Mtu ambaye hajawahi kuimba hata kwaya kanisani anawezaje kuwa msemaji wa Shirikisho la Muziki?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
118,649
220,561
Steve Nyerere ametajwa kuwa Msemaji wa Shirikisho la Muziki Tanzania, haifahamiki aliyemteua kwenye cheo hicho ni nani, vigezo vilivyotumika kwenye uteuzi huo haramu havijulikani, wala malengo ya kufanya hivyo, bali ni dhahiri kwamba mteuliwa hajawahi kuonekana akiimba hata kwaya au kaswida popote nchini Tanzania, hajawahi kuonekana hata akiimba Wimbo wa Taifa lake, huyu anafahamika kama mchekeshaji wa KIWANGO CHA CHINI kabisa ambacho hakiwezi kuchekesha hata mtu mwenye mtindio wa ubongo.

Taarifa zinaonyesha kwamba karibu wanamuziki wote WANAPINGA UTEUZI WAKE, lakini yeye bila mshipa wa aibu anakataa kujiuzulu.

Hivi inawezekanaje kuteua mtu wa aina hii kuongoza muziki?
 
Connection mtu wangu!
avatar.jpg
 
Steve Nyerere ametajwa kuwa msemaji wa shirikisho la Muziki Tanzania , Haifahamiki aliyemteua kwenye cheo hicho ni nani , wala malengo ya kufanya hivyo , Bali ni dhahiri kwamba , Mteuliwa hajawahi kuonekana akiimba hata kwaya au kaswida popote nchini Tanzania , hajawahi kuonekana hata akiimba Wimbo wa Taifa lake , huyu anafahamika kama mchekeshaji wa KIWANGO CHA CHINI kabisa ambacho hakiwezi kuchekesha hata mtu mwenye mtindio wa ubongo .

Taarifa zinaonyesha kwamba karibu wanamuziki wote WANAPINGA UTEUZI WAKE , lakini yeye bila mshipa wa aibu anakataa kujiuzulu .

Hivi inawezekanaje kuteua mtu wa aina hii kuongoza Muziki ?

Moderator mlifuta uzi wangu kuhusu huyu mtu , Je hamtaki tujadili uozo huu ?

Atakuwa mjumbe kwenye ile kamati ya mama sema na mwanao. Hapo fadhila fadhilini hapo.
 
Kuimba kwaya ni taaluma kubwa ya kuhubiri, ikijumuisha utunzi, usomaji na uandishi note,upigaji wa vyombo mbalimbali vya muziki na mambo mengine mengi.
Si sahihi kabisa kuidunisha taaluma hiyo kwa kufananisha na hiyo bongo Flava.
Ungekosoa uteuzi wa msemaji wenu kwa kulinganisha na kitu kingine.
 
Kuimba kwaya ni taaluma kubwa ya kuhubiri, ikijumuisha utunzi, usomaji na uandishi note,upigaji wa vyombo mbalimbali vya muziki na mambo mengine mengi.
Si sahihi kabisa kuidunisha taaluma hiyo kwa kufananisha na hiyo bongo Flava.
Ungekosoa uteuzi wa msemaji wenu kwa kulinganisha na kitu kingine.
Duh
 
Steve Nyerere ametajwa kuwa Msemaji wa Shirikisho la Muziki Tanzania, haifahamiki aliyemteua kwenye cheo hicho ni nani, vigezo vilivyotumika kwenye uteuzi huo haramu havijulikani, wala malengo ya kufanya hivyo, bali ni dhahiri kwamba mteuliwa hajawahi kuonekana akiimba hata kwaya au kaswida popote nchini Tanzania, hajawahi kuonekana hata akiimba Wimbo wa Taifa lake, huyu anafahamika kama mchekeshaji wa KIWANGO CHA CHINI kabisa ambacho hakiwezi kuchekesha hata mtu mwenye mtindio wa ubongo.

Taarifa zinaonyesha kwamba karibu wanamuziki wote WANAPINGA UTEUZI WAKE, lakini yeye bila mshipa wa aibu anakataa kujiuzulu.

Hivi inawezekanaje kuteua mtu wa aina hii kuongoza muziki?
Kwan msemaji kazi yake ni nini hasa kwenye taasisi?!
 
Waliofanya hivyo inaonyesha jinsi ambavyo hawako serious.Yaani taifa limeishiwa hadi watu wa ajabu ajabu wanapata nafasi kama hizo alafu tunategemea sanaa ipige hatua.
 
Back
Top Bottom