Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,510
- 9,299
Mke asimulia jinsi mumewe alivyofanya unyama kwa kuwalipua na mafuta ya petroli akiwa na mtoto
Mkazi wa kijiji cha Mlazo, wilaya ya Chamwino, Mkami Mbarahi (19) na mwanaye wenye umri wa miezi mitatu wamelazwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma baada kujeruhiwa kwa moto na mumewe, kwenye maeneo mbalimbali ya mwili.
Tukio hilo lilitokea Juni, 28 mwaka huu kijijini hapo, ambapo mumewe anayejulikana kwa jina la Elias Warioba anadaiwa kumrushia chupa yenye mafuta ya petroli mkewe akiwa na mtoto mgongoni wakati akipika chakula cha usiku.
Akizungumza akiwa wodi namba 16 katika Hospitali hiyo, Mkami amesema mumewe alimpiga na chupa ya plastiki ambayo ilikuwa na mafuta ya petroli kichwani wakati akipika.
Akisimulia mkasa huo, Mama huyo amesema akiwa jikoni akiandaa chakula cha usiku huku akiwa amembeba mwanaye mgongoni alifika mume wake akiwa na chupa hiyo huku akihoji kwanini anapikia kuni.
“Aliniuliza kwa nini ninapikia kuni na je nikiunguza kibanda cha watu?nilimjibu kwani mimi sina akili mpaka niunguze. Baada ya majibu yangu alinirushia chupa yenye mafuta ambayo ilifunguka na kunimwagikia mimi na mtoto, moto ukatulipukia,”amesema.
Amefafanua kuwa baada ya hali hiyo alikimbia nje akiwa na mtoto akipiga kelele kuomba msaada kwa majirani huku mumewe akiondoka bila kutoa msaada wowote.
“Nimeungua maeneo ya kichwa hadi kifuani na mwanangu ameungua maeneo ya usoni, mikononi, tumboni na miguuni,”amesema.
Kamanda wa polisi mkoani Dodoma, Gilles muroto amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa anashikiliwa na polisi kwa mahojiano.
Mkazi wa kijiji cha Mlazo, wilaya ya Chamwino, Mkami Mbarahi (19) na mwanaye wenye umri wa miezi mitatu wamelazwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma baada kujeruhiwa kwa moto na mumewe, kwenye maeneo mbalimbali ya mwili.
Tukio hilo lilitokea Juni, 28 mwaka huu kijijini hapo, ambapo mumewe anayejulikana kwa jina la Elias Warioba anadaiwa kumrushia chupa yenye mafuta ya petroli mkewe akiwa na mtoto mgongoni wakati akipika chakula cha usiku.
Akizungumza akiwa wodi namba 16 katika Hospitali hiyo, Mkami amesema mumewe alimpiga na chupa ya plastiki ambayo ilikuwa na mafuta ya petroli kichwani wakati akipika.
Akisimulia mkasa huo, Mama huyo amesema akiwa jikoni akiandaa chakula cha usiku huku akiwa amembeba mwanaye mgongoni alifika mume wake akiwa na chupa hiyo huku akihoji kwanini anapikia kuni.
“Aliniuliza kwa nini ninapikia kuni na je nikiunguza kibanda cha watu?nilimjibu kwani mimi sina akili mpaka niunguze. Baada ya majibu yangu alinirushia chupa yenye mafuta ambayo ilifunguka na kunimwagikia mimi na mtoto, moto ukatulipukia,”amesema.
Amefafanua kuwa baada ya hali hiyo alikimbia nje akiwa na mtoto akipiga kelele kuomba msaada kwa majirani huku mumewe akiondoka bila kutoa msaada wowote.
“Nimeungua maeneo ya kichwa hadi kifuani na mwanangu ameungua maeneo ya usoni, mikononi, tumboni na miguuni,”amesema.
Kamanda wa polisi mkoani Dodoma, Gilles muroto amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa anashikiliwa na polisi kwa mahojiano.