Ng'wamapalala
JF-Expert Member
- Jun 9, 2011
- 6,808
- 6,500
Hapana; wazungu wanasema, "hold on, CCM still alive and kicking".
Katika nchi zenye demokrasia, chaguzi zozote zile (ubunge, serikali za mitaa, congress, senate, nk) kipindi cha kati (midterm) huwa ni mwiba mkali kwa chama na serikali iliyoko madarakani. kwa ujumla, utendaji wake kwa kipindi hiki huwa unakabiliwa na changamoto nyingi na ngumu.
Ni katika kipindi hiki, utekelezaji wa ilani ya uchaguzi huwa bado haujakamilika, ni muda ambao pia chama na serikali yake hugundua kama kuna baadhi ya ahadi hazitekelezeki, vilevile ni muda ambao chama na serikali hukumbwa na kashfa za hapa na pale zinazowafanya wananchi waanze kuwa na wasiwasi au kukata tamaa na utekelezaji wa yale chama kiliwaahidi kwenye ilani ya uchaguzi.
Na hapo ndipo ombwi linapotokea kati ya chama, serikali na wananchi. Kwa wana siasa na vyama vya upinzani ambavyo ni makini, huu ndiyo muda wa mavuno kisiasa. "Step in and fill the vacuum" kwa sababu katika kipindi hiki, chama na serikali tawala hupoteza nguvu ya hoja katika ulingo wa kisiasa kwa vile wananchi walichokuwa wanakitegemea hawajakipata (ahadi) na hata kama watakuwa wamekipata kitakuwa hakijakamilika kwa vile utekelezani wa ilani ya uchaguzi huwa ni katika kipindi kizima cha utawala kisheria kwa mujibu wa katiba(miaka mitano).
Chama makini kama CHADEMA (samahani kwa kutogusia vyama vingine) wameliona hili na wanajitahidi katika uhamasishaji na uvunaji kisiasa (M4C) lakini changamoto na tatizo kubwa linalokikabili chama ni utegemezi wa watu mashuhuri wachache katika uhai wake kijamii. Chama kinaonekana kuwa hai pale wanapokuepo na wakiondoka kinalala(domant) au pia kinaondoka.
CHADEMA wameweza kupambana kihoja kwa mafanikio katika ulingo wa siasa katika chaguzi ndogo na katika mikutano inayoendelea (m4c) lakini siyo jambo la ajabu kufanikiwa kama wanavyopenda jamii eamini. Sababu kuu za mafanikio nimezielezea hapo juu. Kazi kubwa katika siasa ni ujumbe kukubalika na Natumaini hata wataalamu wa mambo ya siasa watakubaliana nami.
Ninapatwa na wasiwasi pale uvunaji wa kisiasa utakuwa ni kwa maandalizi ya uchaguzi mkuu kwa nchi nzima. Ninasema hivi kwa sababu, kwanza, watu muhimu au maarufu ndani ya chama watahitajika kwenye majimbo yao ya uchaguzi , pili, muda ni mfupi wa kampeni katika uchaguzi mkuu ambazo zinachukua kama miezi miwili na tatu, upatikanaji wa nyenzo(pesa, usafiri).
Chama hai si kile tu chenye nyenzo bali pia lazima kiwe na mizizi hai na matawi hai kwa maana lazima kiwe na jumuiya na wanachama hai kuanzia kaya mpaka taifa. Na kwa hili CCM inakuwa na mafanikio(advantage), kuna wengine watapinga lakini kwa aliye makini, kwa hili halina ubishi na imekuwa hivyo kwa vile kilishika hatamu (one party), kikajiimarisha kabla ya kuruhusu ushindani wa vyama vingi na hakikurudisha hizo nyenzo kwa wananchi wake.
Nakubaliana pale Mwalimu Nyerere na wachunguzi wa maswala ya kisiasa wanaposema adui mkuu wa CCM ni CCM yenyewe na siyo vyama vya upinzani. CCM itaondolewa madarakani na wana CCM. Mitafaruku ndani ya CCM na Utendaji mbovu wa serikalini ndiyo adui wa uhai wa CCM. Adui mkuu wa vyama vya upinzani ni CCM na pia viongozi maarufu wakorofi ndani ya chama. Marumbano ya hivi karibuni ndani ya CUF (Maarim Seif na Hamad) na CHEDEMA(Shibuda na BAVICHA) huku pande moja ikiishutumu pande nyingine kuwa imepandikizwa na CCM ni ishara tosha .
