Muhimbili: Hivi Waziri wa Afya anafanya nini?

Ntemi Kazwile

JF-Expert Member
May 14, 2010
2,182
307
Naandika kwa masikitiko baada ya kukumbana na mkasa wa kushindwa kuhudumiwa katika hospitali yetu ya taifa (MNH) kwa sababu CT scan ambayo mgonjwa wangu alitakiwa kupimwa ili aendelee na matibabu, hii ni hospitali kubwa zaidi ya kitaifa na bado haina basic working tools je hizo hospitali za mikoa na wilaya zina vitendea kazi?

Katika kujaribu kujua ni kwa nini MNH wanayo CT scan machine moja mbovu nilifuatilia kwenye mtandao kujua kifaa hiki kinagharimu kiasi gani na kugundua kuwa mashine moja, 2010 Refurbished MX 8000 16 Slice IDT CT scan, inauzwa kwa kati ya US$340,000 na $355,000 (sawa na malipo ya siku tatu tuliyokuwa tunawalipa Dowans/Richmond). Kwa maana nyingine kumbe pesa tunayo ila tatizo ni namna tunavyozitumia.

Ili kuokoa maisha ya mgonjwa wangu nimelazimika kulipa takribani laki mbili zaidi kuliko vile ningelipa kama ya kwetu (MNH) ingekuwa inafanya kazi, kwa maana hiyo nimeingizwa kwenye matumizi makubwa zaidi kutokana na uzembe wa viongozi wetu kuweka vipaumbele sawa sawa
 
Naandika kwa masikitiko baada ya kukumbana na mkasa wa kushindwa kuhudumiwa katika hospitali yetu ya taifa (MNH) kwa sababu CT scan ambayo mgonjwa wangu alitakiwa kupimwa ili aendelee na matibabu, hii ni hospitali kubwa zaidi ya kitaifa na bado haina basic working tools je hizo hospitali za mikoa na wilaya zina vitendea kazi?

Katika kujaribu kujua ni kwa nini MNH wanayo CT scan machine moja mbovu nilifuatilia kwenye mtandao kujua kifaa hiki kinagharimu kiasi gani na kugundua kuwa mashine moja, 2010 Refurbished MX 8000 16 Slice IDT CT scan, inauzwa kwa kati ya US$340,000 na $355,000 (sawa na malipo ya siku tatu tuliyokuwa tunawalipa Dowans/Richmond). Kwa maana nyingine kumbe pesa tunayo ila tatizo ni namna tunavyozitumia.


Ili kuokoa maisha ya mgonjwa wangu nimelazimika kulipa takribani laki mbili zaidi kuliko vile ningelipa kama ya kwetu (MNH) ingekuwa inafanya kazi, kwa maana hiyo nimeingizwa kwenye matumizi makubwa zaidi kutokana na uzembe wa viongozi wetu kuweka vipaumbele sawa sawa

FAIZAFAXY na vibaraka wote wa Mafisadi ktk CCM- Kifaa kinachotajwa kinagharimu Shilingi za Kitanzania 553,800,000/= tu fedha ambazo zingeweza kupatikana kama mfumo wa kifisadi wa CCM kulipana posho mara mbili ungeweza kuondolewa hivyo kufanywa wabunge wasipate posho ya kikao ya Shilingi 80,000/= kama inavyopendelkezwa na bajeti ya mbadala ya upinzani; hivyo kwa siku kiasi cha Shs 28,560,000/= kingeweza kuokolewa kutoka kwa wabunge 357 na na baada ya siku 19 tu Muhimbili wangeweza kununuliwa kifaa hicho na kuongezwa kingine ii kuwahudumia wananchi baada ya kutimia siku 38 katika kikao hichi cha bajeti.

Vifaa vingine kama hivi na vyaa inaz ingine pia vingeweza kupatikana kwa hospitali zote hapa ngini kama posho wanazolipana watumishi wa kada ya juu wa Serikali ya CCM pia wangesimamishiwa posho za vikao wanazolipana kwa kazi ambazo wanalipwa mishahara. Huko Serikalini wanalipana posho za kufikia hata milioni kwa kiako kimoja.
 
FAIZAFAXY na vibaraka wote wa Mafisadi ktk CCM- Kifaa kinachotajwa kinagharimu Shilingi za Kitanzania 553,800,000/= tu fedha ambazo zingeweza kupatikana kama mfumo wa kifisadi wa CCM kulipana posho mara mbili ungeweza kuondolewa hivyo kufanywa wabunge wasipate posho ya kikao ya Shilingi 80,000/= kama inavyopendelkezwa na bajeti ya mbadala ya upinzani; hivyo kwa siku kiasi cha Shs 28,560,000/= kingeweza kuokolewa kutoka kwa wabunge 357 na na baada ya siku 19 tu Muhimbili wangeweza kununuliwa kifaa hicho na kuongezwa kingine ii kuwahudumia wananchi baada ya kutimia siku 38 katika kikao hichi cha bajeti.

Vifaa vingine kama hivi na vyaa inaz ingine pia vingeweza kupatikana kwa hospitali zote hapa ngini kama posho wanazolipana watumishi wa kada ya juu wa Serikali ya CCM pia wangesimamishiwa posho za vikao wanazolipana kwa kazi ambazo wanalipwa mishahara. Huko Serikalini wanalipana posho za kufikia hata milioni kwa kiako kimoja.


