Mt KILIMANJARO

Kituko

JF-Expert Member
Jan 12, 2009
9,555
9,330
100_0141.JPG
Hii picha ilinisikitisha sana, nimeipiga Juzi tu katika hilo eneo la Makuti (Zimbabwe) ni umbali wa Km 63 kutoka Chirundu border post (Border ya Zambia na Zimbabwe)

Katika hicho kibao Mlima Kilimanjaro unaonyeshwa upo umbali wa 2772km kutoka hapo Makuti, na unaonyeshwa kuwa huo mlima upo Kenya

Nilijiuliza sana, Yaani mpaka wa leo bado Dunia inafahamu Kilimanjaro ipo Kenya?

Kwa kweli sikujisikia Vizuri, nilipofika Harare nilenda moja kwa moja mpaka Umoja House (Ulipo ubalozi wa Tanzania), kwa bahati mbaya sikumkuta Balozi (Hadadi Rajabu), lakini nilikutana na mama Mmoja wa Kizanzibar nae wala hajui kinachoendelea anasema hajawahi kuona hicho kibao, nikamwambia hii ndio picha hebu fatilieni, aliniambia hilo ni jukumu la TANAPA

Nikaaga na kuendelea na Hamsini zangu huku roho ikiniuma sana
 
Mkuu wako ubalozini kwaajili ya salary tu,kama umepeleka na ushahidi wa picha lakini unaambiwa ni kazi ya TANAPA. Ina maana hao watu wa ubalozi hata kupokea taarifa yako kwa mshtuko hakuna. Mkuu kweli inatia uchungu sana unakumbuka kipindi kile watu wa wizara walijiandalia per diem kwenda china kutangaza utalii. Kumbe ilikuwa ni kwenda kujilipa tu,hakuna hatua yoyote waliyochukulia hata kinachoendelea ni siri.
 
sisi tumelaaniwa wavivu sana wakutekeleza majukumu yetu!!tatizo serikalini hakuna Key Performance Indicators hilo ni kosa kubwa
 
tumelogwa sisi, na aliyetuloga alisha kufa, hakuna wa kutegua tego
 
usishangae sana mkuu hawako kwa ajili hiyo na wala hawajitambui wenyewe wajijua wapo kwa ajili ya
kusikilizia ni lini mkuu wa nchi ama waziri flani anaenda kutembelea ktk nchi walipo ili wamwandalie waweze kupata asilimia 10 kutoka sehemu zitazonufaika na ziara hizo baaaasi hamna la zaidi kwa kutetea maslahi ya nchi na hii yote ni sababu
ya kupeana kazi kwa kujuana na wala si cvs.uwajibikaji wa kweli utakuwepo pale tu watu watakapoanza kuajiriwa kwa kuzingatia taaluma bila kujali undugu na kujuana...
 
huyo mama anapigwa nao kweli yaani ..tanapa wwao wana mabalozi kila nchi? inasikitisha kweli..ina maana hata wewe uliyeeleka hivi picha kwake na wewe ni tanapa..narudia tena huyo mamam anapigwa mjengo
 
kaka wewe unashangaa,unathan mabalozi hawayaoni hayo matangazo?wanayaona sana, kwani mimi nilikua inchi flan nje ya africa nikakuta kuna tangazo la utalii lipo karibu kabisa na ubalozi wa tanzania na linakaribisha watalii kutembelea mlima kilimanjaro ambao upo kenya co tanzania na balozi kila cku analiona,nikajaribu kuulizia pale ubalozin kila mtu akawa anasema hausiki na hilo swala.
 
