Muafaka wa CUF na CCM

kwa wale watanganyika ambao wameshikilia bango kwamba zanzibar hakuna matatizo basi ningewaomba kile kipindi cha kampeni na uchaguzi waelekee pemba na wakifika kule hata kama sio cuf basi wajifanye cuf, kisha warudi tena hapa ukumbini waseme zanzibar hakuna matatizo, mie ningewaomba ndugu zangu wasiongelee jambo wasilolijua. tunajua yaliotukuta na yaliowakuta wazee wetu ambao wengine ni marehemu kwa sasa mungu awalaze pema. mjue tu kwamba inakera kusema kwamba hakuna matatizo wakati sisi tunawajua watu ambao washapoteza maisha kupitia matatizo yaliokuwepo, kama mnasubiri tvz ikupeni data za waliouwawa basi mtasubiri mpaka kiama, ila kama mnataka ukweli kutoka kwa waathirika basi waathirika tupo wengi.
 
rafiki yangu Kibunango kumbe unaota, kam huoti basi kimbilia Muhimbili haraka kwani Malaria inakuja, Leo kama Tanzania watasema cuf wameshinda uchaguzi Zenj ndio imetoka na anaebisha ndie atakuwa mhaini, kumbuka Abod Jumbe alikwishia wapi? na yeye alikuwa raisi mzima kama unavyotaka tuseme kwahiyo zenj tulieni
Taratibu unaanza kufahamu, sakata la Aboud Jumbe lililokwenda kwa jina la machafuko ya hali ya hewa na blah blah nyingi, ilikuwa ni moja ya salamu tu kuwa Zenj hawapo tayali kuburuzwa ama kumezwa... kuelekea serikali moja. inakupasa kukumbuka kuwa vilivyoungana ni jamhuri ya watu wa Zenj na jamhuri ya Tanganyika na kupatikana kwa Jamhuri ya Muungano wa TZ... sasa kama unaota kuwa Zenj itamezwa na Tz Bara, inabidi umwone daktari mapema...
 
Kibunango,
hebu kasome tena kwanini Jumbe aliuzuliwa, sio kajiuzulu, alipouzuliwa, Jumbe alikuwa anataka kuiweka Zenj kwenye ramani lakini Tanzania walimuona ndio alipoitwa akapewa karatasi asome na mwisho atie saini na alizuiliwa kufika huko kwa muda mrefu au hujuwi,Mulipoleta Bilali tulisemaje alipita?
 
Back
Top Bottom