Changamoto kubwa na ngumu itakayovikabili vyama ya siasa (CHADEMA, CUF) ni katika uchaguzi wa mgombea urais kwa sababu vitaenda katika uchaguzi mkuu ujao vikiwa na matumaini hasa ya mgombea wake kushinda uchaguzi tofauti na mwaka 1995-2010 . Misuguano ya nani atapeperusha bendela ya kiti cha Urais itavifanya vyama hivi kumegeka au kushikamana lakini kuna uwezekano mkubwa wa vyama hivi kupata misukosuko mikubwa au kumegeka kwa vile itakuwa ni kwa mara ya kwanza kupatwa na changamoto hii kubwa wakati CCM waliisha ipitia katika awamu mbili za uchaguzi.
Katika siasa, wiki moja ni ndefu, safari ni ndefu zaidi katika miaka miwili na nusu. Wanaodiriki kusema CCM imekwisha huku akichukua mifano ya vyama vingine vilivyokuwa vikongwe katika Nchi za Kenya (KANU), zambia (UNIP) wakati mazingira ya kisiasa ni tofauti wanajiliwaza au wanaota ndoto za mchana lakini iwapo CHADEMA kwa Tanzania bara na CUF kwa Tanzania visiwani watashikamana kisiasa na kujinasua na changamoto nzito ya uchaguzi wa wagombea hasa kiti cha urais na kuendelea na kasi waliyonayo kwa sasa wakati baadhi ya watendaji ndani ya CCM wakiendelea na utendaji wa kimazoea. Kuna uwezakano mkubwa Tanzania ikaingia mwaka 2016 ikiwa kwenye mabadiriko makubwa ya kisiasa ambayo hayajawahi kutokea katika historia nchini.
Kwa jinsi ishara zinavyoonyesha, kwa sasa hakuna lisilowezekana katika medani ya kisiasa nchini wakati huohuo, waswahili anasema, usione simba kanyeshewa ukadhani ni paka.
Katika nchi zenye demokrasia, chaguzi zozote zile (ubunge, serikali za mitaa, congress, senate, nk) kipindi cha kati (midterm) huwa ni mwiba mkali kwa chama na serikali iliyoko madarakani. kwa ujumla, utendaji wake kwa kipindi hiki huwa unakabiliwa na changamoto nyingi na ngumu.
Ni katika kipindi hiki, utekelezaji wa ilani ya uchaguzi huwa bado haujakamilika, ni muda ambao pia chama na serikali yake hugundua kama kuna baadhi ya ahadi hazitekelezeki, vilevile ni muda ambao chama na serikali hukumbwa na kashfa za hapa na pale zinazowafanya wananchi waanze kuwa na wasiwasi au kukata tamaa na utekelezaji wa yale chama kiliwaahidi kwenye ilani ya uchaguzi.
Na hapo ndipo ombwi linapotokea kati ya chama, serikali na wananchi. Kwa wana siasa na vyama vya upinzani ambavyo ni makini, huu ndiyo muda wa mavuno kisiasa. "Step in and fill the vacuum" kwa sababu katika kipindi hiki, chama na serikali tawala hupoteza nguvu ya hoja katika ulingo wa kisiasa kwa vile wananchi walichokuwa wanakitegemea hawajakipata (ahadi) na hata kama watakuwa wamekipata kitakuwa hakijakamilika kwa vile utekelezani wa ilani ya uchaguzi huwa ni katika kipindi kizima cha utawala kisheria kwa mujibu wa katiba(miaka mitano).
Chama makini kama CHADEMA (samahani kwa kutogusia vyama vingine) wameliona hili na wanajitahidi katika uhamasishaji na uvunaji kisiasa (M4C) lakini changamoto na tatizo kubwa linalokikabili chama ni utegemezi wa watu mashuhuri wachache katika uhai wake kijamii. Chama kinaonekana kuwa hai pale wanapokuepo na wakiondoka kinalala(domant) au pia kinaondoka.
