Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,712
Ni jana tu jamaa yangu mmoja aliambiwa na baba yake kuwa;"nitakusapoti kwenye ndoa yako lakini usimuoe huyo mwanamke ulie nae",kijana alipomuuliza baba yake sababu ya kumkataa mchumba wa kijana wake,mzazi alisema eti kabila la huyo mwanamke hawajatulia.Mzee yule akamuorodhezea makabila mengine kwamba asijidanganye kuoa,makabila hayo ni Wanyiramba(hili ndilo kabila la mchumba wake),Wahaya,Wasukuma wa Nasa na Wachaga wa Machame.Mzee yule alidai kuwa Wahaya na Wanyiramba wanasifa zinazofanana yaani vicheche.Wasukuma wa Nasa na Wachaga wa Machame nao wana sifa zinazofanana yaani Uchawi,wanakawaida ya kuwaua waume zao baada ya kupata mafanikio.Kwanza nikiri kuwa hoja hizi zina ukweli.Lakini pia ukweli huo ulikua una nguvu sana zamani sio sasa.Ni vyema jamii ikaacha kuyahukumu makabila hayo leo.Nasema hayo kwani leo ni vigumu sana kumjua mwanamke mwadilifu kwa misingi ya kabila.Tabia za kupenda kufanya ngono hovyo na kwenda kwa waganga iko karibu kwa kila mwanamke,kama ni karibu kila mwanamke basi inayahusu makabila yote(hata wanaume wana tabia hizi ila kwa malengo tofauti).Nadhani huu ni wakati wa kubadilika na kuishi kiuhalisia na sio kimazoea!!