Titans
JF-Expert Member
- Dec 31, 2010
- 1,459
- 3,366
nilikua nasikiliza WAPO radio FM kuna habari kutoka Tabora ikimnukuu doctor Slaa kuwa ana ushahidi wa kutosha kuwa mtoto wa Kigogo mmoja wa CCM alikamatwa na madawa ya kulevya huko China July mwaka huu.
mwenye ile thread kuhusu hii issue aiunganishe hapa chini..nimeitafuta sijaipata humu.
nawasilisha.
mwenye ile thread kuhusu hii issue aiunganishe hapa chini..nimeitafuta sijaipata humu.
nawasilisha.
Mtoto wa kigogo akamatwa na mihadarati China.
Mtoto anayeaminika kuwa wa mmoja wa viongozi wa juu wa serikali ya JK anatuhumiwa kukamatws na madawa ya kulevya katika uwanja wa ndege nchini China zinazokisiwa kuwa na thamani y ash bilioni nne za Kitanzania.
Tukio hilo zito linalogusa moja kwa moja uadilifu wa kigogo huyo wa serikali limemsukuma jana Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa kumtaka Rais jakaya Kikwete kuwaambia ukweli Watanzania juu ya tuhuma hizo alizodai zinaigusa serikali yake.
Akihutubia umati mkubwa wa watru katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana mjini Sikonge mkoani Tabora, Dk Slaa alisema kuwa taarifa za uhakika kutoka China zinasema kuwa Julai mosi mwaka huu vijana wenye asili ya Afrika walikamatwa Uwanja wa Ndege wa Hong Kong wakiwa na madawa ya kulevya zenye thamani ya Sh bilioio 4 ambapo mkuu wa kitengo cha mihadarati uwanjani hapo Yiu-Kwong alitaja majina ya vijana hao wawili, likwemo jina la kijana anayedaiwa kuwa mtoto wa mmoja wa viongozi wa serikali ya TZ.
"Mimi nemepokea taarifa hii kutoka China moja kwa moja. Tunamtaka Rais kikwete aseme ukwewli ni upi, maana taarifa hizi sasa zimeanza kuzagaa kwenye mitandao kuwa mtoto huyo wa kigogo serikalini kwake amekamatwa na dawa za kulevya huko China," alisema Dr Slaa.
Aliongeza: "Tangu zianze kujulikana hazojakanushwa mahali popote. Tunamtaka aeleze yeye maana alishindwa kutaja majina ya wauza mihadarati………………….
Hii ni sehemu ndogo ya habari hiyo katika Tanzania Daima la leo Jumamosi ambayo ndiyo stori yake kuu ukurasa wa mbele.