Barubaru
JF-Expert Member
- Apr 6, 2009
- 7,161
- 2,323
Amani iwe nanyi,
Nimepokea habari za msiba wa Mzee wetu Abisae Stephen aliyekuwa mtangazaji mkongwe sana na mwandamizi wa Radio Tanzania.
Nimeelezewa amefariki dunia Juzi hospitali akiwa anasumbuliwa na maradhi. Na maiti yake imesafirishwa jana 12 aug kwenda kuzikwa kwao Moshi.
Hakika Tanzania wamepoteza mwanahabari mahiri sana na mzoefu katika tasnia ya habari nchini humo.
Kwa tuliowahi kufanya nae kazi japo kwa kipindi kifupi, Alikuwa ni mtu mcheshi sana na alikuwa mahiri sana kwa lugha mbalimbali za kigeni. Aliweza kuongea lugha zaidi ya tano ukiondoa lugha yake ya kikabila ya kichaga.
Wengi tulizoea kumwita Kaka au hata Mz wa Lugha.
Hakika ni msiba mkubwa na nashangaa mpaka leo waandishi wa habari huko Tz wameacha kuandika msiba huu.
Hakika Mola amlaze pahala panapo stahiki.
Ni Mimi
Bi Nasriyah Saleh Al Nahdi.
Doha
Nimepokea habari za msiba wa Mzee wetu Abisae Stephen aliyekuwa mtangazaji mkongwe sana na mwandamizi wa Radio Tanzania.
Nimeelezewa amefariki dunia Juzi hospitali akiwa anasumbuliwa na maradhi. Na maiti yake imesafirishwa jana 12 aug kwenda kuzikwa kwao Moshi.
Hakika Tanzania wamepoteza mwanahabari mahiri sana na mzoefu katika tasnia ya habari nchini humo.
Kwa tuliowahi kufanya nae kazi japo kwa kipindi kifupi, Alikuwa ni mtu mcheshi sana na alikuwa mahiri sana kwa lugha mbalimbali za kigeni. Aliweza kuongea lugha zaidi ya tano ukiondoa lugha yake ya kikabila ya kichaga.
Wengi tulizoea kumwita Kaka au hata Mz wa Lugha.
Hakika ni msiba mkubwa na nashangaa mpaka leo waandishi wa habari huko Tz wameacha kuandika msiba huu.
Hakika Mola amlaze pahala panapo stahiki.
Ni Mimi
Bi Nasriyah Saleh Al Nahdi.
Doha