Mtoto wa miaka 10 agundua udhaifu wa Instagram

STUNTER

JF-Expert Member
Dec 15, 2015
13,077
17,208
Mvulana wa umri wa miaka 10 nchini Finland ameshangaza wengi baada ya kugundua
udhaifu katika mtandao wa kijamii wa Instagram.

Mvulana huyo kwa jina JANI ametunukiwa $10,000 (£7,000) baada ya kugundua udhaifu huo uliowezesha mtu kuingia kwenye mtandao huo wa kusambaza picha na kufuta maoni ya watu.

Jambo la kushangaza zaidi ni kwamba kisheria haruhusiwi kutumia mtandao huo hadi atimize umri wa miaka 13. Facebook, inayomiliki Instagram, ilichukua hatua
upesi na kuondoa udhaifu huo. Sasa, ndiye mtu mchanga zaidi kutunukiwa pesa kwa kugundua udhaifu katika mitandao ya kampuni hiyo.

Aliandikia wasimamizi wa mtandao huo barua pepe Februari kuwafahamisha kuhusu ugunduzi wake. Wataalamu wa mtandao huo walimfungulia akaunti ndipo aweze kuthibitisha madai yake na akafanikiwa.

=====================

Instagram gives £7000 to 10-year-old who revealed security flaw

Justin Sullivan
Image sharing appInstagramhas given a 10-year-old Finnish boy £7,000 as a reward for finding asecurityflaw in the platform.

Jani, who lives in Helskini, found asecurityflaw that meant he could delete other users' comments. The company say it "quickly fixed" the flaw but rewarded the boy for disclosing the information.

To prove he had found the security vulnerability Jani (his surname was not revealed) deleted a comment on a test account set-up by staff at Instagram. However, the method worked on other accounts.

Facebook, which owns Instagram, has a "bug bounty" for developers and hackers who can undercover flaws in security.

"We recognise and reward security researchers who help us to keep people safe by reporting vulnerabilities in our services," it says.


Chanzo: Instagram hacked by 10 year old boy (Wired UK)
 
Facebook wamempa zawadi ya dola 10,000 za Kimarekani kijana mdogo wa miaka 12 kama zawadi baada ya kijana huyo kugundua udhaifu kwenye utengenezaji wa app ya Instagram.
Mtoto huyo ni raia wa Finland aligundua kosa kwenye code ya app ya Instagram ambayo inaweza muwezesha mtu mwenye ujuzi wa udukuzi kuweza kufuta ‘comment’ zozote za watu katika app hiyo.

Kijana huyo amepewa dola 10,000 za kimarekani ambazo ni takribani Tsh 22,000,000 | Ksh 1,000,000.

Makampuni makubwa kama Facebook na Google wanautaratibu wa kuruhusu wadukuzi (hackers) kugundua udhaifu wa teknolojia zao na pale wanapojitokeza na kuzionesha basi huwa wanapatiwa zawadi ya pesa.

Kijana huyo amesema kubobea katika fani ya usalama wa kimtandao ndio lengo lake na anahamu sana ya kuja kufanya kazi katika eneo hilo la teknolojia.
Kijana huyu wa Finland ambaye jina lake limefichwa kutokana na ombi la baba yake amekuwa moja ya hackers wadogo zaidi kuwahi kupokea zawadi za kazi ya namna hii. Baba yake amesema kijana huyu na kaka yake wanatumia masaa kadhaa kila siku kuchunguza code za mitandao na huduma mbalimbali kuona kama watagundua makosa. Hii ni mara ya kwanza kwa kupata pesa kutokana na juhudi hizo.

Wenzetu huanza kuwaweka karibu watoto na masuala ya teknolojia mapema zaidi, je unaona mtazamo gani wa hali ilivyo nchini kwetu kutuwezesha kufikia viwango hivi?

Source teknokona
 
Huku kwetu angeshitakiwa na sheria ya mitandao
Natamani sana Ku code lakini kwa hali ya kimaisha ya kifamilia imekua ngumu sana upatikanaji wa vifaa kama vile computers kwetu sis inakua ngumu sana kutokana na upatikanaji Mdogo wa fedha kingine kinatokana na familia zetu, wazazi wanashindwa kutambua mahitaji ya mtoto pindi anapoanza kujielewa na kujua nikitugani anahitaji kujifunza badala yake wanamforce kujifunza vitu ambavyo vipo njee ya matakwa ya mtoto
 
Huku kwetu angeshitakiwa na sheria ya mitandao
Natamani sana Ku code lakini kwa hali ya kimaisha ya kifamilia imekua ngumu sana upatikanaji wa vifaa kama vile computers kwetu sis inakua ngumu sana kutokana na upatikanaji Mdogo wa fedha kingine kinatokana na familia zetu, wazazi wanashindwa kutambua mahitaji ya mtoto pindi anapoanza kujielewa na kujua nikitugani anahitaji kujifunza badala yake wanamforce kujifunza vitu ambavyo vipo njee ya matakwa ya mtoto
 
Uku kwetu tumejawa na ujinga mtoto akishinda kwenye kompyuta mzazi atataka kumchapa kisa kwann hatakikusomaanashinda kwenyemitandao tu
 
Natamani sana Ku code lakini kwa hali ya kimaisha ya kifamilia imekua ngumu sana upatikanaji wa vifaa kama vile computers kwetu sis inakua ngumu sana kutokana na upatikanaji Mdogo wa fedha kingine kinatokana na familia zetu, wazazi wanashindwa kutambua mahitaji ya mtoto pindi anapoanza kujielewa na kujua nikitugani anahitaji kujifunza badala yake wanamforce kujifunza vitu ambavyo vipo njee ya matakwa ya mtoto
Mpaka sasa umepiga hatua gani?

Unao ujuzi wa kutengeneza hata programu ndogo ndogo
 
Uku kwetu tumejawa na ujinga mtoto akishinda kwenye kompyuta mzazi atataka kumchapa kisa kwann hatakikusomaanashinda kwenyemitandao tu
Hao watoto/vijana huko kwenye computer unajua wanachofanya?
Computer /simu janja vimekuwa majanga kwa vijana wetu badala ya advantage!
Uwape access ta hivyo vitu kwa tahadhari kuu!
 
Bongo watoto wetu wakikaa kwnye computer wanaanza kucheza magame tu au kuchek porno if you gve them acces ya internet
 
Hao watoto/vijana huko kwenye computer unajua wanachofanya?
Computer /simu janja vimekuwa majanga kwa vijana wetu badala ya advantage!
Uwape access ta hivyo vitu kwa tahadhari kuu!
Kuna aina mbili ya watumiaji wa hivi vifaa kuna users and producers kwaiyo we unaangalia mtoto wako yupo upande gan kati ya pande izo mbili
 
Mbona kama pesa aliyopewa haiendani na u'nyeti wa alichogundua?
 
Back
Top Bottom