TANZIA Mtangazaji wa Clouds FM, Ephraim Kibonde afariki dunia. Azikwa makaburi ya Kinondoni,Dar es Salaam

R.I.P Ephraim Kibonde.
Bwana alitoa Bwana ametwaa na jina lake lihimidiwe.
Tutakukumbuka kwa mema mengi. Ucheshi wako uwapo kazini. Ulinogesha sana Kipindi cha Jahazi.
Sasa Jahazi bila Kibonde ni pengo Kubwa.
 
Watu wanakufa kila siku sema wakitokea watu maarufu watu huwa hatuamini na kuona dah jamaa amekufa mapema imekuaje jamaa ametutoka, na huwa tunaanza kujitasmini kuwa tumrudie Mungu jamani maisha ni mafupi, ukweli ni kwamba watu wanasahau baada ya maziko, ukweli ni kwamba matendo yetu yabadilike tuishi kwa kumpendeza Mungu tupendane, tuthaminiane hakika hatujui saa wala wakati,
RIP EPHRAHIM KIBONDE
 
Kwetu huwa tunaamini kuwa mzee mwenye familia kubwa (wajukuu na vitukuu) akifariki basi husindikizwa na mjukuu au kitukuu.

R. I. P KIBONDE.
 

Habari za hivi punde ni kuwa mtangazaji maarufu wa Clouds FM, Ndugu Ephraim Kibonde amefariki dunia alfajiri ya leo tarehe 7 Machi 2019.

Kibonde alianza kusumbuliwa na presha akiwa katika msiba wa marehebu Ruge Mutahaba huko Bukoba mkoani Kagera na kuhamishiwa hospitali ya Bugando jijini Mwanza ambapo mauti yamemkuta.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza pamoja na Mkuu wa Vipindi wa Clouds FM, Sebastian Maganga wamethibitisha kutokea kwa kifo hicho.

Bwana ametoa, Bwana ametwaa

Mwaka jana Ephraim Kibonde alimpoteza mkewe mama Sara Kibonde. Zaidi soma >TANZIA: Ephraim Kibonde afiwa na Mke wake Sara Kibonde - JamiiForums

View attachment 1039958
Ephraim Kibonde akiwa na mkewe enzi za uhai wao​

Mungu wangu! Kuna ' Jinamizi ' gani hapo CMG jamani? Poleni tena CMG, wana Tasnia nzima ya Habari na Utangazaji nchini, Familia yake na Wadau wengine wote. Si vizuri mbele ya Mungu kuhisi Jambo baya juu ya tukio fulani ila kwa matukio kama haya kama Binadamu kale ka ' Element ' ka kuhisi Vitu vingine labda ni Mkosi / Nuksi lazima katakuja tu. Inasikitisha na inauma mno na sana.

R.I.P Kamarada Ephraim Kibonde.
 
Asee,nimeumia sana ,nasikitika kwa Mara nyingine kaka angu Kibs Ephraim Kibonde umetutoka ,mbaya zaidi nilishindwa kuja kumzika Shemeji yangu Mkeo Sarah kibonde ,na sasa wewe pia umetangulia nashindwa pia kuja kukuzika ,lkn tutaonana Tena

Msalimie Mkeo Sarah ,msalimie Boss Ruge, wasalimie wote huko

Nakumbuka mengi siwezi weka yote ,ila nakuombea kwa Mungu

R.I.P Kaka angu Ephraim Kibonde 'kibs'

MTC | 101|
 
Habari za hv punde kua huyu mtangazaji wa cluz media group ametutoka dunia.
Pole ndugu jamaa na familia kwa ujumla kwa kumpoteza kijana mchapa kazi.
Kama taifa na tasnia ya habari akika tumepoteza mtu makini sana.
Pumzika kwa amani mungu akupunguzie na azabu kabli.



Sent from my iPhone using JamiiForums
kawombe Unatumia Iphone unavyoandika ni balaa umesoma chekechea kweli?? Napata wasi wasi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kuna watu hapa duniani wanajiona miungu watu,,wananyanyasa wenzao,,wanatesa wenzao ,,wanaombea watu wengine vifo,,wanajiapiza kuua wenzao,,wanaua wenzao,,wanapiga wenzao,,wanawafunga wenzao,,wanapiga watu lisasi,,wanawakata mapanga,,wanateka watu,,wananyonga watu na kuwafunga kwenye viroba na kuwatupa baharini..

kupitia hii misiba iwe funzo wote ipo siku Mungu akiamua tutalala
 
Back
Top Bottom