Mtoto Alhaji wa Makonda anawakilisha kundi kubwa kwa mamilioni ya watanzania.

Escrowseal1

JF-Expert Member
Dec 17, 2014
4,432
4,222
Naanza kwa kuwachana watanzania wenzetu hasa makundi haya muhimu .

1. Wabunge wanaojiongezea malipo yasiyo na uhusiano na Hali halisi ya watanzania

2. Viongozi kama mawaziri na makatibu wakuu mnaotumia nafasi zenu hadi kutuhumiwa kununua majumba Dubai na Africa ya kusini, mikocheni nk

3. Enyi maraisi mnaotaka hata mkiwa hampo hadi wenza wenu walipwe kiinua mgongo ambacho hawajachangia kwenye mifuko ya jamii

4.Wakurugenzi mlioko karibu na hao wananchi ambao wengi mmekuwa kama mashetani kwa matendo yenu tunayoyaona huko.

5.Viongozi wa dini mnaotumia dini zenu kujitajirisha kwa kuwanyonya waumini wenu mkitumia neno la Mungu huku waumini wenu mkiwadanganya utajiri wa kufikirika.

6.vyombo vya ulinzi na usalama ,mahakama msiosimamia dhuluma kuleta usawa katika jamii.

Ujumbe wangu Leo ni mmoja Tu. Mtoto Alhaji aliyekuwa muuza ndizi kutunza familia akiwa chini ya miaka 12 anawakilisha kundi kubwa Sana kwa mamilioni katika jamii yetu.

Huruma na machozi na kujigaragaza havitasaidia bila kutambua kuwa hii keki inamhusu kila mtanzania na kuhakikisha mnapunguza gap la walionacho

Mwl Nyerere ndo pekee machozi yake yangeweza kuni convince kuwa yanamaanisha ila kwenu nyie binafsi national ni machozi ya mamba tu .

Muwe na usiku mwema .
 
Back
Top Bottom