Haya ni matokeo ya kuteua mabalozi kwa utashi wa kiitikadi za chama na urafiki na kuzawaidiana. Most wa mabalozi wetu hawajui nini wanatakiwa kufanya zaidi ya kuwezesha ziara za viongozi kama v.a.s.co. Ukiwatoa hao mabalozi wetu kuna watu kama TTB{ Tanzania Tourism Board} wao wanakimbilia kupeana posho kwenda ulaya wakati mtu wa hapo South Africa ua Malawi hawajui Wapi Mt. Kilimamjaro ulipo.
 
kweli inasikitisha lakini hata ulaya na america wanajuwa kilinjaro ipo kenya

je utakubali kuwa kuna watanzania wengi tuu hawajui kitu kuhusu Mt. Kilimanjao? Nimewahi kuwasikia vijana tena wanafunzi wa vyuo vikuu wakieleza kuwa kuna milima mitatu ambayo ni Kilimanjaro, Mawenzi na Kibo na kati ya hiyo yote Kilimanjaro ndiyo mrefu. Kitu ambacho si sahihi hata kidogo
 
au labda wakenya ndio wanaotangaza knjaro ipo kwao

Wamekuwa wakitangaza Knjaro unapandika kiurahisi upande wao kuliko Tz na kwamba uko kwao...lakini hii ni ya zamani wakati ule Tz tulikuwa tumelala hatukemei kwa nguvu kuwa mlima ni wetu na upo Tz.

Kituko nikupe hongera kwa hatua uliyochukua ya kwenda ubalozini ingawaje majibu uliyopata yanakatisha tamaa. Huyo mwanamke mzenji kweli kabisa yaani anaona ni kazi ya Tanapa??ingekuwa ni mimi ndo kanijibu hivo wallahi ningewaka koz i dont give a monkey's ass naongea na nani as long as ni kazi yako kulinda rasilimali na sura ya nchi yetu. mshenzi wa adabu watu kama hawa wanatia hasira sana basi tu
 
Ni kweli watu wapo Ubalozini hata huwezi kujua wanafanya nini,
Hiyo ndio picha yetu Watanzania. Hakuna hata mtu mmoja mwenye uchungu na uzalendo wa kweli wa nchi yake, nchi zingine unakuta kila Raia ana bendera na anakuwa proud na vitu vinavyoitambulisha nchi yake, lakini kwa Tanzania hilo hakuna kabisa
 
Usikute hata huyo Balozi alikuwepo ila wakakupotezea tu. Kwa kweli inakera sana jinsi hii mijitu ya ubalozi inavyochukulia vitu poa!
 
View attachment 51152
Hii picha ilinisikitisha sana, nimeipiga Juzi tu katika hilo eneo la Makuti (Zimbabwe) ni umbali wa Km 63 kutoka Chirundu border post (Border ya Zambia na Zimbabwe)

Katika hicho kibao Mlima Kilimanjaro unaonyeshwa upo umbali wa 2772km kutoka hapo Makuti, na unaonyeshwa kuwa huo mlima upo Kenya

Nilijiuliza sana, Yaani mpaka wa leo bado Dunia inafahamu Kilimanjaro ipo Kenya?

Kwa kweli sikujisikia Vizuri, nilipofika Harare nilenda moja kwa moja mpaka Umoja House (Ulipo ubalozi wa Tanzania), kwa bahati mbaya sikumkuta Balozi (Hadadi Rajabu), lakini nilikutana na mama Mmoja wa Kizanzibar nae wala hajui kinachoendelea anasema hajawahi kuona hicho kibao, nikamwambia hii ndio picha hebu fatilieni, aliniambia hilo ni jukumu la TANAPA

Nikaaga na kuendelea na Hamsini zangu huku roho ikiniuma sana

wakati mungine huwezi kulaumu tanapa, hawa walioandika hicho kibao inaonyesha wana ulimbukeni fulani, wavivu wa kutafuta habari au wapo remote area hakuna njia yoyote ya kupata habari , dunia nzima inajua kilimanjaro ipo tanzania cnn kila siku inatangaza, internet etc
 
Watu wanapiga bao kwa ujinga wa watanzania. Hao ndiyo mabalozi wanaoteuliwa na CCM hata elimu hamna!
 
lakini pamoja na yote ndugu yangu at leas ungenunuwa spray color ufute huo ujinga ulioandikwa hata wange kuuliza ungewajibu kilichoandikwa ni uongn
 
Back
Top Bottom