Kwa watu hawa unaowaeleza hiki kwao ni sawa na msamiati wa Kichina, sijui kama watakuelewa!
 
Inasikitisha sana.Walau wewe ulikuwa nayo hiyo laki mbili ya kujazia,sasa wenzangu na mimi ambao ndiyo majority,hapo diagnosis isingefanyka tena na mgonjwa angerudishwa nyumbani akajifie
 
Huku mikoani ndo usiseme hizo huduma za Afya, jana ITV News Tanga kina mama wajawazito wanalala wawili kwa kitanda, dawa hakuna, mgonjwa akiandikiwa inabidi akanunue, huduma bure kwa wajawazito, watoto chini ya miaka 5, wazee kuanzia 60yrs, wenye magonjwa sugu....bado bajeti finyu ya Afya. Mungu tusaidie, vipaumbele 6 alivyovitaja jana mkuu wa kaya sikusikia Afya ikitajwa.
 
Huku mikoani ndo usiseme hizo huduma za Afya, jana ITV News Tanga kina mama wajawazito wanalala wawili kwa kitanda, dawa hakuna, mgonjwa akiandikiwa inabidi akanunue, huduma bure kwa wajawazito, watoto chini ya miaka 5, wazee kuanzia 60yrs, wenye magonjwa sugu....bado bajeti finyu ya Afya. Mungu tusaidie, vipaumbele 6 alivyovitaja jana mkuu wa kaya sikusikia Afya ikitajwa.

Mkuu mbona dawa zinaozea kwenye bohari ya taifa, MSD?

Halafu wanapanga mipango kuwa ifikapo mwaka 2012 kila mtoto awe anapata chakula shuleni, awe na laptop yake na kila shule iwe na umeme... kwa hali inavyokwenda hizi ahadi haziwezi kutekelezeka chini ya utawala wa CCM
 
Katika mambo yanayosikitisha ulimwenguni ni juu ya uwajibikaji wa madaktari wa Muhimbili N.H.

Nimetembelea wagonjwa mbalimbali katika hospitali hii, nikagundua bila kuwa na hongo hakuna tiba kwa mgonjwa wako. Madaktari wanapita kama hawakuoni kabisa. Juzi kuna jirani yangu alipata ajali ya kugongwa na gari. Alipata ajali hiyo saa moja jioni akapelekwa Muhimbili. Baada ya kutokumuona na chumba chake kufungwa siku tatu mfululizo na simu kutopatikana ikabidi tuanze utaratibu wa kufuatilia, tukamkuta muhimbili hana fahamu tangu allipofikishwa hospitalii hapo na amelazwa mlango wa kuingilia katika korido. Kilichoniuma ni bada ya kuulizia manesi wakasema anatakiwa kufanyiwa kipimo cha 'sitiskan' ambacho hakipo hapo hospitali (kibovu). Mtu huyu kwa hali yake alipaswa kuwa ICU nikashangaa namkuta pale mahali akiwa hajapata msaada wowote kbs!!! Ninavyoongea sasa hivi ni marehemu aliyekaa hosp siku tatu bila tiba!!

Jambo la pili kwa Serikali ni kuwa hivi kama zipo pesa 50m kumsafirisha Mbowe kwenda Arusha pasipo kumhoji, serikali inashindwa kutumia pesa hizo kununua kipimo hicho??

Pia hizo pesa zisingeweza kuongeza jengo (wodi) au basi hata vitanda vya wagonjwa mpaka watu wanalala chini??

Hii serikali haina mipango inayomfaidia mwananchi, watu wanatumia mabilioni katika kampeni na kusahau kabisa wagonjwa na wahitaji mbalimbali

Wana JF nadhani wakati umefika kuitoa mwaka 2015, haiifai jamii yetu kabisa
 
Hospitali zote za Serikali hazina msaada kwa wananchi, usipokuwa na hela hupati matibabu, bora hata hospitali binafsi sema uwezo wetu ndio huu mdg kwa walalahoi, natamani wote tungekuwa na kipato kizuri tuwaachie hayo mahospitali yao ( wao wanatibiwa nje) wawalaze hata mama zao huko na mabibi zao maana hata watoto wao wanatibiwa nje, Hii serikali yakishenzi kabisa mi naichukia kama nini . Mungu si atuondolee hii serikali jamani atupe viongozi wenye akili na wanaongoza nchi kwa maslahi ya wote na sio wanaojifikiria wao tu. POLE SANA KAKA YANGU.
 
Hayo ndiyo mambo ya msingi ya kuwaeleza watanzania kwa nini ccm haifai kuendelea kuwa kwenye madaraka, mtu anapata ajali alafu anakosa huduma mpaka anakufa!! du! hii kweli TZ na bado tutashuhudia mengi maana kila mmoja ananza taratibu kujenga ubinafsi yaani anaangalia maslahi yake kwanza, maslahi wakati unalipwa mshahara! anyway hata hao walio juu wanalipwa mishahara lakini wabinafsi.

Dawa ni kubadili mfumo.
 
miezi sita nyuma tulisikia malalamiko ya wananchi,hakuna mabadiliko yoyote ndio maana leo madaktari wanagoma,pamoja na madai mengine wanadai uboreshaji wa mazingira ya hospitali zetu.
 
Back
Top Bottom