo, hasa kwa pale SUA na kama atahitaji ufafanuzi wa hii kozi usisite kuuliza), incase akipata ana uhakika wa 100% maana nna uhakika bado ni priority.

Kutokana na matokeo yake na kama home mnajiweza basi aiache hiyo geomatic (sina hakika ni priority) japo tzhumoally katoa mapendekezo yake hapo juu!!! Pia ningependekeza aweke civil ya DIT kama mbadala wa hiyo geomatic
Naona angeeka hivi...
1. Civil Engineering (Ardhi University)
2.Civil engineering (DIT)
3.Irrigation and water resouces Engineering (SUA)
4.Architecture (ARDHI) au Civil ya UDSM (Kama mbadala wa geomatic)
5.Electrical Engineering (UDSM)

NB. Awe makini sana kwenye kuchagua vyuo ili kuepuka usumbufu wakati wa masomo yake.
Karibu.

mkuu kwa kuongezea geomatics ni priority..geoinformatics ndio sio priority..
 
Last edited by a moderator:
mkuu kwa kuongezea geomatics ni priority..geoinformatics ndio sio priority..
Nimekupata mkuu, nlichanganya na geoinformatics!!! ila kuna waliopata mikopo kwenye hiyo geomatics na je geomatics ndio survey ile ya miaka ile? au ni tofauti na survey??
 
Nimekupata mkuu, nlichanganya na geoinformatics!!! ila kuna waliopata mikopo kwenye hiyo geomatics na je geomatics ndio survey ile ya miaka ile? au ni tofauti na survey??

yaah geomatics ndio exactly land survey wameibadilisha jina saiv kama sikosei tokea mwaka 2005/2006..na mm ninaowajua wote wamepata mkopo na wameniambia ambao wapo mwaka wa kwanzs na wa pili saiv wote walipata mkopo..geoinfo imetolewa kutoka katika geomatics..ila geomatics ndio baba...
 
Detector tony,

Google the word "MUST", or Mbeya University of science.....
Then utaona website ya chuo, ingia na utaona sehemu wanakuambia "download admission form" au joining instructions.
Hizo joining instructions hazitumwi, ni wajibu wako kuzi-download zinazokuhusu na kuzijaza as appropriate.
Haya , kazi kwako...
 
Detector tony,

Google the word "MUST", or Mbeya University of science.....
Then utaona website ya chuo, ingia na utaona sehemu wanakuambia "download admission form" au joining instructions.
Hizo joining instructions hazitumwi, ni wajibu wako kuzi-download zinazokuhusu na kuzijaza as appropriate.
Haya , kazi kwako...


Comrade,unaposema hivyo unamaanisha watu wanaosoma Bachelor Degree au hata Ordinary Diploma? naomba kufahamu coz nimechaguliwa huko
 
Back
Top Bottom