CHADEMA wameweza kupambana kihoja kwa mafanikio katika ulingo wa siasa katika chaguzi ndogo na katika mikutano inayoendelea (m4c) lakini siyo jambo la ajabu kufanikiwa kama wanavyopenda jamii eamini. Sababu kuu za mafanikio nimezielezea hapo juu. Kazi kubwa katika siasa ni ujumbe kukubalika na Natumaini hata wataalamu wa mambo ya siasa watakubaliana nami.
Ninapatwa na wasiwasi pale uvunaji wa kisiasa utakuwa ni kwa maandalizi ya uchaguzi mkuu kwa nchi nzima. Ninasema hivi kwa sababu, kwanza, watu muhimu au maarufu ndani ya chama watahitajika kwenye majimbo yao ya uchaguzi , pili, muda ni mfupi wa kampeni katika uchaguzi mkuu ambazo zinachukua kama miezi miwili na tatu, upatikanaji wa nyenzo(pesa, usafiri).
Chama hai si kile tu chenye nyenzo bali pia lazima kiwe na mizizi hai na matawi hai kwa maana lazima kiwe na jumuiya na wanachama hai kuanzia kaya mpaka taifa. Na kwa hili CCM inakuwa na mafanikio(advantage), kuna wengine watapinga lakini kwa aliye makini, kwa hili halina ubishi na imekuwa hivyo kwa vile kilishika hatamu (one party), kikajiimarisha kabla ya kuruhusu ushindani wa vyama vingi na hakikurudisha hizo nyenzo kwa wananchi wake.
Nakubaliana pale Mwalimu Nyerere na wachunguzi wa maswala ya kisiasa wanaposema adui mkuu wa CCM ni CCM yenyewe na siyo vyama vya upinzani. CCM itaondolewa madarakani na wana CCM. Mitafaruku ndani ya CCM na Utendaji mbovu wa serikalini ndiyo adui wa uhai wa CCM. Adui mkuu wa vyama vya upinzani ni CCM na pia viongozi maarufu wakorofi ndani ya chama. Marumbano ya hivi karibuni ndani ya CUF (Maarim Seif na Hamad) na CHEDEMA(Shibuda na BAVICHA) huku pande moja ikiishutumu pande nyingine kuwa imepandikizwa na CCM ni ishara tosha .
Changamoto kubwa na ngumu itakayovikabili vyama ya siasa (CHADEMA, CUF) ni katika uchaguzi wa mgombea urais kwa sababu vitaenda katika uchaguzi mkuu ujao vikiwa na matumaini hasa ya mgombea wake kushinda uchaguzi tofauti na mwaka 1995-2010 . Misuguano ya nani atapeperusha bendela ya kiti cha Urais itavifanya vyama hivi kumegeka au kushikamana lakini kuna uwezekano mkubwa wa vyama hivi kupata misukosuko mikubwa au kumegeka kwa vile itakuwa ni kwa mara ya kwanza kupatwa na changamoto hii kubwa wakati CCM waliisha ipitia katika awamu mbili za uchaguzi.
Katika siasa, wiki moja ni ndefu, safari ni ndefu zaidi katika miaka miwili na nusu. Wanaodiriki kusema CCM imekwisha huku akichukua mifano ya vyama vingine vilivyokuwa vikongwe katika Nchi za Kenya (KANU), zambia (UNIP) wakati mazingira ya kisiasa ni tofauti wanajiliwaza au wanaota ndoto za mchana lakini iwapo CHADEMA kwa Tanzania bara na CUF kwa Tanzania visiwani watashikamana kisiasa na kujinasua na changamoto nzito ya uchaguzi wa wagombea hasa kiti cha urais na kuendelea na kasi waliyonayo kwa sasa wakati baadhi ya watendaji ndani ya CCM wakiendelea na utendaji wa kimazoea. Kuna uwezakano mkubwa Tanzania ikaingia mwaka 2016 ikiwa kwenye mabadiriko makubwa ya kisiasa ambayo hayajawahi kutokea katika historia nchini.
Kwa jinsi ishara zinavyoonyesha, kwa sasa hakuna lisilowezekana katika medani ya kisiasa nchini wakati huohuo, waswahili anasema, usione simba kanyeshewa ukadhani ni paka.