Kwanini wananchi wa Nyatwali hawajalipwa fidia zao na sasa mwaka umepita tangu wafanyiwe tathmini?.

koryo1952

JF-Expert Member
Mar 7, 2023
382
764
Sisi wananchi wa Nyatwali tunaitupia lawama Serikali juu ya kutolipwa fidia zetu na tangu tufanyiwe tathmini imepita mwaka moja sasa. Haturuhusiwi kufanya maendeleo kwa kujenga makazi mapya, kuendeleza kilimo cha kisasa , kupanda miti ya kudumu kwenye maeneo yetu n.k. tukisubiri fidia ambayo mpaka sasa hatujapata malipo. Sheria ya tathmini inatamka kwamba mwananchi kama hatalipwa kwa muda muafaka na miezi sita ikapita basi huyo mwananchi anastahili kulipwa asilimia 7 zaidi ya tathmini yake aliyoiwekea saini. Hivyo kwa ucheleweshaji huu tutadai asilimia 7 zaidi ya malipo yetu. Mwaka huu pia mwaka wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Vijiji vitatu vilivyoko kwenye Kata ya Nyatwali tayari vimefutwa na wananchi bado tunaishi kwenye vijiji hivyo, Je tutafanyaje uchaguzi huo?. Tunaiomba Serikali itulipe haraka iwezekanavyo ili tujue mahali pa kwenda.
 
Jibu lipo nimeweka barua ya DED wa Bunda post yangu imefutwa
Hiyo barua itakutokea puani, nyaraka zote zenye nembo "SIRI", na hazijawa downgraded, ukinaswa nayo, jela ni uhakika. Ngoja wakuwekee mtego humuhumu mtandaoni, unadhani umejificha kwa jina feki.

Hizo nyaraka ziko chini ya sheria ya usalama wa taifa, na hiyo sheria vifungo vyake sio vya kitoto
 
Sio kila mtu lay man wa sheria kama wewe kaka .we kaka hivyo hivyo,anyway nipe kifunga cha sheria kinachosema hivyo tuazie hapo kwanza kwa mtumishi wa Umma.
 
Back
Top Bottom